Hivi mlianzaje biashara zenu, mbona wengine tunakwama?

Hivi mlianzaje biashara zenu, mbona wengine tunakwama?

Wakubwa hapa leo najaribu kuelezea madhira tunayopitia vijana tunaojitafuta, tunapata mawazo mengi na kuchora mipango mingi sana ya mafanikio...

ukifungua notebooks zetu utaona tumeandika mipango mingi ya kutoboa ila tunakosa jinsi ya kuanza.
Binafsi natamani kuwa na biashara flani ila kila nikijaribu kuanza nashindwa, muda ninao ila ninachokosa Ni (1) Rasilimali fedha (2) Rasilimali watu.

Yaani kwenye mitaji tunafeli sana, sometimes tunatamani hata kushikwa mkono na waliotangulia kufanikiwa lakini haiwezekani.

Huwa najiuliza kwanini waliofanikiwa wanakuwa na ugumu wa kumsaidia mtu kuanzisha project zake ila wapo tayari hela zao mkatumie wote kwenye starehe alafu akiachana na wewe baada ya bata hakuachii hata senti 5[emoji23][emoji23] atakununulia kitu ila sio kukupa fedha mkononi. Kuna siri gani hapo?

MASWALI MUHIMU
1. Hivi nyie mlifanikiwa vipi kuanza biashara zenu na zikaenda?
2. Hela(mtaji) mlipata wapi?

3. Siri ya kuwa mfanyabiashara ni ipi?

ASANTENI SANA[emoji120][emoji120]
Mtaji wa fedha na watu + ubabe unatoboa. Ukicheka na nyani utavuna mabua. Na bongo nyani ni wengi sana.
 
Ukiweza kubana matumizi na kuacha vitu visivyokuwa na umuhimu na biashara utaweza
 
Wakubwa hapa leo najaribu kuelezea madhira tunayopitia vijana tunaojitafuta, tunapata mawazo mengi na kuchora mipango mingi sana ya mafanikio...

ukifungua notebooks zetu utaona tumeandika mipango mingi ya kutoboa ila tunakosa jinsi ya kuanza.
Binafsi natamani kuwa na biashara flani ila kila nikijaribu kuanza nashindwa, muda ninao ila ninachokosa Ni (1) Rasilimali fedha (2) Rasilimali watu.

Yaani kwenye mitaji tunafeli sana, sometimes tunatamani hata kushikwa mkono na waliotangulia kufanikiwa lakini haiwezekani.

Huwa najiuliza kwanini waliofanikiwa wanakuwa na ugumu wa kumsaidia mtu kuanzisha project zake ila wapo tayari hela zao mkatumie wote kwenye starehe alafu akiachana na wewe baada ya bata hakuachii hata senti 5[emoji23][emoji23] atakununulia kitu ila sio kukupa fedha mkononi. Kuna siri gani hapo?

MASWALI MUHIMU
1. Hivi nyie mlifanikiwa vipi kuanza biashara zenu na zikaenda?
2. Hela(mtaji) mlipata wapi?

3. Siri ya kuwa mfanyabiashara ni ipi?

ASANTENI SANA[emoji120][emoji120]
Majibu mazuri yatakayotolewa hapa nadhani yatasaidia sana maana hii ni changamoto kwa vijana wengi miaka hii...
 
Mtaji wa fedha na watu + ubabe unatoboa. Ukicheka na nyani utavuna mabua. Na bongo nyani ni wengi sana.
[emoji23][emoji23] + ubabe umenikumbusha kitu kuna mwana hawez kunisahau maisha yake yote.
 
Kuanzisha Biashara ni kugumu sana hapa Tz, hasa kama hujawahi kuendesha biashara ni lazima mtaji wa kwanza upotee, ndo ukipata wa pili ndo utaanza kuelewa biashara
Kuna mtu aliwahi kuniambia kuwa, kuanzisha biashara ni sawa na mtu anayeanza kusoma darasa la kwanza. Sasa fikiria uanze kujifunza a, b, c, d.........na baadaye kuziunganisha herufi hizi ili kupata neno, na hatimaye uunganishe maneno ili upate sentensi!
Hivyo inahitaji muda kuyamaster maeneo hayo kabla hujahitinu shule! Vivyo hivyo katika biashara.....kuna hatua za kupitia mpaka kufikia kuielewa biashara. Utaanguka mara kadhaa lakini usikate tamaa, inuka na uendelee kujikongoja kusonga mbele.
Ukifika hatua za juu katika biashara yako......umeielewa, mtaji umekua, una network; panua biashara yako kwa kuweka projects tofauti tofauti (project portfolio). Hii itakusaidia ikitokea project moja ikifeli, basi zilizobaki zitaibeba ile iliyofeli (risk diversification). Mbinu hii inatumiwa sana na wafanyabiashara wakubwa. Usiweke nayai yote kwenye kapu moja, kwani hilo kapu likiponyoka na kuanguka, mayai yote yatapasuka, lakini ukiweka tofauti, mengine yatabaki!
 
"Mzigo unaisha na hela siioni"

Huoni kama hilo lilikuwa ni tatizo la kiuendeshaji badala ya kulaumu ugumu wa biashara? Maana kuuza uliuza ila pesa ndio ulishindwa kuitunza.
Biashara hizi zina changamoto nyingi sana ndugu yangu, ukiona watu wanafilisika usidhani ni wapumbavu.Mtu huwezi kufilisika kama stock ipo,unafilisika kwa sababu stock inaisha na pesa haionekani.

Na wala haihusiani na utunzaji wa fedha maana kama mimi pesa ya dukani nilikua hata siitumii kwa matumizi binafsi.

Waulize wafanyabiashara watakuambia,unauza siku nzima ikifika jioni unajikuta una elfu 10 zingine hazipo
 
Biashara hizi zina changamoto nyingi sana ndugu yangu, ukiona watu wanafilisika usidhani ni wapumbavu.Mtu huwezi kufilisika kama stock ipo,unafilisika kwa sababu stock inaisha na pesa haionekani.

Na wala haihusiani na utunzaji wa fedha maana kama mimi pesa ya dukani nilikua hata siitumii kwa matumizi binafsi.

Waulize wafanyabiashara watakuambia,unauza siku nzima ikifika jioni unajikuta una elfu 10 zingine hazipo
Naelewa hiki unachokisema, mimi pia kwa namna moja ama nyingine nimewahi kuwa mhanga ndiomaana nikasema tatizo ni utunzaji wa fedha, ikiwa unaona fedha zinapotea katika mazingira yasiyoeleweka kwanini usitafute ufumbuzi wa hilo tatizo hadi unafikia kufirisika?

Maana yake baishara ni nzuri ila umesindwa kudhibiti huo upotevu wa fedha.
 
Mimi nimepoteza jumla ya milion 300 hadi nikajuatia Bora ningezifanyia ngono nisingeumia.
Bora upoteze Hela kwenye starehe kuliko kwenye biashara,nilichoambulia ni uzoefu wa kutosha kuhusu mapito mbalimbali ya biashara na uwekezaji lakini sijakata tamaa Leo hata nipate billion 800 siwezi zuzuka na Hela.

Aisee kumbe bado sijapoteza Wacha nikaze boot la jeje
 
Ukipata watu ambao tayari wametangulia kwenye hicho ambacho unataka kufanya kisha wakushike mkono kimawazo na ukakubali kujifunza kwao, ni lazima utoboe bila kupoteza kiasi kikubwa cha fedha kama wanavyosema wadau humu.

Usithubutu kuanza biashara bila kuwa na mzoefu yoyote, lakini pia usithubutu kukabidhi pesa zako za mtaji kwa huyo mzoefu, kwake tumia uzoefu wake tu, akili na rasilimali iwe ni juu yako.
Madini kama haya huwa tunaya-save kwenye notebook.
Baadae tunayapitia deeply.
Mkuu umeongea kitu kikubwa sana hapa.
 
Tuliaanza kwa kukwama kama wewe tulianguka na kupoteza mitaji mara nyingi sana lakini tulivumilia
Yes Kuna kipindi hata pesa ya marejesho tuliuza assets tulizopata lakini tukasimama Tena[emoji123]
 
Hamna kundi linalo choma mtaji kama hao wastaafu kwa kutumia kuinua mgogo chao, mtu anaanzisha duka la pombe kwa 30m kodi ya jengo 500k sales 50,000 kwa siku faida negative baada ya mwaka ana funga af anafungua duka la nafaka la 20m kwasbb pesa anao lina kata tena kwasbb hajui misimu ya mazao.....hivo hivo mpaka anafilisika na kuokoka kanisani anatoa ushuhuda.
Mstaafu simshauri pesa yake ya kiinua mgongo awekeze kwenye biashara kwa sababu hana uzoefu nayo

Kimbilio lao ni kujenga nyumba za wapangaji hasa hawa wa majiji makubwa kama Dar. Kama ana eneo zuri zaidi lenye pililapilika ajenge fremu za biashara za kupangisha
 
Shida biashara za vijana wa siku hizi zinachekesha sana, unakuta dogo ana idea, full theory kabisa ukianza kumuuliza maswali hana majibu.

You are selling the product u didnt invent,
The formula u didnt discover,
Yaan idea haina potential yyt zaidi ya story za vijiweni tu, hajui RR iko vp, biashara za hvo walifanikiwa waloanza zamani kabla ya kuwepo kwa ushindani, sasa hivi lazima uwe na kitu unique au special.

Tutakununulia bia na soda tu, lakini kwa ideas uchwara hatukupi hata mia, hapo bora nikununulie bia ntamchangia mmiliki wa bar
NAKAZIA
 
Back
Top Bottom