Hitimisho langu juu ya swali la Mungu na Atheists

Hitimisho langu juu ya swali la Mungu na Atheists

JumaKilumbi

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2022
Posts
432
Reaction score
507
Katika uzi nilioufungua jukwaani hapa nilioutumia kuwaalika Atheists kuleta hoja za kuthibitisha kuwa Mungu hayupo ili tujifunze kuhusu misingi yao, wachache hawakunielewa kwa kudhani nilitaka mabishano, ila nimepata hitimisho lifuatalo
  1. Baadhi ya Atheists wanashindwa kuelewa Mungu huyu (kama atajavyo na Quran na Biblia) anawezaje kuwepo wakati sifa zake zinajikanganya. Mfano kuwa na hasira na kuwa na huruma, kuwa muweza wa vyote n.k
  2. Atheists hawana maelezo mbadala yanayokubalika juu ya asili ya Dunia hii na UIlimwengu kwa ujumla.

  3. Atheists baadhi wanatatizwa na uwepo wa matatizo hapa Duniani, hivyo wanaona Mungu muweza wa vyote hayupo. Kwa maana angekuwepo angeyaondoa haya matatizo
  4. Baadhi hawana uhakika juu ya uwepo wa Mungu wanataka kumjua zaidi lakini si kwa kupitia hizi ‘mainstream religion’ kwa maana kwao wanaona ni uzushi.
  5. Baadhi wamechanganyikiwa, wanashindwa kuielewa hata kidogo dhana ya Mungu.
  6. Atheists wengi wako ‘on offensive’ wanashambulia hoja za Waumini na unapowaweka mazingira ya kuwalazimu kuthibitisha hoja zao inakuwa mtihani.
  7. Atheists wengi hupata chochote cha kusema kwa kushambulia hoja za waumini Dini wengi wao hawana hoja ukiacha kushambulia za waumini Dini.
  8. Wachache sana ni wakweli, na wana fikra huru.
Dini za Kumfuata Ibrahimu, UHindu, na Ubudha kwa uchache zimekuwa na mchango mkubwa sana ktk kuijenga jamii kama tuionavyo leo, lakini hilo haliondoi ukweli kuwa Dini hizi hizi pia zilichangia kuleta maafa makubwa kwa wanaadamu, lakini faida zake kijamii ni nyingi kuliko maafa yake.

HITIMISHO LANGU;
Awali nilidhani Atheists wana hoja za kusikiliza linapokuja suala la Mungu, lakini nimegundua wao wamejawa mashaka, hawana majibu ila maswali ambayo wanayakataa majibu yake, wengi wanakariri hoja na hawako tayari kupokea mabadiliko.

Hivyo basi, ninaamini Mungu yupo kwa mujibu wa Quran aliyoletewa Muhammad (PBUH)

Nimalize kwa nukuu ya Profesa nguli Jordan B. Peterson
“You can only find out what you actually believe (rather than what you think you believe) by watching how you act. You simply don’t know what you believe, before that. You are too complex to understand yourself.”
Jordan B. Peterson
 
Nmeshindwa kumthibitisha huyo Mungu katika hali halisia na hata yeye hana shida ya Kujidhihilisha dhahili,
ila kutwa machawa wa huyo Mungu mnateseka kutaka kutuamisha vitu ambavyo hata nyie hamna ushahidi navyo zaidi ya hekaya na blaa blaa za kale tu.

Nmepigwa chenga za mwili na akili juu ya origin of life mnataka kurahisisha mambo magumu kujibiwa na maswali mepesi,

Mungu ni nadharia tu isiyo katika uhalisia na huna ushahidi wenye ithibati kumthibitisha

Alamsiki
 
Ninachoona hapa dini peke yake hazitoshi kupruv kuwa mungu yupo. Kutokuwepo Kwa pruv ya mungu haimaanish kuwa hayupo. Spirits zinakuwa na utata zinapokutana na sayansi ya Empirical. Dini ni kitu ambacho empirically hakifikiki. Mm nafikiri, kama sayansi yenyew imewekwa matatani na matumiz ya MAGIC (Occults) na kuonyesha kwamba Kuna vitu can not be touchable or seen. God may be there. Matatizo tunayoyaona kama umaskini, ulevi, umalaya na uuaji yanasababisha na vitu vingine kabisa "beyond of what we perceive as normal". Kuna mfumo tunaoish nao ukibadilika hayo matatizo / dhambi hitaziona tena.
 
Ninachoona hapa dini peke yake hazitoshi kupruv kuwa mungu yupo. Kutokuwepo Kwa pruv ya mungu haimaanish kuwa hayupo. Spirits zinakuwa na utata zinapokutana na sayansi ya Empirical. Dini ni kitu ambacho empirically hakifikiki. Mm nafikiri, kama sayansi yenyew imewekwa matatani na matumiz ya MAGIC (Occults) na kuonyesha kwamba Kuna vitu can not be touchable or seen. God may be there. Matatizo tunayoyaona kama umaskini, ulevi, umalaya na uuaji yanasababisha na vitu vingine kabisa "beyond of what we perceive as normal". Kuna mfumo tunaoish nao ukibadilika hayo matatizo / dhambi hitaziona tena
Nakubaliana nawe mia fil’ mia Mkuu.
Jambo hili linahitaji umakini kuliendea na si kuleta mchezo wa maneno.
 
Nmeshindwa kumthibitisha huyo Mungu katika hali halisia na hata yeye hana shida ya Kujidhihilisha dhahili,
ila kutwa machawa wa huyo Mungu mnateseka kutaka kutuamisha vitu ambavyo hata nyie hamna ushahidi navyo zaidi ya hekaya na blaa blaa za kale tu.

Nmepigwa chenga za mwili na akili juu ya origin of life mnataka kurahisisha mambo magumu kujibiwa na maswali mepesi,

Mungu ni nadharia tu isiyo katika uhalisia na huna ushahidi wenye ithibati kumthibitisha

Alamsiki
Vizuri, bahati mbaya kwako hauna hoja ya kuthibitisha hayupo.
 
Hutumika hivyo siku hizi, lakini wazo lenyewe la dini halina ubaya.
Labda kama huijui historia ya dini mkuu. Tokea kuanza kwake dini ilikuwa na lengo la kupumbaza akili za watu na ilitumika kama zana ya kitawala.

Ili uweze kutawala watu waendee kwanza na dini na vitisho vingi ambavyo ni vyakufikirika.

Kuna jamaa hapo juu amesema 'religion creates fear'. Na hilo ndio kusudio kubwa la dini. Ili wawezw kuwatawala lazima wawatishe kwanza.
 
Labda kama huijui historia ya dini mkuu. Tokea kuanza kwake dini ilikuwa na lengo la kupumbaza akili za watu na ilitumika kama zana ya kitawala.

Ili uweze kutawala watu waendee kwanza na dini na vitisho vingi ambavyo ni vyakufikirika.

Kuna jamaa hapo juu amesema 'religion creates fear'. Na hilo ndio kusudio kubwa la dini. Ili wawezw kuwatawala lazima wawatishe kwanza.
Sipingi kuwa dini huleta hofu,
Sipingi kuwa dini ilitumika kama silaha ya utawala,

Huo ni ukweli ambao nadhani unafahamika.

Wakati tunaeleza hayo tusisahau dini zina nafasi gani kwenye maisha yetu wanaadamu, tangu tumeanza kustaarabika.
 
Mtoa mada yupo brainwashed, hayuko tayari kuwaza kwa kina. Mtu kama huyu ni ngumu ku jadili kwa kuwa tayari ana majibu.

Waislamu wanakuwa brainwashed wakiwa wadogo sana.

Kama unataka kujadili theists na atheists ni lazima uwe open minded.
 
Sipingi kuwa dini huleta hofu,
Sipingi kuwa dini ilitumika kama silaha ya utawala,

Huo ni ukweli ambao nadhani unafahamika.

Wakati tunaeleza hayo tusisahau dini zina nafasi gani kwenye maisha yetu wanaadamu, tangu tumeanza kustaarabika.
Nafasi ya dini sio hoja kubwa na ya msingi. Bali kushindwa ku prove uwepo wa Mungu ndio kunafanya watu wasiamini hizo dini.
 
Back
Top Bottom