Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Hotuba inasemekana haionekani sehemu yoyote kwa mujibu wa Mzee Said.
Huko kwenye archieve kumebaki ile picha Nyerere akiwa na soksi ndeefu hadi magotini.
Tulishaambiwa kuwa Sykes alitunza nyaraka zake vema sana na ameziona, sijui hakuona draft ya hotuba ya UN!

Wanasayansi wa siasa wanasema, siasa ni kitu 'fuid' kwamba kubadilika kwake ni suala la dakika na sio siku. Kuanzia mwaka 1950 hadi Nyerere alipokwenda UN kulikuwa na mabadiliko makubwa sana. Sina uhakika hiyo hotuba iliyokuwa katika mfumo wa siasa ilishindwaje kubadilika(stagnant) hadi isome vile vile.

Alipofika Dar alikuwa na MA, na alishakuwa na exposure tayari katika masula ya kimataifa.
Mwaka 1950 Nyerere alikuwa hajajulikana sana katika medani ya siasa.
Kama hotuba iliandikwa mwaka 1950, je ilikusudiwa ikasomwe lini na nani ndani ya UN?

Nguruvi3,

Ndugu yangu unaleta hoja nzuri ambazo mimi zinanisisimua tatizo unachukuliwa na hamaki kidogo.

Hii habari ya archive na soksi ndefu ya nini kaka inachafua murua wako isingelikuwa hapo.

Ngoja nikutoa shaka katika hilo la soksi ndefu.

Katika moja ya uzi wangu nilipoona hili suala kaptula linapewa uzito usiostahili nilisema mimi baba yangu akivaa kaptula na stockings akenda kazini. Abdulwahid Sykes akivaa kaptula na stockings akiwa Market Master pale Kariakoo na watu walomuona katika kivazi hicho wu hai. John Iliffe katika "A Modern Histrory of Tanganyika" ameielezea ile picha ya waasisi wa TANU na yeye kenda mbali zaidi kwa kusema kuna tofauti ya mavazi kati ya waasisi waliotoka kwenye majimbo (provinces) na akina Abdulwahid.

Nakuomba sana ndugu yangu tuliache hili la nguo kwa hakika halina tija. Tuzungumze yale yatakayotuongezea ufahamu zaidi wa historia ya nchi yetu.

Nakuomba soma Cranford Pratt, "A Critical Phase in Tanganyika" ameeleza kirefu kuhusu memorandum iliyoandikwa 1950 na TAA Political Sub Comitteee ambayo ilipelekwa kwa Gavana Edward Twinning. Hotuba iliyosomwa Umoja wa Mataifa 1955 imenyambuliwa mle ndani.

Humu ndani nimeeleza kwa kirefu kuhusu jambo hili lakini kama hamuamini wala isiwe tabu hotuba hiyo ni moja tu katika mengi katika historia ya Tanganyika ambayo niko tayari wakati wowote kueleza kwa ajili ya faida ya wanaukumbi.

Kuhusu Nyaraka za Sykes wala usifanye maskhara. Uzione kwa jicho lako ndiyo utaamini. Illife alizitumia hizo kupitia bint yake Abdu, Daisy Sykes kuandika historia ya African Association katika miaka ya katikati ya 1960 wakati Daisy alipokuwa mwanafunzi wake Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Naweka hapa "observations" zangu kuhusu hizi nyaraka kwa faida ya wanaukumbi:

...aliniruhusunisome majalada yake binafsi, barua zake, shajara na kumbukumbu nyinginezo zaukoo wa Sykes. Ally Sykes alinifahamisha kuwa kumbukumbu hizi zilikuwa ndani yasefu ambayo haikupatwa kufunguliwa kwa zaidi ya miaka therathini. Nikiyapitiamajalada yake nilishangazwa na utaratibu wa Ally Sykes wa kupanga kila kitu nakila kipande cha habari mahali pake hata kingekuwa kidogo namna gani wakati ulewa harakati. Ally Sykes ana barua ya mwaka 1954 iliyoandikwa kwa penseli tokakwa Zuberi Mtemvu kwenda kwake akimtaarifu juu ya mazungumzo aliyokuwanayo(Mtemvu) na Nyerere kuhusu yeye na TANU; stakabadhi ya hundi ya posta toka kwaAlly Sykes kwenda kwa Japhet Kirilo wakati wa Mgogoro wa Ardhi ya Wameru;nakala ya barua isiyokuwa na tarehe kutoka TAA kwenda kwa Malkia Elizabethiliyotiwa saini na viongozi wote wa TAA: Rais Julius Nyerere, Makamu wa RaisAbdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi, Naibu Katibu Dossa Aziz, MwekaHazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes ikimpongeza Malkia kwakutawazwa; barua ya mwaka 1952 toka kwa Rashid Mfaume Kawawa kutoka Bukobakwenda kwa Ally Sykes ikimfahamisha juu ya hali ya siasa katika Kanda ya Ziwa;barua ya mwaka 1963 toka kwa Lady Judith Listowel, Kenneth Kaunda, Julius Nyerere,Kasela Bantu, Chifu Thomas Marealle ...orodha haina mwisho. Baadaye nilipofanyautafiti kuhusu maisha ya baba yake, Kleist Sykes, nilikuja kufahamu kwambatabia hii ilirithiwa kutoka kwa baba yake ambae alikuwa akiweka ndani ya jaladakila kipande cha karatasi kilichokuwa na habari iliyostahili kukumbukwa. Nijambo la kuhuzunisha kwamba sikuweza kupewa shajara za Abdulwahid ambazonilielezwa kwamba baadhi ziko katika hati-mkato na hadi leo hazijafasiriwa.Shajara hizi nimezioana kwa macho yangu lakini kwa kukosa idhini sikuwezakuzifungua na kuzisoma. Vilevile vilevile sikuweza kupata kumbukumbu halisi zaVita Kuu ya Kwanza zilizoandikwa na Kleist Sykes kwa mkono wake mwenyewe.Hapana shaka yoyote kwamba nyaraka hizi ni hazina zenye thamani isiyo na mfanowake. Ni matumaini yangu kwamba siku moja nchi yetu itakubali na kuthaminimchango wa Abdulwahid katika taifa la Tanzania na nyaraka hizi kama kielelezocha harakati dhidi ya ukoloni, zitakubalika na zitawekwa chini ya hifadhi yaNyaraka za Taifa kwa faida ya vizazi vijavyo."Waungwana hawabanani.

Mohamed
 
Mkandara, pamoja na heshima yote kwangu kwa mzee Said hili la yeye kutumia mamlaka ya watu wasioweza kuulizika (aidha wamekufa au hawataji kwa majina au hajawauliza walio hai) linasumbua sana. kwa mfano Mkapa ni mmoja wa watu waliokuwepo tena ni kijana wakati haya mengi yanatokea na alikuwa ni Mhariri. Lakini sioni hata mara moja Bw. Said akisema kaenda kumuuliza! Mama Maria hataki kumuuliza - kwa kuogopa kumfedhehesha japo anadai mama huyo "anajua yote"; Wakati anaandika kitabu ilimchukua karibu miaka mitano kufanya utafiti wake hadi kuchapa mwaka 1998 - muda wote huo Nyerere alikuwa hai hajawahi kumuuliza badala yake anatusimulia kuwa ni Prof. Othman ambaye alienda kwa Nyerere - na Prof. Othman hayupo - hatuwezi kumuuliza!

Go figure..

Mkapa alikuwepo wakati AA na TAA zina asisiwa? hivi mkapa anaweza kuwa na habari za Abdul Wahid Sykes na ujio wa Nyerere Dar. zaidi ya Ali Sykes? Hivi huyu Mkapa wakati TANU inaanzishwa alikuwa na la kuongelea? Jamani, pumba zingine taratibuni.
 
Mkapa alikuwepo wakati AA na TAA zina asisiwa? hivi mkapa anaweza kuwa na habari za Abdul Wahid Sykes na ujio wa Nyerere Dar. zaidi ya Ali Sykes? Hivi huyu Mkapa wakati TANU inaanzishwa alikuwa na la kuongelea? Jamani, pumba zingine taratibuni.

Someone wrote this before hiyo comment ya Mkjj

Mwanakijiji,

Tutakwenda awamu baada ya awamu tuanze na hii:
"Ili tume ya uchunguzi ya Waislam iwezekufanya kazi yake vyema na bila upendeleo, ilikuwa lazima ile tume ya Waislamiiombe serikali izuie propaganda iliyokuwa ikiendeshwa na wale waliokuwawamejitenga na EAMWS, wakitumia jukwa la radio ya serikali na magazeti ya TANU.Tume ya Waislam ilikutana na Waziri wa Habari na Utangazaji, Hasnu Makame,ofisini kwake tarehe 20 Novemba, 1968, kujadili tatizo lile. [1]Hii haukusaidia kitu. Propaganda dhidi ya uongozi wa EAMWS iliendelea kwa nguvuzote. Mashambulizi kutoka pande tatu yaliyopangwa vyema yalikuwa kazini. BenjaminiMkapa akitumia gazeti la Nationalist ataandika habari yoyote ya Adam Nasibu,Martin Kiama akitumia Radio Tanzania atatumia habari ile kama habari muhimukatika radio na habari hiyo itatangazwa kutwa nzima huku ofisi ya rais ikiwakimya kwa fitna ile. Lile kundi la waliojitenga na umma wa Waislam Adam Nasibuakiwa kama msemaji wao mkuu wakawa wakati mwingine kwa mastaajabu makubwawakawa wanakiuka hata misingi ya akida ya Tanzania, wakitoa madai ya ubaguzi arangi, wakikazania lazima EAMWS ivunjwe. Adam Nasibu alinukuliwa na TheNationalist akisema kuwa: "Waislam lazima wafahamishwe kwa nini EastAfrican Muslim Welfare Society iwe na katiba ambayo inaendana na mwelekeo wanchi. Hatujui nafasi ya Aga Khan katika nchi yetu na ndiyo maana tunamkataa." [1]
Lakini cha kushangaza zaidi ilikuwa uleukimya wa serikali kuhusu matakwa ya kundi la Adam Nasibu lililokuwa likidaikuwa Waislam wachanganye dini na siasa katika suala hili, wakati ilikuwaikijulikana wazi kuwa kufanya hivyo ni mwiko mkubwa katika siasa za Tanzania. Haya yote mbali, lile la kushangaza hasa nakitu ambacho kilikuwa kigeni katika Tanzania ilikuwa yale madai ya kuingizaubaguzi wa rangi katika siasa za Tanzania. Ilikuwa inastaajabisha kuonamagazeti ya TANU yaliyokuwa na sifa ya kuheshima haki za binadamu yakichapishana kuzipa uzito wa hali ya juu habari za kundi dogo la Waislam waliokuwawanawalaumu Waislam wenzao wa Kiismailia kwa kutozaliwa weusi. Miaka kumiiliyopita watu wa Tanganyika, Waislam wenyewe waliokuwa ndiyo walioanzisha nakuijenga TANU, walipambana vikali dhidi ya siasa za kibaguzi za Zuberi Mtemvuna chama chake cha African National Congress. Mtemvu alishindwa na matokeo yakeikawa Tanganyika kuwa na serikali ya watu wote isiyobagua rangi na ikitawalaraia wa rangi zote kwa misingi ya haki. Kwa ajili hii nchi ikawa haina msuguanokwa ajili ya ubaguzi wa rangi. Haya matokeo mapya yalikuwa hayaendani namisingi ya TANU.
Ilipofikia hali hii, rais wa EAMWS, TewaSaid Tewa na makamo wake Bibi Titi Mohamed, waliamua kulipeleka suala hili kwaJuluis Nyerere, Rais wa Tanzania na mwenyekiti wa TANU, chama tawala. chanzocha uadui huu inatulazimu turudi nyuma hadi mwaka wa 1963, katika siku zamwanzo za uhuru, katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU [1]uliofanyika Ukumbi wa Karimjee.
Kama ilivyokwishaelezwa hapo mwanzonikuwa mwaka 1963 ulikuwa mwaka wa mambo mazito. Ilikuwa ndiyo mwaka ambao KanisaKatoliki liliteua wagombea wake wapambane na wagombea wa TANU waliokuwa Waislamkatika uchaguzi wa serikali za mitaa kule Kigoma na Bukoba. Ulikuwa ndiyo mwakaambao Rais wa TANU, Nyerere alipombana na EAMWS kupitia Bilali Rehani Waikela.Mwaka Watu hawa walikuwa wakichekeana jino pembe. Lakini ili tuelewa mwaka wa 1963 ndiyo ulikuwa mwaka ambaoHalmashauri Kuu ya TANU ilivunja Baraza la Wazee wa TANU lililokuwalimetawaliwa na Waislam kwa madai kuwa baraza hilo lilikuwa ëlikichanganya dinina siasaí. Mwaka 1963 ulikuwa mwaka muhimu kwa Halmashauri Kuu ya TANU kwasababu ilikuwa mwaka ambao ilifanya maamuzi nyeti ya kidini. Mwaka ule BibiTiti na Nyerere walishambuliana kwa maneno ndani ya Halmashauri Kuu yA TANUkuhusu jambo jingine tena la dini lililokuwa likihusu EAMWS.
Wanakamati wawili wa Halmashauri Kuu yaTANU, Selemani Kitundu na Rajab Diwani, waliiomba Halmashauri Kuu ya TANUimjadili Aga Khan na nafasi yake kama patroni wa EAMWS. Kitundu na Diwaniwalidai kuwa wana habari Aga Khan anataka kuitawala Tanganyika kupitia Waislamna EAMWS. Kwa ajili hii basi wakapendekeza EAMWS ifungiwe. Nyerere aliwaungamkono Selemani Kitundu na Rajab Diwani. Bibi Titi akasimama kishujaa dhidi yaDiwani, Kitundu na Nyerere, akasema hakuna kati yao aliyekuwa na haki yakuifungia jumiaya yoyote ya Waislam. Kama walikuwepo watu ndani ya EAMWS ambaowalikuwa wanakwenda kinyume na sheria basi watu hao wapelekwe mahakamani nasheria ichukue mkondo wake. Bibi Titi akaendelea na kusema kuwa EAMWS imekuwepokabla ya TANU na siku zote imekuwa ikitoa huduma kwa Uislam. Inasemekana hasirazilipanda na kukawa na kutoleana maneno kati ya Bibi Titi na Nyerere. Bibi Titiakamwambia Nyerere yeye hamuogopi yeyote ila Allah.
Tuhuma zile dhidi ya Aga Khan na EAMWShazikuweza kuthibitishwa na Halmashauri Kuu ya TANU ikaliacha jambo lile kwawakati ule. Lakini Nyerere alikuwa amefedheheka. Kuanzia hapo akajenga chukidhidi ya Bibi Titi na kumweka Rajab Diwani na Selemani Kitundu karibu yake.Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1965 Bibi Titi na Tewa wakapoteza viti vyao kwawatu ambao walikuwa hata hawafahamiki ñ A.M. Mtanga na Ramadhani Dollah.Iliaminika kuwa Nyerere alikuwa anahusika na kuanguka kwa Bibi Titi na Tewa.Kuanzia hapo mambo yakawa dhahiri. Nyerere alikuwa amewatangazia vita wotewawili, Bibi Titi na Tewa. Nyerere alikuwa sasa ana imani kuwa wale maadui zakewawili walikuwa wamekwisha kisiasa. Lakini kilichokuwa kkimuudhi Nyerere zaidiilikuwa taarifa ambazo alikuwa akizipata kuwa Tewa alikuwa akipewa mapokezimakubwa sana na Waislam katika ziara zake huko mikoani kama rais wa EAMWS. [1]
Sasa mwaka wa 1968, Bibi Titi na Tewawalipokwenda kumuona Nyerere kuhusu jambo lililokuwa linawahusu Waislam,Nyerere alikuwa amejitayarisha vyema. Kiwanuka ameueleza mkutano huu vizurisana: "Viongozi hawa wawili wa Waislamwalimueleza Mwalimu masikitiko yao jinsi radio ya serikali na magazeti ya TANUyalivyokuwa yakiandika habari kuhusu matatizo yale ya Waislam. Walidai kuwaTANU ilikuwa ikichanganya dini na siasa. Waliokuwa wakimtahadharisha kuhusujambo hilo hawakuwa wengine ila marafiki zake wa zamani na wa kutumainiwa, Tewana Bibi Titi. Marafiki wa kutumainiwa kwa sababu ilikuwa Titi aliyemuunga mkonoNyerere katika siku za mwanzo za TANU, pale Suleiman Takadir ñ mmoja wa wazeewa TANU ñ aliposema kuwa TANU ilikuwa na Ukristo kama Mwalimu na Rupia, rais namakamo wake walivyokuwa Wakristo. Yeyemwenyewe akiwa Muislam hasa, aliipatia TANU ushindi kwa kuthibitisha kuwaTanzania, Tanganyika kama ilivyokuwa ikijulikana wakati ule, ilikuwa mbele, naUislam unafuata nyuma. Leo, alikuwa anazungumzia jambo ambalo yeye mwenyewealilishinda katika miaka ya 1950. Jibu walilopata kutoka kwa Mwalimu lilikuwa lakusisimua. Mpashaji wangu habari anasema lilikuwa jibu la mkato. ëMmeamuakunipiga vita, jiandaeni." [1]
Mwalimu Nyerere alikuwa anawaambia TewaSaid Tewa na Bibi Titi Mohamed uso kwa macho wajiandae kwa kile kilichokuwadhahiri: vita ya msalaba dhidi ya umoja wa Waislam. Sheikh Suleiman Takadiraliyaona haya na aliiomba TANU toka mwaka wa 1958 pawepo na uhakika kuwaWakristo ambao walikuwa wanapanda migongo ya Waislam na kuchukua uongozihawatakuja kuwafanyia uadui Waislam pale Waislam watakapokuwa sasa wanatakakugawana madaraka ya kuongoza nchi sawa na Wakristo baada ya uhuru. Tewa SaidTewa, muasisi wa TANU, waziri katika serikali ya kwanza ya uhuru, balozi katikaJamuhuri ya watu wa China na Rais wa baraza la Tanzania la EAMWS, pamoja naBibi Titi, mwanamke aliowakusanya wanawake wote nyuma ya Mwalimu Nyerere naTANU, walikuwa wakisemwa na Nyerere kama vile watoto wadogo wa shule waliokuwawatukutu kwa sababu tu, walikuja kumfahamisha Rais kuhusu kukiukwa kwa maadiliambayo ilihitaji yeye ashughulikie mara moja na kutoa uamuzi."
 
Hili ni swali zuri sana; kwa kweli siyo changamoto kama unavyoiona na ni changamoto ambayo naamini itakuja kujibiwa na Waislamu wengine. Toka mwanzo wa historia yetu yamekuwepo makundi mbalimbali ya kisiasa. Hata kwenye suala la dini ni hivyo hivyo. Kitu ambacho wengi tumefanikiwa katika mjadala huu ni kuonesha kuwa:

a. Ulichoandika katika kitabu hiki siyo historia bali ni simulizi tu ambalo halina ushahidi wa historia zaidi ya hisia.
b. Unatumia dini kuangalia historia na kuweka tafsiri ya kidini kwa kutumia historia na kudai "wazee" wako si kwa sababu ni wazee wa historia yetu bali ni kwa sababu ya kuwa unakubaliana nao kuwa ni dini moja.
c. Wapo watu ambao nina uhakika nao wazee wao walikuwa ni Waislamu na walikuwa upande mwingine kabisa wa kina Takadir na kina Sheikh Amir.

Hivyo watakuja Watanzania ambao wataiokoa historia yetu kutoka mikononi mwa mtazamo wa kidini na kuiweka mahala pake hasa. Wale ambao watawaunganisha wazee wetu katika umoja wao na uzalendo wao siyo kwa dini zao bali kwa Utanganyika na Utanzania wao. Litakapotokea hilo kitabu chako kitabakia kama simulizi la majaribio tu na mapungufu yake yatawekwa bayana. Ninatumaini hili litatokea mapema zaidi.


Kina Mkandara?

a) Simulizi zilizokufanya uwajue wote waliotajwa, simulizi zilizokufanya uelewe kuwa katiba ya TANU ilikuwa ni "COPY and PASTE", simulizi zilizokufanya uamini kuwa Waislaam ndio watakuja kujibu yote haya, simulizi zinazokufanya uulize kuhusu Ndege ya Rais wakati watu wanamuongelea Mshume. Laiti ungeweza kulitafsiri neno "history" kiswahili usingeliita "Historia" the nearest lingekuwa hiyo "simulizi". Simulizi za Mohamed Said zina ushahidi kamili, Jee, Nyerere hakupokelewa na Abdul Wahid Sykes kama alivyosimulia Mohamed Said?

b) Na hao wazee walikuwa dini ipi? Na yeye unaesema si wazee wake, unaweza kutuambia wazee wake ni wepi na kwanini hakuwataja?

c) Tutajie hao watu, ili tuamini huo uhakika wako.

Hayo ni matumaini mema na wote tunaombea iwe hivyo ili waliosahauliwa kwenye Taifa hili wakumbukwe japo kwa majina tu. Mohamed Said kaanzia na wazee wake wa Dar. kwa majina na walipoishi na harakati walizozifanya kabla ya Nyerere kuja na mpaka wakawa nae na mpaka akasahau walikuwa na nyadhifa zipi, na wewe kwa nini usituletee ya wazee wako tuone mchango wao humu au huna wa kuanzia?

Maana pa kuanzia kwa sasa unapo baada ya kazi nzuri ya Mohamed Said, wa kuanzia naona hapo ndio kasheshe, ulianza ukapata jibu lake ukakosa pa kuanza tena ukaja kuanza na EPA, mengine jamani si ya kucheka lakini mnhhhhhh.
 
Serikali hii ambayo inaongozwa na kanisa ambamo ndani yake kuna kina Shein, Bilal, Mwema, Othman na Othman, Shimbo, Kikwete, Mwinyi? Au unamaana Waislamu walioko madarakani watambue kuwa wanawadhulumu Waislamu wenzao? Itakuwaje kama hawataona hilo tatizo? Je, huoni labda ipo haja ya kuangalia nje ya serikali hii kuona watu ambao wanaliona hilo tatizo ambao wako tayari kutengeneza sera ambazo zitahakikisha kuwa hakuna Mtanzania anayefanywa duni katika taifa lake awe Muislamu, Mkristu au Mpagani?

Unafikiri jibu ni lazme litolewe na serikali hii?

Kama wale waliowafukuza waumini kanisani kwa kuwa wameichaguwa CCM? Au tumfate Slaa Daktari wa kanoni? mbona huweki wazi? unaficha ficha? zama za kuficha ficha zimekwisha kijana, sasa tupo kwenye kizazi cha dot com. Utaficha nini kisijulikane?
 
Nguruvi3,
Nakuomba soma Cranford Pratt, "A Critical Phase in Tanganyika" ameeleza kirefu kuhusu memorandum iliyoandikwa 1950 na TAA Political Sub Comitteee ambayo ilipelekwa kwa Gavana Edward Twinning. Hotuba iliyosomwa Umoja wa Mataifa 1955 imenyambuliwa mle ndani.
Mohamed
Hapa ndipo mzee Said unatatiza sana.
Swali langu linalotokana na hoja zako ni kuwa kwa vile sub committee ilishaundwa na tunajua ni ya chama cha TAA, Je, hiyo hotuba iliandikwa ili nani aipeleke kunako husika(kwa gavana kama ni hivyo), nani alikuwa aisome UN? Na hotuba ya uhuru ililenga uhuru wa mwaka gani.
Maana yangu ni kuwa ukinunua mbeleko unajua upo utungo wa mimba kwahiyo yote yalijulikana.
swali ni rahisi na straight forward. Tuache hii ya mwaka 1955 tujibu ile ya 1950
 
Mag3,
Nadiriki kusema kuwa Mohamed ame "hijack" jina na legacy ya Abdulwahid Sykes kwa malengo yake ya kidini. Hata mimi niko karibu na wanae Abdulwahid. They are not exactly thrilled with Mohamed's jihad.

Hao unaojidai upo nao karibu hao ndio wamempa Mohamed Said nyaraka nyingi tu za kitabu chake. Leo nani asiyetaka Baba'ke ajulikane mchango wake katika Historia? unashangaza sana.

Jihad (strive hard in any good cause) ni kujitahidi ni nani asiyependa kujitahidi? wewe?
 

Within One Hour:

Mzee Mwanakijiji Yesterday 23:16 #822

Hili ni swali zuri sana; kwa kweli siyo changamoto kama unavyoiona na ni changamoto ambayo naamini itakuja kujibiwa na Waislamu wengine. Toka mwanzo wa historia yetu yamekuwepo makundi mbalimbali ya kisiasa. Hata kwenye suala la dini ni hivyo hivyo. Kitu ambacho wengi tumefanikiwa katika mjadala huu ni kuonesha kuwa:

a. Ulichoandika katika kitabu hiki siyo historia bali ni simulizi tu ambalo halina ushahidi wa historia zaidi ya hisia.
b. Unatumia dini kuangalia historia na kuweka tafsiri ya kidini kwa kutumia historia na kudai "wazee" wako si kwa sababu ni wazee wa historia yetu bali ni kwa sababu ya kuwa unakubaliana nao kuwa ni dini moja.
c. Wapo watu ambao nina uhakika nao wazee wao walikuwa ni Waislamu na walikuwa upande mwingine kabisa wa kina Takadir na kina Sheikh Amir.

Hivyo watakuja Watanzania ambao wataiokoa historia yetu kutoka mikononi mwa mtazamo wa kidini na kuiweka mahala pake hasa. Wale ambao watawaunganisha wazee wetu katika umoja wao na uzalendo wao siyo kwa dini zao bali kwa Utanganyika na Utanzania wao. Litakapotokea hilo kitabu chako kitabakia kama simulizi la majaribio tu na mapungufu yake yatawekwa bayana. Ninatumaini hili litatokea mapema zaidi.

Mzee Mwanakijiji Today 00:07 #835

Mdondoaji - umesema jambo kubwa sana. Miye binafsi - na nimelisema hili huko nyuma - Mchango wa Bw. Said katika kuandika historia "yetu" ni mkubwa sana kuliko hata anavyojua. Ni kweli kuna mapungufu mengi - na mengine naweza kusema ni makubwa sana - katika kitabu chake lakini all in all ni kitabu ambacho binafsi ningependa kisomwe na watu wengi zaidi lakini kisomwe kwa kutumia uwezo wa kuhoji na umakini wa kutambua ni wakati gani kinachosemwa ni historia na wakati gani ni hisia na hasa kuelewa mapema kabisa the underlying theme ya kitabu chenyewe - kuonesha kuwa Nyerere hakuwa na mchango wa kipekee katika historia ya Uhuru kulinganisha na waasisi wengine wa Taifa letu.

Ninakuhakikishia baadhi ya matatizo mengi ambayo tunayazungumza tatizo lake ni CCM na hili mimi na Said tunakubaliana sana. Tofauti ni kuwa siamini kama CCM ina interests wala uwezo wa kushughulikia matatizo hayo ya kihistoria wakati yeye anaamini kuwa serikali hii hii inaweza kushughulikia matatizo hayo. Sijui uko upande gani katika hilo lakini sentensi yako hapo is telling.
 
Hapa ndipo mzee Said unatatiza sana.
Swali langu linalotokana na hoja zako ni kuwa kwa vile sub committee ilishaundwa na tunajua ni ya chama cha TAA, Je, hiyo hotuba iliandikwa ili nani aipeleke kunako husika(kwa gavana kama ni hivyo), nani alikuwa aisome UN? Na hotuba ya uhuru ililenga uhuru wa mwaka gani.
Maana yangu ni kuwa ukinunua mbeleko unajua upo utungo wa mimba kwahiyo yote yalijulikana.
swali ni rahisi na straight forward. Tuache hii ya mwaka 1955 tujibu ile ya 1950

Nguruvi3,

Niwie radhi kama huwa sifiki katika kimo chako.

Nakupa ushauri mmoja tafuta kitabu chochote cha sheria usome mada ya "the standard of the reasonable man." Utaongeza elimu yako na maswali kama hayo yako utakuwa huniulizi tena.

Sheikh Hassan bin Amir akitumia sana hii mara nyingi likija swali kwake la sampuli hiyo alikuwa akisema, "Tatizo nyinyi hamtaki kusoma laiti ungelisoma isngeliuliza swali kama hilo."

Hata hivyo niakujibu hebu kwanza pata "background" ya jambo lenyewe:
TAA 1950
"Makao Makuu ya TAA mjini Dar es Salaamchini ya Dr Kyaruzi na Abdulwahid ikiungwa mkono na kamati ya siasa sasailikuwa ikiamka kutoka kwenye usingizi mzito. Kilichotakiwa ilikuwa ni kupatamaswala yakutoa changamoto kwa akili za wale wasomi vijana. Uongozi wa chamacha TAA haukuwa na haja ya kuangaza mbali. Changamoto ilikuja kwa sura yaConstitutional Development Committee (Kamati ya Mapendekezo ya Katiba)iliyoundwa na Gavana Edward Twining na mgogoro wa ardhi ya Wameru.
Uingereza ilikuwa ikitawala Tanganyikachini ya kifungu 76 na 77 cha Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Kama mamlaka tawalaUingereza ilitarajiwa kuanzisha na kuendeleza maendeleo ya siasa, uchumi na yakijamii ya Tanganyika hadi kufikia wakati ambao watu wake wangekuwa tayarikujitawala. Lakini Waingereza walifanyakhiyana na hawakutimiza ahadi hiyo. Walijihusisha na kulinda maslahi yaowenyewe ya kikoloni na yale ya watu weupe wachache na wakaendelea kuwapuuzaWaafrika waliokuwa wengi na wenye nchi. [1] Labda kwa kuanua ngomajuani, Gavana Twining alikaribisha mapendekezo kutoka kwa watu mashuhuri, vyamavya ustawi wa jamii na Native Authorities,[1] kutaka mapendekezo yajinsi Tanganyika itakavyotawaliwa. Kamati ya siasa ya TAA ilipeleka mapendekezoyake ambayo yalitiwa sahihi na wajumbe wote wa kamati ya siasa. Sheikh Hassan bin Amir, Abdulwahid Sykes,Vedasto Kyaruzi, Hamza Mwapachu, John Rupia, Stephen Mhando na Said Chaurembo.[1]Katika taarifa yake ya mwaka ya 1950 Abdulwahid aliandika: "Kwa ajili ya maslahi ya Waafrika na kulindamaslahi ya chama hiki na yale ya jumuiya ya Waafrika kwa ujumla, chama kimewekawakili atakayeshauri juu ya mambo ya sheria. Wakili huyo ni Bwana E. E. Seatonwa Moshi. Mara kwa mara amekiandikia chama hiki juu ya masuala mbali mbali yasiasa, na kwa kiasi kikubwa ushauri wake umesaidia wakati chama hiki kilipokuwakikitayarisha mapendekezo juu ya katiba."[1] Abdulwahid alitambua kuwa matatizo mengikuhusu haki za Waafrika yalikuwa masuala ya kisheria ambayo yalihitaji ushauriwa wanasheria. Kwa mara ya kwanza kwa msaada wa Seaton, TAA kilitoa hoja zakezilozotiwa nguvu na ukweli hoja na kwatarakimu zilizoonyesha udhalimu ndani ya mfumo wa kikoloni ambao ulikuwakinyume na Mkataba wa Umoja wa Mataifa. Memorandum ya TAA kwa ConstitutionalDevelopment Committee ambayo Pratt amesema iliandikwa kwa utaalamu wa hali yajuu na uongozi wa makao makuu ya Tanganyika African Association ilipendekezakuwa ndani ya baraza la kutunga sheria. Waafrika watashika nusu ya vitikwa miaka kumi na mbili na baada ya hapo ipigwe kura kuwachagua wajumbe.[1]"

Sasa soma hii hapa chini:

TAA/TANU 1954
"Ajenda yakwanza kujadiliwa chini ya TANUtarehe 9 Julai ilikuwa lile suala la uchaguzi wa wajumbe wa Baraza la KutungaSheria. Katika mwaka 1950 itakumbukwa kuwa TAA, chini ya uongozi wa Abdulwahidna Dr Kyaruzi iliwakilisha memorandum kwa Gavana Twining kueleza mapendekezoyake juu ya mabadiliko ya katiba. Ilishauriwa kwamba ili kufikia kiwango fulanicha maendeleo ya siasa, ilikuwa lazima Waafrika wapitie utaratibu wa maendeleohatua kwa hatua kwa kushiriki katika kuitawala nchi yao. Moja ya mapendekezoilikuwa Waafrika waruhusiwe kuchagua wawakilishi wao wenyewe katika Baraza laKutunga Sheria. Ilikisiwa kwamba haya mabadiliko ya hatua kwa hatua yaruhusiwekuendelea kwa kipindi cha miaka kumi na tatu baada ya hapo Waafrika waruhusiwekuunda serikali yao wenyewe iliyo huru.[1] Hii ilikuwa ajenda muhimu sana na Abdulwahidna Rupia ambao walikuwa wajumbe wa kamati ndogo ya siasa ya TAA iliyorasimumapendekezo hayo walieleza mkutano kwa ufupi juu ya upinzani wa serikali katikakukubali mapendekezo hayo. Ilikubaliwa na wote kwa pamoja kuwa suala lakuanzisha kanuni za kidemokrasia katika uchaguzi wa wajumbe kwenye Baraza laKutunga Sheria lilikuwa muhimu sana na watu lazima wafahamishwe juu ya hakihii."

Ikiwa umesoma "the standard of the reasoble man" na umeshindwa kujua majibu ya maswali yako tutafuta msaada wa wanaukumbi wengine watusaidie. Ndiyo maana muulizaji wa "Aga Khan ni Muislam au si Muislam" sikumjibu maana huwa sipendi kuwa "encourage" wanamnakasha kuuliza vitu ambavyo ni "obvious" vinachachua majadiliano. Kwa hakika kama ulivyosema mwenyewe hili ni swali rahisi.

Mohamed

 
Ndugu zanguni kashfa, kejeli na matusi si sifa ya JF huko mnakoelekea siko mnavunja heshima ya hili jamvi.

Hebu mlanini shetani tulizeni hamaki zenu na tujadili mambo makubwa ya mustkbali ya nchi yetu.

Vinginevyo huu ukumbi utaonekana wa wahuni.

Mohamed

Historia haiegemei katika dini pekee.
Ujaribu kuzungumzia historia kwa mapana na si kwa nguzo ya dini pekee.
 

Within One Hour:


Mwanakijiji,

Dawa yangu mimi ni nyinyi mkaandika kitabu basi.
Vinginevyo itakuwa ni hii "merry go round."

Hamuwezi kujibu kitabu changu kwa sentensi.

James Brenan na Jonathan Glassaman walinileta hadi Northwestern University, Chicago Illinois tukafanya mnakasha mkali. Mimi hawa nawaheshimu ndiyo mabingwa wa mambo haya wapige "google" uone moto wao.

Hivi wako njiani kuwaleta wanafunzi wao Ph D kuja kupitia upya historia ya Tangayika na Nyerere husan mle ambamo hatukubaliani.

Wanatambua ukweli kuwa njia ya wao kunitoa makosa ni kuja na kitabu kingine cha historia ya uhuru wa Tangnayika.

Hebu na nyie waungeni mkono tupate ukweli.


Mohamed
 
wale watoto waliomuua gadaffi walikuwa wanatamka neno ambalo gadafi alikuwa analitamka wakati anapigwa ....Alah Akbar
kwa hiyo nina uhakika waislamu wa Tanzania(waliopo madarakani) wanawakandamiza waislamu wenzao(kina MS ) ..sasa ili kutafuta pa kutokea wanawasingizia wakristo..sehemu kama egypt ,tunis(arap rise ) walikuwa hawana mtu wa kumsingizia kama hawa hapa wa TZ

Umejipambanua sana hapo nilipo RED.

Kuna mifumo mingi sana ya kiutawala inayo tumiwa na watawala katika kutawala. Mmoja ukiwa ule wa gawanya na utawale (divide and rule) na mara nyingi katika mfumo huu utachukua watu wachache sana katika ile jamii husika na kuifanya bora zaidi kwa ajili ya kulinda maslahi yako kwa kuikandamiza ile jamii waliyotokea. ndio maana waswahili wanasema Shoka haliwezi kukata miti mpaka liwekwe kipande cha mti (Mpini)

Sasa tujiulize kama miti yhote itakataa kabisa kuingia kwenye shoka basi shaka hata siku moja halitaweza kukata miti. Ili shoka likate miti ni lazima kitoke kipande cha mti (Mpini) kiwasaliti wenzake na kuingia katika shoka ndipo miti itateketezwa.

Sasa na hao uliowataja na Mpini. Na kumbuka waislam wanatafuta mzizi wa dhulma hizo na hawababaishwi na hiyo Mpini kwani hicho ni kitu kidogo sana kwao wao wanatumia kuelimishna kisha wote kwa pamoja kudai haki yao iliyofichwa na kuporwa.

Kila la kheir
 
Kama wale waliowafukuza waumini kanisani kwa kuwa wameichaguwa CCM? Au tumfate Slaa Daktari wa kanoni? mbona huweki wazi? unaficha ficha? zama za kuficha ficha zimekwisha kijana, sasa tupo kwenye kizazi cha dot com. Utaficha nini kisijulikane?

FF,

Watu waliokuwa na Sheikh Hassan bin Amir Zanzibar baada ya Nyerere kumfukuza Bara walikuwa hawazungumzii mchango wa Sheikh katika kupigania uhuru wala juhudi zake katika kutaka kujenga Chuo Kikuu Cha Waislam kupitia EAMWS walikuwa wakianza historia hiyo Sheikh akijiinamia na kulia.

Walipo jua hivyo wakaacha kabisa.

Hii ikafikia hata baadhi ya wanafunzi wake katika kumuadhimisha wakawa wanasema Sheikh Hassan bin Amir hakuwa mwanasiasa.

Mohamed
 
Mzee Said nimekumbuka swali moja niiltaka kuuliza mzee John Rupia ni miongoni mwa "wazee wako"?

Kuliko unavyoweza kufikiria.

Mwanangu mmoja (mtoto wa kaka yangu) alikuwa anaoa.
Mmoja wa waliotoa hotuba katika harusi ile ni mtoto wa Mzee John Rupia na yeye na mkewe walikuwa meza kuu.

Mohamed
PS: Mwanakijiji hebu niulize maswali ya chemsha bongo haya sasa hayana muhimu katika historia au umechoka? Kama "fatigue" inakunyemelea basi tupumzike sote. Tulochangia hapa jamvini si haba. MS
 
Mwanakijiji,

Dawa yangu mimi ni nyinyi mkaandika kitabu basi.
Vinginevyo itakuwa ni hii "merry go round."

Hamuwezi kujibu kitabu changu kwa sentensi.

James Brenan na Jonathan Glassaman walinileta hadi Northwestern University, Chicago Illinois tukafanya mnakasha mkali. Mimi hawa nawaheshimu ndiyo mabingwa wa mambo haya wapige "google" uone moto wao.

Hivi wako njiani kuwaleta wanafunzi wao Ph D kuja kupitia upya historia ya Tangayika na Nyerere husan mle ambamo hatukubaliani.

Wanatambua ukweli kuwa njia ya wao kunitoa makosa ni kuja na kitabu kingine cha historia ya uhuru wa Tangnayika.

Hebu na nyie waungeni mkono tupate ukweli.


Mohamed
Mohamed,
Wa kutusimulia ili tuandike kama wewe hayupo. Hatuna wazee wetu "Wakristo" waliokuwa TAA ambao wako hai sasa. Mimi ni mmoja wa wanaoogopa sana kuwasemea marehemu. Pili, ukianza simulizi kwa kutumia DINI, KABILA, JINSIA,......, inakuwa sio historia tena.
Halafu, wazee wako hawa, Mohamed hawakuwa na mapungufu hata kidogo kama ulivyomwanika Mwalimu?
 
Historia haiegemei katika dini pekee.
Ujaribu kuzungumzia historia kwa mapana na si kwa nguzo ya dini pekee.

Hili la dini mbona Mohamed Said kisha lijibu sana mpaka sasa inakuwa (kisemeo cha Mohamed Said) "kama santuri iliyokwama". Rudi nyuma uone limejibiwa vipi.
 
Back
Top Bottom