Hivi hii TANESCO ya Maharage si walisema umeme wa grid umeshafika Kigoma?

Hivi hii TANESCO ya Maharage si walisema umeme wa grid umeshafika Kigoma?

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Naangalia taarifa ya habari ITV sasa hivi, nimestaajabu kumuona CEO wa TANESCO Maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea Kigoma. Mimi labda siko Tanzania au sielewi.

Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika Kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.

Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika Kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikuwa naota ndoto.
 
Naangalia taarifa ya habari ITV saa hivi nimestaajabu kumuona ceo wa tanesco maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea kigoma we. Mimi labda siko tanzania au sielewi. Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.
Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikua naota ndoto.

Mkuu kumbe walivyosema kuwa umeme wa grid umefika Kigoma uliamini?! Kweli basi serikali inawaokota wengi!
 
Naangalia taarifa ya habari ITV saa hivi nimestaajabu kumuona ceo wa tanesco maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea kigoma. Mimi labda siko tanzania au sielewi. Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.
Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikua naota ndoto.

Karibu Tz ndugu yangu kuna kideo kiko humu boss wa maharagwe mr February anaelezea kuhusu usambazaji wa umeme Geita. Ukiweza kumwelewa kwenye hiyo video mr kipara basi ata maharagwe utamwelewa tu
 
Umeme wa Grid uliishafika Kigoma, ukiunganishwa kutokea Nyakanazi kupitia Kibondo na Kasulu.
Kuna line nyingine inayotoka Tabora kupitia Uvinza kwenda Kigoma, sina hakika kama iliishakamilika.
Mkoa wa Kigoma unategemea kupata umeme wa Rusumo ambao yamkini utakabidhiwa mwezi July mwaka huu.

Kuna ujenzi wa Mini Hydroelectric Power Station kwenye mto Malagarasi. Nadhani ukiunganishwa wote ....Labda ndio utakamilisha hiyo asilimia 57 iliyobaki.

Huu ni mtazamo wangu tu katika kuchangia kwenye mada yako lakini naamini TANESCO wenyewe watatoa ufafanuzi.
 
Naangalia taarifa ya habari ITV saa hivi nimestaajabu kumuona ceo wa tanesco maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea kigoma. Mimi labda siko tanzania au sielewi. Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.
Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikua naota ndoto.
Tena walifanya tafrija ya kuzima majenereta, na kuwasha gridi ya taifa, tukio lilikuwa mubashara,
Leo kuambiwa gridi ya taifa haijafika Kigoma nimeshangaa sana,
Wanasiasa sio wa kuwaamini sana,

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
Naangalia taarifa ya habari ITV sasa hivi, nimestaajabu kumuona CEO wa TANESCO Maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea Kigoma. Mimi labda siko Tanzania au sielewi.

Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika Kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.

Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika Kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikuwa naota ndoto.
hawa akina maharage ni aina ile ya viongozi wapuuzi.juzi tu nilikuwa pale kigoma mji na sikuona umeme wa gridi.nilichokiona ni kuwa umeme umeishia pale kasulu tu.kigoma mjini hakuna gridi na hata kituo cha kupozea umeme hakuna bali ni umeme wa majenerata.inasemekana kituo cha kupozea umeme kitajengwa Kidahwe njia panda ya kuelekea dar lkn mpaka sasa hakuna maandalizi yoyote.kimsingi gridi imeishi kasulu mjini tu.
 
Naangalia taarifa ya habari ITV sasa hivi, nimestaajabu kumuona CEO wa TANESCO Maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea Kigoma. Mimi labda siko Tanzania au sielewi.

Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika Kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.

Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika Kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikuwa naota ndoto.
Moja kati ya sifa kubwa za Magufuli ilikuwa ni UONGO.
 
Naangalia taarifa ya habari ITV sasa hivi, nimestaajabu kumuona CEO wa TANESCO Maharage akisema umeme wa grid ndio uko asilimia 47 kuelekea Kigoma. Mimi labda siko Tanzania au sielewi.

Nakumbuka kwa masikio yangu nimesikia tena sio mara moja kwamba umeme wa grid ulishafika Kigoma miezi kadhaa sasa imepita. Tena kukawa na maelezo kuhusu kuokolewa gharama kubwa kutokana na kuacha kutumika mafuta mazito.

Leo nashangaa eti kumbe bado umeme wa grid kufika Kigoma. Hebu anayejua vizuri hii issue atujuze labda mimi hizi taarifa nilikuwa naota ndoto.
Pole, Kwa kuamini majambazi
 
Mkuu kumbe walivyosema kuwa umeme wa grid umefika Kigoma uliamini?! Kweli basi serikali inawaokota wengi!

Hahahaaaa tatizo wanaamini sana wanasiasa kwenye TV ,hizo TV wanapewa mshiko kurusha habari za hao wanasiasa na wanasiasa wanaleta uongo uongo kuaminisha umma tu.

Nakumbuka kuna siku kwenye TV alinyanyuka mwenyekiti wa mkoa fulani akieleza mafanikio ya mkoa wake ,akasema wamejenga barabara zote zinazounganisha miji lakini kwakuwa mimi ni mkazi wa eneo hilo nikaona wazi kabisa anawapiga mchanga wa macho maana barabara alizotoja nyingine hata ujenzi haujaanza...lakini nikajua ile ni JUST FOR TV.
 
Daaa mzee wangu anawatesa sana watu ila ndiyo inakunya sasa wenyewe mjue matundu yako wapi.
 
Back
Top Bottom