Hivi kwa nini mtu mzima akiua paka maisha yake yanakuwa mabovu sana

Maisha yako ya hapo awali na hivi sasa yapo sawa?
 
Dah nilivyokuwa mdogo nilimsindikiza mwenzangu alikamata paka kwenda kumpelekea manyaunyau tukapewa 5000 kwa paka mmoja

RIP paka yule

Halafu hapa mitaa ya home kuna mipaka inakera usiku na mikelele ,jiraji yetu alitaka awawekee sumu nikamkataza
Ulifanya jambo zuri kumkataza
 
[emoji124] [emoji124] [emoji124] [emoji124]
 
Haya ni mambo ya Dunia ya tatu si rahisi kuyaelewa hivihivi mpaka wajuvi wa mambo wakufunze ,,,,,,ni sawa na kuruka na ungo ,,sasa jiulize ungo una machine ipi mpaka ikuwezeshe kupaa?
Tuwangoje
 
Great thinkers njoeni mnipe ufafanuzi kuhusu mada yangu
Sijui labda kwa baadhi ya jamii... Ila kwetu hakuna kitu kama hicho. Nina rafiki yangu maeneo ya Tabata alitegea sumu mapaka asbh tukakuta paka karibu 13 wamekufa, lkn kimaisha hy jamaa yangu maisha yk yako poa. Alikuwa ameajiriwa lkn now amesajiri kampuni yake inapiga kazi kimataifa. Mwezi uliopita alikuwa anamalizia taratibu za kiserikali ili afungue kiwanda cha ku pack maji amechimba visimavya kutosha. Nina friend wangu mwingine ni mdada mwezi uliopita ameua mapaka kama ma3 lkn yuko poa. Sasa inawezekana ni imani tu kama ss kwetu wanasema kuua mnyama ambaye umewahi kumlisha/kumpatia chakula kwa mkono wako ni mwiko. Lakini mi niliuwa jibwa langu lilikuwa linazingua na niko poa. Kuna imani zingine zipo zipo tu ila ukiziamini zinafanya kazi.
 
Ukiona hivyo baada ya kuua alirudi kwao kutambika au alimtafuta mtaalamu amzingue/amtibu

Na ndio maana baada ya muda mafanikio yake yakawa makubwa kuliko yale ya hapo mwanzoni.

Ila hakuna anayeua paka bila kupata misukosuko yoyote maishani.
 
Ni imani zisizo na msingi. Paka ni mnyama kama wengine na hana uwezo wa kukupa mikosi. Imani unaijenga wewe kwa kuweka vitu kichwani na kujipa wasiwasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…