Hivi inawezekana ukahama na mita yako ya umeme?

Hivi inawezekana ukahama na mita yako ya umeme?

Hapana haujazilipia hizo bali ulilipua ada ya kuunganishiwa umeme. Hii inadhirishwa na kiasi ulicholipia mfano 27000 kwa vijijini au 177000 kwa mijini

177,000/=
Kama upo ndani ya mita 30 ni Tsh 321000 kwa mijini na vijijini ni Tsh 27000 tu

Hapa umesema 321,000/=

Sijui tuelewe lipi mkuu, mnatuchanganya kwakweli.
 
ELIMIKA NA TANESCO

MWONGOZO KUHUSU KUHAMISHA MITA KUTOKA ENEO MOJA KWENDA ENEO JINGINE


Je mteja anaweza kuhamisha mita kutoka eneo moja kwenda eneo lingine?

Jibu la TANESCO

[emoji3578]Mita ni kifaa kinachotumika kupima matumizi ya mteja kadiri ya matumizi yake.

[emoji3578] Mteja halipii wala kununua mita bali analipia gharama halisi ya kufungiwa umeme (Service line connection fee).

[emoji3578]Mita inaendelea kuwa mali ya TANESCO wakati wote mteja anaotumia umeme.

[emoji3578]Mita ya umeme ikiharibika au kupata hitilafu yeyote ambayo haitokani na uzembe au matumizi mabaya ya mteja, TANESCO inabadilisha mita hiyo kwa gharama zake kwa kuwa ni kifaa chake.

[emoji3578] Wajibu wa mteja wa TANESCO unaanzia baada ya mita kuingia ndani ndio maana mteja au fundi (mkandarasi) haruhusiwi kufanya matengenezo yoyote kwenye mita ya TANESCO, wala kuifungua.

[emoji3578] Mita ya umeme ikishafungwa haiwezi kuhamishwa kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine isipokuwa ndani ya ploti / kiwanja husika na inafanywa na TANESCO kupitia maombi kwa maandishi ya mteja.

[emoji3578] Unapoona hitilafu yeyote kwenye mita au kifaa chochote cha umeme kuanzia kwenye mita kwenda nje toa taarifa TANESCO mara moja na sisi tutaifanyia kazi bila gharama yeyote.

Toa taarifa kupitia [emoji116]

[emoji3578] TANESCO APP

[emoji3578]Facebook/twitter/tanesco yetu

[emoji3578]Instagram:tanesco_official page

[emoji3578]Tovuti: www.tanesco.co.tz

[emoji3578] Barua pepe: Customer.service@tanesco.co.tz

[emoji3578] Huduma kwa wateja
0768 985 100/ 022 219 4400

TANESCO Tunayaangaza Maisha yako
Naomba mnifahamishe gharama za kufungiwa mita ya Luku ktk kibanda changu cha biashara
 
Mita haihamishiki kwa sababu za kiusalama wa mapato, pia mteja hajalipia wala kununua mita ile ni mali ya TANESCO hivyo ukihama unaiacha pale pale kwa kuwa sio mali ya mteja.Kuhusu gharama zimepungua sana kutoa hapo awali
Kwa hii sheria yenu naona kama zimepitwa na wakati
Kwa sasa ni wakati wa kiruhusu mita mtu aweze kuhama nayo maana nyumba moja utakuta ina wapangaji 20 na kila mtu ana mita binafsi kulingana na matumizi yake sasa unapofika muda wa kuhama anaiacha na harudi TANESCO kuripoti mita inabaki kwa mwenye nyumba tuu ilhal mngeruhusu kuhama nayo mngekuwa pia mnaongeza mapato kwani iendako itakuwa bado inatumika
 
Back
Top Bottom