Hivi hizi R na L zimetukosea nini?

Hivi hizi R na L zimetukosea nini?

Ingekuaje ❌ Ingekuwaje ✅
Swala zima ❌ Suala zima ✅
Hata hichi ❌ hata hiki✅

Anza wewe kujifunza uandishi kwanza.
Mtoa mada kwa akili yake anafikiri makosa ya kiuandishi yapo kwenye R na L tu! Ona sasa na yeye mwenyewe alichokifanya.

"Lugha zetu za mama......."✖️

Lugha mama ✔️
 
Wanaochanganya L na R wengi ni vichwa vizito katika kufikiri na kuelewa. Waangalie wengi wenye hilo tatizo utagundua hata uwezo wao kujenga hoja na kuongea ishu zenye mantiki ni mdogo sana.
Nagongea msumari.
 
Mkuu FourTwoNet kuna baadhi ya maneno umekosea kuandika kwevnye uzi wako, ingawa kwenye matumizi ya R na L uko vizuri!

Ningekuwa karibu yako ningekunasa kofi la mdomo

Anyway, hata mimi nilikuwa na tatizo la matumizi ya R na L lakini kwa sasa siwezi kosea tena! Pia matumizi ya X kwenye maneno, mfano Xaxa badala ya Sasa, nn badala ya nini, lakini kwa sasa niko vizuri
Kujirekebisha ni muhimu, na kukosolewa pia mkuu. Naungama na kutubu dhambi zangu.
 
Ingekuaje ❌ Ingekuwaje ✅
Swala zima ❌ Suala zima ✅
Hata hichi ❌ hata hiki✅

Anza wewe kujifunza uandishi kwanza.
Hii imekuwa kama jadi yetu watanzania. Kupenda kubisha tunaposahihishwa. Mwanzisha thread ana point nzuri sana. Haya maneno uliyosahihisha mara nyingi yanaweza kuvumilika lakini siyo hili kosa la R na L.
 
Mtoa mada kwa akili yake anafikiri makosa ya kiuandishi yapo kwenye R na L tu! Ona sasa na yeye mwenyewe alichokifanya.
Tuanzie kwanza hapo kwenye R na L. Nimekubali na nimeelewa maelekezo. Ntakuwa makini.
 
Hii imekuwa kama jadi yetu watanzania. Kupenda kubisha tunaposahihishwa. Mwanzisha thread ana point nzuri sana. Haya maneno uliyosahihisha mara nyingi yanaweza kuvumilika lakini siyo hili kosa la R na L.
Ahsante sana mkuu.
 
Ajabu hata baadhi ya watangazaji wa vituo vya runinga na redio ni waathirika wa kuchanganya R na L.
 
Sipati picha kama JF wangekuwa wameandika jina lao kama "Jamii Folums" ingekuaje.

Au jukwaa hili jina lingeandikwa "Habali na Hoja mchanganyiko sijui ingekaaje hiyo.

Inaeleweka kwamba kila mmoja ametoka maeneo tofauti, hivyo lugha zetu za mama zinaweza kuchangia namna tunavyoweza kutamka na kuongea lugha nyingine, hilo linaeleweka.

Tafrani inakuja kwenye swala zima la kuandika. Kutamka ni rukhsa kukosea, lakini kwenye kuandika, hilo halina mjadala.

Tusipokosoana, matokeo yake hata waandishi wetu wa magazeti na vyombo vya habari na watunzi wa riwaya wataendekeza kosa hili na kupoteza ladha ya lugha.

Utakuta mtu kaandika maneno mengine kwa kuweka hizi herufi vizuri na kwenye sentensi hiyo hiyo kachemsha maneno mengine, hii inamaana amezoea kuona mtu anaandika neno flani kwa kukosea, kwa hiyo anaona ni sawa. Ndio maana shuleni kulikuwa na zoezi la imla.

Siku hizi hata walimu wamezoeshwa na waliokuwa walimu wao, hivyo kupelekea kutokuona kisa hili katika kusahihisha wanafunzi.

Binafsi, nitakuwa nikiingia humu halafu nikute umelipua L na R....sikuachi.

Tukiendekeza tabia hii, hata hichi kiswahili tunachojivunia tutakipoteza.
Mkuu una hoja ya msingi kabisa japo kuna watu wanataka (kama kawaida ya wabongo) kupindisha mada kwa kuleta ubishi wa kijinga kabisa. Makosa kwenye kutumia R na L ni janga la nchi. Kama mtu atakosea kwenye matamshi nitaelewa lakini siyo kuandika ambako tunaanza kufundishwa tangu chekechea.
 
Tuanzie kwanza hapo kwenye R na L. Nimekubali na nimeelewa maelekezo. Ntakuwa makini.
Mara nyingi hizo R na L husababishwa na asili ya watu! Mfano watu wa Kanda ya Ziwa, kimsingi hawana L! Badala yake wana R tu!! Niretee ugari, Niretee Gwajima, nk.

Ukienda Dodoma, Iringa, nk huko hawana R! Badala yake wana L tu! Badala ya kutamka Iringa , wenyeji hutamka Ilinga! Dodoma nako kila neno lenye R, hugeuzwa na kuwa L! 'Napeleka malejesho', nk.

Mifano ni mingi, muda ni mchache.
 
Hii imekuwa kama jadi yetu watanzania. Kupenda kubisha tunaposahihishwa. Mwanzisha thread ana point nzuri sana. Haya maneno uliyosahihisha mara nyingi yanaweza kuvumilika lakini siyo hili kosa la R na L.
Makosa ni makosa tu hata kama kwako yanavumilika, tunatofautiana kiwango cha kuyavumilia….. kama kwako sio tatizo haimaanishi yapo sahihi.

Jenga utamaduni wa kukosoana kama tulivyo sisi akili kubwa, hata muuaji anapofiwa hulia machozi.
 
Matumizi ya lugha na ufasaha wake ni shida kwa watu wengi Sana ndio maana Kuna muda tunashauriwa kuangalia mantiki ya kile alicho andika kuliko kuzingatia matumizi ya lugha kwa usahihi wake.

NB :siungi mkono matumizi yasiyo sahihi ya lugha

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu una hoja ya msingi kabisa japo kuna watu wanataka (kama kawaida ya wabongo) kupindisha mada kwa kuleta ubishi wa kijinga kabisa. Makosa kwenye kutumia R na L ni janga la nchi. Kama mtu atakosea kwenye matamshi nitaelewa lakini siyo kuandika ambako tunaanza kufundishwa tangu chekechea.
Unapokosea wakati wa kukosoa wenzako kubali na wewe kukosolewa ili tujenge uelewa wa pamoja, sijaelewa kwa nini unataka makosa yake yapite bila kupingwa kisa tu kaleta hoja unayoiita janga la kitaifa…. huu utakuwa ubishi kama sio ujuaji wa kipumbavu.

“Usini-diss kwa kiswahili kama hujui hata kukitamka”.
 
Kushindwa kuitamka herufi fulani kwa sababu ya athari ya lugha mama ni jambo linaloeleweka na liko kwa jamii nyingi ila kuchanganya herufi ni jambo lingine kabisa.
Ni kweli baadhi ya watu wa Kanda ya ziwa hawana L, kwa maana hutegemi kumsikia akisema UgoLo badala UgoRo.

Pia unaweza kuwa na shida ya kutamka ila ikifika hadi kuandika mtu bado anachanganya huyo ni kilaza tu.
Mara nyingi hizo R na L husababishwa na asili ya watu! Mfano watu wa Kanda ya Ziwa, kimsingi hawana L! Badala yake wana R tu!! Niretee ugari, Niretee Gwajima, nk.

Ukienda Dodoma, Iringa, nk huko hawana R! Badala yake wana L tu! Badala ya kutamka Iringa , wenyeji hutamka Ilinga! Dodoma nako kila neno lenye R, hugeuzwa na kuwa L! 'Napeleka malejesho', nk.

Mifano ni mingi, muda ni mchache.
 
Ni watangazi vihiyo, na wanapaswa kuondolewa kwenye hivyo vyombo vya habari kabisa kwa sababu wanakuza ukubwa wa hilo tatizo.
Ajabu hata baadhi ya watangazaji wa vituo vya runinga na redio ni waathirika wa kuchanganya R na L.
 
Makosa ni makosa tu hata kama kwako yanavumilika, tunatofautiana kiwango cha kuyavumilia….. kama kwako sio tatizo haimaanishi yapo sahihi.

Jenga utamaduni wa kukosoana kama tulivyo sisi akili kubwa, hata muuaji anapofiwa hulia machozi.
Yapo makosa yanayovumika kwenye kiswahili. Hivi unajua Zanzibar wanaandika ''mwengine'' na sisi tunaandika ''mwingine''?
 
Back
Top Bottom