Hivi mnawezaje kuishi Dodoma?

Mayor of kingstown

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2017
Posts
2,898
Reaction score
4,156
Nianze kwa kusema nimeishi Arusha, Mwanza, Dar Moshi, na sasa hivi nipo Dodoma unaelekea Mwaka sasa nipo huku kwa sababu za kikazi.

HALI YA HEWA
Huu mji toka nifike sijaona mvua, mchana kuna jua kali sana na vumbi halafu jioni na usiku upepo mkali wa baridi kama jangwani karibia napakimbia .

MAKAZI
Kwa sasa hivi Dodoma ujenzi ndo mahala pake lakini watu hawajui kujenga kabisa ,Sidhani hata kama wanatumia ramani kwenye kujenga maana wanajenga manyumba makubwa kama makubwa jinga halafu mabaya hayapakwi rangi wala kupigwa lipu yanaachwa hivyo hivyo na madirishani wakiweka mifuko ya cement, mabox au makaratasi ya magodoro ni kichefuchefu. Ukija kwenye bati ndo huzuni mabati marefu refu kama Mkuki

USAFIRI
Kama huna gari au sio wa kutokea STM au STK etc huku hakufai usafiri haueleweki wala nauli hazieleweki kila mtu na nauli yake .

MAJI
Kwa mara ya kwanza nashuhudia maji ya idara ya maji yana chumvi. Kama huna kazi hapakufai, maji ya kunywa ni ununue bila hivyo utakunywa chumvi uwe na meno kama ndugu zetu wa Arusha.


KAZI
Dodoma ofisi nyingi zinahamia huku lakini sio sehemu bora ya kuja kuanzia maisha kama huna ramani tofauti na mikoa kama Dar, Mwanza na Arusha huku utapauka dakika 2 baada ya kushuka stand

MWISHO
Nisipoona hata mvua hii miezi iliobaki hata kwa mganga nitaenda nihame ofisi.
 
Nakumbuka nilivyoenda Dodoma mara ya kwanza 2019, Juwa liliniwakia wiki moja tu nikawa nimapasukapasuka ngozi ya uso na mikono,nikaacha kodi ya nyumba maeneo ya nkuhungu na vitu vya ndani nikapanda Kapricon kurudi arusha.
 
Nilipangiwa vyuo kadhaa ila UDOM sikuwa nimewahi fika. Nikaenda siku moja kutembea kabla ya kuchagua chuo kipi nisaini, ile siku nimefika Dodoma ndipo kwa mara ya kwanza nikahisi nina matatizo ya macho.

Nilidungwa jua kali nikahisi nipo kwenye zile movie za Hollywood zinazoonyesha Mexico ina uwekundu. Macho yaliuma sioni mbele, kiu kali sijawahi pata, sikuelewa nina njaa au ninaumwa. Hiyo siku nilitakiwa nilale ila usiku umefika nikajikuta kuna baridi. Nikapanda bus la saa nne kuondoka zangu.

Baadae nimerudirudi safari chache nimeona hakuna shida kivile ila afya mgogoro wakiishi uko watapata shida.
 
Kwani,wakati unaingia hapo haukuona kibao chochote kimeandikwa MAKUTUPORA?Mpaka sasa upo kambi ya jeshi.Kwa hiyo uwe mtulivu na uzidishe ukakamavu.Sema ndiyo afande!
 
Nakumbuka nilivyoenda Dodoma mara ya kwanza 2019, Juwa liliniwakia wiki moja tu nikawa nimapasukapasuka ngozi ya uso na mikono,nikaacha kodi ya nyumba maeneo ya nkuhungu na vitu vya ndani nikapanda Kapricon kurudi arusha.
Yani uku ni una pigwa na upepo wa baridi apo apo una chomwa na jua kwa wakati mmoja
 
Bhata zangu nalia dodoma, it's a nicest place to be!
 
sijui imekuwaje serikali ime hamia uku .
 
Kwani wewe ulikuta wanaishi kima au?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…