KERO Hivi Mkandarasi anayejenga Barabara ya Kivulini - Kimara ameitelekeza Barabara? Imeharibika zaidi ya ilivyokuwa awali

KERO Hivi Mkandarasi anayejenga Barabara ya Kivulini - Kimara ameitelekeza Barabara? Imeharibika zaidi ya ilivyokuwa awali

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
WhatsApp Image 2024-12-19 at 13.08.34.jpeg
Miezi minne iliyopita Mkandarasi mzawa alipewa kazi na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kutengeneza barabara ya takribani kilomita tatu kutoka Kimara baruti hadi Kilungule uwanjani.

Mkataba huo ulikuwa ni wa miezi sita kuanzia mwezi wa nane 2024, Agosti 2024 Mkandarasi alianza kujenga barabara hiyo kwa kasi akileta vifusi na kuchimba mitaro hali iliyoleta matumaini kwa wakazi wa eneo hilo licha ya kuwa alizuia njia hiyo kupitika kwa muda mrefu.

Alichimba mitaro na kumwaga vifusi na udongo katikati ya barabara na kuanza kujenga mitaro ya baadhi ya sehemu.

Miezi mitatu baadaye barabara hiyo imesimama huku ikiwa imejengwa mtaro sehemu ya upande mmoja na sehemu kubwa ikiwa bado huku kukiwa na udogo katikati ya barabara na vifaa vingine vya ujenzi

KWANINI BARABARA IMESIMAMA?
Taarifa zinasema kuwa mkandarasi huyo ameishiwa pesa ya kuendeleza barabara hiyo, hivyo kuitelekeza.

Baadhi ya wakazi wa eneo hili na watoa huduma za usafiri wanasema matatizo ya uhaba wa pesa yalianza kuonekana tangu barabara hiyo inajengwa kwani hata vibarua walikuwa hawalipwi.
WhatsApp Image 2024-12-19 at 13.08.32.jpeg

‘Huyu mkandarasi amekimbia hana pesa, kuna wakati alipigana na vibarua wake hapa, wakimdai pesa. Walipigana sana hapa’ – anasema mwendesha Bajaji.

Kiongozi mmoja wa Mtaa huu anadai mkandarasi mzawa ambaye alikataa kumtaja jina, hana pesa na ametelekeza barabara hiyo ambayo sasa imekuwa changamoto mara mbili zaidi ya ilivyokuwa mwanzo.

‘Kabla hajaja barabara ilikuwa mbaya lakini ilikuwa inapitika bila shida yoyote, lakini sasa ni kero.

‘MKANDARASI AMEKUJA KUHARIBU SI KUTENGENEZA’
Alipoanza kujenga barabara hii alifunga kabisa njia kasoro kwa watembea kwa miguu tu, alisababisha watu wenye magari wanaoishi pembezoni mwa barabara hiyo kutafuta maeneo mengine ya kuegesha magari na kurudi majumbani mwao kwa miguu, kero hii ilichukua takribani miezi miwili wenye magari kushindwa kupita.

Hata sasa wenye magari wanalazimika kuzunguka ili waweze kupita hivyo sehemu ya dakika moja au mbili kufika nyumbani inachukua takribani dakika kumi kuzunguka

Hali ilivyo sasa, hata Bodaboda zinapita kwa tabu kwani njia imejaa tope na barabara imeharibika mara mbili zaidi ya ilivyokuwa awali.
Mvua ikinyesha kubwa tu, hakuna mtembea kwa migu, bajaji wala bodaboda inaweza kupita achilia mbali watu wa magari ambao hata sasa hawawezi kupita lazima wazunguke.

Mkandarasi amefanya maisha yamekuwa magumu kwani hata kwa walio na biashara pembezoni sasa hawapati wateja kama ilivyokuwa awali.
WhatsApp Image 2024-12-19 at 13.08.42.jpeg
Madereva wa bajaji na bodaboda wanasema kuwa kituo chao cha mwisho sasa kimehama kutokana na ujenzi huo kwani tangu walipoanza iliwabidi wasifike mwisho wa kituo ili kupisha ujenzi lakini mpaka sasa hawajui hatma ya barabara hiyo

Je, nini kinaendelea? Ni kweli Mkandarasi kaishiwa na mbona TARURA wapo kimya?
 
Poleni sana aiseee.

Rekebisha hapo kwenye muda wa mkataba kuna ukakasi kidogo.

Nadhani alipewa fungu dogo, bila hivyo wanasiasa wangeshakuja kuchukua point 3.

Walau wangewamwagia hata changarawe tu, namna hiyo ni hatari sana.
 
Wengi hawajui mikataba ya ukandarasi ilivyo.
Ukipata mradi, utatakiwa kuanza kazi kwa fedha zako.
Utatakiwa ufanya hiyo kazi mpaka ufikie asilimia flani, mara nyingi 20%.
Ukifikisha hicho kiwango utatakiwa kuomba malipo ya awali ili kuendeleza kazi yako.

sasa hapo kwenye malipo hapo ndio shida ilipo(kwanza hupati, na ukipata sio kwa wakati, na mara nyingi ni baada ya kuwapa pesa wadau).
Sio rahisi mtu kupeleka material, kuchonga barabara, kujenga makalavati halafu akimbie.
Ni kazi zenye stress sana sana. Tegema kupata simu ningi kutoka sijui kwa diwani, mjumbe wa mtaa, mwenyekiti wa halmashauri,mbunge sijui nani na nani. Orodha ni ndefu na wote hao hawana msaada wa wewe kulipwa kwa wakati.
Ndio sbb kampuni za ujenzi toka nje ya nchi ndio zinazo ongoza kufungua kesi za madai kwenye mahakama za kimataifa.
 
Yale yale ya BONYOKWA - KIMARA,
Wiki mbili nyuma Walitangaza kuanza ujenzi mara moja, ajabu leo nimepita huwezi amini, hakuna hata gari moja la kisingizio kuwa Ujenzi umeanza.

Hii nchi kuendelea Mpaka kiyama
 
Back
Top Bottom