Hivi idara ya usalama wa taifa wa Tanzania inahusika na kila kitu hadi uuzaji wa nyanya na vitunguu magengeni?

Sasa kama ni hivyo tutafika kweli?
 
Nilishangaa nilipoona stick za kuchokonolea meno (Tooth Sticks) zinatoka china, tissue yani yale makaratasi yanatoka china. Sasa hiyo financial intelligence unit sio tu kufuatilia miamala ya Chadema na wapinga serikali walipaswa wawe silaha ya kuandaa sera ya maendeleo na kushauri na kusimamia utekelezaji wake, lasivyo tutajeuzwa wategemezi na hii hasara yake tushaiona kwakua hela yetu haina nguvu tunakua forced kununua vitu nje kwa Dola mwisho wa siku ipo siku mkate tutaunuua kwa Million moja ya Tsh, usishangae maana leo hii mkate unauzwa 4000/=, wakati huo ulikua mshahara wa miezi minne wa Mwl. Nyerere alipokua Mwalimu.
 
Mkenya wewe

Sent from my Infinix X656 using JamiiForums mobile app
 
Bila Ujasusi wa kidola na Kiuchumi kufanya kazi hawa ccm watatupigisha Kwata hadi Mwisho wa Dahali.

Kule China Technolojia yao ya Uvuvi ya Mwaka 1990 iko mbele yetu kwa zaidi ya Miaka 50 mbele.

Yaani uvuvi wetu wa mitumbwi na taa za karabai hazifui dafu kwa uvuvi wa China wa Mwaka 90s.

Sasa kama CCM ina Urafiki na undugu wa tangu zamani na Kama Nchi tuna uhusiano mzuri wa Kidiplomasia( kama wanavyodai) kwa nini Ubalozi wetu na makachero wetu wasitumie fursa hii kuomba Technolojia ya China ya Mwaka 90 ambayo kwa wao ilishapitwa na wakati lakini kwetu itatusaidia sana.

Nini kinashindikana? Urafiki wetu na China ni upi hasa?

Hili kwanini hawalioni? Au wanalipuuza?

Enzi za Hayati Dr Magufuli akiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi alitwambia Bahari na maziwa yetu yana samaki wengi sana ambao tangu Kuumbwa Ulimwengu hawajawahi kuvuliwa kutokana na ujuzi duni tunaotumia.

Naliombea Taifa tujikite kwenye vitu vinavyounganisha Wananchi wote na kulete maendeleo.

Kwani.africa tuna shida gani?
 
Hao jamaa wana control kila kitu unachofanya na unachotaka kukifanya na humu ndani afisa vipenyo Aka makachero wapo humu ukitaka kujua zaidi tafuta series inaitwa person of interest utajua mengi zaidi
Nyie mnadanganya sana madogo. Hao jamaa wa kawaida tu hawana hizo sifa mnazowapa. Tunaona madudu mengi sana hapa nchini wao wapo kama hawapo vile. Kifupi ni kuwa mnawabebesha mzigo ambao hawajauweza.
 
Usalama wa taifa wana viwanda vinatengeneza bidhaa hafifu ambaxo hazinunuliki, kwani wewe hujui?
 
Ni kweli HUELEWI. Na KOSA sio lako ni Usalama wa Taifa.
Idara hii ni engine ya nchi kuanzia Siasa, Uongozi, sanaa , Uchumi na kila jambo.
Fikiria vetting ya viongozi imekaa kiwizi wizi na ukabila au Makundi nani analaumiwe?.
Fikiria leo rasilimali za umma zinaibwa nani alaumiwe?.
Kila taasisi za nchi wako kule lkn hakuna kinafanyika. Nani alaumiwe?
Hii nchi imefikia sehemu kweli ya kuwa watu ni chawa wa mtu mwingine kwa kisingizio cha Uanaharakati au uchama dola na kupongeza yasio na maana.

My Take. Labda wakili kuwa hawana meno kazi yao ni kutoa taarifa na wanaowapa wanatia mfukoni. Hivyo chombo kinahitaji mabadiliko
 
Ukiona uchumi wa nchi uko stable, tambua ya kwamba,wazee wa idara ya usalama wa Taifa wamesimama vizuri katika eneo lao. Tatizo letu idara hii inachanganywa na chama Dola.
 
Hakuna lolote.

Usalama wa taifa hawahusiki na mambo ya bamia magengeni!
 
Ukiona uchumi wa nchi uko stable, tambua ya kwamba,wazee wa idara ya usalama wa Taifa wamesimama vizuri katika eneo lao. Tatizo letu idara hii inachanganywa na chama Dola.
Uchumi mzuri hautikani na usalama wa taifa!

Uchumi mzuri ni zao la sera nzuri, utawala bora, utawala wa sheria, ubunifu, uvumbuzi, na uchapaji kazi.

Sitoshangaa endapo huko CCM kuna watu wenye fikra kama zako na ndo maana tuna uchumi mbovu na tuko maskini wa kutupwa maana tunaongozwa na watu wasiojua cha kufanya.
 
Hakuna lolote.

Usalama wa taifa hawahusiki na mambo ya bamia magengeni!
Labda kama huelewi kuwa kabla bamia haijawa gengeni iliingia nchini toka Hollandi kama mbegu ya kawaida au GMO na baadae ikalimwa kwa viritubisho vya ARV lkn muuza genge ni yule mama ambaye tajiri amenunua eneo lao soko akafukuzwa sasa ana genge karibu na barabara au dampo.
Hili jina tu Usalama wa Taifa linasanifu kuwa hawana mipaka kwa ajili ya Taifa.
Au wewe unadhani ni wale wanalinda Raisi na viongozi? Hao ni kitengo kidogo ndanibya idara. Wako majeshini. Wako TRA wako taasisi zote hadi wakulima wa mbogamboga na wafugaji.
Ni hayo tu . Na log off
 
Sawa Bwana Junya mwenzangu,mimi nafanya Biashara ya Cosmetics,wambie TIC wafanye updatio masuala ya Cosmetics and foods yapo TBS na masuala ya Drugs and medical devices yapo TFDA.
Sasa tulejee mada yetu;umo TBS na TFDA,TISS wamo kama wote kuanzia Maabara mpaka kwenye masuala management.
Mashirika yote ambayo yanadili na masuala nyeti kama Afya ya Mtanzania TISS wapo Mkuu.
Ulizungumzia nyanya,kama zinatoka nje ya nchi pia jicho la TISS lipo na kama zinazalishwa nchini basi Madawa yote yanayotumika kwenye Kilimo husika ni lazima yathibitishwe.

Sent from my V2111 using JamiiForums mobile app
 
Sasa naanza kuelewa kwa nini Tanzania ni banana Republic!

Ni kwa sababu ya ujinga kama huu.

Kudhani kuwa usalama wa taifa ndo watengeneza sera za kiuchumi.

Kudhani kuwa usalama wa taifa ni wataalamu wa uchumi na maendeleo!

Hapa tulipo kiuchumi si bahati mbaya wala si ajali.

Ni matokeo ya kutojua cha kufanya.
 
Nyie mnadanganya sana madogo. Hao jamaa wa kawaida tu hawana hizo sifa mnazowapa. Tunaona madudu mengi sana hapa nchini wao wapo kama hawapo vile. Kifupi ni kuwa mnawabebesha mzigo ambao hawajauweza.
Imbecile
 
Wewe kweli junya.

Hata hujui tofauti ya R na L.

Hujui R uitumie wapi. Hujui L inatumika wapi.

Sasa ndo utajua dhima ya usalama wa taifa kweli?
 
Nlitaka kuandika ujinga sijui nn kiliniambia chungulia profile nakuta joined 2006 πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…