Hivi kwanini watu sahihi hawakutani kwenye mahusiano

Hivi kwanini watu sahihi hawakutani kwenye mahusiano

Shida iko kwenye tafsiri ya mtu sahihi, utulivu kabla ya kuamua kuingia kwenye mahusiano na tamaa kutangulia mbele.

Kabla ya kujiuliza huyo mtu sahihi unayemtaka wewe, je yeye naye anakuona wewe ni mtu sahihi kwake?

Kuna tofauti kati ya mtu sahihi na mtu mzuri. Kama wewe huna pesa na maisha yako yana mtazamo wa kuhitaji pesa zaidi ili kuwa yenye furaha basi mtu sahihi kwako huenda akawa ni yule mwenye pesa lakini hiyo haimaanishi huyo mtu atakuwa mzuri kwako kimaisha.

Yote kwa yote, mpaka watu wanaamua kuoana basi ujue wazi wamekutana na kujiridhisha kuwa wao ni watu sahihi waliokutana. Simamia hapo hapo.
 
Wanaume sahihi hatupati wake sahihi , wake sahihi hawapati waume sahihi 😃 Dunia ngumu hii .. hivi kwanini watu sahihi huwa hatukutanagi . Nahisi shetani ana mkono wake katika hili. Unaona dada wa watu anateseka wakati anasifa zote ... kukutana watu wanao pair ni mara chache mara nyingi mtu akiwa negative atakutana na positive , akiwa north atakutana na south
Mimi ngumi mkononi kweli nikutane na ngumi mkononi mwenzangu itakuwaje hapo si tutakufa mapema bora tu nikutane na wanyonge niwanyooshe.
 
Kwani uliruka somo la Sumaku zinavyofanya kazi, South pole inavutana na North pole. Ule ulikuwa mfano tu wa maisha ya huko duniani... Ndo maana misemo nayo imekuwa mingi utasikia , "Mungu anakupa stahili hakupi unachotaka" we ishi tu
Nadhani mtu sahihi ni formality tu, Mungu anakupa unacho stahili, binadam wengi hawaelewi hili na kinachotumaliza tunakuwa tuna idea mtu sahihi kwetu yukoje.
 
Usahihi wako uko kwa kile ulichokipata.
Uwe mvuta bangi upate Muimba kwaya? Utampata mvuta bangi mwenzio.

Kumekucha kumekuchwa 🤣🤣🤣🤣🏃🏃🏃🏃🏃🏃
 
Kwa maana nyingine unasema kwann watu perfect hawakutani kwenye mahusiano. Its simple. Dunia ina operate kwa namna ya kipekee sana kwamba mwenye mapungufu akutane na mwenye ukamilifu fulani ili waboreshane sababu hata huyu mkamilifu atakuja mhitaji huyu wa mapungufu kwenye maeneo fulani huko baadae.

Ukiwa wewe ni muaminifu unakutana na asiyemuaminifu, ukimkazia atabadilika kwa niaba yako.
 
Anayemuona sahihi mwenzake hataki hata kumtaja jina lake.

Amuonaye mzuri, kwa mwenzako kituko.

Usiombe yakukute!
 
Kwani wewe Ulishawahi kuuona huo Mkono wa shetani anao ingiliaga nao Kati??
 
Kama ungemuoa uliyembikiri wala usingekuwa na haja ya kuja kulia lia hapa. Huyo ndiye alikuwa mtu sahihi kwako kiroho. Sasa wewe umeenda kuparamia wake za watu huko waliobikiriwa na waume zao kisha wakakimbiwa kama wewe ulivyofanya kwa uliyembikiri, unategemea mtashabihiana saa ngapi?

Na inasemekana kuwa soulimeti huja mara moja tu katika maisha yako - mtu inatokea tu mna-click hatari. Mnakubaliana. Yaani hakuna juhudi yo yote. Mnakuwa washikaji kabisa na mnaelewana katika level ya undani mno. Sema sasa shida ni kwamba mara nyingi unakutana na soulimeti wako wakati wewe bado hujajitambua. Mtu anakupenda sana kwa dhati kabisa kabisa bila sababu yo yote. Lakini kwa vile hujui hata unachokitafuta kwa mwenza wako wala humjali mpaka huyoo anachoka na kwenda zake. Na hapo sasa ndo kimbembe kinaanza na moto unakuwakia hatari maana kila utakapogusa unakuta pa moto. Soulimeti wako huyoo keshaenda zake.

Ufanye nini basi hili likikutokea? Tulia. Kaa chini upange vigezo vyako vya KIUHALISIA mtu sahihi kwako ni yupi? Vigezo vyako ni lazima vile vya KIUHALISIA na visiwe kama vya yule soulmate wako uliyemwachia akaenda maana wa aina hiyo hutakaa umpate tena.

Na kama bado hujampa soulimeti wako basi tulia. Hatimaye mtatafutana tu maana inaaminika kwamba mtu na soulimeti wake maficho yao huwa yako kwenye koja moja!

Be gentle to your girl. She might be your soulmate...and once you let her go...she is gone! FOREVAAA!!!
 
Mtu sahihi ni nadharia tu kwenye dhana nzima ya mahusiano
Binadamu sio mashine kusema amepangwa kufanya hivi na hivi, ni kiumbe complex sana na hatabiriki kabisa

Mara nyingi sana wale tunao waona wamekutana sahihi huwa ni wale wanaoweza kuvumiliana na kuchukuliana tofauti zao

Tatizo kubwa ni kwamba watu wanaingia kwenye mahusiano wakiwa na matarajio yasio halisi kwasababu ya simulizi au kuona sinema tamthilia vitabu vya simulizi nzuri za mahusiano
 
Back
Top Bottom