Hivi inawezekana ukahama na mita yako ya umeme?

Hivi inawezekana ukahama na mita yako ya umeme?

EvilSpirit

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2017
Posts
10,576
Reaction score
16,644
Swali langu ni je inawezekana ukahama na mita yako ya umeme? Mfano ulipanga chumba cha biashara sehemu na hiyo sehemu hakukuwa na umeme ukafanya michakato TANESCO ukavuta umeme.

Baada ya muda ukajenga chumba chako cha biashara na unataka kuhama hapo ulipopangisha. Je, inawezekana ukawaomba tanesco wakaifungue ile mita na kuja kufungiwa kwenye sehemu yako?
 
Inawezekana, andika barua TANESCO.

Kwa kawaida ile mita ya umeme ni mali ya Tanesco hivyo hata kwenye kuiamisha kwenda kwingine au ukibomoa nyumba na ukataka kujenga tena, lazima kuwajulisha jamaa
 
Kwa uelewa wangu kama icho kibanda umejenga hapo hapo pembeni ya ulipopanga inawezekana unaandika barua inapewa gharama inahamia jengo jipya,kama eneo tofauti na hapo aiwezekani lipia mita nyingine
 
Utahama na mita yako endapo tu utapata ruhusa kutoka ofisi ya TANESCO.

Tofauti na hapo huruhusiwi kuhama na mita bila makubaliano ya TANESCO.

Mita ni mali ya TANESCO na ikiharibika unapewa nyingine bure.
Namaanisha lazima niwasiliane nao.Ila nilikuwa tu nataka kujua kama huwa wanaruhusu
 
Kwa uelewa wangu kama icho kibanda umejenga hapo hapo pembeni ya ulipopanga inawezekana unaandika barua inapewa gharama inahamia jengo jipya,kama eneo tofauti na hapo aiwezekani lipia mita nyingine
Hapana mkuu ni sehemu nyingine kabisa sio hapo
 
Swali langu ni je inawezekana ukahama na mita yako ya umeme? Mfano ulipanga chumba cha biashara sehemu na hiyo sehemu hakukuwa na umeme ukafanya michakato TANESCO ukavuta umeme.

Baada ya muda ukajenga chumba chako cha biashara na unataka kuhama hapo ulipopangisha. Je, inawezekana ukawaomba tanesco wakaifungue ile mita na kuja kufungiwa kwenye sehemu yako?
ELIMIKA NA TANESCO

MWONGOZO KUHUSU KUHAMISHA MITA KUTOKA ENEO MOJA KWENDA ENEO JINGINE

Je mteja anaweza kuhamisha mita kutoka eneo moja kwenda eneo lingine?

Jibu la TANESCO

[emoji3578]Mita ni kifaa kinachotumika kupima matumizi ya mteja kadiri ya matumizi yake.

[emoji3578] Mteja halipii wala kununua mita bali analipia gharama halisi ya kufungiwa umeme (Service line connection fee).

[emoji3578]Mita inaendelea kuwa mali ya TANESCO wakati wote mteja anaotumia umeme.

[emoji3578]Mita ya umeme ikiharibika au kupata hitilafu yeyote ambayo haitokani na uzembe au matumizi mabaya ya mteja, TANESCO inabadilisha mita hiyo kwa gharama zake kwa kuwa ni kifaa chake.

[emoji3578] Wajibu wa mteja wa TANESCO unaanzia baada ya mita kuingia ndani ndio maana mteja au fundi (mkandarasi) haruhusiwi kufanya matengenezo yoyote kwenye mita ya TANESCO, wala kuifungua.

[emoji3578] Mita ya umeme ikishafungwa haiwezi kuhamishwa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine isipokuwa ndani ya ploti / kiwanja husika na inafanywa na TANESCO kupitia maombi kwa maandishi ya mteja.

[emoji3578] Unapoona hitilafu yeyote kwenye mita au kifaa chochote cha umeme kuanzia kwenye mita kwenda nje toa taarifa TANESCO mara moja na sisi tutaifanyia kazi bila gharama yeyote.

Toa taarifa kupitia [emoji116]

[emoji3578] TANESCO APP

[emoji3578]Facebook/twitter/tanesco yetu

[emoji3578]Instagram:tanesco_official page

[emoji3578]Tovuti: www.tanesco.co.tz

[emoji3578] Barua pepe: Customer.service@tanesco.co.tz

[emoji3578] Huduma kwa wateja
0768 985 100/ 022 219 4400

TANESCO Tunayaangaza Maisha yako
 
Swali langu ni je inawezekana ukahama na mita yako ya umeme? Mfano ulipanga chumba cha biashara sehemu na hiyo sehemu hakukuwa na umeme ukafanya michakato TANESCO ukavuta umeme.

Baada ya muda ukajenga chumba chako cha biashara na unataka kuhama hapo ulipopangisha. Je, inawezekana ukawaomba tanesco wakaifungue ile mita na kuja kufungiwa kwenye sehemu yako?
Ile meter imeandikwa kabisa kuwa ni mali ya TANESCO, wewe umekodishiwa tuu, usijaribu kuhamisha utashitakiwa kwa kuhujumu uchumi
 
Nikihama naruhusiwa kuhama na nguzo na nyaya za service line nilizolipia?
Hapana haujazilipia hizo bali ulilipua ada ya kuunganishiwa umeme. Hii inadhirishwa na kiasi ulicholipia mfano 27000 kwa vijijini au 177000 kwa mijini
 
Ila inaniuma sana kuliachia jitu mita ambayo nimeigharamikia 1,250,000/= cha kuingizia umeme naondoka nacho.
 
Hapana haujazilipia hizo bali ulilipua ada ya kuunganishiwa umeme. Hii inadhirishwa na kiasi ulicholipia mfano 27000 kwa vijijini au 177000 kwa mijini
Tulikuwa tunatumia Meter moja na mwenye nyumba aliyetupangisha kibishara
sasa kila mmoja akaweka meter yake kwenye nyumba/Plot hiyo hiyo tukaiacha ya mwenye nyumba, tukawa na meter zetu kwa majina yetu,
Leo mwenye nyumba kanifukuza kwa Mkataba kuisha hataki niendelee, Meter nimeiacha
Je ni ya Tanesco wataitoa au kumpa Mteja mwingine kwa jina langu au itabaki hapohapo.
maana aliyeingia hatumii umeme na ina deni la miaka ya nyuma bado kwisha
Nikiitaka nihame nayo nikaendelee kumalizia nitapewa?
 
Hawa jamaa bana sasa hapa hata nikihama nayo mbona inaendelea kuwa mali yao sijasema kwamba nikihama nayo ndio inakuwa ya kwangu.Nikiacha mita pale nahisi nakuwa kama nimemnufaisha mwenye nyumba.
 
Back
Top Bottom