Kama kuna jambo ambalo limeamsha hisia na vuguvugu za kizalendo kwa kipindi kirefu kilichopita, na kupata sapoti ya wanazuoni wanaoheshimika ndani na nje ya nchi ni hili la bandari.
Pamoja na kuwa wazi kabisa kwamba kuna kila dalili ya kuja kulilia huko mbele ya safari kuwa viongozi wetu wametuingiza chaka, lakini ni dhahiri shairi kabisa kuwa umma hauna ujasiri wa kuamua kinyume na watawala walivyokusudia.
Hii ni tofauti kabisa na jirani zetu flani na sijui ni kwa nini hatujifunzi kutoka kwao.
Hivi ndo kusema kwamba hii Tanganyika ndo nchi nyepesi sana kuitawala au tusubiri kizazi kingine kitakachokuwa na uwezo wa kufanya jambo ili kiheshimiwe na watawala?
Na je hao tutakaoamua kuwasubiri watajifunzia wapi kama hawakuwahi kuona nguvu ya umma ya kizazi kilichokua mbele yao kikifanya jambo likawa jambo?...TAFAKARI KWA KINA.
Pamoja na kuwa wazi kabisa kwamba kuna kila dalili ya kuja kulilia huko mbele ya safari kuwa viongozi wetu wametuingiza chaka, lakini ni dhahiri shairi kabisa kuwa umma hauna ujasiri wa kuamua kinyume na watawala walivyokusudia.
Hii ni tofauti kabisa na jirani zetu flani na sijui ni kwa nini hatujifunzi kutoka kwao.
Hivi ndo kusema kwamba hii Tanganyika ndo nchi nyepesi sana kuitawala au tusubiri kizazi kingine kitakachokuwa na uwezo wa kufanya jambo ili kiheshimiwe na watawala?
Na je hao tutakaoamua kuwasubiri watajifunzia wapi kama hawakuwahi kuona nguvu ya umma ya kizazi kilichokua mbele yao kikifanya jambo likawa jambo?...TAFAKARI KWA KINA.