Hivi mkeo unamuachia Tsh. ngapi unapotaka kwenda kazini?

Hivi mkeo unamuachia Tsh. ngapi unapotaka kwenda kazini?

Melki Wamatukio

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2022
Posts
6,156
Reaction score
10,974
Uzi tayari!

Kiasi gani cha matumizi unachomwachia mkeo ili kukidhi mahitaji ya kutwa na maandalizi ya chakula cha jioni?

Ambao hatujaoa njooni tujifunze hapa!

1656310711931.png
 
Mimi nikiwa na nafasi ya salio naacha matumizi ya mwezi mzima huku kila kitu kikiwa ndani.

Sitaki kero ya kuamka na madeni mwishowe unakuwa unaadopt mazingira ya madeni

Ila wanawake wakorofi, utamuachia laki mbili ya matumizi lakini still atakuomba pesa ya vocha.

Utamuwekea kila kitu ndani cha kupika lakini still atakuuliza leo tunakula nini.
 
Mimi ninanunua mchele,unga maharage gas na mkaa then kwa siku HAKUNA formula itategemea na siku hiyo nataka kula Nini kwa mfano nyama Basi lazima niache 5000 ambayo NI nusu uzuri tuko wawili TU hatuna mtoto na wife NI mama wa nyumbani Bado sijamuanzishia mradi...

Ila kumbuka hapo nakuwa nishaenda naye sokoni weekend kununua vitunguu nusu vya 2000,nyanya za 3000, karoti 1000,hoho 1000, dagaa wa 3000 ,nyanya chungu 1000,..tangawizi za 1000, n.k.....af sometimes na Nazi ya buku muhimu kila siku na asbh ye namwachiaga jero anapenda mihogo au mandazi anakunywa na chai ...so kwa wastani jua NI 2000-5000,,, sometimes inavuka 7000...
 
Uzi tayari!
Kiasi gani cha matumizi unachomwachia mkeo ili kukidhi mahitaji ya kutwa na maandalizi ya chakula cha jioni?

Ambao hatujaoa njooni tujifunze hapa!

Ninachofanya! Wanapanga bajeti ya mwezi mzima (mke akishirikiana na dada wakazi au waliopo home), kwamba nyama watakula kwa wiki mara ngapi? Maharagwe? Samaki? Kuku au vyovyote vile ila mboga za majani ni lazima kila mlo!!N afaka pia unga wa ugali, mchele, ngano,makande, ndizi, na n.k. zinalika kiasi gani kwa siku/wiki/mwezi. Dharura isikosekane, wageni wamo.

Hii inafanya kunakuwa na urahisi kujua kwa wiki ni kiasi gani cha mlo, na kwa mwezi vinahitajika bila kusahau mahitaji mengine kama gesi, mafuta, umeme, mkaaa,maji na n.k.

Wakishapata bajeti kuu ya mwezi mzima katika mlo, wanapiga bajeti ya vitu vidogo vidogo kama nyanya, vitunguu, mayai, mikate, maandazi kwa siku wanatumia kiasi gani na kisha wanaijumlisha kwa mwezi.

Mwisho bajeti kuu ya mlo inajumlishwa na ya matumizi ya siku inapatikana gharama ya mwezi mzima. Nampa wife hiyo hela kinachobaki kinakwenda kwenye maendeleo na mambo mengine!!

Hii mbinu inasaidia kuhakikisha mlo kamili unalika nyumbani na unaweza kufuatilia vyema ili kuimarisha malezi!!

Mi nikiamka asubuhi sina ninachouliza wala kuulizwa lakini hata katikati ya mwezi ukifulia, home uhakika upo. Hakuna kinachokosekana.

Pia, utajua kipato chako kwa mwezi kinakwenda vipi na namna gani ufanye kuleta maendeleo.

NB: Mambo ya kutoa hela kila siku utaona maisha magumu na mtagombana tuu!! Mjenge mkeo katika bajeti ya kila mwezi, mwanzoni inatesa ila akizoea na mwenyewe atafurahi.
 
Back
Top Bottom