Hitimisho: Mkataba wa Tanzania na Emirati ya Dubai kupitia DP World tumeukataa!

Hitimisho: Mkataba wa Tanzania na Emirati ya Dubai kupitia DP World tumeukataa!

Kwanini "wachache" wameamua kuulinda na kuupigania huu mkataba kwa nguvu zote bila kujali maoni ya wengi?
Nini kimejificha nyuma ya pazia hadi kutumia cheap labour kama; baba level, kitenge na hadi steave nyerere?
Mbona serikali imekosa hekima jamani kuna nini awamu hii? Haijiulizi kwanini "wenye ufahamu" wote wanaupinga?
 
Ukimya nao ni jibu!.

Hoja karibu zote zimejibiwa

Ni kweli uwezaji wa DPW, utaleta tija.

It's true hoja za ubatili hazina majibu, ila hata kama kuna ubatili, IGA sio mkataba ni MoU tuu ya makubaliano kuiruhusu Tanzania kuingia mkataba na DPW. Mkataba ni HGA, utakuwa mzuri, japo kisheria, kukiisha tokea issues za ubatili, then ubatili huo unakuwa void ab initio, ila sisi huu ubatili wa mkataba huu tumeufanya kuwa ni ubatili wa voidable ambao unarekebishika.

Maadam wawakilishi rasmi wa Watanzania ni Bunge letu Tukufu, kama Bunge letu limeridhia, ni Watanzania tumeridhia.

Mfumo wetu wa utawala ni kupitia representation, Bunge letu ndio wawakilishi wetu, wakisema ndio, ni ndio, wewe Mwananchi huwezi kusema sio!. Itakubidi usubirie miaka 5, umfute kazi mwakilishi wako!.

Kilicho ridhiwa ni IGA, ni MoU ya makubaliano kuiruhusu Tanzania kuingia mkataba na DPW kutuendeshea Bandari zetu. Mkataba wa uendeshaji unaitwa HGA, hii HGA bado haijaingiwa, serikali yetu imepokea maoni ya Watanzania na itayajumuisha kwenye HGA, hivyo HGA itakuwa ni nzuri.

Sii kweli, sii yote, kuna mambo mengi, makubwa mazuri ya mkataba huu tumeyakubali, na machache mabaya wananchi tumeyakataa ila wawakilishi wetu, wabunge wetu na Bunge letu limekubali kila kitu.

Ukomo hauwepogi kwenye international treaties!, IGA ni MoU tuu sio mkataba, ukomo utakuwepo kwenye HGA ambayo ndio mkataba.

Mfumo wetu wa utawala ni spoon fed top down, serikali ikisema ni imesema, wewe Mwananchi huwezi kuikatalia.

Hata tukipuuzwa hatuwezi kuchukua hatua zozote zaidi ya kusubiria 2025 tuiadhibu CCM kwa kui vote out!. Hili pia haliwezekani kwasababu hata tukii vote out CCM, aje nani?, kwa vile hakuna mtu mbadala wa kuja, then tutaendelea na CCM mpaka atakapopatikana mbadala.

Mama anatakiwa kunyamaza kimya kabisa huku kazi nzuri ikiendelea.

P
Kweli nimeamini Kaka yangu umezeeka... sio tena yule niliyekuwa namfahamu ana-host TV shows kali za hoja nzitonzito za MOTOMOTO.
 
Ila huyu Mama SSH hakuwa hivyo, nahisi kuna "kidudu mtu" mahali!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji115]wewe ni kichekesho tena unachekesha sana unajua kwanini samia anamchukia Nyerere kuliko Magufuli ???? Je unajua kwanini mtoto wa kiume wa karume wamemkalia kooni kule zanzibar [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] mimi nilicheka sana nilipo msikia na yule binti wa karume fatma karume ana mshabikia Samia nilisema moyoni kuwa kweli wanawake akili zao ni ndogo sana kung'amua mambo ....kwa kifupi sababu zinazo mfanya samia kumchukia nyerere ndiyo hizo hizo zinazo mfanya kumchukia Abeid karume
 
Samia ameshindwa kuongoza nchi, hajui yuko ikulu kuwatumikia watanganyika, yeye kwa ujinga wake anajiona ndie bosi wetu mwenye mamlaka ya kutufanyia vile atakavyo, hana akili wala hajielewi.
 
Watanzania tumezungumza. Tumezungumza kwa kauli zetu kalikali kama msumari na waziwazi kuliko utandawazi. Tumezungumza kupitia Wanasheria, Maprofesa, Maaskofu, Masheikh, Wanasiasa, Wasomi hadi wananchi wa kawaida. Tumeuzungumza mkataba wa DP World kuliko hata Bunge letu.

Tumeuzungumza makataba kwa kuukosoa-kulingana na vifungu vyake. Tumepuuza hoja zisizo na haja za viongozi wa kiserikali na kichama waliojaribu kututoa kwenye hoja. Tumewapuuza kwa kuendelea kutetea tunachokiamini na tulichokiona kimkataba.

Najua kuwa Serikalini na chamani anasakwa 'mchawi' wa jambo lote hili. Yule aliyetuwekea wazi Mkataba wa DP World na Tanzania juu ya Bandari. Ilipangwa jambo hili lifanywe kimyakimya. Liiishe kimyakimya. Baada ya kubumburuka na kuanza kujadiliwa, tunaambiwa kuwa tunatoa maoni na yatazingatiwa. Inashangaza!

Hadi sasa, pamoja na ukimya wa Rais na Mwenyekiti wetu wa CCM juu ya hili, hakuna kiongozi yeyote wa Serikali au CCM aliyajibu hoja za haja za wakosoaji wa mkataba. Nguvu kubwa imeelekezwa kwenye kuuaminisha umma kuwa uwekezaji Bandarini utaleta tija. Hoja zetu ni juu ya ubovu na ubatili wa mkataba. Hizo hazina majibu.

Ni rahisi kuhitimisha bila kutisha kuwa Mkataba wa DP World tumeukataa. Na mambo yake yote tumeyakataa. Kukosekana kwa ukomo na maslahi ya kimkataba tumekukataa. Maelezo ya Serikali na viongozi wa CCM tumeyakataa. Tunasubiri tupuuzwe sauti zetu ili tuchukue hatua zetu!

Rais na Mwenyekiti wangu Mama Samia, huna lolote juu ya Mkataba wa DP World la kutuambia?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Igoma, Mwanza)
Hii imeenda ,Hii imeenda kabisa.
 
Watanzania tumezungumza. Tumezungumza kwa kauli zetu kalikali kama msumari na waziwazi kuliko utandawazi. Tumezungumza kupitia Wanasheria, Maprofesa, Maaskofu, Masheikh, Wanasiasa, Wasomi hadi wananchi wa kawaida. Tumeuzungumza mkataba wa DP World kuliko hata Bunge letu.

Tumeuzungumza makataba kwa kuukosoa-kulingana na vifungu vyake. Tumepuuza hoja zisizo na haja za viongozi wa kiserikali na kichama waliojaribu kututoa kwenye hoja. Tumewapuuza kwa kuendelea kutetea tunachokiamini na tulichokiona kimkataba.

Najua kuwa Serikalini na chamani anasakwa 'mchawi' wa jambo lote hili. Yule aliyetuwekea wazi Mkataba wa DP World na Tanzania juu ya Bandari. Ilipangwa jambo hili lifanywe kimyakimya. Liiishe kimyakimya. Baada ya kubumburuka na kuanza kujadiliwa, tunaambiwa kuwa tunatoa maoni na yatazingatiwa. Inashangaza!

Hadi sasa, pamoja na ukimya wa Rais na Mwenyekiti wetu wa CCM juu ya hili, hakuna kiongozi yeyote wa Serikali au CCM aliyajibu hoja za haja za wakosoaji wa mkataba. Nguvu kubwa imeelekezwa kwenye kuuaminisha umma kuwa uwekezaji Bandarini utaleta tija. Hoja zetu ni juu ya ubovu na ubatili wa mkataba. Hizo hazina majibu.

Ni rahisi kuhitimisha bila kutisha kuwa Mkataba wa DP World tumeukataa. Na mambo yake yote tumeyakataa. Kukosekana kwa ukomo na maslahi ya kimkataba tumekukataa. Maelezo ya Serikali na viongozi wa CCM tumeyakataa. Tunasubiri tupuuzwe sauti zetu ili tuchukue hatua zetu!

Rais na Mwenyekiti wangu Mama Samia, huna lolote juu ya Mkataba wa DP World la kutuambia?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Igoma, Mwanza)
Sawa asa what next? Msitumi?
 
Maadam wawakilishi rasmi wa Watanzania ni Bunge letu Tukufu, kama Bunge letu limeridhia, ni Watanzania tumeridhia.
Wabunge hawa hawakuchaguliwa na wananchi, bali walipitishwa na wanaccm tu, kwasabb uchaguzi wa mwaka 2020 uliibiwa (hazikuibiwa kura, bali uliibiwa uchaguzi).

Ni ville tu watanzania ni watu wa hewala hewala, vinginevyo pangechimbika.
 
Mbona mapema kuukataa!! Mm na familia yangu pamoja na ukoo wangu tunataka bandari yetu tu.
Asante
 
Back
Top Bottom