Hivi hii harufu ya baadhi ya mitaa ya jijini Dar naisikia peke yangu tu?

Hivi hii harufu ya baadhi ya mitaa ya jijini Dar naisikia peke yangu tu?

Wakuu Kwema!

Aisee! Baada ya kutoka kuzurura huko Duniani, sitaki kupataja nisijeonekana najikosha hapa, na wenye nongwa zao na vijiba vya roho wasije nitolea mvuke wa ushubwada. Ila ifahamike tuu nimetoka huko Dunia ilipo.

Kwa kweli Dar inanuka vibaya mno. Inanuka vitu mfano wa mavi, sijasema ni mavi jamani Ila ni Kama hivyo.

Yaani Asilimia kubwa ya Maeneo yananuka chemba za maji taka. Nashindwa Kueleza hapa. Sitaki kugombana na wenye DAR Yao, sitaki kabisa. Maana najua wapo wanayoipenda, ikumbukwe siiongelei Jambo hili Kwa ni mbaya lakini naongea ili Jambo Fulani lifanyike.

Alafu ukiwaona wakazi wa Dar ni Kana kwamba hawaisikii hiyo harufu, pengine wamekuwa sehemu ya harufu yenyewe, sijasema watu wa DAR mnanuka chemba za maji taka 😃😃😃. Maana wenye hasira hamkosekani.

Hata hivyo akili yangu ikanambia sio rahisi watu WA DAR kuisikia hiyo harufu mbaya ya mavi Kwa maana maisha yao ni yataabu Sana. Taabu zimeua mishipa ya Nostril ndani ya pua. Hawezi kunususa tena.

Hasa watu masikini wapanda Daladala, hawa ndio wanaoonja joto ya jiwe,hata hivyo wenyewe ni Kama joto Hilo hawalisikii kwani taabu imewafubaza na kuwafanya waone kila kitu Kama kipo Sawa.

Kipindi nasoma pale Udsm wala sikuwa najua DAR inanuka, nimekaa zaidi ya miaka mitano Kama sio sita sikuwa naona hizo harufu. Labda Maeneo ya Tandale huko na viunga vya makazi ya WALIA NA MUNGU watu fukara apeche Alolo.

Najiuliza niliwezaje kuishi miaka mitano kipindi kile?

Nafikiri serikali ipitie tena miundombinu ya taka hasa mitaro ya maji taka ili mji usiwe jiji la harufu mbaya.

Wananchi wa Dar nanyi mjitahidi kuwa wasafi hata Kama mmezoea harufu yenu mbaya kumbukeni wageni Kama Sisi tunaotoka Duniani tunakujaga pia kuwasalimu.

Muwe na Haya hata kidogo.

Taikon nitakuwa DAR Kwa wiki tatu mfululizo kabla sijaenda kudhuru Zanzibar nikielekea kuchumbia Visiwa vya Comoro.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Dah..kwa hili la kusikia harufu....usikute Dar nzima tunaumwa uviko ila hatujijui 🤣🤣🤣🤣🤭
 
Tena pale Makumbusho Stend ndio sitaki kupasikia.
Pananuka utadhani nini. Nusura Nitapike lakini ajabu ni kuwa Mimi pekee ndiye niliyeonekana kukerwa na harufu Ile watu wengine hata hawana habari
Unamanisha Michael Jackson angetua bongo angesemaje khs jiji kunukia?
 
Ndio maana wana darusalama mnapenda kuzibuana mitaro ya maji machafu kumbe mnaishi pahala panukapo na harufu mmeizoea
 
Sijafika huko Mkuu Ila nitaenda.

Maeneo mengi Yananuka hasa Maeneo ya Stend za Daladala.

Kesho nitakuwa na ziara ya Maeneo ya Posta yote, Feri, Upanga, na Kidogo Namanga
Hili wengi watakubishia na wana haki ya kufanya hivyo. Wana haki kwa sababu bila mtu kusafiri nje ya Tanzania na kwenda nchi zilizoendelea utakuwa unadhani Dar kila kitu kipo sawa. Haya uliyoandika kuna watu watadhani ni utani lakini mimi nimeyashuhudia mara nyingi. Ukitoka sehemu kama Ulaya ukifika Dar vitu vifuatavyo ni dhahiri. 1. Harufu mbaya (jiji lote) 2. Watu wachafu kupindukia. 3. Watu, Nyumba, magari na kila kitu viko disorganized.
 
Harufu imekithiri kweli ila sio Dar tu hata Nairobi pananuka kwa kweli

Ila hiyo mitaro naona inafukiwa vingi sio kinyesi tu labda na watu pia maana sio kwa harufu hiyo
 
Sawa Bhana mtu wa DAR. Wewe si ndiye Shemeji YANGU wa Tandale.

Jaribuni kuwa wasafi hata kidogo.

Vijana wadogo mmeathirika kisaikolojia kisa harufu za Chemba za maji taka.

Pumbavu
Ahhahaha
 
Hili wengi watakubishia na wana haki ya kufanya hivyo. Wana haki kwa sababu bila mtu kusafiri nje ya Tanzania na kwenda nchi zilizoendelea utakuwa unadhani Dar kila kitu kipo sawa. Haya uliyoandika kuna watu watadhani ni utani lakini mimi nimeyashuhudia mara nyingi. Ukitoka sehemu kama Ulaya ukifika Dar vitu vifuatavyo ni dhahiri. 1. Harufu mbaya (jiji lote) 2. Watu wachafu kupindukia. 3. Watu, Nyumba, magari na kila kitu viko disorganized.


Na watu wameathirika kisaikolojia.

Wanahasira na kupayuka payuka tuu
 
Harufu tumeshaizoea sisi, tena ukiziba pua watu wataona unajisikia. Ila usijali, ndani ya muda mfupi na wewe utaizoea Harufu yetu pendwa.

Karibu tena Dar.
 
Back
Top Bottom