Hivi kuna Mganga anayeweza kumuua Mchawi?

Hivi kuna Mganga anayeweza kumuua Mchawi?

Si kweli kwamba mganga na mchawi wanatoa nguvu zao toka chanzo kimoja. Waafrika tumeaminishwa na wazungu kuwa Uganga ni kitu kibaya na kinatoka kwa shetani. Kwanza ni vema kujua tofauti ya uganga na uchawi. Hivi ni vitu viwili tofauti.
Mchawi yupo kwa ajili ya kuangamiza, kuharibu, kutia mikosi, na hata kuvuruga mambo mema. Kwanini? Uchawi ni roho ya uharibifu toka kwa shetani.

Uganga ni nini? Ni uponyaji, urejeshaji, ujengaji, uuwishaji, utabibu, na urekebishaji. Ndo maana kwa kiswahili asilia daktari anaitwa mganga. Ndo maana tuna Mganga Mkuu wa serikali, Mkoa na kadhalika. Neno Daktari si kiswahili.
Uganga ni utaalamu ambao uhitaji mafunzo ya muda mrefu, ambayo uhusisha utaalamu wa kibaiolojia na kikemia, kwa kutumia mimea kuweza kutibu wanyama, binadamu na hata mimea yenyewe. Utaalamu huu uambatana na kujua saikolojia ya mwili wa binadamu, wanyama na mimea yenyewe.

Nitajikita katika Uganga asilia wa utabibu, ambao upo kila sehemu duniani. Uganga asilia uhitaji mafunzo ya muda mrefu, na umejikita zaid ktk matumizi ya mimea. Mtu aweza jifunza unganga kupitia kwa mtu akimuonesha aina tofauti za mimea na namna inavyoweza kutibu magonjwa mbalimbali.
Mara nyingi uganga huu uambatana na nguvu za kinyota, uwezo wa kisaikolojia, ramli, nguvu za asili za ukoo au miujiza. Uganga haupo kuuwa wala kuangamiza. Bali utokea tu pale kuna ulazima wa kufanya hivyo, na mara nyingi utoa onyo mara kadhaa kabla ya kuangamiza au kuuwa. Na hii itafanyika kama kuna jambo au tukio lililoumiza zaidi.

Tofauti ya Uchawi na Uganga, mchawi hawezi tibu, bali ni kuangamiza. Na mchawi asilimia kubwa nguvu zake ni za giza. Hakuna upatano baina ya mganga na mchawi. Ndo maana wachawi wengi hujitahidi waangamize mganga au kuuwa. Waganga kutokana na nguvu kadhaa za kiroho, kiukoo, uweza kuzuia nguvu za kichawi. Kuzuia huku hakuwafanyi wao kuwa wachawi la hasha!

Uganga unatofautiana, kwakua swali ni iwapo mganga anaweza muuwa mchawi nitajibu kwa mlengo huo. Mganga mwenye nguvu, anauwezo huo. Ila hafanyi tu kuuwa kama mchawi anavyo fanya. Mganga atauwa mchawi kama mchawi kafanya jambo baya la kuumiza na kuleta masononeko kwenye jamii au familia.
Na mara nyingi mganga atatoa onyo ili muhusika au mchawi ajisalimishe na kutubu. Inaposhindikana ndo hapo mganga atauwa mchawi. Na wakati mwingine kama mganga ajafurahishwa basi uamua kumuuwa mchawi bila kuonya iwapo huyu mchawi atajiona yeye ni yeye.
Tukumbuke swala la kuuwa, hata madakitari wetu wanauwezo wa kuuwa mtu wanapoona kunahitajika. Hivyo nguvu za uuaji zinatofautiana.

Mchawi uchukua muda mpaka kumuuwa mtu. Uanza kumroga na kuleta mikosi kwa huyo mtu. Ushindana na roho au nyota ya huyo mtu hadi kummaliza. Niliambiwa mchawi uondoa roho ya mtu wakati wa jua na si usiku. Usiku anautumia kulegeza nguvu za kiroho alizo nazo mhusika.
Ni mara chache inatokea akikuua usiku, ila roho yako itaondoka wakati wa jua.

Katika maisha yangu, nilishuhudia mganga mmoja, ambae waliuwa mwanae. Huyu mganga aliumia na kutamka. waliofanya hivyo wote watakufa. Na kweli hawa wachawi walikuwa kumi walioshirikiana kuuwa. Mmoja baada ya mwingine walianza kuumwa. Nakumbuka kuna mchawi mmoja hakuwahi kufahamika ni mchawi. Yeye alikuwa na dawa ya kuoga akiroga uchawi utaonekana kwa mtu mwingine si yeye. Hivyo walipokuja waganga kutambua wachawi yeye hakutambulika. Bali uchawi wake aliuweka kwa mchawi mwingine alie tambulika.

Lakini kwa huyu mganga alinasa, aliumwa na kuanza kwenda kwa wanganga kutafuta dawa, kila alipofika kwa mganga fulani aliambiwa umechezea sehemu mbaya, utakufa. Hatuna dawa ya kukutibu. Hospitali na kwa waganga ilishindikana. Nikimtembelea huyu mchawi, alitia huruma. Aliongea kwa shida huku machoni akiwa na aibu kubwa. Tulijuana nae kwa miaka kadhaa na alikuwa mtu mwema kwangu. Ndo maana niliona nikamjulie hali.

Lakini siku Mganga huyu anafanya yake ili waliomroga mwanae wafe nilikuwepo. Tulienda nae wote eneo la kaburi. Wala hakutumia uchawi. Sipendi kusema hapa namna alivyofanya wachawi wote kumi wakafa. Ila niseme Mganga mwenye ujuzi wa hali ya juu, ambae yupo kwa tiba tu na kinga anauwezo wa kuondoa uhai wa mchawi kama kuna jambo la kuumiza limetokea na hatumii uchawi!

Waganga wengi wananguvu za kiroho, wanalindwa wasipate athari za kichawi kwa nguvu ambazo wao wamekingwa nazo. Ila mchawi akikuta mganga ambae si imara na huyu mganga anazuia mchawi huyo asifanye mambo yake basi mchawi anauwezo wa kumroga au kumuuwa mganga.

Mganga mara nyingi uletewa jonzi au maono, ndo maana anajua mambo kadhaa. Ila mchawi hana jonzi au maono anaporoga. Yeye inambidi ajibadilishe, awe kwenye mfumo wa roho chafu, au awe katika maumbile mengine ili akaroge.
Ni mara chache mganga anaweza akaingia ktk ulimwengu wa roho akapotea usimuone. Hii hutokea pale tu kuna jambo maalum mganga inabidi afanye. Na hii uwezeshwa na nguvu za kiroho alizonazo.

Waganga wana mengi mazuri shida fani imeingiliwa na matapeli. Waganga wengi wazuri hawahitaji fedha. Na wanajua mambo mengi, dawa nyingi. Na hawa mchawi hawezi kuwagusa. Wanaweza kukupa kinga ya mchawi asifikirie kukudhuru, au akitaka kukudhuru hakuoni. Hawa waganga hawapendi kuuwa kabisa.
Mganga na mchawi ni vitu viwili tofauti. hata majini hayapendi wachawi. Yaani ni uadui mkubwa. Ni kwanini Majini ni adui wa uchawi? Ni somo refu linahitaji muda.
Na katika uganga, upo wa majini, yaani umetokana na majini. Upo uganga umetokana na mizimu katika koo. Upo uganga unaotokana na mashetani, niseme huu mara nyingi si mzuri unakonekisheni na nguvu za kichawi.

Uchawi nao unatofautiana, kuna wanga, hawa mara nyingi hawana madhara, wanacheza tu, wakija kwako usiku ni kukubeatua kukusumbua yaani vituko vya kila aina. Lakini Mchawi halisi huyu anaroga, anauwa, anaharibu na kuangamiza. Huyu ni hatari sana kuliko mwanga wa kawaida ambae mara nyingi ni kucheza na kukusumbua tu. Hawezi kukuua.
Uko vizuri. Ni wachache sana waliokuelewa. Wengine wanakurupuka tu.
 
Mbona unapayuka na kupaniki mdogo wangu ...nimeshafanya kazi huko NIMR unapopaongelea na nadhani unachanganya mada hapa.

Sijakataa utabibu /uganga unaohusisha miti shamba, asili ya dawa karibu zote zinatokana na miti. Ninachopinga ni waganga waotumia mashetani wa kijini katika kuagua watu.

Mfano mdogo unaweza kunambia ni mti gani unaotumika na hawa waganga kupiga ramli?

Pia ukija kwenye mada kuhusu majini vilevile utakaa? Hakuna sehemu niliochanganya kuhusu mashetani ba majini.

Majini ni viumbe vilivyoumbwa kwa miale ya moto, na ushetani ni sifa ya kiumbe muasi aliyekengeuka kwa mola wake,shetani anaweza kuwa mwanadamu au jini!!! Nafahamu ninachokiongea kijana
Sijapayuka wewe ndo umepaniki. Hakuna kupayuka kwa maandishi, kupayuka inakuwa na sauti. Elewa matumizi ya maneno.
Kufanya kazi NIMR si kigezo. Wewe ndo ulikuja kwa maneno yasiyo na msingi. Hapa tukijitangaza tumefanya kazi wapi utashangaa.

Shetani ni shetani na jini ni jini. Kwanza uwezi mwona shetani, lakini waweza muona jini. Mara nyingi jini anaweza jibadili akawa kitu chochote. Lakini shetani ni roho chafu isiyoonekana.

Unaweza ukaishi na jini, ukamtuma kazi yoyote akafanya. Wapo majini wapole na wastaarabu, mpaka uwauzi ndo wanaweza kukutesa. Na ni marafiki. Na mara nyingi ili wawe rafiki na binadamu wanajibadili kuwa binadamu, mwaweza ongea vizuri tu. Nashukuru mara kadhaa nimeonana na majini. Ni rafiki wazuri.

Na ujue kuna watu baadhi ya maeneo wanafuga majini na kuishi nao.
Ila uwezi fuga mashetani.
Mashetani ni roho chafu zisizoonekana kwa macho ya nyama bali katika ulimwengu wa roho. Na masetani yapokuangamiza na kuharibu.

Narudia jini na mchawi hawapatani. Na jini hampendi kabisa mchawi.
So usilazimihe mambo usiyoyajua. Sema ufundishwe.

Kuna mizimu pia. Hii ni miungu. Ina nguvu za kimungu na uabudiwa. Zinauwezo wa kufanya lolote, kuangamiza au kubariki.
 
Sijapayuka wewe ndo umepaniki. Hakuna kupayuka kwa maandishi, kupayuka inakuwa na sauti. Elewa matumizi ya maneno.
Kufanya kazi NIMR si kigezo. Wewe ndo ulikuja kwa maneno yasiyo na msingi. Hapa tukijitangaza tumefanya kazi wapi utashangaa.

Shetani ni shetani na jini ni jini. Kwanza uwezi mwona shetani, lakini waweza muona jini. Mara nyingi jini anaweza jibadili akawa kitu chochote. Lakini shetani ni roho chafu isiyoonekana.

Unaweza ukaishi na jini, ukamtuma kazi yoyote akafanya. Wapo majini wapole na wastaarabu, mpaka uwauzi ndo wanaweza kukutesa. Na ni marafiki. Na mara nyingi ili wawe rafiki na binadamu wanajibadili kuwa binadamu, mwaweza ongea vizuri tu. Nashukuru mara kadhaa nimeonana na majini. Ni rafiki wazuri.

Na ujue kuna watu baadhi ya maeneo wanafuga majini na kuishi nao.
Ila uwezi fuga mashetani.
Mashetani ni roho chafu zisizoonekana kwa macho ya nyama bali katika ulimwengu wa roho. Na masetani yapokuangamiza na kuharibu.

Narudia jini na mchawi hawapatani. Na jini hampendi kabisa mchawi.
So usilazimihe mambo usiyoyajua. Sema ufundishwe.

Kuna mizimu pia. Hii ni miungu. Ina nguvu za kimungu na uabudiwa. Zinauwezo wa kufanya lolote, kuangamiza au kubariki.
Mpaka hapo sina haja ya kuendelea na mjadala na wewe kwasababu unaonesha kujivunia ujinga wako hadharani.

Ngoja nikupe ilmu ndogo tu. Hayo maneno mawili Jini (jinni) na shetani (shaytwaan) asili yake ni kiarabu. Kwahiyo ili kuipata maana halisi ya hayo maneno ni lazima urudi kwenye lugha ya kiarabu ambayo nina uhakika kuwa huijui.

Jinni (jini) ni kiumbe aliyeumbwa na Mungu kabla ya mwanadamu na waliishi katika uso huu wa ardhi miaka mingi kabla ya kuumbwa kwa Adam. Asili ya maumbile yao ni moto wakati mwanadam asili yake ni udongo mweusi wa mfinyanzi.

Shetani (shaytwaan) ni sifa ya kiumbe muasi (mchochea maasi) , sifa hii anaweza kuwa nayo mwanadamu na vilevile anaweza kuwa nayo Jini.

Kwahiyo basi kuna mashetani wa kijini na mashetani wa kibinadamu vilevile. Majini wamegawanyika makundi mawili kuna waja wema na kuna mashetani (waovu), hawa mashetani kiongozi wao ni Iblis. Iblis anawatuma kuja ardhini kuchochea dhambi na uasi kwa wanadamu. Na pia mashetani wa kibinaadamu nao huwa ni mawakala wa iblis, anawatumia kuchochea maasi na uasi kwa wanadamu wengine.

Tukirudi katika point yako unayosema kuwa shetani haonekani na jini anaweza kuonekana, hapa sio kweli. Mashetani wa kibinadamu wanaonekana waziwazi ,wakati mashetani wa kijini wao hawaonekani.Mungu amemuwekea mwanadamu pazia katika macho yake asiweze kuyaona majini katika umbile lao ila mwanadamu anaweza kumuona jini pale tu jini atakapochukua umbile la mdudu au mnyama au mtu.

Jini anaweza kuchukua umbile la mbwa mweusi,ng'e,nyoka au hata umbile la mwanadam...hapa ndipo binadamu atakapoweza kumuona ila kwenye umbile lake halisi mwanadamu huwezi kumuona jini.

Ukimuacha Nabii Suleyman bin dawood hakuna mwanadamu mwingine aliyepewa kibali cha kuyamiliki majini na kuyatumikisha .Ukimuona mwanadamu anafuga majini na kuyatuma yamfanyie kazi jua kuwa huyo ni mshirikina na ni wakala wa Iblis. Majini hayakai kwa mtu ikiwa mtu huyo hayatumikii majini kwa kuyatolea sadaka ya vichinjwa n.k (kuyaabudu).
 
Sijapayuka wewe ndo umepaniki. Hakuna kupayuka kwa maandishi, kupayuka inakuwa na sauti. Elewa matumizi ya maneno.
Kufanya kazi NIMR si kigezo. Wewe ndo ulikuja kwa maneno yasiyo na msingi. Hapa tukijitangaza tumefanya kazi wapi utashangaa.

Shetani ni shetani na jini ni jini. Kwanza uwezi mwona shetani, lakini waweza muona jini. Mara nyingi jini anaweza jibadili akawa kitu chochote. Lakini shetani ni roho chafu isiyoonekana.

Unaweza ukaishi na jini, ukamtuma kazi yoyote akafanya. Wapo majini wapole na wastaarabu, mpaka uwauzi ndo wanaweza kukutesa. Na ni marafiki. Na mara nyingi ili wawe rafiki na binadamu wanajibadili kuwa binadamu, mwaweza ongea vizuri tu. Nashukuru mara kadhaa nimeonana na majini. Ni rafiki wazuri.

Na ujue kuna watu baadhi ya maeneo wanafuga majini na kuishi nao.
Ila uwezi fuga mashetani.
Mashetani ni roho chafu zisizoonekana kwa macho ya nyama bali katika ulimwengu wa roho. Na masetani yapokuangamiza na kuharibu.

Narudia jini na mchawi hawapatani. Na jini hampendi kabisa mchawi.
So usilazimihe mambo usiyoyajua. Sema ufundishwe.

Kuna mizimu pia. Hii ni miungu. Ina nguvu za kimungu na uabudiwa. Zinauwezo wa kufanya lolote, kuangamiza au kubariki.
Hatuwezi kuelewana kwasababu ndani yako una imani ya kishirikina. Kitendo cha kusema kuwa mizimu ni miungu inaonesha kuwa hujui kitu na hujui hiyo mizimu ni nini! Pia tukirudi ktk suala unalodai kuwa jini na mchawi hawapatani ni uongo tu.

Majini wamegawanyika makundi mawilj , wapo waliomuamini Mungu na wapo waliomkataa Mungu.Kama ilivyo kwa wanadamu leo wapo wanaomuamini Mungu na wapo wanaomkataa Mungu.

Majini wasiomuamini Mungu ndio huitwa masheytwaan wa kijini na hawa ni marafiki kindakindaki na wanadamu wasiomuamini Mungu. Kama unavyoona mlevi rafiki yake ni mlevi mwenzie.

N wapo majini ambao ni wachamungu hawa nao ni marafiki na wanaadamu ambao ni Wachamungu na huwa hawaingilii maisha ya mwanadamu kama kumuingia mwilini na kumtumikisha. Wao wanaishi maisha yao kama wao ila hawa wasiomuamini Mungu ndio unaowaona wakiingilia maisha ya wanaadamu kwa kuwaingia kwenye miili yao na hata kuwadhuru. Pia huwatumikia wale wanaadamu ambao wamekubali kuwaabudu na kuwatii. Mfano humletea pesa na vito vya thamani mwanadamu ambae amekubali kuwatii,kuwaabudu na kuwanyenyekea.Pia huweza kutumwa kwenda kuwadhuru watu ambao wanatakiwa kudhuriwa na huyo mtu anayewafuga n.k

Mara nyingi majini yanayofugwa na mwanadamu huwa yamekimbia adhabu ujinini kutokana na makosa mbalimbali waliyoyafanya kama wizi,uuaji au ubakaji, so wanakuja nchi kavu kwa wanadamu na kuomba hifadhi kwa mwanadamu na mwanadamu huyo akikubali kuwapa hifadhi katika mwili wake na makazi yake ndio huahidi kumtumikia mwanadamu huyo kwa masuala nbalimbali.

Naongea haya nikiwa nishakaaa na watu wenye haya masheytwaan katika miili yao na hata kuongea na hayo majinj yenyewe.
 
Habarini wana JamiiForums,

Nimejaribu kujiuliza maswali, Kuhusu Uchawi na Uganga, sasa nikaja kugundua kwamba Hakuna Mganga asiye Mchawi na ingawa siyo wachawi wote ni waganga.

Sasa kinacho nifanya nije kwenu nikujua wataalaamu wa haya maswala kama wanaweza nipa Jibu ya swali langu, Kwamba Inawezekana kweli kukawepo Mganga ambaye anaweza kuwauwa wachawi? Maana mganga ni mchawi mwezao na kinachozidi tu ni kuwa mganga ana kipawa cha kutafuta dawa za tiba za miti shamba ila mchawi hawezi, sasa najiuliza ikiwa mganga ni watiba je anawezaje kuuwa Mchawi ikiwa nayeye ni mchawi je ana uwezo gani wazida zaidi ya miti shamba ya kutibu uchawi ulio fanywa na wachawi wenzake?

Kwanini nimewaza hivi ni jinsi ambayo unaweza kwenda kwa mganga aka kwambia ulichofanyiwa ila kamwe hata kwambia ni nani kafanya ikiwaaliye fanya ni mchawi ila kama aliye fanya siyo mchawi anakutajia jina la yule aliye kuendea kwa mganga kukuloga.

Sasa Basi kwa wale wajuzi wa mambo Naombeni mniambie kuna mganga yeyote hapa Tanzania mwenye uwezo wa kuuwa mchawi?

Asanteni.
nimemkumbuka dr manyaunyau na profesa maji maref
 
Back
Top Bottom