Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa


Hizi sasa ni bange, umekula ndugu yangu?????
 

Nyie hivi mnaona kuwa Mag3 anasimulia? Mbona hamumuulizi yeye simulizi zake na matusi juu, ni kama nani? "Credibility issue", mtu ambae anaficha hata jina lake, wasifa na wadhifa wake mnamuamini kuliko aliyejitambulisha yeye nani na anafanya nini?
 
If your ideas represents the thoughts of the so called "wazee wako''this land would have ended up an islamic state if their religious ideas were left untreated.Tanganyika/Tanzania would never be one and united.Sudan is a good example.
 
Nyie hivi mnaona kuwa Mag3 anasimulia? Mbona hamumuulizi yeye simulizi zake na matusi juu, ni kama nani? "Credibility issue", mtu ambae anaficha hata jina lake, wasifa na wadhifa wake mnamuamini kuliko aliyejitambulisha yeye nani na anafanya nini?

Faiza,

Mag3 ameshalitolea maelezo swali lako la kutaka ajitambulishe kwa majina yake halisi kama alivyofanya sheikh mohamed. Na hata wewe umeulizwa swali hilo hilo na ukalitolea maelezo. Kwa jinsi ulivyojieleza na jinsi mag3 alivyojieleza, maelezo yenu yamefanana, kwani hata wewe hatujakufahamu kikamilifu, kwani si wote tunaoishi kariakoo hadi tujue kwamba faizafoxy ndiye faiza omary ama vinginevyo!

Kwa mujibu wa taratibu za JF, kila mmoja yuko huru kujiandikisha kwa jina analolitaka. Na hapa tumekuwa tukijadili mambo mengi sana bila kutaka kufahamu majina halisi ya wachangiaji, tunachoangalia hapa ni source na credibility ya habari husika. Hakuna ushahidi wa wazi hapa JF kwamba wanaotumia majina yasiyohalisi (nicknames) kwamba si credible ama reliable source. Wala hakuna ushahidi wa wazi kwamba wanaotumia majina yao halisi ndio pekee wanakuwa credible ama reliable source.

Suala la cheo na kazi ya mwanaJF yeyote si lazima aviseme hapa, ni hiari yake kama akiamua kujitambulisha ama kutojitambuylisha hiyo si hoja ya msingi ya kujadili hapa. Kama unadhani hiyo ni hoja ya msingi, hapa si mahali pake, unaweza kuifungulia thread na utapata majibu yake. Ni vizuri ukafahamu kuwa si suala la kumuamini huyu na kutomuamini yule. Tunachotafuta hapa ni "facts" kutoka kwenye masimulizi yao. Mambo yanayosemwa hapa si kwamba yote ni mageni masikioni mwetu bali kuna baadhi ni mageni na ndiyo hayo tunayotaka yajisimamie kwa ushahidi madhgubuti ili tuweze kuyaamini na kuyapokea.
 

At least mimi umenijuwa natoka Kariakoo, na naitwa Faiza na nyumbani kwetu ni wapi, Jee Mag3 ameeleza hayo au kasema hizo Mag ni herufi za majina yangu matatu? Unanchekesha, anyway, tuachane na haya turudi kwenye mada, nimejifunza jambo moja zuri kutoka hapa: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...anchi-miaka-50-ya-uhuru-wa-tanganyika-43.html


Mwita Maranya, naona tunatoka nje ya mjadala na mada husika na sidhani kama hii inakusaidia wewe au mimi kuijuwa Tanzania imetoka wapi, iko wapi na inakwenda wapi. Naomba sana tuache kujadili yetu binafsi na turudi kwenye mada, mimi nakupa ushindi kwa yote, wewe ni hodari sana na unastahili kila sifa, hongera sana, sasa turudi kwenye mada.
 

Faiza,

Hapo nyekundu umesema jambo la maana sana ambalo ndilo lilitakiwa kuwa lengo letu.

Sihitaji unipe ushindi kwakuwa mimi sishindani na wewe hapa, nilichofanya ni kujaribu ku balance hii story kutokjana na baadhi ya allegation zako.

Vinginevyo nakubaliana na wewe kabisa kwamba tujikite kwenye mnakasha husika. Sheikh Mohamed bado ana mengi ya kusimulia na kwa upande mwingine Mag3 anayo mengi ya kubalance simulizi za sheikh mohamed. Sisi wengine hapa tunafaidika sana na huu mnakasha kwakuwa hii ni moja kati ya mijadala michache sana na adhimu sana kwa mustakabali wa historia ya nchi hii. Kama huu mnakasha ungekuwa hauna manufaa ama kitisho chochote kwa ustawi na maelewano ya watanzania tusingekuwa hapa hadi muda huu, pengine mjadala ungekuwa ushakwisha muda mrefu.
 


Nguruvi3,

"Sivalon amefichua kuwa Kanisa limeweza kujenga himayayake ambayo inahodhi 75% za viti katika Bunge la Tanzania.Kati ya viti hivyo 70% vipo mikononi mwa Wakatoliki na vilivyobakivimegawika kati ya Waislam na Wakristo wa madhehebu nyingine."

Hebu fananisha ingekuwaje kama Waislam wangehodhi 75% na Wakristo 25% mngeliweza kustahamili?

Hii ndiyo dhulma tuipigiayo kelele na tumezunguka nchi nzima kuwaeleza Waislam kuwa wakati wa kuondoa hii dhulma umefika.

Vyombo vya habari chini ya mfumokristo umetupiga "blackout."

Mohamed
 

Brother MS,

Hiyo nukuu/argument hapo juu.....its too low and weak ku-rely upon...........unless useme na uthibitishe kuwa watu walikuwa wakilazimishwa kuchaguwa wakristo........
Ukiangalia Jiografia ya Tanzania tu unaweza pia kupata jibu kwa huyo mwandishi wako uliyemnukuu............
 
Let us assume kuwa 'nidhulma kama unavyodai', solution gani unapendekeza ili kuondoa
 
OPPORTUNITY COST ya hii kitu ni ELIMU ambayo wanafilosopia wanasema ni ufunguo wa maisha
 
OPPORTUNITY COST ya hii kitu ni ELIMU ambayo wanafilosopia wanasema ni ufunguo wa maisha

Huu ni mchezo kama mchezo mwingine ambao watu wengi tunaotoka pwani tunacheza baada ya kazi.

Hii ni sawa na Sehemu nyingi za tanganyika ukiondoa mikoa ya pwani watu wengi baada ya kazi wanajiburudisha katika vilabu vya pombe.

Na kama umezunguka vizuri Tanganyika , utaona watoto wengi sana wanatumika kuchunga ng'ombe na mbuzi na kondoo. jambo ambalo Pwani hakuna zaidi ya kuvua samaki.
 

Nafikiri ndugu yangu kama utabahatika kukisoma hichi kitabu cha Padre Silvalon cha" Kanisa katoliki na siasa za Tanzania Bara 1953-1985 " kimefumbua mengi sana na utaona nini kanisa kimefanya kwenye siasa zenu huko Tanzania.

naomba ukisome (mimi nilikinunua huko Dar es salaam pale kanisa la St Joseph kwenye bookshop yao Cathedral ipo karibu na Tume ya kudumu ya uchunguzi au Snow cream.

nakushauri ukitafute na kukisoma
 
Let us assume kuwa 'nidhulma kama unavyodai', solution gani unapendekeza ili kuondoa

Nguruvu3,

Si wewe wa kutuuliza sisi Waislam swali hilo. Sisi hatukutuhumu wewe kwa lolote. Mimi hapa jamvini nimejitahidi kueleza hali ya mambo ilivyo nchini kwetu kwa kutegemea kuwa wengi watakapolijua hili tatizo ndiyo nji ya kwanza ya kutafuta suluhisho.

Wengi kama nawe unavyoona hawaamini kuwa lipo tatizo na sasa kuna "shift" kwenye graphics, bao, mkole nk. Hii ni dalili kuwa kazi tuliyonayo Waislam mbele yetu kwa kuwapata ndugu zetu kwa njia ya ustaarabu bado ngumu.

Ama kwa Waislam wenyewe kote tulipopita mikoani mafanikii ni makubwa pasi kiasi. Neno "mfumokristo" linafahamika vyema kabisa. Na katika kutatua hili tatizo wamekuja na na kauli mbiu "kushugulika" wengine huongeza "kushughulika vizuuuri." Hizo "u" za kuvuta sijajua maana yake.

Nchi yetu ina vyombo vya usalama naamini taarifa zishakwenda kwa wahusika na bila shaka wametoa nini kifanyike kuondoa hili janga linalonyemelea taifa letu.

Waislam ni watu wa subira.
Tunasubiri.

Sasa namaliza kwa kusema wewe huoni tatizo sasa kama hakuna tatizo hata nikikupa mapendekezo ya kuondoa tatizo itasaidia nini ndugu yangu?

Mohamed
 
Barubaru naongeza rejea nyingine na maelezo kidogo kwa faida ya wanaukumbi:

"Hivi sasa kuna vitabu viwilivilivyoandikwa na Wakristo wenyewe vinavyothibitisha kuwa Wakristo wametumianyadhifa zao katika serikali kuuhujumu Uislam na Waislam. Jan P van Bergenkatika kitabu chake, Development and Religion in Tanzania,(1981) [1]ametoboa siri kuhusu uadui aliokuwa nao Rais Mstaafu, Nyerere dhidi ya Uislamna Waislam. Kitabu kinaeleza kwa ufasaha jinsi Nyerere wakati alipokuwamadarakani alivyokuwa akifanya mikutano ya siri na viongozi wa Kanisa kuwekamikakati ya kuupa nguvu Ukristo. Katika mikutano hiyo Nyerere aliwahakikishiaviongozi wa Kanisa kuwa anaaunga mkono Ukristo. Kitabu hicho kinaeleza jinsiNyerere alivyotimiza ahadi yake hiyo kwa Kanisa kwa kuhakikisha kuwa anawapaWakristo nafasi za juu katika serikali na chama. Kitabu hiki kilikuwa kinauzwaCatholic Bookshop, Dar es Salaam. Lakini ilipokuja kudhihirikia Kanisa kuwakitabu hiki kilikuwa kinatoa habari nyeti na siri za Kanisa kuhusu njama dhidiya Waislam, kwa haraka sana kikaacha kuuzwa. [1] Hadi hivi sasa kitabuhicho ni marufuku kuletwa tena Tanzania.
Kitabu cha pili nicha Dr John C. Sivalon, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi1985 (1992). [1]Kitabu hiki kinaeleza njama ndani ya serikali kuuhujumu Uislam. Sivalonanafichua kuwa kuanzia mwaka 1961 baada ya Tanganyika kupata uhuru, Kanisalilikuwa na hofu mbili. Hofu ya kwanza ilikuwa umoja wa madhehebu za Kiislamkati ya Sunni, Bohora, Ismailia na Ithnasheri. Hofu ya pili ilikuwa kuhamishwakwa makao makuu ya EAMWS kutoka Mombasa kuja Dar es Salaam. Kanisa lilikuwalinahofu kuwa mali walizokuwanazo Waasia Waislam zikitiwa katika harakati za Waislamambao walikuwa na nguvu kubwa katika uwanja wa siasa zitaathiri maslahi ya Ukristo katika Afrika yaMashariki. Kwa ajili hii Kanisa likatanganza kuwa Uislam ni adui wake naikaanza mikakati ya hujma dhidi ya Uislam ili kuudhoofisha."

Mohamed
 
initiation ceremonies put a brake on developments and at worst r degrading

Hii ndi imekuwa siraha yenu mnaposhindwa na hoja.
Waisilam wa zamani walio kuwa wanaambiwa na Nyerere "nitabadirisha pwani kuwa bara ,na bara pwani"(kwenye ujenzi wa ofisi mpya ya Tanu pale Lumumba,walipogoma kuvunjwa msikiti wa Manyema) na wao wanachekelea sio wale wa wale leo.
 

Mzee Mohamed,

Kimsingi naweza kukubaliana na wewe kwamba inawezekana kweli huo mgawanyo wa viti vya bunge ndivyo ulivyo.

Lakini jambo linalonitatiza ni kwamba, kwa kuwa wabvunge wetu wanapatikana kwa njia ya sanduku la kura, inakuwaje wakatoliki wahodhi 70% ya viti vya bunge?? Hii ni kusema population ya wakatoliki ni kubwa kiasi hicho? mbona kuna mahali nimesoma katika mnakasha huu kwamba population ya waislamu ni 70% ya watanzania.

Ningependa kufahamu wakatoliki wanawezaje kuhodhi 70% ya viti vya bunge, kwani hata maeneo yenye wakatoliki wengi kuna wabunge wasio wakatoliki. Mustafa Akunaay mathalani ni muislamu lakini ni mbunge wa mbulu ambako wakazi wengi ni wakatoliki. Inawezekana likawa swali jepesi ama la kuchekesha lakini lengo langu unifungue macho kwamba wakatoliki wanawezaje kuhodhi kiasi kikubwa cha viti vya bunge?? Mbinu gani wanaitumia kuendesha Dhulma hii?
 
Let us assume kuwa 'nidhulma kama unavyodai', solution gani unapendekeza ili kuondoa
Hawezi kuwa na jibu hata kidogo kwa sababu hajui yeye anataka nini isipokuwa kitu gani kiondoke. Yaani kwa madai yao mfumo Kristu uondoke na hawana cha ku replace kwa sababu kwa kila utakachokiweka ni mfumo kristu kwao, as a matter of fact hata demokrasia ni mfumo kristu.

Binafsi nisichokipenda kutoka kwa hawa jamaa zetu ni pale wanapoitumia dini kueneza siasa zao, nimeshamwambia Mohammed Said, Islaam ni dini inayosimama peke yake na kwa wanadamu wote, tunachogombea sote ni UTU wetu ambao uko well defined ktk kuran na mtu yeyote anatakiwa kupigania haki hizo kama binadamu. Lakini haiwezekani mtu ukapigania haki zako wewe kwa sababu ya jina lako la dini ama imani yako isipokuwa pale dini inapokatazwa...

Mfano mzuri wa Islaam ni kama demokrasia..Leo hii dunia nzima vita vinatokea kwa sababu ya kukosekana kwa demokrasia, hivyo wananchi wataidai demokrasia ilokosekana ili kurekebisha mapungufu yoyote yaliyopo ya kiutawala na sii kutazama makundi ya watu kujaribu kupendelea kundi moja ama kudhoofisha kundi jingine ili kufikia usawa wa kiutawala. Sijui kama nimeeleweka!

Wanachokiomba kina Mohammed Said, ni Udini yaani ktk siasa za kibaguzi ni kama vile kabila fulani linabaguliwa, hivyo ili nao wapate kutesa kwa zamu kama wenzao, wanataka wampate kiongozi ama viongozi wao ambao watawawezasha kubadilisha upepo wa kimfumo kutoka kabila moja kwenda lao, kama Kenya walivyokuwa wakidai Wajaluo miaka ya Kenyatta.

Kwa sura hii, Wajaluo hawakutaka hujenga Demokrasia isipokuwa ni ktk mfumo ule ule wa ukabila, yaani Wajaluo nao wanataka kushika nchi ili wawakandamize Wakikuyu wakati wao wakipanda kimaisha ili kufikia usawa...Na wala sii swala la kuwatazama wao kama wanaokandamizwa ili wawezeshwe, hapana wanachokitafuta ni kuanguka kwa Mkikuyu..Na huyo mkikuyu hawezi kukubali akielewa kwamba utawala ukiwa chini ya Mjaluo yeye ndiye atakuwa muathirika...Kinacholkiliwa hapa ni ule mfumo wa kupokezana yaani na sisi sasa ni ZAMU YETU.

Kwa hiyo, kwa mtu mwenye upeo mkubwa ataelewa kwamba kinacholiliwa hapa na waislaam njaa hawa ni kwamba ilikuwa zamu yao, pengine wakati wa Uhuru au kabla ya Uhuru na Nyerere akawanyang'anya tonge mdomoni. Na kila napowasoma Waislaam wenye siasa kali it's all about when is our turn?.. hakuna anayelilia demokrasia iliyopotea na wala hawataki kujihusisha na siasa kuhakikisha Ukabila au Udini ndio unapigwa vita na sii apendelewe nani na kwa zamu zipi..

Hili ni tatizo ambalo tunalo sii tu kwa dini zetu bali lipo hata ktk Muungano wetu na Zanzibar. Watu wanatazama hizi kutesa kwa zamu na ndio maana wanahesabu Wazanzibar wangapi, waislaam wangapi, wachagga wangapi yote haya ni matokeo ya imani mbovu za kibaguzi kinyume cha Uislaam au niseme demokrasia. Na ndio maana Maalim Seif Hamad, Bilal, Nahoda, Shamhuna wote hawa baada ya kupewa nafasi ya kutesa mashambulizi hakuna tena.. It's all about them ktk kutesa kwa zamu!

Hizi ndizo siasa za Waislaam wa Tanzania ambao wanataka sana kuitumia dini vibaya wakati wao wenyewe wanashindwa kuona kwamba demokrasia imepotea nchini na viongozi wao wa kiislaam ndio vipaza sauti na wanafiki wakubwa ktk uchochezi. Mwinyi ndiye aliyefungua mahusiano ya kitafa na Israel, Mwinyi ndiye aliua Balukta na kuwafunga ama kuua viongozi wake, Mwinyi ndiye aliyeweka mkataba wa MoU na misamaha ya kodi, Mwinyi ndiye aliyeruhusu Ma Casino na kadhalika lakini pembeni hudai ati kuna mfumo kristu wakati yeye ndiye mjenzi wa mfumo huo huo, lakini waulize watakwambia hakuna rais kama Mwinyi.

Mkuu hawa waislaam njaa ndio wanaifanya kazi yetu sisi tunaotoa Dawa iwe ngumu zaidi. Na kibaya zaidi wameingia hata ktk kazi zetu kiasi kwamba Uislaam leo unaonekana kama ni Ugaidi, ni imani inayotawaliwa na Udini kwa sababu wanashindwa kupigania haki zao hapo walipo isipokuwa kwa kutumia jina la dini ili wapate wanachama wengi wakipitia jina la dini..Lakini pamoja na yote haya, Islaam italindwa na Mwenyezi Mungu pale Waislaam wenyewe wameshindwa kuilinda...
 

Kwa hiyo mkuu wewe unataka mfumo kristo uendelee kwakuwa hakuna mfumo wa ku-replace

Kwa hiyo wewe unasema hela za serikali (umma) zipelekwa kanisani through MoU kwakuwa hatuna namna ya ku-replace

Kwa hiyo mkuu UTU kwako ni waislamu kubaguliwa kwasababu ya dini yao ...lakini wakidai haki iwe usaliti

Nilifkiri ulisema wewe ni Muislam ..na unasema waislam wameshindwa wewe umefanya nini kuu-linda uislamu?

Nini maana ya uislam?
 
Let us assume kuwa 'nidhulma kama unavyodai', solution gani unapendekeza ili kuondoa

Mzee Nguruvi3

Niendelee kukiri kama mnakasha huu umetupa elimu kubwa mno... hii ni nadra kuipata darsani.

Ila nadhani kuna matatizo ya msingi katika nchi hii ambayo ufumbuzi wake pekee ni mijadala ya wazi. Tutake tusitake, kuna matatizo mazito yanayohusishwa na kubaguliwa kwa waislamu. Haya kwa umri wangu mdogo nilianza kuyasikia tangu enzi za iliyokuwa '' Warsha ya Waandishi wa Kiislamu'' ikiongozwa na almarhuum Sheikh Mdidi. Baadae nikaja kuendelea kuyasoma kwenye Annuur zaidi ya miaka 20 kama Mzee Nguruvi3 anavyokiri.

Tahadhari iliyotolewa hapo juu si ya kupuuzwa. Kama yasemwayo si sahihi au ni uzushi...njia pekee ya kung'amua ukweli wake ni kijadala ya wazi. Sasa ukiona kuna kundi moja la watu linakataa hata kujadiliana juu ya kadhia hii ujue imma linaogopa juu ya kinachosemwa kuwa kitajulikana. Nakumbuka kusoma kwenye Mwebechai Killing cha Prof Njozi..akimnukuu Mzee Bori Lila jinsi ya Pannel ile ya kufanya selection ya vijana wa form five ilivyo kata majina ya vijana wa Kiislam wenye sifa. Mzee huyu mpaka amefariki hakuwahi kuhojiwa na watu wa upande mwingine iliijulikane kuwa tuhuma zake ni sahihi au si sahihi.

Mzee Nguruzvi3... hali hii tusiipuuze hata kidogo, tension ni kubwa mno na makongamano yameongezeka hatujui next step itakuwa ni ipi. Leo JK anasemwa vibaya baada ya kuthubutu kusema kama uchaguzi wa 2010 ulitawaliwa na udini. Huyu ni kiongozi wa kwanza kuthubutu kukiri kama kuna udini katika nchi yetu. Wa kwanza kabisa katika kueleza inequalities katika elimu alikuwa ni Nyerere mara tu baada ya uhuru. Akiwaeleza Waisalmu kuwa anafahamu gap lililokuwepo katiya ya waislamu na wakristo katika elimu na akawaahidi kuwa baada ya Tanzania huru hii imbalance atajitahidi kuiondosha..nadhani ndio ile moove ya kutaifisha mashule ya dini ilipoanza.

Niungane na mtoa hoja ya maridhiano katika kutafuta sulhu ya hali hii tuliyonayo. Ni mkariri mchangiaji mmoja humu ndani juu ya kauli mbiu yake ya '' Mficha Maradhi Kifo humuumbua''. Tanzania tunalo tatizo la jamii moja kuhisi kama linakandamizwa,limiachwa nyuma na linakuwa regarded kama kundi la daraja la pili. Ni mijadala ya wazi pekee ndio itayotoa taswira ya kadhia hizi.

Sheikh Yahya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…