Hivi mnawezaje kuishi Dodoma?

Hivi mnawezaje kuishi Dodoma?

Nimeishi mikoa takribani 21 ya TZ BARA, ukiacha Kagera, Rukwa, Ruvuma, Katavi na Mtwara. Kila eneo kuna raha zake na karaha zake:-

DAR - msimu wa mvua hakufai, ni mji wa starehe na utafutaji pesa..kila biashara inatoka!
ARUSHA/MOSHI - mji wa starehe haswaa, na gharama za maisha zipo juu, hali ya hewa safi
MWANZA - pilika nyingi, starehe na biashara kadhaa
KIGOMA - hali nzuri ya hewa, vyakula kibao bei nusu, hakunaga njaa!
IRINGA - mji wa vyakula, hali ya hewa bariiiidi
DODOMA/SINGIDA - mvua chache kwa mwaka, baridi na upepo mkali kiangazi, maisha simpo!
nk...nk.....

Hata hivyo, binadamu tumeumbwa kuyazoea mazingira. Kwa mpambanaji wa kweli mbali na maradhi, kila mji/mkoa unaweza kuishi na mambo yakaenda.
 
Nianze kwa kusema Nimeishi Arusha,Mwanza ,Dar Moshi, na saivi nipo Dodoma una elekea Mwaka sasa nipo uku kwa sababu za kikazi.

HALI YA HEWA
Huu mji toka nifike sijaona mvua ,mchana kuna jua kali sana na vumbi afu jion na usiku upepo mkali wa baridi kama jangwani karibia napakimbia .

MAKAZI
kwa saivi Dodoma ujenzi ndo mahala pake lakini watu hawajui kujenga kabsa ,Sizani ata kama wana tumia ramani kwenye kujenga maana wana jenga ma nyumba makubwa kama makubwa jinga afu mabaya hajapakwi rangi wala kupigwa lipu yana achwa ivyo ivyo. na madirishani wakiweka mifuko ya cement ,mabox au makaratasi ya magodoro ni kichefuchefu
Ukija kwenye bati ndo huzuni mabati marefu refu kama Mkuki

USAFIRI
Kama huna gari au sio wa kutokea STM .au STK etc uku hakufai usafiri aueleweki wala nauli hazieleweki kila mtu na nauli yake .

MAJI
Kwa mala ya kwanza nashuhudia maji ya idara ya maji yana chumvi l. kama huna kazi apakufai .maji ya kunywa ni ununue bila ivyo utakunywa chumvi uwe na meno kama ndugu zetu wa Arusha .


KAZI
Dodoma ofisi nyingi zina amia uku lakini sio sehemu bora ya kuja kuanzia maisha kama huna ramani tofauti na mikoa kama Dar,Mwanza na Arusha uku uta pauka dk 2 baada ya kushuka stand

MWISHO
nisipo ona ata mvua hii miezi ilio baki ata kwa mganga taenda nihame ofisi
Huo ni uongo mkubwa, Mimi sio mwenyeji wa Dodoma,Hali ya Dodoma ni nusu jangwa sikatai,ardhi yake Ina rutuba sana,mshindi na mazao hawatumii mbolea za viwandani.Kuhusu ujenzi mafundi Kwa kweli ni ghari kulinganisha na kwetu Mbeya!Nyumba nyingi zimejengwa kwa kufuata ramani zilizokuwepo zamani ikiitwa CDA,Hayo mengine ni yeye kutokubaliana kuishi Dodoma.Pana fursa nyingi sana,Mfano ufugaji,kilimo,hakuna zao halikubali Dodoma ni Wewe tuu kujipanga.Nina miaka kumi sitamani kurudi Mbeya.Maana ardhi Mbeya ni finyu sana.
 
Dodoma ina wingu una weza zani mvua ina nyesha kila wakati kumbe linawapa moyo tu..usha kutana na nyoka wa ngapi hadi leo
Hivi toka lini mvua ndio imekuwa main factor? mikoa mingi yenye kupata mvua nyingi kwa mwaka tena nyingi sana lakini haina fusra. Mimi nahisi kunachuki nyingi sana kutoka kwa wakazi wa Dar ile kuchukuliwa hadhi ya kisiasa au cake kugawanywa tu imekuwa kero kwao. Nchi hii watu wamepata shida sana ilikuwa ukitaka chochote lazima uende Dar sasa leo watu wanayapata maeneo yao na kikubwa mji wa Serikali ukikamilika 100% ndio basi Dar ni biashara tu.
 
😂😂Mwanzoni nilivyokuja nilisema nini hiki. Lakini kukaa Kaa nikaona kumbe ni mindset tu. Umesema upo kikazi halafu unauliza wanajengaje bila ramani? Dodoma ipi unajenga bila ramani.?
Kuweka Frame za mbele tu walitaka turudi jiji eti kibali Cha mchoro tukapate.😂
Nakuelewa changamoto uliyopata kutoka Arusha ghafla tu uhamie Dodoma ni majonzi ya muda kiukweli.
 
Dabalo umenikumbusha mbali sana,hivi bwawa lipo bado

Ova
Mkuu kama miti enzi za primary tulipandishwa sana na hapo unakabidhiwa mti au kipande cha bustani ukihudumie lakini nilipita baada ya miaka mingi, bado hali ipo vile vile

Nadhani ujangwa ni uoto wa asili na ili kuuondoa bhasi utahitaji nguvu ya zyada sana

By the way dodoma ya leo hii haina ubovu huo ukiilinganisha na ile ya zaidi ya miaka 15 iliyopita wakati ndo naingia. Ni bhasi tu binadamu tuna chaguo zetu binafsi
 
😂😂Mwanzoni nilivyokuja nilisema nini hiki. Lakini kukaa Kaa nikaona kumbe ni mindset tu. Umesema upo kikazi halafu unauliza wanajengaje bila ramani? Dodoma ipi unajenga bila ramani.?
Kuweka Frame za mbele tu walitaka turudi jiji eti kibali Cha mchoro tukapate.😂
Nakuelewa changamoto uliyopata kutoka Arusha ghafla tu uhamie Dodoma ni majonzi ya muda kiukweli.
Uko sahihi mkuu hakuna kujenga bila kuwapa Ramani,Zamani ramani zilikuwa mpaka ukachague CDA!,Sasa hivi jiji.
 
Back
Top Bottom