Hivi kweli kuna cha kujifunza kutokana na uchaguzi wa Afrika Kusini kama taifa?

Hivi kweli kuna cha kujifunza kutokana na uchaguzi wa Afrika Kusini kama taifa?

hakuna ambacho kingefanikiwa hata chembe. By the way mapinduzi attempts zilifanyika zaidi ya hiyo but ilikua ngumu na itakua ngumu mno as we go on šŸ’
Baada ya Nyerere kuona vile ilibidi ang'atuke maana alijua tuendako ni kubaya. Hata hayo mapinduzi yasipofanikiwa, kitendo tu cha kufanyika kutapelekea mageuzi makubwa maana itakuwa ni wakeup call kwa majizi ya kura.
 
Amani na Haki ni Chupa na kifuniko. Unategemea Amani idumu hutendi Haki? Basi Haki imeshindikana punguzia Waliokupa mamlaka (wananchi) mizigo mfano Kodi, Afya nafuu, Fursa sawa kiuchumi, (Na Ajira kama wakati wa JK. Yeye aliweza vipi?)
Hata jela, tunawaona wafungwa na mgwanda yao wakitumikishwa, je, wana amani!? Wana raha? WaTz kukaa kimya pamoja na shida zetu zote wanasiasa/watawala wasifikiri ndo amani hiyo. Hata mfiwa hucheka pia ...nk
 
Nadhani Tanzania bado ni darasa na shule kuu ya kipekee mno ya demokrasia barani Africa. Ni nchi pekee ya wananchi wasiozingatia ukabila, ukanda wala rangi ya mtu kwenye uchaguzi.

Shukrani za kipekee ni kwa Baba wa Taifa Mw.J.K Nyerere kutujengea kama Taifa, utamaduni, mila na desturi hii ya kutokubaguana kulingana na misingi isiyofaa, iliyotuepusha na ubaguzi wa aina zote na kuchochea utu, heshma, haki na usawa kwa binadamu wote...

Kama Taifa, hatuna budi kuitunza na kujivunia tunu hii muhimu sana, iliyokijita ndani ya mioyo ya waTanzania na inayotufanya kijilikana na kufahamika duniani kama kisiwa cha amani.

La muhimu ni AMANI na kwamba kasoro na dosari katika uchaguzi haziepukiki.

Mungu Ibariki Tanzania :whatBlink:
Uchaguzi wa Afrika ya kusini umengozwa na vijana waliozaliwa baada ya ubauguzi wa randi; kwa hiyo hawaelewi chochote kuhusu ANC kuleta uhuru, wao wanaangalia maisha yao ya sasa. Hakuna ajira, mabomba hayana maji masafi, hgakuna umeme wa uhakika. Wanatake mageuzi ya kiuchumi, siyo tena sera za "ANC iliondoa ubaguzi na kuleta uhuru"

Tanzania haiweizx kujifunza kwa sababu vijana wengi wa kitanzania wanarubuniwa kirahisi sana na CCM
 
Mi nadhani Cha kujifunza ni kuwa jamii iliyo elimika haidanganyiki kirahisi hapa kwetu watu wamenyimwa elimu ndio maana wamegeuka chawa wakupigia kelele watawala
Ni vile TU hawasemi ila wa SA wengi wanataka DA irudi haraka madarakani sema ni vile wanavutavuta upepo kidogo
Kizazi kijacho kitawarudisha madarakani.
 
Uchaguzi wa Afrika ya kusini umengozwa na vijana waliozaliwa baada ya ubauguzi wa randi; kwa hiyo hawaelewi chochote kuhusu ANC kuleta uhuru, wao wanaangalia maisha yao ya sasa. Hakuna ajira, mabomba hayana maji masafi, hgakuna umeme wa uhakika. Wanatake mageuzi ya kiuchumi, siyo tena sera za "ANC iliondoa ubaguzi na kuleta uhuru"

Tanzania haiweizx kujifunza kwa sababu vijana wengi wa kitanzania wanarubuniwa kirahisi sana na CCM
Hakuna kurubuniwa sema serikali ni wezi waliamua wote wawe wezi linalokuwa na liwe.Haiwezekani ndani ya miaka 10 eti hakuna waziri au kiongozi wa juu aliyefikishwa mahakamani kwa rushwa, ukiona hivyo ni kwamba wamekubalina kutosemana.
 
ANC yaani CCM ya Africa kusini umeshindwa kupata kura zinazoweza kukifanya kuunda serikali.
Inabidi waungane na Chadema ya kule kuunda serikali.
Anhaa, pia huo ni utaratibu mzuri sana, sasa nimeamini kipo cha kujifunza hapo
 
Anhaa, pia huo ni utaratibu mzuri sana, sasa nimeamini kipo cha kujifunza hapo
We acha tu CCM waendelee kuiba na kusinzia.
Watakuja kukumbuka shuka kumekucha.
Bashir alitamba kabisa kwamba hawawezi kuachia Dola. Kufumba na kufumbua Dola imeshikwa na wengine.
 
Uchaguzi wa Afrika ya kusini umengozwa na vijana waliozaliwa baada ya ubauguzi wa randi; kwa hiyo hawaelewi chochote kuhusu ANC kuleta uhuru, wao wanaangalia maisha yao ya sasa. Hakuna ajira, mabomba hayana maji masafi, hgakuna umeme wa uhakika. Wanatake mageuzi ya kiuchumi, siyo tena sera za "ANC iliondoa ubaguzi na kuleta uhuru"

Tanzania haiweizx kujifunza kwa sababu vijana wengi wa kitanzania wanarubuniwa kirahisi sana na CCM
Ukiangalia mahudhurio ya wapiga kura, ni mapema sana kutoa hitimisho la makundi kutokana na umri.
2024 mahudhurio (Turn out) ni ya chini sana 58.6% ukilinganisha na yale ya juu (max turn out) 1999 (89.3%). Tofauti ni takriban 30%, ni namba kubwa sana.

Mi nadhani vijana wengi hawakwenda kupiga kura kabisa, kutokana na kupuuzia mpango mzima wa demokrasia.
Na hili ndilo kubwa la kujifunza kwa Tanzania. kwasababu kama mpango mzima wa upigaji kura kama njia ya kidemokrasia ya kumchagua kiongozi(viongozi) atayetatua matatizo ya wananchi utashindwa kutekeleza au kumpata kiongozi atayetimiza lengo kuu, mpango huo hautakuwa na maana. Na wananchi watasusia kwenda kupiga kura. Na siku mahudhurio yakiwa chini ya 50%, sidhani kama kutakuwa na uhalali wa chama au kiongozi aliyechaguliwa kuwaongoza wananchi.

Na kwa mantiki hiyo Afrika kusini imeokolewa na 8,6% tu, vinginevyo si ANC wala chama kingine chochote kingekuwa na uhalali wa kuiongoza Nchi hiyo.
 
Hata kama ni cha "ubwabwa" mradi wafkishe 50%+1 ya kura zte. Sioni jinc watakavoungana na Julius Malema ...
 
Back
Top Bottom