Hivi kutoka kuwa Mkuu wa JKT mpaka kuwa Mkuu wa Mkoa ni kupanda au kushuka?

Mambo Mengine Yanatia Kinyaa!!
Teuzi Hizi Sijui Huwa Wanawaza Nini
Mikoa ya mipakani yenye viashiria vya uchochezi huwa wanawekwa wanajeshi tena wenye ngazi ya juu kwa ajili ya kudhibiti mienendo ya waasi...

Mtwara na Ruvuma kwa sasa nazo zimepewa RC wanajeshi pengine kwa ajili ya kupambana kwa namna yoyote na wale waasi wa Msumbiji...

Mikoa kama Kagera na Kigoma ni karibu kila muhula utakuta ma RC ni watu wa jeshi...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Geshi Jeshi Mipakani
 
CDF wengi huwa wanatokea JKT.

Huyu naye alikua ana andaliwa kama mwenda zake angekuwepo kwa sababu alionekana ni mti wa maagizo yake.
Nimeona Mkuu wa JKT, Brigedia Jenerali Charles Mbuge ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Je, amepanda au ameshuka?

 
Hapana , si kushuka. Huenda amestaafu. Aliyekuwepo kabla yake naye alikwenda kuwa wa mkoa fulani nyanda za juu kusini
Yaani ni kama wamemshusha kiaina maana alikuwa anaandaliwa na mwenda zake kuwa mkuu wa majeshi alipandishwa vyeo harakaharaka kuliko kawaida,Mbuge kwakweli alijua kuicheza ngoma ya jiwe busungu akasome
 
Yeah nakumbuka alirukishwa vyeo hatari,alitoka luten kanali mpaka Brigedia General bila kwenda hata kozi then baada ya muda mfupi akapewa umeja jeneral na kupewa madaraka ya kuongoza JKT.
Baada ya miezi 6
 
Mkuu wa Majeshi ndo atampigia RC (Mwakilishi wa Rais) salute
 
Huyu ndo alihujumu ajira 800 za vijana wa JKt na kuwaita waasi
 
Mkuu wa Majeshi ndo atampigia RC (Mwakilishi wa Rais) salute
sio kweli....ikiwa RC ambae ni mwanajeshi...anajua protocal za kijeshi na siku hiyo wakikutana huku RC akiwa amevaa uniform...atakae anza kupiga saluti ni RC...SALUTI ata mgambo asie na cheo chochote anaweza kupigiwa
 
Kutoka kuwa kuu wa taasisi overall inchi nzima mpaka kuwa confined Kwenye kimkoa kimoja!
mnatafsiri mambo kishule shule.

mkuu wa kitengo ndani ya jeshi,hawezi kuwa sawa na mkuu wa mkoa mzima.
mkuu wa jkt anaripoti kwa mnadhimu,halafu mkuu wa majeshi.
mkuu wa mkoa anaripoti kwa rais moja kwa moja.
hiyo ni kuonyesha kuna kamanda hapo,halafu kuna kiongozi.kwamba sasa anakwenda kujibia taasisi zaidi ya moja eneo fulani.
hata kiukubwa mkoa mmoja una watu,na pilika nyingi kuliko hiyo jkt nzima.

kinachopungua hapo labda ulaji ulaji.
 
hakuna shida mkuu wakivaa uniform wote yeye atapiga salute.

ila huyu asipovaa cdf atapiga[emoji1787][emoji1787].huo ndio utamu wa jeshi.
 
Hiyo demotion mnazozungumzia labd kwenye field zenu huko za jeshi,lakini kiutawala amepanda cheo yupo level moja na Waziri na anareport moja kwa moja kwa Rais.
 

Overall will never be equal to partitioned or portioned
 
Komenti ya DHAHABU....👍
 
Duuuuhhhh akili zingine bwana.
Kwahiyo DSO ni mkuu kuliko RPC kwakuwa DSO kateuliwa na Rais na RPC kawekwa na IGP?
Hapo kapata demotion ya kushkaji.
Amepanda......

Kutoka UKAMISHNA wa kuripoti kwa mkuu wa JESHI LA ULINZI mpaka UKAMISHNA wa KURIPOTI KWA RAIS.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…