Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Historia ya Uhuru isimuliwavyo na Mohammed Said yakosolewa

Sijui ni mods au nini kinatokea thread michango yangu inafutwa hapa..
Sio mbaya
Nashauri ufanye uchunguzi wa kitaalam kujua kwanini wanafunzi wanafeli nadhani kifeli kwao hakuna uhusiano na dini zao..
Mmekuwa na viongozi wengi tena wasomi wa hiyo dini yenu sijajua kwanini hawaoni hayo unayaoyaita malalamiko ya dhuluma dhidi ya dini yenu
Mimi binafsi niwe mkweli, nawachukulia watu wa dini ya kiislam Tanzania kuwa ni walalamikaji sana na wasioridhika daima mpaka washike hatamu ndipo watajiona hawaonewi, wakati huo nchi ina makundi mengi ya kidini sijawahi ona wakilalama kama waislam, halafu sizioni hizo fursa za kiuchumi, kijamii au kisiaasa anazopata MTU kutokana na kuwa wa dini ile au hii kikubwa nayaona madhira ya watanzania kukosa huduma stahiki hayabagui dini, watu hawana maji, madawa hospitalini, shule hazina vitendea kazi, wafanyakazi hawana malipo mazuri, na kadhia nyingine nyingi bila kujali dini...
Sasa hii dhana ya dhuluma kwa waislamu bado inanitia mashaka sana wakati huo hao waislamu ndio wamekuwa wakipewa Mali za serikali kwa upendeleo, sijaona wasabato wakipewa majengo bure waanzishe chuo kikuu bali waislamu hupewa, sijawahi ona ndani ya taasisi ya kiislamu kuna MTU wa dini nyingine atapewa Uhuru wa kuabudu bali wailasmu wamepewa misikiti ndani ya majengo ya wakristo, ni ikitokea kuna taasisi ya serikali kiongozi wa juu ni muislam basi tegemea atakoleza ajenda ya kuwakusanya waislamu toka pande zote wafanye kazi kwenye taasisi hiyo na watajitahidi hata kama kuna msikiti mita mia mbili kutoka ofisi iliko watataka humo ndani ujengwe mwingine na zifuatwe sheria za kiislam eneo hilo....
Huu ndio uislam ninaoushuhudia mtaani niishipo....

Teteeni imani zenu msikandamize wengine kwa hila ya aina yoyote, suala la imani MTU halazimishwi ni Uhuru wa kuchagua, na wakati mwingine MTU anaweza iga imani kwa kufurahishwa na matendo ya muumini....Mungu akiamua kuwataka watu wawe wa imani Fulani hakuna force ya nje itakayozuia...ishini kwa upendo...
Avriel,
Unataka kufanya mjadala katika somo usilolijua na ndiyo maana hata kuandika kwako kuna shida.

Katika uandishi dot zinakuwa tatu...
Jifunze uandishi soma ndiyo uingie katika mijadala.
 
Na kweli, penye ukweli uongo hujitenga. Mnakasha huu uliwafungua wengi macho na nawapa asante nyingi wote mlioshiriki kutoka pande zote...hii nayo itabaki kuwa historia iliyoandikwa na wengi hapa jamvini, JF idumu! Mungu awabariki!
 
Avriel,
Unataka kufanya mjadala katika somo usilolijua na ndiyo maana hata kuandika kwako kuna shida.

Katika uandishi dot zinakuwa tatu...
Jifunze uandishi soma ndiyo uingie katika mijadala.
Ndio umejibu hoja hivyo?
Aliekuambia Mimi mwandishi mzuri nani?
Bila shaka ukiachilia mbali huo uzuri wa uandishi umeelewa nilichoandika tena kwa kiswahili kisichokosewa, achana na nukta mia au elfu .........
Waislam wanapenda kulalama sana nchi hii wakati madhira ya uongozi mbovu nchini huwaathiri watu wote bila kujali dini zao,sasa mnashangaza mnapotaka kujiona ninyi ni maalumu kwa dini yenu kuliko wengine ndani ya nchi......ni ukweli usiofichika kuwa mna ajenda za kimkakati kuhakikisha mnachukua hatamu ya kidola ili mtimize matakwa yenu, jambo hilo ndilo linawatia hofu watanzania wengi wenye kuwatizama kwa jicho la tatu.

Tambueni ya kwamba taifa hili lina wananchi wengi Wa imani tofauti tofauti nanyi sio special kuliko wao na ni asili ya imani zao tu kutokulalama ndio maana kuna mambo mnayalazimisha hamuwaoni wakiwajibia bali wanawatizama tu muendelee na mikakati yenu kwani kufanikiwa kwayo ni kazi isiyo nyepesi.
 
Hakika!
Na kweli, penye ukweli uongo hujitenga. Mnakasha huu uliwafungua wengi macho na nawapa asante nyingi wote mlioshiriki kutoka pande zote...hii nayo itabaki kuwa historia iliyoandikwa na wengi hapa jamvini, JF idumu! Mungu awabariki!
 
Mimi ni Wa kike, napenda kukusahihisha hapo kidogo.
Hakuna MTU anaepingana na historia ya kweli hata kidogo tena unatupatia fursa ya kujifunza mengi ambayo hatukupata kuyasoma mashuleni, unachopingwa hapa Mzee Mohammed Said na maandiko yako kuyaelekeza zaidi katika dini yako na hisia nyingi ambazo hazina usahihi ya kwamba watu Wa dini yako wanakandamizwa, wakati huo uovu unaotendwa na viongozi madhara huwafikia watanzania wote bila kujali dini zao.......
Mnatoa wapi hizo hisia hasi?
Avriel,
Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika haiko kama hivyo unavyotamani wewe iwe.

Historia ya TANU mimi naijua vizuri sana kwa kuwa waasisi wake mimi ni wazee wangu.

Nilipoona imeandikwa sivyo ndipo niliponyanyua kalamu na kuandika kusahihisha historia hiyo iliyokuwapo.

Hebu soma kipande hiki hapo chini nimemuandikia kijana mmoja leo asubuhi.

Soma na unifahamishe kama historia hii inafanana hata kwa mbali na historia ya TANU na uhuru unayoijua wewe:

"Napenda kuchangia kidogo niyajuayo kuhusu Chief David Kidaha Makwaia.

Kwanza mimi nilipata bahati ya kukutana na Chief Kidaha hapa Dar es Salaam
mwaka wa 1968.

Mwanae Edward Makwaia nilikuwa nasomanae darasa moja St. Josephs Convent School basi siku moja akaniambia kuwa baba yake amekuja kutoka Nairobi kwa hiyo nimsindikize kwenda kumwamkia.

Hivi ndivyo nilivyobahatika kumuona Chief Kidaha.

Lakini wakati ule mimi mtoto sikuwa najua kwa nini Chief Kidaha alikuwa anaishi
Kenya.

Chief Kidaha baada ya uhuru aliwekwa kizuizini Tunduru kupitia Preventive Dentition Act ya 1962 na baada ya kutoka aliamua kuhama nchi na kwenda Kenya.

Chief Kidaha Kidaha ni mtoto wa Chief Makwaia Mohamed Mwandu wa Busiya.

1566962505965-png.1191693

mohamedsaidsalum.blogspot.com
CHIEF EDWARD ANTHONY MAKWAIA WA BUSIYA
Chief Makwaia Mohamed Mwandu Nimeona tangazo la Busiya Chiefdom katika mitandao ya kijamii na nikaangalia, ‘’clip,’’ yake. Hili ni ta...
mohamedsaidsalum.blogspot.com mohamedsaidsalum.blogspot.com

Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes katika miaka ya 1980s nilikutana na Chief Kidaha Makwaia kwenye Nyaraka za Sykes kupitia barua aliyoandika Dr. Wilbard Mwanjisi.

Dr. Mwanjisi alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanganyika African Government Servant
Association (TAGSA) mwaka wa 1951 aliandika makala kali sana katika jarida la chama, makala ambayo aliwashambulia Waingereza kiasi Rashid Kawawa akiwa mwanakamati wa Halmashauri Kuu ya TAGSA aliandika barua kuonya kuwa makala hiyo isichapwe bila ya kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya TAGSA.

Katika makala hii Dr. Mwanjisi aliitaja hotuba ya Chief Kidaha Makwaia ndania ya LEGCO kuwa ni hotuba muhimu sana na akamsifia Chief Kidaha Makwaia kuwa ni mwanasiasa makini wa kupigiwa mfano (‘Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA’ 22 nd December, 1951(Sykes' Papers),

Katika hotuba hiyo Chief Kidaha alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha na siasa.

Kitu ''interesting,'' katika kipindi hiki ni kuwa Chief Kidaha alikuwa na mazungumzo na Katibu wa TAA, Abdul Sykes, mazungumzo haya yakifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes, Abdul akijaribu kumshawishi Chief Kidaha aingie TAA ili wamchague kama Rais kisha waunde TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Mazungumzo haya hayakufanikiwa.

Baada ya uhuru Dr. Mwanjisi na yeye aliwekwa kizuizini na kama alivyofanya Chief Kidaha baada ya kutoka kizuizini alikwenda kuishi Kenya.

Na bahati mbaya sana waandishi wa historia ya TANU hawakutaka kufanya mahojiano yoyote na marehemu Ally Sykes katika historia ya TANU na kwa hili historia iliyokuja kuandikwa ikakosa mengi muhimu katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii ndiyo sababu Chief Kidaha Makwaia haonekani kokote katika historia ya kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Ningependa kuhitimisha kwa kueleza kuwa baada ya kutawazwa kwa Malkia Elizabeth, uongozi wa TAA ulituma salamu za pongezi kwa Malkia kwa kutawazwa kwake barua ya pongezi ilitiwa sahihi na Rais wa TAA Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi Budohi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes."

Bwana Avriel,

Hii ndiyo historia ya TANU na nimezishika nyaraka hizo kwa mikono yangu na nimezisoma kwa macho yangu nazijua fika kama primary source zilizonisaidia kuandika historia hii.

Soma kitabu cha Abdul Sykes ndani kuna mengi yatakayokushangaza.

Hayo hapo juu ni Waingereza wanasema, "tip of the ice berg," yaani ni kitu kiduchu na ni kidogo sana.

Haifai mtu kunga'nga'nia ujinga wakati elimu ya kujifunza ukawa mwerevu ipo na ya bure.

Mimi hapa natoa elimu, darsa la historia bila khiyana bure kabisa sitozi senti moja.

Vyuo Vikuu Marekani na kwingi duniani huniita kwa gharama zao kusomesha hii historia wenyewe wanaita, "corrective history."
 
Sajosojo,
Hukuweka hizo ''prejudice,'' na nilijua hutaweza sasa umekuja na mengine.

Hofu yako kama ni Uislam nakuwekea hapo chini makala tatu zinazoeleza vipi dini (ukipenda Uislam) ulivyowaunganisha Watanganyika katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika:
  1. https://www.jamiiforums.com/threads...mu-julius-nyerere-dar-es-salaam-1952.1565401/
  2. https://www.jamiiforums.com/threads...-kuundwa-kwa-tanu-1954.1565864/#post-30901522
Usifanye haraka ya kutaka kunijibu soma ujifunze historia na hali ya siasa ilivyokuwa Dar es Salaam ya miaka ile kuanzia 1929 Kleist na wenzake walipounda African Association hadi 1950s wanae Abdul na Ally walipoingia katika uongozi wa TAA tena kwa kuwapindua wazee wao wakiongozwa na Thomas Saudtz Plantan aliyekuwa rais wa TAA wakati ule.

Usitishike na historia hii wewe jiulize kwa nini wakati hawa vijana wanachukua uongozi mwaka wa 1950 waliona lazima waunde TAA Political Subcommittee na katika wajumbe wa kamati hiyo wawepo Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, John Rupia, Steven Mhando, Hamza Mwapachu na Abdul Sykes?

Mapadri walikuwapo jiulize kipi kiliwazuia wao kujitokeza mbele kupambana na Waingereza?

Jiulize pia kwa nini Kenya walikuwa Wakikuyu peke yao ndiyo walionyanyua silaha kupigana
na Waingereza?

Lazima ipo sababu.
Kutaka kujua matukio kama haya ndiyo usomi.
Ni kweli masheikh na maustadhi walisaidia taifa kwa kupigania Uhuru na mapadri na wachungaji hawakufanya hivyo....
Tueleze sasa tufanyeje juu yao?
Watu wabadili imani waingie kwa masheikh?
Tunawashukuru waarabu walioleta utamaduni wao kwetu tukapata imani ya dini wakapatikana wananchi Wa imani hiyo waliopigania Uhuru na historia ikaandikwa nao wakamchagua mzanaki kutoka butiama kuongoza taifa kwa niaba yao...
Asanteni sana sasa ni taifa huru kabisa.
 
Avriel,
Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika haiko kama hivyo unavyotamani wewe iwe.

Historia ya TANU mimi naijua vizuri sana kwa kuwa waasisi wake mimi ni wazee wangu.

Nilipoona imeandikwa sivyo ndipo niliponyanyua kalamu na kuandika kusahihisha historia hiyo iliyokuwapo.

Hebu soma kipande hiki hapo chini nimemuandikia kijana mmoja leo asubuhi.

Soma na unifahamishe kama historia hii inafanana hata kwa mbali na historia ya TANU na uhuru unayoijua wewe:

"Napenda kuchangia kidogo niyajuayo kuhusu Chief David Kidaha Makwaia.

Kwanza mimi nilipata bahati ya kukutana na Chief Kidaha hapa Dar es Salaam
mwaka wa 1968.

Mwanae Edward Makwaia nilikuwa nasomanae darasa moja St. Josephs Convent School basi siku moja akaniambia kuwa baba yake amekuja kutoka Nairobi kwa hiyo nimsindikize kwenda kumwamkia.

Hivi ndivyo nilivyobahatika kumuona Chief Kidaha.

Lakini wakati ule mimi mtoto sikuwa najua kwa nini Chief Kidaha alikuwa anaishi
Kenya.

Chief Kidaha baada ya uhuru aliwekwa kizuizini Tunduru kupitia Preventive Dentition Act ya 1962 na baada ya kutoka aliamua kuhama nchi na kwenda Kenya.

Chief Kidaha Kidaha ni mtoto wa Chief Makwaia Mohamed Mwandu wa Busiya.

1566962505965-png.1191693

mohamedsaidsalum.blogspot.com
CHIEF EDWARD ANTHONY MAKWAIA WA BUSIYA
Chief Makwaia Mohamed Mwandu Nimeona tangazo la Busiya Chiefdom katika mitandao ya kijamii na nikaangalia, ‘’clip,’’ yake. Hili ni ta...
mohamedsaidsalum.blogspot.com mohamedsaidsalum.blogspot.com

Wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes katika miaka ya 1980s nilikutana na Chief Kidaha Makwaia kwenye Nyaraka za Sykes kupitia barua aliyoandika Dr. Wilbard Mwanjisi.

Dr. Mwanjisi alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanganyika African Government Servant
Association (TAGSA) mwaka wa 1951 aliandika makala kali sana katika jarida la chama, makala ambayo aliwashambulia Waingereza kiasi Rashid Kawawa akiwa mwanakamati wa Halmashauri Kuu ya TAGSA aliandika barua kuonya kuwa makala hiyo isichapwe bila ya kujadiliwa na Halmashauri Kuu ya TAGSA.

Katika makala hii Dr. Mwanjisi aliitaja hotuba ya Chief Kidaha Makwaia ndania ya LEGCO kuwa ni hotuba muhimu sana na akamsifia Chief Kidaha Makwaia kuwa ni mwanasiasa makini wa kupigiwa mfano (‘Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA’ 22 nd December, 1951(Sykes' Papers),

Katika hotuba hiyo Chief Kidaha alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha na siasa.

Kitu ''interesting,'' katika kipindi hiki ni kuwa Chief Kidaha alikuwa na mazungumzo na Katibu wa TAA, Abdul Sykes, mazungumzo haya yakifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes, Abdul akijaribu kumshawishi Chief Kidaha aingie TAA ili wamchague kama Rais kisha waunde TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Mazungumzo haya hayakufanikiwa.

Baada ya uhuru Dr. Mwanjisi na yeye aliwekwa kizuizini na kama alivyofanya Chief Kidaha baada ya kutoka kizuizini alikwenda kuishi Kenya.

Na bahati mbaya sana waandishi wa historia ya TANU hawakutaka kufanya mahojiano yoyote na marehemu Ally Sykes katika historia ya TANU na kwa hili historia iliyokuja kuandikwa ikakosa mengi muhimu katika harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hii ndiyo sababu Chief Kidaha Makwaia haonekani kokote katika historia ya kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Ningependa kuhitimisha kwa kueleza kuwa baada ya kutawazwa kwa Malkia Elizabeth, uongozi wa TAA ulituma salamu za pongezi kwa Malkia kwa kutawazwa kwake barua ya pongezi ilitiwa sahihi na Rais wa TAA Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi Budohi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes."

Bwana Avriel,

Hii ndiyo historia ya TANU na nimezishika nyaraka hizo kwa mikono yangu na nimezisoma kwa macho yangu nazijua fika kama primary source zilizonisaidia kuandika historia hii.

Soma kitabu cha Abdul Sykes ndani kuna mengi yatakayokushangaza.

Hayo hapo juu ni Waingereza wanasema, "tip of the ice berg," yaani ni kitu kiduchu na ni kidogo sana.

Haifai mtu kunga'nga'nia ujinga wakati elimu ya kujifunza ukawa mwerevu ipo na ya bure.

Mimi hapa natoa elimu, darsa la historia bila khiyana bure kabisa sitozi senti moja.

Vyuo Vikuu Marekani na kwingi duniani huniita kwa gharama zao kusomesha hii historia wenyewe wanaita, "corrective history."


"Katika hotuba hiyo Chief Kidaha alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha na siasa"
Kumbe hata mzungu alikataza wafanyakazi wasijishughulise na siasa!!! Hatari saaaana
 
Ni kweli masheikh na maustadhi walisaidia taifa kwa kupigania Uhuru na mapadri na wachungaji hawakufanya hivyo....
Tueleze sasa tufanyeje juu yao?
Watu wabadili imani waingie kwa masheikh?
Tunawashukuru waarabu walioleta utamaduni wao kwetu tukapata imani ya dini wakapatikana wananchi Wa imani hiyo waliopigania Uhuru na historia ikaandikwa nao wakamchagua mzanaki kutoka butiama kuongoza taifa kwa niaba yao...
Asanteni sana sasa ni taifa huru kabisa.
Avriel,
Unauliza ufanyeje kwani kuna mtu amekuambia ufanye jambo?
Wala hii historia haina uhusiano wowote na Waarabu.

Wala Tanganyika haikuwa huru leo.

Lakini kwa kuwa umetaja uhuru wa Tanganyika sasa nitakuambia
kwa mara nyingine tena.

Hakuna jamii inayoweza kukubali kufutiwa historia yake.

Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ilipoandikwa na Chuo
Cha CCM Kivukoni historia hii ilifuta mchango wa wazee wangu hiki
ndicho kilichosababisha mimi kunyanyua kalamu na kuandika historia
ya kweli ya TANU kama nilivyohadithiwa na wazee wangu na kwa
msaada wa nyaraka na picha.

Sasa wewe unauliza ufanyeje.
Jibu lako ni hili.

Unaposoma sisi tunawaadhimisha wazee wetu na kutukuza mchango
wao katika kupigania uhuru wa Tanganyika wewe kaa kimya kwa kuwa
huijui historia hiyo kwa hiyo huna sababu ya kutia neno lako kupinga
labda sana sana uliza maswali kwa yale ambayo hayako wazi kwako.

Wajaluo Kenya hawawashambulii wala hawaghadhibiki Wakikuyu
wanapomuadhimisha Dedan Kimathi na Mau Mau.

Sasa wewe usighadhibike unapomsoma Sheikh Hassan bin Ameir
katika historia ya TANU au unapomsoma Sheikh Suleiman Takadir
au Sheikh Yusuf Badi au Sheikh Abdallah Rashid Sembe.

Usighadhibike kwani hawa ndiyo waliokuwa bega kwa bega na Baba
wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
katika TAA kisha TANU
na kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
"Katika hotuba hiyo Chief Kidaha alikuwa anaishauri serikali ya Kiingereza kuondoa ile sheria ambayo ilikuwa inawapiga marufuku Waafrika wafanyakazi wa serikali kujishughulisha na siasa"
Kumbe hata mzungu alikataza wafanyakazi wasijishughulise na siasa!!! Hatari saaaana
Ndio maana tulidai uhuru toka kwa mkoloni ili tuwe uhuru...siyo tumtoe mkoloni mweupe tumwingize mkoloni mweusi!
 
Ndio maana tulidai uhuru toka kwa mkoloni ili tuwe uhuru...siyo tumtoe mkoloni mweupe tumwingize mkoloni mweusi!
Huu mnakasha ni adimu sana. Ndio maana napitia madini ya huyu babbu kila nipatapo wasaa. Tumetoka mbaaaali sana. Ila fikra zetu bado zinatawaliwa na mawazo ya wale tuliowang'oa
 
Dadi,
Upo ushahidi kuwa Waislam ndiyo wanaodhulumiwa kwa ajili ya dini yao na tuhuma hizi zinafahamika kwani si za leo.

Ukitaka ushahidi wa hili soma, ''Religion and Development,'' P van Bergen, Madras 1981, Sivalon J. ''Kanisa Katoliki...'' Peramiho 1992 na Hamza Njozi, ''Mwembechai Killings...'' 2002.

Kitabu cha Njozi kimepigwa marufuku ni kosa la jinai kuwanacho.

Labda kama mimi ni mdini na hao waandishi wengine ni wadini ni kule kulisemea tatizo hili la ubaguzi.
Mohamed,

Waislam siku zote lazima wahisi kuwa wanadhulumiwa kwa sababu:

1. Uislam sio dini tu, bali ni mfumo wa kisiasa pia. Uislam unataka ushike dola ndo ukamilike. Kama dola sio ya Kiislam Uislam hauwezi kukamilika. Kwa hiyo kwenye nchi yoyote ambayo Uislam haujashika dola, Waislam lazima watajiona wanaonewa.

2. Kudhani Quran ndo kila kitu. Kuna Waislam wengi wana mtazamo wa kwamba Quran ndo kila kitu. Kwamba ina elimu yote inayotakiwa kwa binadamu kuweza kuishi na kufanikiwa. Hili linawaletea ufukara Waislam wengi maana wanapitwa na elimu bora zaidi ambazo zingeweza kuwasaidia kwenye maisha yao. Hili huwa ni tatizo zaidi pale ambapo elimu mpya inapokinzana na Quran.
 
Mohamed,

Waislam siku zote lazima wahisi kuwa wanadhulumiwa kwa sababu:

1. Uislam sio dini tu, bali ni mfumo wa kisiasa pia. Uislam unataka ushike dola ndo ukamilike. Kama dola sio ya Kiislam Uislam hauwezi kukamilika. Kwa hiyo kwenye nchi yoyote ambayo Uislam haujashika dola, Waislam lazima watajiona wanaonewa.

2. Kudhani Quran ndo kila kitu. Kuna Waislam wengi wana mtazamo wa kwamba Quran ndo kila kitu. Kwamba ina elimu yote inayotakiwa kwa binadamu kuweza kuishi na kufanikiwa. Hili linawaletea ufukara Waislam wengi maana wanapitwa na elimu bora zaidi ambazo zingeweza kuwasaidia kwenye maisha yao. Hili huwa ni tatizo zaidi pale ambapo elimu mpya inapokinzana na Quran.
Dadi...
Hapana hulifahamu tatizo hiki si kitu ambacho wewe unaweza ukafanya mjadala wa maana.

Inataka kwanza uisome historia ya Tanganyika kabla na baada ya uhuru ndipo utaelewa tatizo lenyewe.

Serikali inatambua tatizo hili.
 
Dadi...
Hapana hulifahamu tatizo hiki si kitu ambacho wewe unaweza ukafanya mjadala wa maana.

Inataka kwanza uisome historia ya Tanganyika kabla na baada ya uhuru ndipo utaelewa tatizo lenyewe.

Serikali inatambua tatizo hili.

Hamna kitu kama hicho. Fanya toba umrejee mola wako salama. Usitake kutuharibia amani nchini mwetu kwa propaganda za kipuuzi.
 
Mohamed Said anataka tuiamini zaidi Historia isiyoandikiwa, hadithi alizosimuliwa zaidi na wazee wake, ni vigumu sana kuiamini Historia ya aina hiyo hata kama kuna ukweli fulani kwenye maelezo yake ya Historia na kasoro nyingi kwenye Historia yenye mkono wa TANU.
 
Mohamed Said anataka tuiamini zaidi Historia isiyoandikiwa, hadithi alizosimuliwa zaidi na wazee wake, ni vigumu sana kuiamini Historia ya aina hiyo hata kama kuna ukweli fulani kwenye maelezo yake ya Historia na kasoro nyingi kwenye Historia yenye mkono wa TANU.
Hukumsikia nyerere alichoeleza aliongea na wazee wa dar,kwamba wengi walikua waislam,mkiristu yeye na rupia tu,na Mara moja moja Nani sijui
 
Basi leteni ya ukweli bila chenga

Hivi walioandika kuwa red indians waliuwawa na nchi yote kuchukuliwa au Aborigines wa Australia kumalizwa
Halafu wakaja watoto wasooijua historia wakasema ilikuwa ya kutunga hamjui wengi wataamini kweli walitunga?

Hata leo kuna watu hawaamini kama vita ya kwanza na ya pili iliwahi kutokea unabisha Google

Wengine wanabisha kuwa holocaust haikutolea na hakuna wayahudi waliuwawa

Kila mmoja aamini anachoamini maana wengine wamezaliwa juzi juzi na dini wanazikataa pia kutwa unaambiwa leta ushahidi
 
Mohamed Said anataka tuiamini zaidi Historia isiyoandikiwa, hadithi alizosimuliwa zaidi na wazee wake, ni vigumu sana kuiamini Historia ya aina hiyo hata kama kuna ukweli fulani kwenye maelezo yake ya Historia na kasoro nyingi kwenye Historia yenye mkono wa TANU.
Huyu mzee amejaa hila na ni tapeli mkubwa! Binafsi namchukulia kama mhalifu ngazi za kina Osama
 
Huyu mzee amejaa hila na ni tapeli mkubwa! Binafsi namchukulia kama mhalifu ngazi za kina Osama
Mzizi...
Kuna ibra moja kubwa sana katika historia hii.

Kuna wanaonisikiliza nikilimaza wakati wa maswali huonyesha mshangao kuwa imekuwaje historia ya ukombozi wa nchi ikabadilishwa (doctored) na ikawekwa historia nyingine ambayo kwa miaka mingi ikawa inasomeshwa shuleni na vyuoni?

Mimi hutoa majibu.

Lakini wapo wengi kutoka hapa nyumbani historia hii huwatia ghadhabu kiasi hutoa matusi, vitisho na kusema maneno yasiyopendeza.

Mara ya kwanza mwaka wa 1988 gazeti la Africa Events (London) lilipochapa makala yangu ''In Praise of Ancestors,'' ambayo ndani nilimtaja Abdul Sykes, Ally Sykes, John Rupia, Saadan Abdu Kandoro na Al Jamiatul Islamiyya katika harakati za TANU toleo zima la gazeti lilikusanywa.

Toleo lililofuatia ikachapwa makala kutoka kwa Dr. Mayanja Kiwanuka wa CCM Dodoma iliyojaa kebehi na vitisho dhidi yangu.

Alihitimisha kwa kunitukana na kuniita ''pygmy.''

Matusi, kejeli na vitisho yote nimeyakusanya kwa kipindi cha miaka 20 na In Shaa Allah iko siku tutayachapa hapa barzani.

Mzizi...ananiita ''tapeli mkubwa,'' ''mhalifu.''
Akili imemruka anatoa matusi na haya ni kawaida kwa mtu aliyeghadhibika.

Hawezi kufikiri hadi atulie na akili yake irejee.
Hujiuliza kwa nini wanakasikrika kwa mimi kuandika historia ya wazee wangu?

Nini kinawachoma?
Wangependa kama historia hii nisingeiandika na tukawa na historia ambayo haina ukweli?

Hiki ndicho kiichokusudiwa mwanzo walipofuta historia ya kweli ya TANU na kupachika nyingine?

Sasa historia ya kweli ipo.
Tufanyeje?

1648564917793.png
 
Back
Top Bottom