Hivi hizi R na L zimetukosea nini?

Hivi hizi R na L zimetukosea nini?

FourTwoNet

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2022
Posts
1,236
Reaction score
2,512
Sipati picha kama JF wangekuwa wameandika jina lao kama "Jamii Folums" ingekuaje.

Au jukwaa hili jina lingeandikwa "Habali na Hoja mchanganyiko sijui ingekaaje hiyo.

Inaeleweka kwamba kila mmoja ametoka maeneo tofauti, hivyo lugha zetu za mama zinaweza kuchangia namna tunavyoweza kutamka na kuongea lugha nyingine, hilo linaeleweka.

Tafrani inakuja kwenye swala zima la kuandika. Kutamka ni rukhsa kukosea, lakini kwenye kuandika, hilo halina mjadala.

Tusipokosoana, matokeo yake hata waandishi wetu wa magazeti na vyombo vya habari na watunzi wa riwaya wataendekeza kosa hili na kupoteza ladha ya lugha.

Utakuta mtu kaandika maneno mengine kwa kuweka hizi herufi vizuri na kwenye sentensi hiyo hiyo kachemsha maneno mengine, hii inamaana amezoea kuona mtu anaandika neno flani kwa kukosea, kwa hiyo anaona ni sawa. Ndio maana shuleni kulikuwa na zoezi la imla.

Siku hizi hata walimu wamezoeshwa na waliokuwa walimu wao, hivyo kupelekea kutokuona hili katika kusahihisha wanafunzi.

Binafsi, nitakuwa nikiingia humu halafu nikute umelipua L na R....sikuachi.

Tukiendekeza tabia hii, hata hichi kiswahili tunachojivunia tutakipoteza.
 
Uchanganyaji wa kiuandishi kwa hizi herufi L na R ni ujinga wa mtu. Sitarajii mwenye kadhia hiyo akaandika Engrish badala ya English. Au cal badala ya car. Au almy badala ya army. Au Geoglaphy badala ya Geography. Au Doctol badala ya Doctor. Ila kwenye uandishi wa uwasilishaji wa masuala anuwai kwa lugha ya Kiswahili uchangaji wa hizi herufi mbili utazikuta (L na R).

Kinachomaanishwa ni kuwa: Mtu anaweza akaathiriwa na lugha mama kimatamshi lakini si kiunadishi. Kwani yapo maneno mengi kimatamshi na kiuandishi yanatofautiana lakini hayakuwa ni yenye kuchanganywa. Laiti kama hili lingelikuwa sababu basi watu tungelikuwa ni wenye kukosea sana kwenye uandishi lakini ni kinyume chake.

Ajabu iliyokubwa humkuti akichanganya herufi hizo kiuandishi kwenye jina lake, la baba hata la ukoo. Kama jina lake ni Erick ataandika hivyo hivyo! La babaye likiwa Gabriel linaandikwa pasipo kukosewa! Ni ujinga tu wa watu kuchanganya hizo herufi. Ukijiona ni mwenye hiyo hitilafu angalau soma magazeti yatakusaidia kiuandishi.
 
Sipati picha kama JF wangekuwa wameandika jina lao kama "Jamii Folums" ingekuaje.

Au jukwaa hili jina lingeandikwa "Habali na Hoja mchanganyiko sijui ingekaaje hiyo.

Inaeleweka kwamba kila mmoja ametoka maeneo tofauti, hivyo lugha zetu za mama zinaweza kuchangia namna tunavyoweza kutamka na kuongea lugha nyingine, hilo linaeleweka.

Tafrani inakuja kwenye swala zima la kuandika. Kutamka ni rukhsa kukosea, lakini kwenye kuandika, hilo halina mjadala.

Tusipokosoana, matokeo yake hata waandishi wetu wa magazeti na vyombo vya habari na watunzi wa riwaya wataendekeza kosa hili na kupoteza ladha ya lugha.

Utakuta mtu kaandika maneno mengine kwa kuweka hizi herufi vizuri na kwenye sentensi hiyo hiyo kachemsha maneno mengine, hii inamaana amezoea kuona mtu anaandika neno flani kwa kukosea, kwa hiyo anaona ni sawa. Ndio maana shuleni kulikuwa na zoezi la imla.

Siku hizi hata walimu wamezoeshwa na waliokuwa walimu wao, hivyo kupelekea kutokuona kisa hili katika kusahihisha wanafunzi.

Binafsi, nitakuwa nikiingia humu halafu nikute umelipua L na R....sikuachi.

Tukiendekeza tabia hii, hata hichi kiswahili tunachojivunia tutakipoteza.
Naunga mkono hoja - 100%. Mimi nikiona story imeandikwa kwa kuchanganya R na L, huwa hamu ya kuendelea kusoma inaniisha. Huwa sielewi kabisa inakuwaje mtu mzima unachanganya R na L, tena unaandika kwa kiswahili. Sio kuandika tu, ata kuongea. "Kalibu" badala ya "Karibu". "Ushulu" badala ya Ushuru. Nashindwa kuelewa kwanini watu wanakosea.

Na wengine pia huwa wanaacha "H" kwenye kuandika, na hivyo kuleta tofauati ya usomaji kwenye story. Mfano, lengo ni kusema "Huku", anaandika "uku".
 
Naunga mkono hoja - 100%. Mimi nikiona story imeandikwa kwa kuchanganya R na L, huwa hamu ya kuendelea kusoma inaniisha. Huwa sielewi kabisa inaluwaje mtu mzima unachanganya R na L, tena unaandika kwa kiswahili. Sio kuandika tu, ata kuongea. "Kalibu" badala ya "Karibu". "Ushulu" badala ya Ushuru. Nashindwa kuelewa kwanini watu wanakosea.

Na wengine pia huwa wanaachuku "H" kwenye kuandika, na hivyo kuleta tofauati ya usomaji kwenye story. Mfano, lengo ni kusema "Huku", anaandika "uku".
Hapo kwenye H....nilikuwa mhalifu asee....kusema kweli nalitazama hilo.

Hapa sasa ni mwendo kwa kukamua. Nikikuta tu mchemsho, nakaanga.
 
Wanaochanganya L na R wengi ni vichwa vizito katika kufikiri na kuelewa. Waangalie wengi wenye hilo tatizo utagundua hata uwezo wao kujenga hoja na kuongea ishu zenye mantiki ni mdogo sana.
Naunga mkono hoja - 100%. Mimi nikiona story imeandikwa kwa kuchanganya R na L, huwa hamu ya kuendelea kusoma inaniisha. Huwa sielewi kabisa inakuwaje mtu mzima unachanganya R na L, tena unaandika kwa kiswahili. Sio kuandika tu, ata kuongea. "Kalibu" badala ya "Karibu". "Ushulu" badala ya Ushuru. Nashindwa kuelewa kwanini watu wanakosea.

Na wengine pia huwa wanaacha "H" kwenye kuandika, na hivyo kuleta tofauati ya usomaji kwenye story. Mfano, lengo ni kusema "Huku", anaandika "uku".
 
Mkuu FourTwoNet kuna baadhi ya maneno umekosea kuandika kwenye uzi wako, ingawa kwenye matumizi ya R na L uko vizuri!

Ningekuwa karibu yako ningekunasa kofi la mdomo

Anyway, hata mimi nilikuwa na tatizo la matumizi ya R na L lakini kwa sasa siwezi kosea tena! Pia matumizi ya X kwenye maneno, mfano Xaxa badala ya Sasa, nn badala ya nini, lakini kwa sasa niko vizuri
 
Back
Top Bottom