Mkuu
Mzalendo Uchwara,
Rais wa Tanzania ni sehemu ya Bunge, ndiye analiunda, anateua watendaji wakuu wa Bunge, anaidhinisha sheria zote zinazotungwa na Bunge, na kulivunja Bunge.
Bunge likitunga sheria, kwa mujibu wa Ibara ya 97 ya katiba, rais asipoipitisha, atairudisha Bungeni kwa mara ya kwanza, wairekebishe. Sheria iliyokataliwa na rais inaporudishwa Bungeni, Bunge likijiona sheria hiyo iko sawa, hivyo linamlazimisha rais aipitishe, litairudisha kwa mara ya pili, Rais asipokubali kuipitisha, rais atalivunja Bunge kwa kuitisha uchaguzi Mkuu wa wabunge tuu.
The same process applies kwa Bunge likiataa kupitisha jina la Waziri Mkuu, watalirudisha kwa rais, ili abadilishe, rais asipobadilisha, atalivinja Bunge, na kuitisha uchaguzi wa wabunge.
Na kuvunjwa kwa tatu kwa Bunge ni likigoma kupitisha bajeti kuu ya serikali
Kuvunjwa kwa nne kwa Bunge, ni likikataa kupokea ripoti ya CAG.
Rais hawezi kulivunja Bunge, likitumia ibara ya 46A kumuondoa rais madarakani.
P