Hivi ingekuwaje 2015 kama tusingempata Hayati Magufuli kwa nchi ilipokuwa imefikia?

Hivi ingekuwaje 2015 kama tusingempata Hayati Magufuli kwa nchi ilipokuwa imefikia?

Magufuli hakuheshimu katiba, aliminya haki za wananchi, Alileta siasa za biashara za kununua watu, Aliiba chaguzi serikali za mitaa na uchaguzi mkuu kwa kiwango cha Kutisha, Aliua watu Zanzibar, Akaunda magenge ya wasiojulikana, wakateka, wakaua watu hivihivi bila hofu, Akatumia pesa za nchi bila due process, Alikuwa mkanda, Akanajisi bunge, vyombo vya habari na mahakama, Alikuwa katili alivunja nyumba za wananchi wakati kuna zuio la Mahakama, Akateua na kulinda viongozi washenzi kama akina Sabaya na Makonda, Alikuwa muongo, msanii asiye na lugha za staha.

Kiufupi huyo Magufuli wako alikuwa tje worst president, hatuwezi kumuweka katika kundi la marais wazuri wa nchi hii
aisee kumbe
 
Maisha yangekuwa Ni [emoji481][emoji512][emoji594][emoji594][emoji594][emoji597]
 
Uchumi na demokrasia ndio maisha yenyewe ya wananchi kama aliharibu hayo hakuna alichofanikiwa.
"Kwangu Mimi JPM alichohalibu ni swala la uchumi na democracy tu lakini kwa vitu vingine huyu jamaa alikua kichwa Sana tukichukulia na nchi ilipokua imefkia."

Naweza kukubaliana na wewe kwa kiasi fulani, mengine ni kuendekeza sana kupata sifa binafsi mpaka kufikia kusema vitu kama hakuna corona ambayo ilichangia vifo vya wengi. Lakini kuna vitu lazima tukubali amejitahidi especially miundombinu.
 
Nawasalimu ndugu zangu, natumai hamjambo wote.

Ndugu zangu sote tunakumbuka ni wapi nchi yetu ilipokuwa imefkia kwa ufupi ilikuwa inaenda shimoni kwa maana kila kitu kiliharibika na alihitajika kiongozi mwenye kaliba ya JPM kuitoa nchi Mahali ilipokuwa.

Nani hakumbuki hata viongozi wa upinzani waliwahi sema tunahitaji Rais dikiteta? Na kweli walikuwa sahihi kabisa manake tulikuwa pabaya mno.

Fikirieni nchi hadi tukawa hatuna Tena ndege, shirika la reli limekufa, huduma za jamii zimezolota kabisa. Kwa ufupi tufika pabaya mno kama nchi na suluhisho ilikua ni lazima apatikane mtawala kama JPM ili aweke nchi sawa kwanza ili baadaye ndo tuje tupate kiongozi.
Tatizo la JPM Naona alifanya kazi hadi akapitiliza.

Kwangu Mimi JPM alichoharibu ni suala la uchumi na democracy tu lakini kwa vitu vingine huyu jamaa alikuwa kichwa sana tukichukulia na nchi ilipokuwa imefikia.

Nawakumbusha Tena kwa tulipokuwa tumefika ilikuwa ni lazima tumpate JPM ili kuiweka nchi kwenye mstari.

Kwa hiyo tumpe sifa zake na yale mabaya aliyofanya tuchukue kama Somo ili tusonge mbele ndugu zangu.
Maisha yange kuwa kawaida tu kama ilivyo
 
Wewe ni ukiaji wa uchumi unangalia mengi sio hayo tu, kipindi cha Magufuri Miundombunu muhimu ilijengwa ambayo niyakukuza uchumi,amefufua mashirika mengi ya uzalishaji yaliyokuwa yamekufa,amejenga mji wa Dodoma, alijitaidi sana kupunguza foreen ktk jiji la dar-as-salaam ambao ilikuwa inapoteza mabilion ya shiling.Kama uwekezaji ndio ungelikuwa ni ndio kiashiria cha kukuza uchumi,ktk utawala wa Kikwete Tanzania ingelikuwa uchumi wa juu na si wakati, maana Kikwete ali leta wawekezaji wa kila aina lakini hata uchumi wa chini atukufika kwa miaka 10,alafu jua ya kwamba kuwa na uchumi wa kati sio kila Mtu atakuwa na pesa mfukoni, Kenya wanauchumi nzuri kuliko Tanzania kwa miaka mingi lakini nenda Kenya angalia maisha yao,hautatamani kuishi Kenya.Hata huko Ulaya wenye chumi kubwa zaidi kuliko huku sio kila Mtu anapesa.
Tanzania ni kubwa na watanzania ni wengi hivyo vipaumbele vya Magu ni kfunika kombe mwanaharamu apite,na si vinginevyo.
 
Back
Top Bottom