Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
AMESEMA ALIYESEMA NITAWAFELISHA WANAFUNZI KWA HISTORIA ZANGU ZISIZO NA VYANZO VYA KUAMINIKA
Lupweko said:
Mzee utawafelisha watoto kwenye mitihani yao kwa historia zako ambazo hazina vyanzo vya kuaminika
Lupweko,
Mimi sina historia iliyo yangu.
Historia ni kama ilivyotendwa na wahusika hao ndiyo wenye historia yao.
Wala vitabu nilivyoandika mimi haviko katika mtaala kwa hiyo hakuna mwalimu anaesomesha kitabu changu katika shule za Tanzania kwa hiyo uwezekano wa mwanafunzi kufeli mtihani haupo kabisa.
Labda tuzungumze historia ya Maji Maji na yale ambayo mimi nimeyasahihisha katika historia hiyo na nitakuwekea ushahidi.
Majemadari wa Maji Maji walinyongwa na Wajerumani na kuzikwa katika kaburi la halaiki isipokuwa mmoja Songea Mbano ambae jina lake khasa ni Abdulrauf Songea Mbano.
Katika hao walionyongwa yuko mwanamke mmoja ambae siku zote anatambulishwa kwa jina moja tu la Mkomanile.
Jina lake huyu mama ni Khadija.
Jiulize kwa nini majina ya Kiislam yameondolewa kwa hawa mashujaa?
Majemadari hawa wote walikuwa Waislam na walipopitishiwa hukumu ya kunyongwa Father Johannes kutoka Peramiho aliwaendelea na kuwaambia kuwa endapo wataukana Uislam na kuwa Wakristo hukumu ya kuuliwa itafutwa.
Father Johannes wa Peramiho akawabatiza baadhi na kuwapa majina ya Kikristo.
Ukisoma majina ya hawa yaliyoandikwa katika mnara wa kumbukumbu ya Maji Maji, Mahenge, Songea utaona majina yao ya Kiislam hayapo yameandikwa majina ya Kikristo.
Ushahidi wa haya unatokana katika utafiti niliofanya na mwingine katika haya ninayokueleza hapo juu upo katika kitabu cha Prof. James Giblin kuhusu Maji Maji: ''Lifting the Fog of War,'' (2010).
Kuwa vyanzo vyangu haviaminiki si kweli.
Usijipotezee nafasi ya kujifunza kwa hofu isiyokuwa na sababu.
Ama kuhusu kufeli wanafunzi hawa wamashafelishwa kwa kusomeshwa historia iliyoandikwa kwa ghilba.
Nakuwekea hapo chini picha ya Prof. Giblin ofisini kwake University of Iowa akiwa ameshika kitabu cha Abdul Sykes.
Prof. Giblin ni mwalimu wa African History chuoni hapo.
Huu ni mwaka wa 2011.
PICHA:
1. Prof. James Giblin.
2. Mnara wa kumbukumu wa majemadari 66 wa Maji Maji walionyongwa na Wajerumani hapo penye mnara ndipo lilipo kaburi lao.
3. Kaburi la Abdulrauf Songea Mbano
4. Abdulrauf Songea Mbano
Lupweko said:
Mzee utawafelisha watoto kwenye mitihani yao kwa historia zako ambazo hazina vyanzo vya kuaminika
Lupweko,
Mimi sina historia iliyo yangu.
Historia ni kama ilivyotendwa na wahusika hao ndiyo wenye historia yao.
Wala vitabu nilivyoandika mimi haviko katika mtaala kwa hiyo hakuna mwalimu anaesomesha kitabu changu katika shule za Tanzania kwa hiyo uwezekano wa mwanafunzi kufeli mtihani haupo kabisa.
Labda tuzungumze historia ya Maji Maji na yale ambayo mimi nimeyasahihisha katika historia hiyo na nitakuwekea ushahidi.
Majemadari wa Maji Maji walinyongwa na Wajerumani na kuzikwa katika kaburi la halaiki isipokuwa mmoja Songea Mbano ambae jina lake khasa ni Abdulrauf Songea Mbano.
Katika hao walionyongwa yuko mwanamke mmoja ambae siku zote anatambulishwa kwa jina moja tu la Mkomanile.
Jina lake huyu mama ni Khadija.
Jiulize kwa nini majina ya Kiislam yameondolewa kwa hawa mashujaa?
Majemadari hawa wote walikuwa Waislam na walipopitishiwa hukumu ya kunyongwa Father Johannes kutoka Peramiho aliwaendelea na kuwaambia kuwa endapo wataukana Uislam na kuwa Wakristo hukumu ya kuuliwa itafutwa.
Father Johannes wa Peramiho akawabatiza baadhi na kuwapa majina ya Kikristo.
Ukisoma majina ya hawa yaliyoandikwa katika mnara wa kumbukumbu ya Maji Maji, Mahenge, Songea utaona majina yao ya Kiislam hayapo yameandikwa majina ya Kikristo.
Ushahidi wa haya unatokana katika utafiti niliofanya na mwingine katika haya ninayokueleza hapo juu upo katika kitabu cha Prof. James Giblin kuhusu Maji Maji: ''Lifting the Fog of War,'' (2010).
Kuwa vyanzo vyangu haviaminiki si kweli.
Usijipotezee nafasi ya kujifunza kwa hofu isiyokuwa na sababu.
Ama kuhusu kufeli wanafunzi hawa wamashafelishwa kwa kusomeshwa historia iliyoandikwa kwa ghilba.
Nakuwekea hapo chini picha ya Prof. Giblin ofisini kwake University of Iowa akiwa ameshika kitabu cha Abdul Sykes.
Prof. Giblin ni mwalimu wa African History chuoni hapo.
Huu ni mwaka wa 2011.
PICHA:
1. Prof. James Giblin.
2. Mnara wa kumbukumu wa majemadari 66 wa Maji Maji walionyongwa na Wajerumani hapo penye mnara ndipo lilipo kaburi lao.
3. Kaburi la Abdulrauf Songea Mbano
4. Abdulrauf Songea Mbano