Hitimisho: Mkataba wa Tanzania na Emirati ya Dubai kupitia DP World tumeukataa!

Hitimisho: Mkataba wa Tanzania na Emirati ya Dubai kupitia DP World tumeukataa!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Watanzania tumezungumza. Tumezungumza kwa kauli zetu kalikali kama msumari na waziwazi kuliko utandawazi. Tumezungumza kupitia Wanasheria, Maprofesa, Maaskofu, Masheikh, Wanasiasa, Wasomi hadi wananchi wa kawaida. Tumeuzungumza mkataba wa DP World kuliko hata Bunge letu.

Tumeuzungumza makataba kwa kuukosoa-kulingana na vifungu vyake. Tumepuuza hoja zisizo na haja za viongozi wa kiserikali na kichama waliojaribu kututoa kwenye hoja. Tumewapuuza kwa kuendelea kutetea tunachokiamini na tulichokiona kimkataba.

Najua kuwa Serikalini na chamani anasakwa 'mchawi' wa jambo lote hili. Yule aliyetuwekea wazi Mkataba wa DP World na Tanzania juu ya Bandari. Ilipangwa jambo hili lifanywe kimyakimya. Liiishe kimyakimya. Baada ya kubumburuka na kuanza kujadiliwa, tunaambiwa kuwa tunatoa maoni na yatazingatiwa. Inashangaza!

Hadi sasa, pamoja na ukimya wa Rais na Mwenyekiti wetu wa CCM juu ya hili, hakuna kiongozi yeyote wa Serikali au CCM aliyajibu hoja za haja za wakosoaji wa mkataba. Nguvu kubwa imeelekezwa kwenye kuuaminisha umma kuwa uwekezaji Bandarini utaleta tija. Hoja zetu ni juu ya ubovu na ubatili wa mkataba. Hizo hazina majibu.

Ni rahisi kuhitimisha bila kutisha kuwa Mkataba wa DP World tumeukataa. Na mambo yake yote tumeyakataa. Kukosekana kwa ukomo na maslahi ya kimkataba tumekukataa. Maelezo ya Serikali na viongozi wa CCM tumeyakataa. Tunasubiri tupuuzwe sauti zetu ili tuchukue hatua zetu!

Rais na Mwenyekiti wangu Mama Samia, huna lolote juu ya Mkataba wa DP World la kutuambia?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Igoma, Mwanza)
 
Tunaukatalia mkataba wa DP World kwenye key boards. Tutoke front na mabango. Thubutuuu. Ila nchi nzima ikihamasishwa inawezekana. Ila Tanzania Sisi makondoo tunapitusha tu hata kama si Sawa. Hii ya DP World ingekuwa ni Zanzibar usingeruhusiwa huu mkataba. Ninakuhakikishia Wazanzibari Wana uchungu na Mali zao kuliko Sisi na ndiyo maana imekuwa Rahisi kutuuza Sisi makondoo.
 
Kwa uchungu huu Hii nchi haitokuja kaa salama.. serikali wameziba masikio wameona mbwai mbwai tu kufanya unyambilisi kwa Watanganyika.. nadhani ifike zamu ujumbe ufike Dunia nzima kuwa Mfalme wa Dubai kumbe ni jambazi
 
Mpaka kieleweke.

Nafikiri utakuwa ni wakati muafaka kusema sha sha basi. Hakuna haja ya CCM wala Serikali yake kurudi mezani.

Turudishieni Bandari yetu sisi Watanganyika


CCM must go. Afresher CCM inahitajika, enyi wa sasa Pumzikeni, Kaeni pembeni, mjitafakari na kujitathmini.
 
Bahati mbaya huu mkabata maza hajausoma hata page moja na yeye anausikia kama sisi tu ndiyo maana amekaa kimya hajui hata kinachoendelea
Yale ya Zakhia Megji yamejirudia tena.

Yule mama akiwa waziri wa fedha ulisainiwa mkataba mmoja wa hovyo alipobanwa bungeni akadai hata yeye haufahamu vizuri maana hakuusoma kwakua alipokua anatoka ofisini alikimbiziwa mkataba kwenye gari akausaini tu bila hata kusoma.

Hivyo unachosema siajabu hata kwa situation hii it is more likely the same.
 
Hadi sasa, pamoja na ukimya wa Rais na Mwenyekiti wetu wa CCM juu ya hili,
Ukimya nao ni jibu!.
hakuna kiongozi yeyote wa Serikali au CCM aliyajibu hoja za haja za wakosoaji wa mkataba.
Hoja karibu zote zimejibiwa
Nguvu kubwa imeelekezwa kwenye kuuaminisha umma kuwa uwekezaji Bandarini utaleta tija.
Ni kweli uwezaji wa DPW, utaleta tija.
Hoja zetu ni juu ya ubovu na ubatili wa mkataba. Hizo hazina majibu.
It's true hoja za ubatili hazina majibu, ila hata kama kuna ubatili, IGA sio mkataba ni MoU tuu ya makubaliano kuiruhusu Tanzania kuingia mkataba na DPW. Mkataba ni HGA, utakuwa mzuri, japo kisheria, kukiisha tokea issues za ubatili, then ubatili huo unakuwa void ab initio, ila sisi huu ubatili wa mkataba huu tumeufanya kuwa ni ubatili wa voidable ambao unarekebishika.
Ni rahisi kuhitimisha bila kutisha kuwa Mkataba wa DP World tumeukataa.
Maadam wawakilishi rasmi wa Watanzania ni Bunge letu Tukufu, kama Bunge letu limeridhia, ni Watanzania tumeridhia.

Mfumo wetu wa utawala ni kupitia representation, Bunge letu ndio wawakilishi wetu, wakisema ndio, ni ndio, wewe Mwananchi huwezi kusema sio!. Itakubidi usubirie miaka 5, umfute kazi mwakilishi wako!.

Kilicho ridhiwa ni IGA, ni MoU ya makubaliano kuiruhusu Tanzania kuingia mkataba na DPW kutuendeshea Bandari zetu. Mkataba wa uendeshaji unaitwa HGA, hii HGA bado haijaingiwa, serikali yetu imepokea maoni ya Watanzania na itayajumuisha kwenye HGA, hivyo HGA itakuwa ni nzuri.
Na mambo yake yote tumeyakataa.
Sii kweli, sii yote, kuna mambo mengi, makubwa mazuri ya mkataba huu tumeyakubali, na machache mabaya wananchi tumeyakataa ila wawakilishi wetu, wabunge wetu na Bunge letu limekubali kila kitu.
Kukosekana kwa ukomo na maslahi ya kimkataba tumekukataa.
Ukomo hauwepogi kwenye international treaties!, IGA ni MoU tuu sio mkataba, ukomo utakuwepo kwenye HGA ambayo ndio mkataba.
Maelezo ya Serikali na viongozi wa CCM tumeyakataa.
Mfumo wetu wa utawala ni spoon fed top down, serikali ikisema ni imesema, wewe Mwananchi huwezi kuikatalia.
Tunasubiri tupuuzwe sauti zetu ili tuchukue hatua zetu!
Hata tukipuuzwa hatuwezi kuchukua hatua zozote zaidi ya kusubiria 2025 tuiadhibu CCM kwa kui vote out!. Hili pia haliwezekani kwasababu hata tukii vote out CCM, aje nani?, kwa vile hakuna mtu mbadala wa kuja, then tutaendelea na CCM mpaka atakapopatikana mbadala.
Rais na Mwenyekiti wangu Mama Samia, huna lolote juu ya Mkataba wa DP World la kutuambia?
Mama anatakiwa kunyamaza kimya kabisa huku kazi nzuri ikiendelea.

P
 
Yale ya Zakhia Megji yamejirudia tena.

Yule mama akiwa waziri wa fedha ulisainiwa mkataba mmoja wa hovyo alipobanwa bungeni akadai hata yeye haufahamu vizuri maana hakuusoma kwakua alipokua anatoka ofisini alikimbiziwa mkataba kwenye gari akausaini tu bila hata kusoma.

Hivyo unachosema siajabu hata kwa situation hii it is more likely the same.
Wewe mkuu mama wa kizanzabar anaweza kukaa kusoma word by word kabisa? hata Waziri mwenyewe alionyeshwa pakusaini maisha yakaenda hajausoma
 
Maadam wawakilishi rasmi wa Watanzania ni Bunge letu Tukufu, kama Bunge letu limeridhia, ni Watanzania tumeridhia.

Kilicho ridhiwa ni IGA, ni MoU ya makubaliano kuiruhusu Tanzania kuingia mkataba na DPW kutuendeshea Bandari zetu. Mkataba wa uendeshaji unaitwa HGA, hii HGA bado haijaingiwa, serikali yetu imepokea maoni ya Watanzania na itayajumuisha kwenye HGA, hivyo HGA itakuwa ni nzuri.
P
Siku zote mwenye nguvu ni muwakilishwa siyo muwakilishi ....inaelekea ulisomea ujinga kwenye sheria sijui kama unajua maana ya neno kuwakilisha ....pale muwakilishi anapo kwenda kinyume na muwakilishwa wewe unadhani ni nani mwenye nguvu. Muwakilishi mbunge anawakilisha kile alichotumwa na wananchi wake tu
 
Watanzania tumezungumza. Tumezungumza kwa kauli zetu kalikali kama msumari na waziwazi kuliko utandawazi. Tumezungumza kupitia Wanasheria, Maprofesa, Maaskofu, Masheikh, Wanasiasa, Wasomi hadi wananchi wa kawaida. Tumeuzungumza mkataba wa DP World kuliko hata Bunge letu.

Tumeuzungumza makataba kwa kuukosoa-kulingana na vifungu vyake. Tumepuuza hoja zisizo na haja za viongozi wa kiserikali na kichama waliojaribu kututoa kwenye hoja. Tumewapuuza kwa kuendelea kutetea tunachokiamini na tulichokiona kimkataba.

Najua kuwa Serikalini na chamani anasakwa 'mchawi' wa jambo lote hili. Yule aliyetuwekea wazi Mkataba wa DP World na Tanzania juu ya Bandari. Ilipangwa jambo hili lifanywe kimyakimya. Liiishe kimyakimya. Baada ya kubumburuka na kuanza kujadiliwa, tunaambiwa kuwa tunatoa maoni na yatazingatiwa. Inashangaza!

Hadi sasa, pamoja na ukimya wa Rais na Mwenyekiti wetu wa CCM juu ya hili, hakuna kiongozi yeyote wa Serikali au CCM aliyajibu hoja za haja za wakosoaji wa mkataba. Nguvu kubwa imeelekezwa kwenye kuuaminisha umma kuwa uwekezaji Bandarini utaleta tija. Hoja zetu ni juu ya ubovu na ubatili wa mkataba. Hizo hazina majibu.

Ni rahisi kuhitimisha bila kutisha kuwa Mkataba wa DP World tumeukataa. Na mambo yake yote tumeyakataa. Kukosekana kwa ukomo na maslahi ya kimkataba tumekukataa. Maelezo ya Serikali na viongozi wa CCM tumeyakataa. Tunasubiri tupuuzwe sauti zetu ili tuchukue hatua zetu!

Rais na Mwenyekiti wangu Mama Samia, huna lolote juu ya Mkataba wa DP World la kutuambia?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Igoma, Mwanza)
Mjinga mmja asiye hata na kibanda Cha kulipa Kodi anaongea upuuzi..

Umeukataa wewe na nani? Unajua hata biashara wewe nyumbu?
 
Mjinga mmja asiye hata na kibanda Cha kulipa Kodi anaongea upuuzi..

Umeukataa wewe na nani? Unajua hata biashara wewe nyumbu?
Wangefanya demonstration hata ya kutoka huko kwny maandamano wanayoyahamasisha Kila siku tungeona kwli wanamaanisha....lakini wanabaki kubwekea tu hmu mitandaoni....halafu wanaposema watanzania wameukataa...ni lini ilipigwa hata kura kusema asilimia kubwa hawataki.....kiongozi wa dini au mwanasiasa kusema hataki au anakubali kitu flani haimaanishi amewasilisha mawazo ya watu woote anaowaongoza....kama Wana uchungu saana waingie barabarani kilazima alaf tuone...sio kubwekabweka Kila siku hmu ndani thread mpya Kila dakika
 
Back
Top Bottom