Hivi hii nchi ni ya nani haswa? Serikali ipo kwa maslahi ya nani haswa?

Hivi hii nchi ni ya nani haswa? Serikali ipo kwa maslahi ya nani haswa?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
20220813_002214.jpg

Tarehe 09 Desemba 1961 ni siku ambayo bendera ya Tanzania (Tanganyika) ilipandishwa kuashiria nchi huru yenye kujitawala na kujiamulia mambo yake bila kuingiliwa na taifa lolote la nje.

Leo tunakaribia miaka 61 ya uhuru lakini bado wananachi wa Tanzania wanaishi kwa kudra za watawala. Bado uhuru wa Watanzania haujawa defined na kufikiwa katika uhalisia wa uhuru.

Elites wachache ndani ya nchi ndiyo ambao wanaishi kwa ule uhuru wenye maana ya uhuru. Tumefikia mahala ambqpo tunaficha majina yetu halisia ili kuweza kusema ya moyoni kwa sababu ukithubutu kusema lolote linalowakaza tabaka la wenye uhuru utaishia kuwekewa matanga ama utatengenezewa kesi ambazo utafungwa ushike adabu.

Katiba ya Nchi imeonesha kabisa kuwa haina mlinzi kwa sababu walioapa kuilinda ndiyo wanaoongoza kuipuuza. Kwa mfano
  1. Kuzuia makusanyiko halali ya kisiasa kwa vyama vya upinzani ni uamuzi wa HOVYO sana
  2. Kutunga sheria za kibaguzi na kuzitekeleza kama ilivyo sheria ya pensheni, sheria ya kuadhibu wanaowakosoa viongozi, sheria inayounda Bodi za Mazao zinazodhibiti soko dhidi ya wakulima na sheria nyinginezo zinazofanania ubaguzi ni wazi nchi si ya wananchi
  3. Tumeona askari wetu wakitumikia siasa wakiwa kazini na wakiwa wamestaafu ambapo Katiba imezuia hilo. Maana yake ni kwamba nchi inaendeshwa na waliohuru dhidi ya wananchi wanaoishi kwa kudra ya wamiliki wa Uhuru
  4. Miaka 61 ya Uhuru bado maji, umeme, elimu, afya na mengine muhimu ni mambo magumu na ya kufikirika kwa wananchi waliowengi
  5. Katiba mpya ambayo ni hitqji la msingi kwa mazingira ya sasa ya siasa za vyama vingi, inasubiri kudra ya walio HURU maana inaonekana inatishia uhuru wa wenye kumiliki Uhuru wa nchi hii
  6. Sheria inayohusu misafara ya viongozi inawapuuza wananchi ambao kimsingi ndiyo wanaokamuliwa kodi zao ili kuiendesha nchi
  7. Kitengo cha maafa kinapokea bajeti miaka yote lakini hakijawahi kuwa effective hadi leo.
  8. Serikali inanunua zana na silaha kali kwa minajili ya kuwatishia, kuwapiga, kuwaumiza na kuwashughulikia wananchi ambao wanaohoji wamiliki wa uhuru.
  9. Wananchi wanalimwa kodi kubwa kubwa na tozo mbalimbali ambazo wanaambiwa ni kwa minajili ya maenedeleo yao lakini taifa linaambiwa na wenye Uhuru kuwa hela hizo zinatolewa na Rais ambaye kimsingi halipi kodi.
  10. Serikali imewekeza kwenye kusimika mitambo imara kiteknolojia inayowafuatilia na kuwadukua wananchi wake wanaohoji mwwnendo na haiba za wqliojimilikisha uhuru wa nchi.

Hebu tuelimishane hapa, hii nchi ni nani haswa anapaswa kuitwa mwenye nchi, kwa nini tumefikia hapa?
 
Dua la kuku halimpati mwewe,

ila tusijali tupo kwenye evolution ndani ya miaka 500 tutapata mabadiliko.
 
Nchi hii Ni ya watanzania na serikali IPO kwa ajili ya kuwatumikia watanzania wote bil kujali itikadi zao za kisiasa, hii inathibitishwa na kazi kubwa iliyofanywa na serikali yetu tangia kupata Uhuru wa nchi hii, jiulize tulipokuwa tunapata Uhuru tulikuwa na vituo vingapi vya Afya na Leo tunavyo vingapi,jiulize tulikuwa na madakitari wangapi na Sasa tunao wangapi,hapa ukipata jibu utaona kazi ya kutukuka ya serikali hii katika kuwatumikia watanzania

Jiulize tulikuwa na shule ngapi za msingi, sekondari na vyuo vikuu tulipokuwa tunapata Uhuru na Leo Hali ipoje,jiulize tulikuwa na walimu,wahadhiri,wangapi na Leo tunao wangapi?

Jiulize Barabara za lami zilikuwa I'm ngapi na Sasa Hali ipoje, jiulize mikoa mingapi ilikuwa imeunganishwa kwa lami na leo Hali ipoje?jiulize watu walikuwa wanasafiri kwa muda wa siku ngapi kutoka mikoani Hadi dar na leo wanafika kwa muda gani?

Kwa ufupi kila utakapokwenda utakuta kazi kubwa imefanyika chini ya serikali ya CCM mpaka Leo hii,ndio sababu ya Kuendelea kuaminiwa na watanzania mpaka leo, hakuna secta ambayo imeachwa nyuma au kusahaulika
 
Nchi hii Ni ya watanzania na serikali IPO kwa ajili ya kuwatumikia watanzania wote bil kujali itikadi zao za kisiasa, hii inathibitishwa na kazi kubwa iliyofanywa na serikali yetu tangia kupata Uhuru wa nchi hii, jiulize tulipokuwa tunapata Uhuru tulikuwa na vituo vingapi vya Afya na Leo tunavyo vingapi,jiulize tulikuwa na madakitari wangapi na Sasa tunao wangapi,hapa ukipata jibu utaona kazi ya kutukuka ya serikali hii katika kuwatumikia watanzania

Jiulize tulikuwa na shule ngapi za msingi, sekondari na vyuo vikuu tulipokuwa tunapata Uhuru na Leo Hali ipoje,jiulize tulikuwa na walimu,wahadhiri,wangapi na Leo tunao wangapi?

Jiulize Barabara za lami zilikuwa I'm ngapi na Sasa Hali ipoje, jiulize mikoa mingapi ilikuwa imeunganishwa kwa lami na leo Hali ipoje?jiulize watu walikuwa wanasafiri kwa muda wa siku ngapi kutoka mikoani Hadi dar na leo wanafika kwa muda gani?

Kwa ufupi kila utakapokwenda utakuta kazi kubwa imefanyika chini ya serikali ya CCM mpaka Leo hii,ndio sababu ya Kuendelea kuaminiwa na watanzania mpaka leo, hakuna secta ambayo imeachwa nyuma au kusahaulika
Ndugu nakuulize tu huoni aibu unvyosifia kitu ambacho akipo?

Huoni kama mtoa mada kongea point?
 
Nchi hii Ni ya watanzania na serikali IPO kwa ajili ya kuwatumikia watanzania wote bil kujali itikadi zao za kisiasa, hii inathibitishwa na kazi kubwa iliyofanywa na serikali yetu tangia kupata Uhuru wa nchi hii, jiulize tulipokuwa tunapata Uhuru tulikuwa na vituo vingapi vya Afya na Leo tunavyo vingapi,jiulize tulikuwa na madakitari wangapi na Sasa tunao wangapi,hapa ukipata jibu utaona kazi ya kutukuka ya serikali hii katika kuwatumikia watanzania

Jiulize tulikuwa na shule ngapi za msingi, sekondari na vyuo vikuu tulipokuwa tunapata Uhuru na Leo Hali ipoje,jiulize tulikuwa na walimu,wahadhiri,wangapi na Leo tunao wangapi?

Jiulize Barabara za lami zilikuwa I'm ngapi na Sasa Hali ipoje, jiulize mikoa mingapi ilikuwa imeunganishwa kwa lami na leo Hali ipoje?jiulize watu walikuwa wanasafiri kwa muda wa siku ngapi kutoka mikoani Hadi dar na leo wanafika kwa muda gani?

Kwa ufupi kila utakapokwenda utakuta kazi kubwa imefanyika chini ya serikali ya CCM mpaka Leo hii,ndio sababu ya Kuendelea kuaminiwa na watanzania mpaka leo, hakuna secta ambayo imeachwa nyuma au kusahaulika
Ukizingatia mantiki ya hoja yangu, unachokijibu ni kitu kingine kabisa.

Sishangai ndugu yangu. Mpo wengi sana na hata mimi nilikuwa kama wewe mpaka nilipoahukiwa na Roho Mtakatifu akaikomboa nafsi yangu dhidi ya CCM
 
Back
Top Bottom