Hivi kunywa pombe ni dhambi?

Hivi kunywa pombe ni dhambi?

Eeh hi nayo kali,nipe kwanza hilo Andiko.
Kwaio ukinywea pombe Kanisani au Msikitini sehemu takatifu takatifu haina shida eti?
Wapi nimetaja kanisani pombe Kuna mazingira ukinywa ni haramu na Kuna mazingira ni halali kunywa pombe nyumbani kwako au sehemu iliyotulia ujazwe na Roho usinywe pombe sehemu ya bar au club
lakini pia unapotaka kutafuta mtotot mke wako usinywe pombe ni haramu
 
Wagalatia 5:19-21
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Kama una mpango wa kuingia Mbinguni au Peponi acha pombe,
inauwezo mkubwa wa

Wagalatia 5:19-21
Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,
husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Kama una mpango wa kuingia Mbinguni au Peponi acha pombe,
inauwezo mkubwa wa kukukwamisha kuingia mbinguni.

1 Wakorintho 6 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
⁹ Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
¹⁰ wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.

Mbingu ni ya watu safi,sober.
Mfano tu mdogo.
Kama kazini kwako huruhusiwi kwenda umelewa, je Mbinguni si zaidi.
Kati ya Mungu na Mwanadamu wa kuheshimiwa zaidi ni yupi?
Basi pombe haifai kwa mtu mwenye nia ya kwenda Mbinguni.
Tumieni akili kidogo. Wewe ni mgalatia au mkoritho? Acheni hizo bana. Sisi watz hatumo kabisa humo,tuacheni tufurahi. Mbona umalaya mbafanya? Mnakomaa tu pombepombeee!
 
Tumieni akili kidogo. Wewe ni mgalatia au mkoritho? Acheni hizo bana. Sisi watz hatumo kabisa humo,tuacheni tufurahi. Mbona umalaya mbafanya? Mnakomaa tu pombepombeee!
Mm akili kidogo niliyotumia ni hii kwamba kama kazini kwangu si ruhusiwi kwenda nimelewa ,je Mbinguni si zaidi?
Ķama kwa mganga siwezi pigiwa manyanga nimelewa je kwa Mungu si zaidi?
Kama mahakamani siwezi sikilizwa nikiwa nimelewa je kwa Mungu si zaidi?
Ndio maana nakubaliana na wagalatia na Wakorintho,
Maana kama ww tu huwazi kwa akili ndogo kma hii yangu basi kuna mahali akili yako haifikirii ikafika.
Mada ni pombe ingeletwa mada ya umalaya nayo tungeisemea kitu hapa.
 
Wakuu, jana nimetoka kwenye mishe zangu nikapitia bar flani ya jirani kupooza koo kidogo.

Wakapita walokole flani hivi tunafahamiana nikawapungia mkono,wakaniita pembeni,jambo Lao kubwa likawa wananiambia eti niache kunywa pombe kwani unywaji wa pombe ni dhambi kubwa sana.

Nikawaitikia ila baadae nikafungua Biblia kutafuta mstari wowote unaosema kuwa kunywa bia ni dhambi lakini sijaona popote palipoandikwa hivyo.

So labda na nyie mnisaidie kujua wakuu,je kunywa pombe ni dhambi au sio dhambi?
Ungemfungulia biblia asome hapa
 

Attachments

  • IMG_3624.jpeg
    IMG_3624.jpeg
    219.7 KB · Views: 3
Wakuu, jana nimetoka kwenye mishe zangu nikapitia bar flani ya jirani kupooza koo kidogo.

Wakapita walokole flani hivi tunafahamiana nikawapungia mkono,wakaniita pembeni,jambo Lao kubwa likawa wananiambia eti niache kunywa pombe kwani unywaji wa pombe ni dhambi kubwa sana.

Nikawaitikia ila baadae nikafungua Biblia kutafuta mstari wowote unaosema kuwa kunywa bia ni dhambi lakini sijaona popote palipoandikwa hivyo.

So labda na nyie mnisaidie kujua wakuu,je kunywa pombe ni dhambi au sio dhambi?
Sàsa hukuelewa nini? Walokole wamekwambia kunywà POMBE ni dhambi kubwa sana.
Wewe ukafungua biblia kutafuta mstari ulioandika kunywa BIA ni dhambi.
Mbona hayo ni maandishi tofauti? Huwezi kuona neno BIA.
Tafuta kile ulichoambiwa na walokole, POMBE.
 

1 Wakorintho 6:9-10​


Au je, hamjui kwamba watu wabaya hawataurithi ufalme wa Mungu? Msijidanganye! Watu wanaoishi maisha ya uasherati, wanaoabudu sanamu, wazinzi, au walawiti, wezi, wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyanganyi, hao wote hawatashiriki ufalme wa Mungu.
 
But as long as naamini dini ni mambo ya uwongo. Basi wewe fanya chochote unachojiskia kufanya, kama hakikufarakanishi na mwenzako hicho ni chema
 
Kila kitu kisizidi uwezo wako kukihimili.Too much of anything is harmful.Lokoles huwa wenyewe kila kitu ni kibaya kwao.Yani ilimradi usifurahie maisha.Wapo medieval ages kila muda.
na hivyo vyote wanavyokataza hadharani, wao wenyewe wanavifanya kwa siri....lokoles ni wanafiki NAMBARI wani..🚮🚮
 
Screenshot_20241212-072151.jpg

Mithali 31: 4-6

Hapo mstari wa 6 masikini tumeruhusiwa kunywa tusahau shida zetu.

Tuendelee kula vyombo.
 
Back
Top Bottom