Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Asante MS kwa kunitukana kuwa sijafunzwa. Sina haja ya kukuthibitishia ila fahamu tu kuwa nimelelewa vema na WAZAZI wangu na WALIMU WANGU PIA WANAMCHANGO WA THAMANI KWANGU, hawa wote hakuna aliyenipa sumu ya ubaguzi wa aina yoyote. Nimekuelewa, sikujua kumbe nimekukwaza sana nilipokuambia kuwa Mada yako inalenga kuwatenganisha WATANZANIA kwa misingi ya UDINI. INAWEZEKANA WEWE NDIYE HUKULELEWA VEMA na wazazi wako, KWA maana ya kuwa walikupa SUMU kama ile wanayopewa watoto wa KIYAHUDI na KIPALESTINA ili nawe uje utupe sisi, matokeo ya hiyo sumu daima huonekana ukubwani kwa matendo wanayotenda. Sina haja ya kukupa details ya kinachotokea mid-east kwa sa7 unajua, kama hujui pole.

Anayekupinga unamuona adui, Huo ndio mtazamo wa watu wa mid--east nawe uko hivyo--nihabarishe wazazi wako walikupeleka upande upi (Palestina au Israel) baada ya kulizika kuwa sasa sumu imeingia vema ktk damu yako kufanya mazoezi(internship).
Maandishi yako yanalenga kuwatenganisha WATZ kwa misingi ya UDINI. SASA sisi tunashuhudia wengine tunashangaa nini kinaendelea ktk nchi hii maana watu wamezunguka nchi nzima kumlaani NYERERE, nilikuwa sielewi ila sasa nimeelewa baada ya kusoma makala zako za sumu kwa WATZ nao bila kufikiri wakalichukua kichwa kichwa. Mafundisho yako yana agenda ya siri ambayo matokea yake yaja--ni suala la wAKATI TU.
TUKUE VIZURI NA TUZEEKE VIZURI TUSIWATENGANISHE WATZ TO FULLFIL OUR INTEREST.
KUMBUKA TANZANIA SIO YA DINI, KABILA AU UKANDA FULANI, UNAPOANDIKA HISTORIA YA NCHI HII PLEASE DO NOT RELY UPANDE FULANI

Nina marafiki wengi sana ambao siabudu nao ktk madhehebu na wengine ni dini tofauti nami, kilichotukutanisha nao sio madhehebu au dini zao bali UTANZANIA ULITAMALAKI BILA UBAGUZI WA DINI, KABILA wala UKANDA.
 

Hayo maneno ungewauliza maaskofu wanaopokea hela za umma kuendeleza kanisa ( uwizi)

Hayo maneno ungewauliza kwanini serikali ya nyerere iliamua kufuta historia ya sahihi ya wazee wa kiislamu (kwasababu ya udin na ubaguzi)

Hayo maneno ungewauliza kwanini serikali ya nyerere ulibagua na kuchagua viongozi wakatoliki kwa miaka 24..

Sasa ubaguzi ufanywe na wengine wewe umlaumu mohammed
 
Mgalanjuka,

Niwie radhi hebu niulize tena hilo swali kwa njia nyepesi kitu kimoja baada ya kingine nipate kujua khasa kinachoulizwa ni nini.

Mohamed

Sawa nitajaribu kuvunja haya kwa wepesi wa kadri yake.. Je historia hii ya wazee wako uloiandika ndio nguzo kuu ya madai yanayoonekana katika hoja zako? Historia pekee si katiba au itikadi maana haipaswi kuwa na matarajio ya mwandishi kama jinsi tunavyokusoma katika baadhi ya majibu yako. Hapo ndo napata shida kwamba kwa nini utumie "historia" kama itikadi yenye matarajio fulani mbeleni? Huoni sasa hii unayoandika tayari inakuwa biased kwa kuwa wewe una matarajio ya matokeo ya unachoandika? Hilo moja...
 

Mgalanjuka,

Kweli nashindwa kupata "gist" ya swali lako.
Niwie radhi.

Mohamed
 

Mwakaboko,

Sijakutukana.

Uliposema kuwa umezaliwa baada ya uhuru nikajua wewe kwangu ni mdogo na nikatumia lugha tutumiayo watu wa pwani katika kumkanya mtoto mdogo ili awe na heshima.

"Mtoto aliyefunzwa."

Haina maana hukufunzwa.
Huenda umefunzwa lakini unataka kuonyesha ujuba tu, machachari ya ujana na utoto.

Lakini kama kweli wewe ni kijana mwenye adabu hutoingia tena humu kwa makeke kama yale.


Mohamed
 
Kigarama, ahsante kwa kuninyanga maneno niliyokua naelekea kuandika.
Kuna uelewa tofauti wa mambo. Kiarabu na Uislam ni vitu viwili tofauti. Uislam umekuja katika lugha ya kiarab lakini uislam si uarabu.
Kuna waarabu waislam ma waarabu wakristo. Irab za kiarabu hazi 'qualify' mtu kuwa muislam na wala jina la kiarabu halimfanyi mtu awe mwislam.
Hata utamaduni wa kiarabu sio utamaduni wa kiislam bali waarabu wame take advantage ya mambo yote mawili.

Kwa wale waliowahi kufika nchi za kiarabu watakubaliana nami kuwa Uislam wa sehemu husika unakuwa influenced na utamaduni wa eneo hilo. Uislam wa Yemen ni tofauti na wa Saudia na Oman kwa maana kuwa Koran inabaki ile ile lakini kuna viitu vya tamaduni vimechombezwa katika Uislam. Kwa mantiki hiyo Tareq Azizi akiandika barua kwa kiarabu haimfanyi awe muwislam! Lugha ya mawasiliano kati ya Jidawi wa Fatah na Haniya wa Hamas ni kiarabu, lakini wote ni waislam? Kuna misconception kubwa sana.

Waarabu walikuja kwa biashara za halali na za utumwa. Moja ya vitu muhimu katika biashara ni mawasiliano na hivyo ilibidi watu wajifunze lugha ya kiarabu, ukiangalia historia karne za waarabu kila jambo lilikuwa katika Irab za kiarabu lakini hiyo haimaanishi kuwa hawa walikuwa Waislam.
Mtu anapodhani maandishi ya kiarabu ni ushahidi wa Uislam, inasikitisha sana.

Kuna mmoja amesema tuangalie kama barua zilianza na neno Bismillah n.k. Hapa kuna misconception pia kwasababu hata kama mtu ataanza kwa jina la mwenyezi mungu bado anaweza kudanganya au kutokuwa na imani au kutoheshimu hilo jina. Alqaeeda wakitaka kuua huwa wanaanza na maneno ya kumtaja mwenyezi mungu. Taliban wakitaka kuua wanaanza kwa jina la mwenyezi mungu. Walibomu London mikanda yao waliorekodi walianza kwa jina la mwenyezi. Kuanza barua kwa neno kwa jina la mwenyezi... hakuthibitishi kuwa mtu ni muislam bali mtu ametumia utamaduni wa kiisalam katika mawasiliano.
 

Tena unaweza kwenda mbali tu kuwa wao kina Sykes walikuwa ni wasaliti wa Waafrika wenzao hasa ukizingatia wanatoka kabila la Wazulu (kina Shaka) ambao walipigana na hawa wageni. Kama kina Sykes wanatukuzwa kwa kuja kupigana na Waafrika hadi kusababisha kina Mkwawa kujinyonga sidhani kama tunaweza kusema walifanya hivyo wakijali Uislamu. Umoja kwa Waislamu ni fardh sasa inakuwaje Muislamu apigane na Muislamu mwenzake akimtumikia Mkristu na aonekane ni shujaa?
 
Mwanakijiji,

Hili nimelijibu huko nyuma lakini nakwekea hapa:

Huo ndiyo ukweli wala hakuna wa kupinga.

Wazulu, Wamanyema na Wanubi baba za Kleist Sykes, Ibrahim Hamis na Mzee bin Sudi ambao ndiyo walikuja kuasisi African Association walikuwa askari wa kikoloni ambao waliletwa Tanganyika na Herman Von Wissman kuja kupigana na Bushir bin Salim na Mkwawa.

Haya nimeyaeleza katika kitabu changu wala sikuwapamba huu ni ukweli wa kihistoria ambao upo.

(Babu yangu mkuu Samitungo Muyukwa Mwekapopo yeye alitokea Belgian Congo na alikuwa kwenye boma Shirati ambako babu yangu alipozaliwa).

Huyu babu yangu kama wenzake walileta mapinduzi ya siasa katika Tanganyika.Yeye alikuwa katika kamati ya ndani AA Tabora habari zake nishazieleza humu na vipi aliwekwa kizuizini na Nyerere 1964 kwa shutuma ya kupanga njama za kupindua serikali mwaka 1964.

Kama ulivyosema "historia inaleta viroja" watoto wa hawa wa mamluki kutoka nje ya mipaka ya Tanganyika ndiyo wakapanda mbegu ya utaifa wa Tanganyika. Huwezi leo ukaandika historia ya Tanganyika usimtaje Kleist Sykes, Ibrahim Hamis, Mzee bin Sudi, watoto wa Affande Plantan, Thomas, Schneider na Mashado.

Licha ya hayo Kleist, Mzee bin Sudi na Schneider wakajenga na msingi wa umoja wa Waislam wa Tanganyika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ambao ndiyo uliokuja kuasisi TAA na kuunda TANU 1954.

Katika kitabu cha Judith Listowel, "The Making of Tanganyika" kuna kipande kizuri sana kinachoeleza vurugu alofanya Schneider Pltann Ukumbi wa Arnoutoglo mwaka wa 1950 mbele ya ofisa Mzungu akidai lazima TAA iiitishe mkutano wachague viongozi wapya. Vurugu hili ndilo lililomtia Dr Vedsto Kyaruzi na Abdulwahid Sykes katika uongozi wa TAA.

Mashado Plantan ndiyo mtu wa kwanza kumjenga Nyerere katika gazeti lake Zuhra na hili ndilo lilikuwa mdomo wa TANU chama kilipoasisiwa mwaka 1954. Nitamaliza kwa kueleza kuwa si kama hawa "wageni" kwa ukweli wakiitwa "watu wa kuja" walipata mteremko, la hasha walipata upinzani mkubwa kuwa kile wenyeji walichoona "kimbelembele" chao.

Katika kitabu cha Abdu Sykes nimeeleza misuguano hii kwa undani zaidi.

Mohamed
 
Mashaalah ! mnakasha unatufikisha mahali pazuri sana, sasa ile hoja ya kuwa Waislam walipigania uhuru peke inajijibu. Ile hoja kuwa wakati waislam wanaharakati za kupambana na mkoloni, wakristo walisaidia mkoloni ina kufa 'natural death'.
Sasa tuna ushahidi kuwa wakati waislam wanapigana na ukoloni kuna waislam walimsaidia mkoloni. Hawa waliomsaidia mkoloni kumpiga mwenzao ndio tunaambiwa walipanda mbegu za utaifa wa Tanganyika!

Hoja ya kutuhumu wakristo sasa imeji eliminate na imefika tamati kwa neno si kweli.

Mnakasha uendelee
 
Huu ndiyo uzuri wa JF lazima utapa faida na mimi nakiri kweli ndugu zangu nafaidika sana na michango yenu. Kuna mengi najifunza hapa jamvini.

Mohamed
 

Nguruvi3,

Huo ndiyo ukweli kuwa Wamanyema, Wazulu na Wanubi waliingia Tanganyika kutoka nje na walikuwa watumishi wa Wajerumani na walipigana dhidi ya wazalendo wa nchi hii.

Hilo ni wazi kabisa.

Mabadiliko yalikuja kuletwa na watoto wao ambao walizaliwa katika utawala wa Waingereza. Naweka tena kwa faida ya wanaukumbi:

"Wazulu, Wamanyema na Wanubi baba za Kleist Sykes, Ibrahim Hamis na Mzee binSudi ambao ndiyo walikuja kuasisi African Association walikuwa askari wakikoloni ambao waliletwa Tanganyika na Herman Von Wissman kuja kupigana naBushir bin Salim na Mkwawa. (Babu yangu mkuu Samitungo Muyukwa Mwekapopo yeyealitokea Belgian Congo na alikuwa kwenye boma Shirati ambako babu yangualipozaliwa).
Huyu babu yangu kama wenzake walileta mapinduzi ya siasa katika Tanganyika.Yeyealikuwa katika kamati ya ndani AA Tabora habari zake nishazieleza humu na vipialiwekwa kizuizini na Nyerere 1964 kwa shutuma ya kupanga njama za kupinduaserikali mwaka 1964.
Watoto wa hawa wa mamluki kutoka nje ya mipaka ya Tanganyika ndiyo wakapandambegu ya utaifa wa Tanganyika. Huwezi leo ukaandika historia ya Tanganyikausimtaje Kleist Sykes, Ibrahim Hamis, Mzee bin Sudi, watoto wa Affande Plantan,Thomas, Schneider na Mashado.
Licha ya hayo Kleist, Mzee bin Sudi na Schneider wakajenga na msingi wa umojawa Waislam wa Tanganyika Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ambao ndiyouliokuja kuasisi TAA na kuunda TANU 1954.
Katika kitabu cha Judith Listowel, "The Making of Tanganyika" kunakipande kizuri sana kinachoeleza vurugu alofanya Schneider Pltann Ukumbi waArnoutoglo mwaka wa 1950 mbele ya ofisa Mzungu akidai lazima TAA iiitishemkutano wachague viongozi wapya. Vurugu hili ndilo lililomtia Dr Vedsto Kyaruzina Abdulwahid Sykes katika uongozi wa TAA.
Mashado Plantan ndiyo mtu wa kwanza kumjenga Nyerere katika gazeti lake Zuhrana hili ndilo lilikuwa mdomo wa TANU chama kilipoasisiwa mwaka 1954. Nitamalizakwa kueleza kuwa si kama hawa "wageni" kwa ukweli wakiitwa "watuwa kuja" walipata mteremko, la hasha walipata upinzani mkubwa kuwa kilewenyeji walichoona "kimbelembele" chao. Katika kitabu cha Abdu Sykesnimeeleza misuguano hii kwa undani zaidi."
 
Sasa Mzee Said kwanini isisemwe kwamba Waislamu walipigania ukoloni wa Mjerumani ili uendelee katika eneo letu na walifanya hivyo wakiwapiga Waislamu wenzao na Waafrika wenzao? Kama hili ni kweli hatuwezi kusema kuwa ni Waislamu ndio walioshiriki kwa kiasi kikubwa kuzima vita vya Maji Maji ambavyo Waislamu wenzao walikuwa wameshiriki kabisa katika kuvianzisha dhidi ya dola ya Mjerumani? Kwa maneno mengine mchango wa Waislamu si tu katika kupigania uhuru (miaka ya baadaye) lakini pia katika kupigania ukoloni udumu (miaka ya mwanzo)?

Na wengine - nahasa ukikisoma kitabu chako - inaonesha watoto wa kina Kleist walimchukia Muingereza kwa sababu ya kuwashindwa Wajerumaini - waliowapa maisha ya kisasa baba zao - na hivyo haikuwa kumpinga Mwingereza kwa sababu ya ubaya wa Ukoloni wake. Yaani their opposition to the British rule was personal rather than principled?
 

Naona mnaanza kujifariji baada ya kubisha bila evidence..
 

Isemwe na nani? mbona unaongelea dhana
 

Mwanakijiji,

Hizo ndizo nondo za kukuwezesheni na nyinyi kuandika kitabu chenu msiachie nafasi hii iwaponyoke.

Mohamed

 
Mwanakijiji,

Hizo ndizo nondo za kukuwezesheni na nyinyi kuandika kitabu chenu msiachie nafasi hii iwaponyoke.

Mohamed


hapana mzee Said hapo ndipo unapokosea; kwa kweli ningekuwa na muda na nafasi ya kuandika historia yetu nisingeandika kama ulivyofanya wewe kwa kuangalia dini vs dini na hivyo kufanya kile unachowatuhumu wengine. Binafsi naamini ni wito na ombi kwako kwamba katika maandishi yako mengine urudi zaidi katika mstari wa kati kama mwanahistoria na kuiandika historia yetu kwa kuangalia historia yenyewe bila kuweka vikolombwezo vya udini ili kuifanya inoge. Nina uhakika ukifanya hivyo siyo tu utakuwa umetoa mchango kwa kuhifadhi historia ya Waislamu bali kwa hakika utakuwa umehifadhi historia yetu kwa usahihi zaidi. Lakini najua hili ni gumu kwako kwa sababu unaangalia "us vs them" na hapa ndipo unakosa ile objectivity and neutrality that history demands of its writers.
 
Kwanza Mwalimu hakuwa mwandishi wa vitabu vya historia ya nchi hii, na hakuna ushahidi mahali popote pale ambapo yeye alikataza hao wanaotajwa leo historia yao kuandikwa.

Hivi kweli walikuwa kwenye hatua za mwisho kupata uhuru. Unajua maana ya hatua za mwisho wewe? Hao wazee wenu walishakwenda UNO kudai uhuru na kuahidiwa kupewa Uhuru? Mwisho kutoka 1954 TANU ilipoanzishwa hadi 1961 ni hatua za mwisho kweli?
 

Exactly ndivyo unavyofikiri kuhus wazee wa kiislamu..poor you
 
 
Hayo maneno ungewauliza kwanini serikali ya nyerere iliamua kufuta historia ya sahihi ya wazee wa kiislamu (kwasababu ya udin na ubaguzi)
Kinachofutwa ni kile kilichoandikwa. Mbona hamtuambii ni nani aliyeandika hiyo historia na nani aliifuta na kwa maagizo ya nani na maagizo hayo yalitolewa lini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…