Hivi inakuwaje msomi wa mambo ya fedha hajui shilingi Elfu 10 ina mnyama gani? Anashindwa kujibu kwenye interview

Kwa hiyo finance Manager anayesimamia mikopo na marejesho hatakiwi kujua hata hela ya marejesho inafananaje?
kwani kuna mtu alishawahi kukosea mahesabu au kuzidisha pesa kwa kutojua mnyama aliyepo kwenye noti ya elfu 10?
 
Kwani mtaala wa fani zao una sehemu watu wanapaswa ku cover Alama katika pesa..?
Kama hakuna basi hio knowledge haina mashiko.
Jiongeze sio kila kitu kiko covered kwenye sylabuss learn outside the box pia
 
Huoni hilo ni swali la kijinga kuwepo kwenye interview...
 
SWALI LA HOVYO SANA NA PANEL NZIMA HAIKUWA MAKINI YOU NEED TO REIEW QUESTIONS HILO SIO SWALI KABISA...FINANCE MANAGER KUJUA NOTI INA PICHA GANI DUUU
 
TEMBO ANASAIDIA NINI KATIKA MAHESABU.....
 
Una
Bahati uko mbali maana hata nilikuuliza unaweza google au kutafuta references. Hata wewe unaweza ukaulizwa swali la kijinga kama hilo ukibananishwa na ukashindwa kujibu.
 
Sijaona mantiki ya hilo swali. Kwenye mambo ya fedha kuna mengi sana sio huo upuuzi wa kuulizana kwenye noti kuna mnyama gani. I believe interview haitapata right person. Wataalam wa interviews zenye kugundua weledi na ujuzi kama say pricewater coopers hawawezi kuuliza huo ujinga.

Unauliza maswali kama hayo ili yasaidie nini kwenye kutafuta mtaalam wa fedha ovyo kabisa
 
Mwl wangu wa Advance Maths aliwahi kuniambia " Ukitaka kupambana na Tembo jifunze kwanza kupambana na sisimizi"
 
Kwa hali niliyoona nadhani tatizo la ajira linasingiziwa wasomi wetu wakipigwa simple questions tu wako weupe vichwani hata swali dogo tu kama hilo ambalo lina match na fani zao kabisa.
Sioni chochote cha kulaumu hapo. Hata leo ukiambiwa uchore bendera ya Taifa kwa kushtukiza, upangilie kama zilivyo, utachemka. Na kadri unavyosoma zaidi, mambo ya zamani ni rahisi kusahau.
 
Watafute mtu mwenye darasa la Saba...akijibu Hilo swali...wampe...kazi...

Hatuwezi dharau taaluma za watu kisa kutojua swali Kama Hilo...

Kama wewe unajua hilo.swali linatosha kumuajiri mhasibu.... Basi fanya wewe hiyo kazi ya uhasibu...Jibu SI unalijua

Rubbish
 
Nlifanya interview Empower...HAWANA Maswali ya KIPUUUZI Kama haya..

WANAKUULIZA maswali yanayoendana na taaaluma..

Sasa mhasibu Kuna topic ya kujua kwanzia shilling hamsini Hadi elfu kumi...Zina Alama gani...

Duties zake...zakila siku atakua anaangalia TEMBO kwenye elfu KUMI...

huyo consultant msimuajiri TENA.....hajui NINI ANAFANYA
 
Yani kundi la watu (na wewe ukiwemo) mnakubaliana kuuliza picha iliyopo kwenye noti ili kupima ubora wa FINANCE MANAGER..!!!?[emoji1745][emoji134]
Yaaani Huyu HR...hajui Majukumu ya Finance Manager?... [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]


Khaaaaaaa.....yaani Manager Ni senior position ... manager Ni kiongozi...
Unamuuliza maswali ya noti ya elfu kumi....

Nawapa swali jingine Noti ya elfu kumi Ina number ngapi ubavuni kwake.....kamuulize hili Head of finance....lazima atakua anajua..
 
Hayo Ni maamuzi yako..Hata ukiamua akae TU nyumbani ...pia Ni sawa
 
We mwenyewe hapo unajikuta una elimu eti below standard mtihani mtihani tu acha kuleta dharau kila kitu kilaumu wasomi wa tz wameshindwa basi ukipata vijpesa kidogo eti wanashindwa kujibu wangejibu wote kwa ufasaha mngewaajiri wote
 
Mkuuu...hatusomi Noti za nchi mbali mbali kwenye uhasibu....plse..

Huyo consultant is a Fool...mlipa kazi ya kuwakosesha watu sio kupata mtu...
 
Just imagine mtu kutoka.Kenya angekuuja kwenye hiyo interview...au unafikria uhasibu Ni fani wanasoma watanzania Tu.....

Mtu akiwa mhasibu anaweza fanya kazi nchi yoyote... Ile..

Ina maana Mimi nikienda kufanya interview Kenya...hili ndo swali natakiwa kuulzwa...

Wewe HR na huyo consultant....Ni mabogus...tena ndo nyie mnaitwa Mediocres.
 
Nlishawai kwenda kwenye interview ya UHasibu ..wakaniuliza. Nitaje Mawaziri wakuu Wote wa Tanzania tangia UHURU....[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]....

Nakuna interview nshaenda Pale CBA bank....nliulizwa maswali nikajiona Sikujiandaaa...vyema....unafeli unakubali kuwa ulitakiwa Ujue Ila hujui....


Acheni kuzadharua Taaluma za watu...kwa kuwapima vitu vya nje ya taaluma yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…