Hivi hiki Kiingereza kwenye Royal Tour kipo sawa?

Hivi hiki Kiingereza kwenye Royal Tour kipo sawa?

Niache Nteseke

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2020
Posts
2,162
Reaction score
2,616


Wakuu habari zenu.

Nimepita kwenye status moja ya mdada nikakutana na hiyo clip ya Royal Tour kukiwa na maongezi kati ya Rais Samia na huyo mzungu.

Kuna kipande Rais Samia anamwambia huyo mzungu kuwa THIS IS BEGINNING OF BEAUTIFUL FRIENDSHIP. Nimejiuliza mara 2 kuhusu hiko Kiingereza je kipo sawa au?

Lakini pia, nnavyojua mimi kwenye ku-shoot movie/documentary/tamthilia kuna actions huwa zinarudiwa kurekodiwa mpaka scene husika inakaa sawa, sasa nnachojiuliza ni kuwa, katika kutengeneza hii Royal Tour hakukuwa na wasaidizi wake au watu wengine pembeni wakati Mh. Rais anaongea?

Lakini pia, wakati wana-edit hawakuskia hiko kipande, kwa sababu sauti nyingine zinaweza kuingizwa hata ukiwa studio, kwani wasingeweza kurekebisha hiko kipande?

Kwa kuwa nilisoma shule za Kata St. Kayumba nikasema niulize wadau kuhusu hiyo sentensi inatakiwa kuwa hivyo ilivyo (THIS IS BEGINNING) au kuna namna ilitakiwa kuwa wakuu?

NAWASILISHA.
 
Haya_Land ni kweli hakuna tatizo kwenye hiyo sentensi...?

Sio inatakiwa kuwa "The beginning ndugu...?"
Ujuaji mwingi sana wabongo mnajifanya wajuvi wa kila kitu yani mnataka kingereza mlichofundishwa darasan kiongelelewe vile vile, kwani nyie mkwenye kiswahili huwa mnafuatilia kanuni zote za utamkaji wa maneno ya kiswahili?
 
Ujuaji mwingi sana wabongo mnajifanya wajuvi wa kila kitu yani mnataka kingereza mlichofundishwa darasan kiongelelewe vile vile, kwani nyie mkwenye kiswahili huwa mnafuatilia kanuni zote za utamkaji wa maneno ya kiswahili?
Ingekuwa Peter kakosea kiswahili hii thread isingeanzishwa.

Amini usiamini...
 
Ujuaji mwingi sana wabongo mnajifanya wajuvi wa kila kitu yani mnataka kingereza mlichofundishwa darasan kiongelelewe vile vile, kwani nyie mkwenye kiswahili huwa mnafuatilia kanuni zote za utamkaji wa maneno ya kiswahili?
Ni ujinga ujinga wa kitoto tuu watu huwezi kuwaweza wanamaarifa ya kitoto sana
 
#Mwanzo alafu kuna Huu ni mwanzo

kingerezaaaa.......
 
"This is the beginning of a beautiful friendship"

Hata hivyo wamejitahidi kiasi chake maana English siyo lugha Mama ya TZ bali ni lugha ya utumwa ingawa sasa hivi ni lugha ya biashara kimataifa [emoji16]

Sawa kiongozi ila hii inaleta picha gani kwa wasaidizi wa Mh. Rais ambao walikuwa nae wakati anarekodi...?

Pili inaleta picha gani kimataifa kwa kumsikia Rais wetu akiongea Kiingereza cha namna hiyo mkuu...?
 
Back
Top Bottom