Hivi kwa sasa unafanya kazi ya ulichokisomea au ulipoteza tu muda na pesa shule funguka

Hivi kwa sasa unafanya kazi ya ulichokisomea au ulipoteza tu muda na pesa shule funguka

Genius Man

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2024
Posts
1,012
Reaction score
2,317
Kijana huyu hapo chini kwenye picha ni mwanasheria lakini anafanya kazi ya kuuza genge baada ya kuona ajira hazieleweki. (eastafricaTv)

Mdau hebu tuambie je Kwasasa unafanya kazi ya ulichokisomea?

Screenshot_20240911-233936.jpg
 
Ni sawa na dokta wa meno, akauze maembe sokoni, wakati kuna wagonjwa wengi mtaani wanahitaji huduma ya meno.
Watu wanaanza kuendea malengo yao wakiwa na changamoto tofauti mkuu. Mimi naweza kuwa na baba strict na anatoa mwongozo, mwingine hana. Mwingine kwao kuna hela mwingine hana. Mwingine aliingia kazini zama za unafuu wa ajira na mitaji mwingine alihitimu Magufuli akiingia madarakani akapiga 'mitano tena' mtaani.

Mwingine kapata network ya mambo yake kirahisi, mwingine karudi kuanzia kujipanga kwao
Sasa huyo daktari wa meno ndio kwanza kahitimu aanze kutung'oa meno na plies? Hana ajira, inabidi aanze na kinachowezekana wakati bado hajawa na nguvu ya kuanzisha clinic, tuwapongeze hawafanyi uhalifu mkuu.

Kingine nafikiri hakuna kupoteza muda katika kuwa na maarifa na kujifunza
 
Ingekuwa vizuri ukaanza kwa kufunguka wewe mkuu.
Mimi nimesomea masuala ya kodi kwa ngazi ya chuo, lakini natumia zaidi nilichosomea ngazi ya sekondari.
Kuna watu nawafahamu wamesoma Kiswahili ngazi ya chuo, lakini wanafanya kazi kama bankers.
Tuendelee kuwa encourage watu kupata maarifa.

Kwa kifupi tu mkuu sisi ni miongoni mwa nchi za watu wengi wenye maarifa madogo, ukiweza ingia hata Dar es Salaam randomly watest wakubwa na vijana kwa maswali ya general knowledge katika masuala ya afya,biashara,historia na jiografia.

Utakutana na watu wanakuelezea kazi za ini kwa sifa za mapafu, kazi za utumbo kwa sifa za moyo🙁
Kazi za manispaa na halmashauri kwa sifa za TRA😳

Kauli kama vile "kwao huko mikoa ya kusini kusini Kigoma,Kigoma, Kagera,Kagera huko"🙂

Ukiweza pia mkuu jitahidi upate maoni ya katiba mpya kipindi cha tume ya Warioba yale maoni kabla hayajawekwa sawa kukidhi mahitaji.

Mpaka leo kuna "wajinga" wanaweza sema anataka kufanya kazi fulani halafu anataja vyeo, utaskia nataka kufanya kazi ya Uraisi badala ya kusema siasa, kufanya kazi ya u IGP badala ya kusema Polisi,unakuwa unajiwazi moyoni huyu mtu hata uwezo wake wa kutengeneza mantiki utakuwa na tatizo.

Kibaya zaidi unakuta wanaoongea hivyo miaka yao ni 20-45. Mpaka unakiri kimoyo moyo kuwa kwa kweli kama taifa tunastahili kuwa hapa tulipo.

Tukiri tu wajinga wengi wamewazidi nguvu wenye maarifa, na silaha sahihi ni kusambaza knowledge, overtime vizazi vitajikomboa.
 
Kijana huyu hapo chini kwenye picha ni mwanasheria lakini anafanya kazi ya kuuza genge baada ya kuona ajira hazieleweki. (eastafricaTv)

Mdau hebu tuambie je Kwasasa unafanya kazi ya ulichokisomea?

View attachment 3093614
Kwa kuwa hii ni mida mibaya , hii mada tutaamka nayo asubuhi japo cha kuwakumbusha tu HESLB wameingia mkataba na NIDA pamoja na RITA 🤣
 
An Accountant, a CPA holder. Nafanya nilichosomea.
Napenda pesa zangu binafsi sana. Mama yangu aliwahi niambia, ningekuwa mwanaume ningekuwa jambazi [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28] Napenda pesa, halafu nazipenda tena. Naipenda na kazi yangu.
Umetishaaaa BL, mathe ulibutuaa haswaaa!!!
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom