Kama ungemuoa uliyembikiri wala usingekuwa na haja ya kuja kulia lia hapa. Huyo ndiye alikuwa mtu sahihi kwako kiroho. Sasa wewe umeenda kuparamia wake za watu huko waliobikiriwa na waume zao kisha wakakimbiwa kama wewe ulivyofanya kwa uliyembikiri, unategemea mtashabihiana saa ngapi?
Na inasemekana kuwa soulimeti huja mara moja tu katika maisha yako - mtu inatokea tu mna-click hatari. Mnakubaliana. Yaani hakuna juhudi yo yote. Mnakuwa washikaji kabisa na mnaelewana katika level ya undani mno. Sema sasa shida ni kwamba mara nyingi unakutana na soulimeti wako wakati wewe bado hujajitambua. Mtu anakupenda sana kwa dhati kabisa kabisa bila sababu yo yote. Lakini kwa vile hujui hata unachokitafuta kwa mwenza wako wala humjali mpaka huyoo anachoka na kwenda zake. Na hapo sasa ndo kimbembe kinaanza na moto unakuwakia hatari maana kila utakapogusa unakuta pa moto. Soulimeti wako huyoo keshaenda zake.
Ufanye nini basi hili likikutokea? Tulia. Kaa chini upange vigezo vyako vya KIUHALISIA mtu sahihi kwako ni yupi? Vigezo vyako ni lazima vile vya KIUHALISIA na visiwe kama vya yule soulmate wako uliyemwachia akaenda maana wa aina hiyo hutakaa umpate tena.
Na kama bado hujampa soulimeti wako basi tulia. Hatimaye mtatafutana tu maana inaaminika kwamba mtu na soulimeti wake maficho yao huwa yako kwenye koja moja!
Be gentle to your girl. She might be your soulmate...and once you let her go...she is gone! FOREVAAA!!!