Hivi kuna Mganga anayeweza kumuua Mchawi?

Hivi kuna Mganga anayeweza kumuua Mchawi?

Aliye fanikiwa ku wauwa wachawi.. ajitokeze anisaidie Number za mtaalamu.. maana kuna watu wanacheza na familia yangu kimazingara.. Maombi yamewashindwa hawa mbwa dawa ni kuwaangamiza tu.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Piga vibao mwenyewe hao wapuuzi...Sijui kama utapata jibu hapa mkuu.
 
Njia ya Kuuwa wachawi.. tuna waondoaje maana maandiko na neno limeshindwa wanaendelea kutu tesa..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mkuu unataka mganga aanze tu kuuwa hao wachawi kwa sababu huwa wanakuroga? Mi navyojua labda ungesema uwekewe kinga ambayo mtu yeyote atakaye jaribu kukuroga litakalomkuta(kifo) ni juu yake ila sio kwamba mganga aanze tu kuuwa.
 
Sasa mchawi awe mganga ili iweje? Nachojua mganga anaweza kukuroga ila haina maana kuwa naye ni mchawi.
 
Yesu aliwahi kujibu hili mayahudi walipomzushia kwamba anatoa pepo kwa kutumia nguvu za beelzebul........akasema kwamba shetani hawezi kumtoa shetani mwenzie. Sasa hao wote, waganga, wachawi, walozi, wanga, wafanya matambiko, waliosimikwa uchifu mkuu wanafanya au wanashiriki nguvu za giza, kwa hiyo wote ni 'manzi ga nyanza' wote wanasubiri hukumu yao pamoja na mkuu wao ibilisi siku ya kiama......​
Kwahiyo na sisi Bar tunaoitana Chief kumbe tuna msala mzito!
 
Mganga na mchawi wote wanatoa nguvu zao toka chanzo kimoja. Hawawezi kuhitilafiana maana wanajenga ufalme mmoja wa nguvu za giza.

Yesu aligusia hili na kusema Shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake....kama ingelikuwa ni hivyo, Ibilisi angesimamishaje himaya yake? Hii ni baada ya baadhi ya wayahudi kumtuhumu kuwa anatoa pepo kwa njia ya Beelzebub mkuu wa pepo....yaani walimaanisha Yesu anatoa pepo kwa kutumia nguvu za giza.

Inahitajika nguvu kubwa zaidi independent ya ile ya Ibilisi ili kuweza kumshinda shetani na mawakala wake kama waganga au wachawi. Nguvu hiyo ni ya Mungu pekee.
 
Mkuu unataka mganga aanze tu kuuwa hao wachawi kwa sababu huwa wanakuroga? Mi navyojua labda ungesema uwekewe kinga ambayo mtu yeyote atakaye jaribu kukuroga litakalomkuta(kifo) ni juu yake ila sio kwamba mganga aanze tu kuuwa.
Kinga yenyewe ni jini tena waganga wengi wanatumie vile viini vya NDIZI, vinawekwa kwenye kona zote za nyumba, sasa huyu jini mwanzoni atawapukutisha wale wachawi wabishi watakaokusumbua. Maana wengine wakishaona una kinga wanasepa ila wengine watataka kushindana nguvu ndo watakuwa kitoweo cha huyu jini uliyopewa. Ila wachawi wakishajua kuwa hapo kwako hapaingiliki hawatokuja na jini nalo linakosa damu, kwahiyo mwishowe wale mnaoishi kwenye hiyo nyumba yenye hilo zindiko la jini mnakuwa target la hilo jini na mtaanza kuona MAUZAUZA na mambo mengi kuwa siyo au hata vifo kutokea...
 
Waganga ni wachawi...

Wachawi wanaweza kuuana kutegemea na nguvu na motive...

Hivyo mganga anaweza muua mchawi
 
Habarini wana JamiiForums,

Nimejaribu kujiuliza maswali, Kuhusu Uchawi na Uganga, sasa nikaja kugundua kwamba Hakuna Mganga asiye Mchawi na ingawa siyo wachawi wote ni waganga.

Sasa kinacho nifanya nije kwenu nikujua wataalaamu wa haya maswala kama wanaweza nipa Jibu ya swali langu, Kwamba Inawezekana kweli kukawepo Mganga ambaye anaweza kuwauwa wachawi? Maana mganga ni mchawi mwezao na kinachozidi tu ni kuwa mganga ana kipawa cha kutafuta dawa za tiba za miti shamba ila mchawi hawezi, sasa najiuliza ikiwa mganga ni watiba je anawezaje kuuwa Mchawi ikiwa nayeye ni mchawi je ana uwezo gani wazida zaidi ya miti shamba ya kutibu uchawi ulio fanywa na wachawi wenzake?

Kwanini nimewaza hivi ni jinsi ambayo unaweza kwenda kwa mganga aka kwambia ulichofanyiwa ila kamwe hata kwambia ni nani kafanya ikiwaaliye fanya ni mchawi ila kama aliye fanya siyo mchawi anakutajia jina la yule aliye kuendea kwa mganga kukuloga.

Sasa Basi kwa wale wajuzi wa mambo Naombeni mniambie kuna mganga yeyote hapa Tanzania mwenye uwezo wa kuuwa mchawi?

Asanteni.
Kimsingi,jibu ni Vifaa & Uzoefu
Mchawi mwenye uwezo Mkubwa ana access ya kumzima Mganga.

Mganga mwenye uwezo Mkubwa ana uwezo wa kumzima mchawi..

Wakikutana uwezo sawa..
Wanafanya makubaliano Abc bhasi.

Kinachotofautisha Kati ya Mganga na Uchawi ni Vipaumbele bhasi..
 
Mganga na mchawi wote wanatoa nguvu zao toka chanzo kimoja. Hawawezi kuhitilafiana maana wanajenga ufalme mmoja wa nguvu za giza.

Yesu aligusia hili na kusema Shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake....kama ingelikuwa ni hivyo, Ibilisi angesimamishaje himaya yake? Hii ni baada ya baadhi ya wayahudi kumtuhumu kuwa anatoa pepo kwa njia ya Beelzebub mkuu wa pepo....yaani walimaanisha Yesu anatoa pepo kwa kutumia nguvu za giza.

Inahitajika nguvu kubwa zaidi independent ya ile ya Ibilisi ili kuweza kumshinda shetani na mawakala wake kama waganga au wachawi. Nguvu hiyo ni ya Mungu pekee.
Si kweli kwamba mganga na mchawi wanatoa nguvu zao toka chanzo kimoja. Waafrika tumeaminishwa na wazungu kuwa Uganga ni kitu kibaya na kinatoka kwa shetani. Kwanza ni vema kujua tofauti ya uganga na uchawi. Hivi ni vitu viwili tofauti.
Mchawi yupo kwa ajili ya kuangamiza, kuharibu, kutia mikosi, na hata kuvuruga mambo mema. Kwanini? Uchawi ni roho ya uharibifu toka kwa shetani.

Uganga ni nini? Ni uponyaji, urejeshaji, ujengaji, uuwishaji, utabibu, na urekebishaji. Ndo maana kwa kiswahili asilia daktari anaitwa mganga. Ndo maana tuna Mganga Mkuu wa serikali, Mkoa na kadhalika. Neno Daktari si kiswahili.
Uganga ni utaalamu ambao uhitaji mafunzo ya muda mrefu, ambayo uhusisha utaalamu wa kibaiolojia na kikemia, kwa kutumia mimea kuweza kutibu wanyama, binadamu na hata mimea yenyewe. Utaalamu huu uambatana na kujua saikolojia ya mwili wa binadamu, wanyama na mimea yenyewe.

Nitajikita katika Uganga asilia wa utabibu, ambao upo kila sehemu duniani. Uganga asilia uhitaji mafunzo ya muda mrefu, na umejikita zaid ktk matumizi ya mimea. Mtu aweza jifunza unganga kupitia kwa mtu akimuonesha aina tofauti za mimea na namna inavyoweza kutibu magonjwa mbalimbali.
Mara nyingi uganga huu uambatana na nguvu za kinyota, uwezo wa kisaikolojia, ramli, nguvu za asili za ukoo au miujiza. Uganga haupo kuuwa wala kuangamiza. Bali utokea tu pale kuna ulazima wa kufanya hivyo, na mara nyingi utoa onyo mara kadhaa kabla ya kuangamiza au kuuwa. Na hii itafanyika kama kuna jambo au tukio lililoumiza zaidi.

Tofauti ya Uchawi na Uganga, mchawi hawezi tibu, bali ni kuangamiza. Na mchawi asilimia kubwa nguvu zake ni za giza. Hakuna upatano baina ya mganga na mchawi. Ndo maana wachawi wengi hujitahidi waangamize mganga au kuuwa. Waganga kutokana na nguvu kadhaa za kiroho, kiukoo, uweza kuzuia nguvu za kichawi. Kuzuia huku hakuwafanyi wao kuwa wachawi la hasha!

Uganga unatofautiana, kwakua swali ni iwapo mganga anaweza muuwa mchawi nitajibu kwa mlengo huo. Mganga mwenye nguvu, anauwezo huo. Ila hafanyi tu kuuwa kama mchawi anavyo fanya. Mganga atauwa mchawi kama mchawi kafanya jambo baya la kuumiza na kuleta masononeko kwenye jamii au familia.
Na mara nyingi mganga atatoa onyo ili muhusika au mchawi ajisalimishe na kutubu. Inaposhindikana ndo hapo mganga atauwa mchawi. Na wakati mwingine kama mganga ajafurahishwa basi uamua kumuuwa mchawi bila kuonya iwapo huyu mchawi atajiona yeye ni yeye.
Tukumbuke swala la kuuwa, hata madakitari wetu wanauwezo wa kuuwa mtu wanapoona kunahitajika. Hivyo nguvu za uuaji zinatofautiana.

Mchawi uchukua muda mpaka kumuuwa mtu. Uanza kumroga na kuleta mikosi kwa huyo mtu. Ushindana na roho au nyota ya huyo mtu hadi kummaliza. Niliambiwa mchawi uondoa roho ya mtu wakati wa jua na si usiku. Usiku anautumia kulegeza nguvu za kiroho alizo nazo mhusika.
Ni mara chache inatokea akikuua usiku, ila roho yako itaondoka wakati wa jua.

Katika maisha yangu, nilishuhudia mganga mmoja, ambae waliuwa mwanae. Huyu mganga aliumia na kutamka. waliofanya hivyo wote watakufa. Na kweli hawa wachawi walikuwa kumi walioshirikiana kuuwa. Mmoja baada ya mwingine walianza kuumwa. Nakumbuka kuna mchawi mmoja hakuwahi kufahamika ni mchawi. Yeye alikuwa na dawa ya kuoga akiroga uchawi utaonekana kwa mtu mwingine si yeye. Hivyo walipokuja waganga kutambua wachawi yeye hakutambulika. Bali uchawi wake aliuweka kwa mchawi mwingine alie tambulika.

Lakini kwa huyu mganga alinasa, aliumwa na kuanza kwenda kwa wanganga kutafuta dawa, kila alipofika kwa mganga fulani aliambiwa umechezea sehemu mbaya, utakufa. Hatuna dawa ya kukutibu. Hospitali na kwa waganga ilishindikana. Nikimtembelea huyu mchawi, alitia huruma. Aliongea kwa shida huku machoni akiwa na aibu kubwa. Tulijuana nae kwa miaka kadhaa na alikuwa mtu mwema kwangu. Ndo maana niliona nikamjulie hali.

Lakini siku Mganga huyu anafanya yake ili waliomroga mwanae wafe nilikuwepo. Tulienda nae wote eneo la kaburi. Wala hakutumia uchawi. Sipendi kusema hapa namna alivyofanya wachawi wote kumi wakafa. Ila niseme Mganga mwenye ujuzi wa hali ya juu, ambae yupo kwa tiba tu na kinga anauwezo wa kuondoa uhai wa mchawi kama kuna jambo la kuumiza limetokea na hatumii uchawi!

Waganga wengi wananguvu za kiroho, wanalindwa wasipate athari za kichawi kwa nguvu ambazo wao wamekingwa nazo. Ila mchawi akikuta mganga ambae si imara na huyu mganga anazuia mchawi huyo asifanye mambo yake basi mchawi anauwezo wa kumroga au kumuuwa mganga.

Mganga mara nyingi uletewa jonzi au maono, ndo maana anajua mambo kadhaa. Ila mchawi hana jonzi au maono anaporoga. Yeye inambidi ajibadilishe, awe kwenye mfumo wa roho chafu, au awe katika maumbile mengine ili akaroge.
Ni mara chache mganga anaweza akaingia ktk ulimwengu wa roho akapotea usimuone. Hii hutokea pale tu kuna jambo maalum mganga inabidi afanye. Na hii uwezeshwa na nguvu za kiroho alizonazo.

Waganga wana mengi mazuri shida fani imeingiliwa na matapeli. Waganga wengi wazuri hawahitaji fedha. Na wanajua mambo mengi, dawa nyingi. Na hawa mchawi hawezi kuwagusa. Wanaweza kukupa kinga ya mchawi asifikirie kukudhuru, au akitaka kukudhuru hakuoni. Hawa waganga hawapendi kuuwa kabisa.
Mganga na mchawi ni vitu viwili tofauti. hata majini hayapendi wachawi. Yaani ni uadui mkubwa. Ni kwanini Majini ni adui wa uchawi? Ni somo refu linahitaji muda.
Na katika uganga, upo wa majini, yaani umetokana na majini. Upo uganga umetokana na mizimu katika koo. Upo uganga unaotokana na mashetani, niseme huu mara nyingi si mzuri unakonekisheni na nguvu za kichawi.

Uchawi nao unatofautiana, kuna wanga, hawa mara nyingi hawana madhara, wanacheza tu, wakija kwako usiku ni kukubeatua kukusumbua yaani vituko vya kila aina. Lakini Mchawi halisi huyu anaroga, anauwa, anaharibu na kuangamiza. Huyu ni hatari sana kuliko mwanga wa kawaida ambae mara nyingi ni kucheza na kukusumbua tu. Hawezi kukuua.
 
Kinga yenyewe ni jini tena waganga wengi wanatumie vile viini vya NDIZI, vinawekwa kwenye kona zote za nyumba, sasa huyu jini mwanzoni atawapukutisha wale wachawi wabishi watakaokusumbua. Maana wengine wakishaona una kinga wanasepa ila wengine watataka kushindana nguvu ndo watakuwa kitoweo cha huyu jini uliyopewa. Ila wachawi wakishajua kuwa hapo kwako hapaingiliki hawatokuja na jini nalo linakosa damu, kwahiyo mwishowe wale mnaoishi kwenye hiyo nyumba yenye hilo zindiko la jini mnakuwa target la hilo jini na mtaanza kuona MAUZAUZA na mambo mengi kuwa siyo au hata vifo kutokea...
Mkuu wewe unazungumzia kinga ya nyumba ila mimi nilikusudia mtu mwenyewe kujikinga na si kuikinga nyumba, hata hivyo umeeleza vitu vipya kwa upande wangu kwamba kuna zindiko la nyumba lenye makubaliano ya jini kumpa kafara ya damu za wachawi.
 
Waganga ni wachawi...

Wachawi wanaweza kuuana kutegemea na nguvu na motive...

Hivyo mganga anaweza muua mchawi
Kwani mchawi ana sifa zipi hadi useme mganga nae ni mchawi maana mimi sielewi?
 
Kwani mchawi ana sifa zipi hadi useme mganga nae ni mchawi maana mimi sielewi?

Mganga hutumia nyenzo zile zile atumiazo mchawi...huu tunaoita uganga wa kienyeji ni aina mojawapo ya uchawi (uchawi upo wa aina nyingi)
 
Mganga hutumia nyenzo zile zile atumiazo mchawi...huu tunaoita uganga wa kienyeji ni aina mojawapo ya uchawi (uchawi upo wa aina nyingi)
Ni aina moja ipi hiyo ya uchawi ambayo unasema ndio tunaita uganga? Maana nachojua si kila mganga anajua masuala ya kichawi au yale wanayoyajua na kuyafanya wachawi na pia mchawi hawezi kuwa mganga kwa sababu tu ni mchawi. Uganga ni fani nyengine na mchawi yupo kwenye fani nyengine, ingawa yeyote anaweza akaroga hata mganga anaweza kuroga ila hiyo haina maana unakuwa mchawi.

Niliwahi kumshuhudia yule mganga manyaunyau alikuwa anakimbiza sijui dude gani(uchawi) sasa anapita mule mitaani akikimbiza hicho kitu ambacho wengine hatukuwa tukikiona kwa macho,alikuwa anazama hadi kwenye mifereji na akiona paka anakamata ananyonya damu. Cha ajabu wakati anapita kuna baadhi ya wamama ambao walikuwa wanahisiwa ni wachawi(sio waganga) walikuwa wanakimbia wenyewe wala manyaunyau hakuwa akishughulika nao.
Kwahiyo hapo utaona mchawi ni mtu mwengine tofauti na mganga na ndio maana huwa wananyolewa nywele.
 
Ni aina moja ipi hiyo ya uchawi ambayo unasema ndio tunaita uganga? Maana nachojua si kila mganga anajua masuala ya kichawi au yale wanayoyajua na kuyafanya wachawi na pia mchawi hawezi kuwa mganga kwa sababu tu ni mchawi. Uganga ni fani nyengine na mchawi yupo kwenye fani nyengine, ingawa yeyote anaweza akaroga hata mganga anaweza kuroga ila hiyo haina maana unakuwa mchawi.

Mtu akiwa na uwezo wa kuroga, tafsiri ya moja kwa moja inamueleza kuwa mtu huyo anafanya mambo ya kichawi, hivyo ni sahihi kuitwa mchawi...

Screenshot_20220131-170031-2.png
 
Mtu akiwa na uwezo wa kuroga, tafsiri ya moja kwa moja inamueleza kuwa mtu huyo anafanya mambo ya kichawi, hivyo ni sahihi kuitwa mchawi...

Screenshot_20220131-170031-2.png
Hata hapo tu utaona uchawi umeelezwa kuwa ni kitu chenye kusababisha madhara sasa utalinganishaje na uganga ambao hutumika kutibu? Ukiangalia maana ya mchawi utaona inasema kuwa ni mtu ambaye huaminiwa kwamba anaweza kuwadhuru watu kwa kuwaroga, hivyo ni tofauti na uganga ni kazi ya kuwaponya watu ni utabibu.

Kiuhalisia mchawi ni zaidi ya mtu kuweza kuroga tu ndio maana nikasema tunaona wachawi wakinyolewa nyewele kama kuondolewa nguzu za kichawi, kitu ambacho huwezi kusema utamnyoa nyewele mtu kisa tu anaweza kuroga jambo fulani.
 
Mganga wa kweli anakupa dawa ambayo unaweza kumuuwa panya anaekusumbua nyumbani. Ukifanikiwa kumuuwa na kumchoma hadi kijivi, punde utasikia mtu kaugua ghafla na kufa. Huyo panya ndiye mchawi.
 
Guys..
Naombeni anaye Jua sumu kali inayoweza kuwekwa kwenye Sindano kiasha akidungwa mtu hachukui dakika 5.

Nimepata dawa ya Kumkamata Mchawi na kumgandisha na pia kumuachia apotee.. nimefany ikafanya kazi nikawaona nika wahoji kisha nika waachia.. sasa naona wameniona mjinga wanaendeleea kuja.. nataka niki wateg round hii ni wadunge sindano kisha nowaachie wakafie makwao.

Kama una jua sumu kali au jina la dawa kama hiyo niambieni tafadhali.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom