Historia ya TANU siku zote imeandikwa na makosa

Historia ya TANU siku zote imeandikwa na makosa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1680665325455.jpeg

''Mwalimu Nyerere na Historia'' (1980)
Kitabu cha Prof. G.A. Mhina
Kitabu hiki nimekuwancho kwa miaka mingi sana.

Lakini kwa kuwa ni kitabu cha picha nilikisoma mara moja tu katika miaka ya 1980 na kikabakia Maktaba.

Sikukigusa tena.

Jana nimeona picha za TANU katika mtandao na haraka nikatambua kuwa picha hizi nimepata kuziona katika kitabu hicho hapo juu.

Ndipo nilipokitafuta kitabu hiki na kuanza kukipitia.

Kwa hakika nilistarehe sana na picha nilizozikuta ndani ya kitabu hiki ikawa kama vile naziona picha zile kwa mara ya kwanza.

Katika moja ya picha ambayo ilinivutia kwa kosa nililoliona katika maelezo ya picha hiyo ni hiyo hapo chini:
Maelezo ya picha hii ya waasisi wa TANU ni kuwa hao ni waanzilishi wa TAA.
Vipi linaweza kufanyika kosa kama hili?

Picha hii ya Waasisi wa TANU mwaka wa 1954 ni maarufu sana.
Hili mosi.

Pili hapajakuwapo na picha ya waasisi wa African Association iliyoanzishwa mwaka wa 1929.

Ingawa nimabahatika kupata picha mbili za waasisi wa chama hicho - picha ya Kleist Sykes na picha ya Mzee bin Sudi.

Tukirejea kwenye picha hiyo ya Waasisi wa TANU kuna kisa kirefu kuhusu picha hiyo iliyowekwa hapo.

Picha hiyo imechezewa kwa kutiwa mkono.

Katika picha yenyewe ya Waasisi wa TANU Ally Sykes, Tewa Said Tewa na Kasella Bantu hawamo.

Hawa walijitoa kwa kjuwa walikuwa ni watumishi wa serikali na sheria ilikuw ainawakataza kujihusisha na siasa.

Ilipokuwa inapigwa picha wao walikaa pembeni.

Angalia picha halisi hapo chini:

1680668656991.jpeg

Kasella Bantu kapachikwa kati ya Abdul Sykes na Chief Patrick Kunambi.
Kazi hii ilifanywa na Idara ya Picha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Siku zote kila nikiangalia picha hiyo iliyotiwa mkono hujiuliza kama haja ilikuw akuwaweka waasisi wote wa TANU kwa nini hazikuwekwa pia picha za Ally Sykes na Tewa Said Tewa.

Tuendelee kubakia katika hili suala la picha hii ya Waasisi wa TANU.

Katika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere, ''Nyerere Biography,'' kitabu kinaeleza kuwa picha hii ilipigwa na kamera ya Denis Phombeah yeye mwenyewe akiwa mpigaji wa picha hiyo.

Abbas Sykes alikuwapo katika mkutano wa kuasisi TANU lakini hakuwa mjumbe bali kijana mdogo wa kutumwa na kaka yake Abdul Sykes na wajumbe wengine wa mkutano kufanya hiki na kile katika mkutano ule.

Abbas Sykes amenieleza kuwa picha ya Waasisi wa TANU ilipigwa na mpiga picha maarufu Dar es Salaam jina lake Gomez.

Abbas Sykes anaeleza kuwa walimsubiri Gomez ambae studio yake ilikuwa Acacia Avenue kwa muda hakutokea.

Abdul Sykes akamwambia Abbas achukue baiskeli ya TAA amfate wakapishana.

Wakati Abbas Sykes anamfuata Gomez yeye kumbe alikuwa njiani akija New Street kuwapiga picha waasisi wa TANU.
Katika kitabu hiki cha ''Nyerere na Watanzania,'' kuna picha hapo chini ya baiskeli ya kwanza ya TANU.

Bila shaka hii ndiyo baiskeli ya kijana mdogo Abbas Sykes alipanda kumfata mpiga picha Gomez:

1680670609858.jpeg

Baiskeli ya TANU

1680670807126.jpeg

Picha niliyopigwa na Gomez 1956
Mwandishi ni huyo kushoto kulia ni ndugu yangu Kapufi Yunge
Ukiangalia picha hii utaona nimeshika kitabu.

Mama anasema nilikuwa situlii kwenye kiti ndipo Gomez akanipa kitabu nishike.

Studio ya Gomez ilikuwapo hadi miaka ya 1980.
 
Mhina atakuwa wale waliopewa pesa na wakoloni kuharibu history.

Wakoloni waliharibu history kusudi ili waafrika wasije kujaa chuki.

Later on walitumia mawakala wao waliobaki nchini kuharibu history
 
Mambo ya historia ukitaka jamii isimame na wewe basi wafanye wawe na uhakika wa mlo then waambie unayotaka.

Vinginevyo utatwanga maji kwenye kinu, angalia historia ya Zanzibari kuna watu wengi tu hawasemwi kisa hawaendani na mtu kama wewe mtoa mada.


Narudia huwezi kupata historia yenye ukweli 💯% wakati mnaongoza kupotosha kwengine!.
 
Tatizo lako mzee wangu Said Mohamed,ni mrengo ulionao ndio maana unakosoa kila kitu cha watu wenye mrengo tofauti na wewe.Lini utaacha,fitina,gubu,chuki binafsi,udini kwa Nyerere na Tanu yake??????

Huyut mzee ni wa kumpuuza.
Mambo ya historia ukitaka jamii isimame na wewe basi wafanye wawe na uhakika wa mlo then waambie unayotaka.

Vinginevyo utatwanga maji kwenye kinu, angalia historia ya Zanzibari kuna watu wengi tu hawasemwi kisa hawaendani na mtu kama wewe mtoa mada.


Narudia huwezi kupata historia yenye ukweli 💯% wakati mnaongoza kupotosha kwengine!.

Ni wa kumpuuza tu.
 
Mambo ya historia ukitaka jamii isimame na wewe basi wafanye wawe na uhakika wa mlo then waambie unayotaka.

Vinginevyo utatwanga maji kwenye kinu, angalia historia ya Zanzibari kuna watu wengi tu hawasemwi kisa hawaendani na mtu kama wewe mtoa mada.


Narudia huwezi kupata historia yenye ukweli 💯% wakati mnaongoza kupotosha kwengine!.
Today,
Sijatwanga maji kwenye kinu.
Kitabu changu kimepokelewa vyema na vyuo vinavyosomesha historia ya Afrika.

Nimetiwa katika miradi kadhaa ya kuandika historia na nimealikwa kwenye vyuo vingi Afrika, Ulaya na Marekani kuzungumza.

Kubwa ni huku kuinusuru historia ya wazee wangu waliopigania uhuru isipotee.
 
Mzeee said ana uchungu sababu Nyerere na Kawawa walikataa udini kwenye chama cha Tanu.Maana hapo mwanzoni kuna wazee wa kariakoo walikua wanaleta udini na ukabila mpaka wakafukuzwa uanachama miaka hiyo ya 1950,s.
Nelson,
Unazungumzia kitu usichokifahamu.
Hakuna wazee katika TANU waliofukuzwa kwa ukabila na udini.

Ila kuna kisa cha Sheikh Suleiman Takadir aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Sheikh Takadir alifukuzwa TANU kwa kuhoji hali ya baadae ya Waislam katika Tanganyika huru.

Hii ni moja ya historia nyeti sana ya TANU.

Nimekieleza kisa hiki kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
View attachment 2576842
''Mwalimu Nyerere na Historia'' (1980)
Kitabu cha Prof. G.A. Mhina
Kitabu hiki nimekuwancho kwa miaka mingi sana.

Lakini kwa kuwa ni kitabu cha picha nilikisoma mara moja tu katika miaka ya 1980 na kikabakia Maktaba.

Sikukigusa tena.

Jana nimeona picha za TANU katika mtandao na haraka nikatambua kuwa picha hizi nimepata kuziona katika kitabu hicho hapo juu.

Ndipo nilipokitafuta kitabu hiki na kuanza kukipitia.

Kwa hakika nilistarehe sana na picha nilizozikuta ndani ya kitabu hiki ikawa kama vile naziona picha zile kwa mara ya kwanza.

Katika moja ya picha ambayo ilinivutia kwa kosa nililoliona katika maelezo ya picha hiyo ni hiyo hapo chini:

YnFMH19802xo0v_7pBN7Z3bxSNYryNnN2sIOSP8sGuOm1UOEMb-H0fUlQRZXBTX1zaDPUd4QoP9BmWZ-KADGil8GzTGprparZk3EQxmkqrsIaUpgmD-bClldpOqczkGseVD89Rze0VATPwu0TIhBN_xUjngSh5-QVf9iDop2mY_gt6p-pxkHtwh0rMfqIHc-D1WvZwecnaSVM62ZpKkjCRqPMx2nQZZymFtDlWrK8OqPzN-bdFAbQNebbS5_XWdN_EQAurPbUYCb2sZ9-JOi0wrSPAdxDsU54hB00ll9iKdSewrSBrmixYaTVqnxkLagN1OWUoNdEr3lxETctRuqKrIFwWkS2sj2XmgodI85d1Zv_S7w-_N235sWnF93elRT6CM5k8l-nQ0YOQpnWh1DEy9lE54dyiEsSs_xVZfLIbhj2shc4zTiZFSz_3zxDci-yzjvkvQm2OQRc0EX4F8llO4gxKd-RyYnOXr-VaWB8ZuAxGDTqKQlvMm8qZY4hHSvwBJaOZ_4WH-5Zb_ci3CmHGW4KXmFOAKXBykeOvI6sm_aLDxGV-yHNNVE3yd8PvbYCSv7jha-KrXSD6wwYqDpu35hUOYvKXQonxqKQVSvC8Nluy5dSIikAAElkYFD-jfA_fJjq3J640egJov_Er9Mr0MP9A-KGeYBw4iqX6pIb9MSuK5yOH7DIPCAU_7wPPTOouyJiC9Pejg_VUz25EN1rpinpIzSuZKIfq4lNTLyE-thDNzZVGDblw4GeVNGjQczZvaPeMk6lcVuxAqCT12aZR4LQENuQJ3qK5IOiZ0irIlngddeTNWnlwvBwlzmDNYQhgWx4S9qIzyFtVlkjcEnle_7b8oqH9BZ4UuVOpENhAW1kRISp_1t30TWmPwJLIFQjoEKfza4N6mIvL_tfmPSsKMhm04A2AvgHKcEL4sn2KjNFQ=w775-h650-s-no

Maelezo ya picha hii ya waasisi wa TANU ni kuwa hao ni waanzilishi wa TAA.
Vipi linaweza kufanyika kosa kama hili?

Picha hii ya Waasisi wa TANU mwaka wa 1954 ni maarufu sana.
Hili mosi.

Pili hapajakuwapo na picha ya waasisi wa African Association iliyoanzishwa mwaka wa 1929.

Ingawa nimabahatika kupata picha mbili za waasisi wa chama hicho - picha ya Kleist Sykes na picha ya Mzee bin Sudi.

Tukirejea kwenye picha hiyo ya Waasisi wa TANU kuna kisa kirefu kuhusu picha hiyo iliyowekwa hapo.

Picha hiyo imechezewa kwa kutiwa mkono.

Katika picha yenyewe ya Waasisi wa TANU Ally Sykes, Tewa Said Tewa na Kasella Bantu hawamo.

Hawa walijitoa kwa kjuwa walikuwa ni watumishi wa serikali na sheria ilikuw ainawakataza kujihusisha na siasa.

Ilipokuwa inapigwa picha wao walikaa pembeni.

Angalia picha halisi hapo chini:

Kasella Bantu kapachikwa kati ya Abdul Sykes na Chief Patrick Kunambi.
Kazi hii ilifanywa na Idara ya Picha Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Siku zote kila nikiangalia picha hiyo iliyotiwa mkono hujiuliza kama haja ilikuw akuwaweka waasisi wote wa TANU kwa nini hazikuwekwa pia picha za Ally Sykes na Tewa Said Tewa.

Tuendelee kubakia katika hili suala la picha hii ya Waasisi wa TANU.

Katika kitabu cha maisha ya Julius Nyerere, ''Nyerere Biography,'' kitabu kinaeleza kuwa picha hii ilipigwa na kamera ya Denis Phombeah yeye mwenyewe akiwa mpigaji wa picha hiyo.

Abbas Sykes alikuwapo katika mkutano wa kuasisi TANU lakini hakuwa mjumbe bali kijana mdogo wa kutumwa na kaka yake Abdul Sykes na wajumbe wengine wa mkutano kufanya hiki na kile katika mkutano ule.

Abbas Sykes amenieleza kuwa picha ya Waasisi wa TANU ilipigwa na mpiga picha maarufu Dar es Salaam jina lake Gomez.

Abbas Sykes anaeleza kuwa walimsubiri Gomez ambae studio yake ilikuwa Acacia Avenue kwa muda hakutokea.

Abdul Sykes akamwambia Abbas achukue baiskeli ya TAA amfate wakapishana.

Wakati Abbas Sykes anamfuata Gomez yeye kumbe alikuwa njiani akija New Street kuwapiga picha waasisi wa TANU.
Katika kitabu hiki cha ''Nyerere na Watanzania,'' kuna picha hapo chini ya baiskeli ya kwanza ya TANU.

Bila shaka hii ndiyo baiskeli ya kijana mdogo Abbas Sykes alipanda kumfata mpiga picha Gomez:

View attachment 2576879
Baiskeli ya TANU

View attachment 2576880
Picha niliyopigwa na Gomez 1956
Mwandishi ni huyo kushoto kulia ni ndugu yangu Kapufi Yunge
Ukiangalia picha hii utaona nimeshika kitabu.

Mama anasema nilikuwa situlii kwenye kiti ndipo Gomez akanipa kitabu nishike.

Studio ya Gomez ilikuwapo hadi miaka ya 1980.
Je hakuna historia ya bara ya watu wengine kupigania uhuru wa Tanganyika ni dar tu. Hakuna haja ya kuweka dini katika siasa
 
Je hakuna historia ya bara ya watu wengine kupigania uhuru wa Tanganyika ni dar tu. Hakuna haja ya kuweka dini katika siasa
Don,
Kitabu cha Abdul Sykes kina historia yote ya wazalendo waliohusika na siasa za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mwanzo tu wa kitabu katika utangulizi nimeweka kwa muhtasari wazalendo niliokutananao katika Nyaraka za Sykes ambao hawamo katika historia ya TANU.

Ndani ya kitabu nimeeleza historia ya Ali Migeyo wa Kamachumu, Salum Mpunga, Sharifa bint Mzee na Yusuf Chembera wa Lindi, Bilal Waikela, Zarula bint Abdulrahman, Nyange bint Chande wa Tabora, Yusuf Olotu, Mama bint Mwalimu, Amin Kinabo, Halima Selengia, Lucy Lameck wa Moshi, Haruna Iddi Taratibu na Yusuf Suleiman wa Dodoma.

Uislam huwezi kuukwepa katika historia ya uhuru wa Tanganyika kama vile huwezi kukwepa kutaja Wakikuyu katika kupigania uhuru wa Kenya.
 
Nelson,
Unazungumzia kitu usichokifahamu.
Hakuna wazee katika TANU waliofukuzwa kwa ukabila na udini.

Ila kuna kisa cha Sheikh Suleiman Takadir aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Sheikh Takadir alifukuzwa TANU kwa kuhoji hali ya baadae ya Waislam katika Tanganyika huru.

Hii ni moja ya historia nyeti sana ya TANU.

Nimekieleza kisa hiki kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Ngoja nipekue pekue makabrasha nikuletee tukio kamila la wazee waliofukuzwa tanu kwa kuendekeza ubaguzi wa kidini
 
Back
Top Bottom