Hivi Bongo tunasoma ili iweje?

Hivi Bongo tunasoma ili iweje?

Wakuu habari,

Hivii Tanzania tuna soma ili iweje.Mataifa yote duniani elimu inatumika kumkomboa mwananchi kutoka mazingira duni na kuyaboresha , kuyatawala mazingira na si mazingira kumtawala mwanadamu.

Hapa nyumbani tuna baadhi ya vyuo venye kozi mbali mbali ambazo kwa macho ya nyama unaona zina tija lakini katika hali halisi vijana wanalalamika ajira hamna.

Na Wakati ajira zikionekana amna kuna utitiri wa mazao na rasilimali zinazolishwa Tanzania na kuuzwa njee kama malighafi na si bidhaa, nashindwa kuelewa sasa kama tuna wanafunzi wanaograduate kila siku na still amna innovations zinazotokana na elimu hizo au adaptation ya teknolojia kutoka nje ili kuongeza thamani malighafi zetu za ndani na ziuzwe njee kama bidhaa kamili sasa tunasoma na kutoa ela ndefu kwenye mikopo ili iweje?

Tanzania inajikuta katika changamoto kubwa za elimu na ajira, huku vyuo vikuu vikitakiwa kuwa injini ya mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.

Hali hii inakinzana na dhima ya elimu duniani, ambayo ni kumkomboa mwananchi kutoka kwenye umaskini na kuboresha mazingira yake.

Vyuo vikuu nchini vinatoa kozi mbalimbali, lakini vijana wanalalamika kuhusu ukosefu wa ajira, wakati huo huo kuna utitiri wa malighafi zinazozalishwa Tanzania na kuuzwa nje kama malighafi tu, bila kuongeza thamani.

Kuna haja kubwa ya kubadilisha mfumo wa elimu ili kuchochea uvumbuzi na teknolojia, na kuongeza thamani ya malighafi za ndani ili ziuzwe nje kama bidhaa kamili.

Kutoa mikopo kwa wanafunzi ni hatua nzuri, lakini inapaswa kuelekezwa kwa njia ambayo itawawezesha kuanzisha miradi yao wenyewe na kuchangia katika maendeleo ya jamii.

Walimu wanapaswa kuwa mifano inayotoa mabadiliko ya kijamii, na elimu inayotolewa inapaswa kuhamasisha ujasiriamali na uvumbuzi.

Ni muhimu kuanzisha vituo vya uvumbuzi ndani ya vyuo vikuu ambavyo vitakuwa kazi yake kuvumbua majawabu ya changamoto za jamii kupitia wanafunzi wa taaluma husika.

Wanafunzi wanapaswa kupata fursa ya kutumia elimu yao kuleta mabadiliko katika jamii kwa kubuni suluhisho za changamoto za kitaifa na kimataifa.

Vyuo kama vile Chuo Kikuu cha Dodoma na Dar es Salaam vinaweza kuwa kiongozi katika kuleta mabadiliko ya kielimu na kijamii.

Elimu inapaswa kuwa chanzo cha tija na maendeleo, na wanafunzi wanapaswa kufundishwa kwa namna inayowawezesha kuwa nguvu ya mabadiliko katika jamii zao.

Tunapaswa kuwa na mtazamo mpya wa elimu na kuhakikisha inatoa thamani halisi kwa jamii yetu. Hii ndiyo njia ya kufikia lengo la kusoma ili kuwa na mabadiliko ya kweli nchini Tanzania na kuwa na vyuo vikuu vinavyochochea uvumbuzi na maendeleo endelevu..
Mfumo wa elimu wa Tanzania sio mbaya kama jinsi wengi wanavyoutizamia, tatizo lipo kwa wananchi na wanafunzi wenyewe ambao hawataki kusoma vitu vinavyoendana na mazingira ya nchi, mfano utakuta mwanafunzi anataka akasome Coz itakayompatia sifa mtaani na kwa ndugu zake badala ya kumpatia ajira, mfano wengi wanataka wasome Human Resources management wengine usafirishaji wengine wasome Sheria wengine social administration wengine civil engineering wengine uhandisi ambapo hizi ni coz ngumu kupata ajira au kujiajiri, Ila Tanzania ni nchi yenye rasilimali nyingi za asili mfano rasilimali watu, rasilimali ardhi, rasilimali maji, rasilimali madini na mbuga za wanyama pamoja na vivutio vingine vya utalii sasa kwanini wanafunzi wasichague coz kuendana na rasilimali zilizopo mfano kilimo, ufugaji, utalii, madini, na uvuvi pamoja na ujasiriamali?
Kwanini tusiende kwenye vyuo vinavyotoa coz ya kuchakata malighafi na kuzalisha Bidhaa ili kujiajiri wenyewe na kujikwamua kiuchumi kwasababu kilimo kipo nchini, na kwanini tusome Coz ambayo utategemea kuajiriwa tu ndy uone matunda ya elimu yako.

Watanzania tuache kuatafuta sifa mitaani tuonekane tumesoma vitu vikubwa ingawa ni vitu visivyo na tija, cha muhimu tutafute elimu yenye tija tukipata nafasi ya kusoma ili tuache kuilaumu serikali kwa ujinga wa watu wenyewe na ukiritimba uliotujaa vichwani wa kusoma ili tupate ajira maofisini huo ni kudumisha ukoloni akilini mwetu.
 
Nyerere ndo chanzo cha ujinga na elimu duni, isipo kua alikua anayaongea ongea nyerere alikua kiongozi mnafiki sanaa alipotezea baba zetu mda na ujinga wake wa ujaama.
Huwezi mlaumu nyerere hivyo hata wewe ungepewa nchi katika hali iliyokuwepo kwa wakati ule usingeweza kufanya kitu tumpe heshima yake alikuwa mbunifu kutumia wachache walioelimika katika kuiongoza nchi, ujinga wamekuwa nao wananchi wa Tanzania wa miaka ya hivi karibuni ambapo wasomi ni wengi na wanashindwa kubadili kitu cha aina yoyote wanabaki kuwa wanafiki kwa waliokosa nafasi ya kusoma,

Wasomi wa Tanzania ni wasaliti wengi wakiwa mtaani wanaongea vya mana kweli ila wakishapata nafasi serikalini hawazungumzi wala hawahoji kitu wala hawaleti mabadiliko yoyote ispokuwa wanageuka chawa wa raisi ili wazidi kupata nafasi za juu na kupata mishahara minono tu. Nyerere ni Baba na babu wa taifa la Tanzania hilo halipingiki na heshma yake itakuwepo milele.
 
Hapa waziri ana masters anafumaniwa akiwa na hawara na mke wake wanatoroka akiendesha gari la serikali kodi yetu. Anapata ajali na kumuua hawara. Cha kushangaza second in command anamtembelea hospitalini kumpa pole. Amepona na amerudi kazini na kupwa lC300 nyingine mpya.
Njia pekee ya kudhibiti embezzlement of the public funds ni kuwalipa viongozi kwa mfumo wa asilimi %.

Yaani kwa mfano kwa taifa zima kabla ya kuandaa bajeti ya mwaka wa fedha kuandaliwe malengo ya Taifa zima kwa ujumla ndani ya huo mwaka, alafu kila wizara ipewe jukumu la kutimiza lengo la taifa ndani ya huo mwaka kufuatana na dira ya taifa, alafu kila wariziri wa wizara husika awe na report maalumu ya utendaji wa utekelezaji wa wizara husika itakayosaidia kujua asilimia za utekelezaji wao kulingana na asilimia walizopatiwa na Taifa.

Mfano kwa mwaka wizara ya elimu inatarajia kujenga shule 1000 kuajiri asilimia 50% ya salimu na kufaulisha kwa asilimia angalau 89% kwa mwaka na inapaswa kuhakikisha yote waliyoagizwa yanatimizwa na kama ikishindwa kutimiza basi zinaangaliwa asilimia walizofanikiwa kuzifikia hapo ndio tunapata asilimia za kutoa mishahara.

Hapo kila waziri mwenye dhamamana angehakikisha wizara yake inafanya kazi kwa umakini ili kufikia malengo na asilimia kubwa ya utekelezaji ili kulinda kiwango cha mishahara yao.

Maana wakitekeleza kwa asilimia ndogo mshahara wao nao unakuwa mdogo.
 
Ni mfumo wetu mbovu ndgu yangu.

Imagine mtu mpaka anafika form 6 hajui hata anasoma ili uweje, ikifika siku anatakiwa kuchagua course ya kusomea chuo. Anachagua ile anayohisi atapewa mkopo kirahisi.

Ingelikua walau mtu akiwa o-level basi anaanza kuspecialize kwenye jambo fulani.
 
Ni mfumo wetu mbovu ndgu yangu.

Imagine mtu mpaka anafika form 6 hajui hata anasoma ili uweje, ikifika siku anatakiwa kuchagua course ya kusomea chuo. Anachagua ile anayohisi atapewa mkopo kirahisi.

Ingelikua walau mtu akiwa o-level basi anaanza kuspecialize kwenye jambo fulani.
Wanafunzi wenyewe hawa wanakuja kuuliza kozi inahusu nini jamii forum na search engine na website za vyuo zipo kazi ipo
 
Wanafunzi wenyewe hawa wanakuja kuuliza kozi inahusu nini jamii forum na search engine na website za vyuo zipo kazi ipo
Ndio kazi za mitandao hiyo mkuu, sasa wamuulize nani na wao hizo course hawazijui na nyingi hata kuzisikia hawajawahi
 
Hii hii elimu, na mapungufu yake yote,lakini imetoa ma injinia, mafundi kibao, wamejaa Vodacom, Tigo, Airtel, ttcl,migodini, na wana maisha mazuri tu, (nimefanya kazi hizo sekta kwa miaka 15),
Wengine walistaafu, walifungua makampuni makubwa tu yametoa ajira Nyingi kwa vijana, kampuni kama BV engineeeing, Horizon, zimejengwa na vijana waliosoma hapa bongo, tena st kayumba, kwa uzoefu wangu TZ hakuna fulsa, serikali na sekta binafsi haziwezi kuajili waalimu wote, wahandisi wote, ma dokta wote, mafundi wote, sekta yetu ya manufacturing ni ndogo Sana, ukiacha viwanda vya wahindi vya nguo, hakuna kiwanda chenye kuzalisha bidhaa za ki tekinolojia kama tairi za gari, vipuri vya magari, electronics goods nk,
Sehemu pekee kijana kutoka chuo, ataweza kutengeneza maisha na kuishi vzr, ni migodini, makampuni ya simu,
Sasa cha kufanya, kwa vijana tafuta degree yako, lakini kichwani weka kabisa kuwa wewe ni raia wa dunia, ukishindwa kupata issue bongo, kwea pipa nenda nje(sio Kenya huko, nao wana shida kama zetu).
Jifunze kizungu vzr, sio hiki cha kuombea maji, namaanisha kile chenyewe,kama wanavyobonga Kenya na Uganda,
Tafuta passport, kwea pipa, omba hata uraia huko nje,
 
Back
Top Bottom