DOKEZO Hivi Msumi ipo Dar es Salaam kweli?

DOKEZO Hivi Msumi ipo Dar es Salaam kweli?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Ile lami waliyoweka katikati ya vumbi na vumbi majuzi january walirudi wakisema wanaiendeleza uelekeo wa kwenda Msakuzi wamechonga barabara mpaka pale njia panda Makabe ila mkandarasi au sijui ndiyo tanroad ana ugomvi na dawasa na tanesco.

Kwamba mmoja ahamishe nguzo mwengine ahamishe bomba miezi inasogea tu na mvua hizi barabara kule walikovuruga kunazidi kuharibika,usikate tamaa japo tunacheleweshwa lakini labda ipo siku kutakaa sawa
Hivi ndicho kipimo halisi cha akili ya muafrika. Imagine mtu anaanza kazi bila coordination na wadau wenzake muhimu. Nadhani kabla ya kuanza ujenzi ilitakiwa tayari kila mdau amehusishwa na kupangiana muda wa kuwajibika kwa kila mmoja yaani TANROAD, DAWASCO na TANESCO .
Kuna ujinga mwingi sana unaofanyika kwa baadhi ya watendaji wa taasisi za serikali NA BAHATI MBAYA SANA HATA WANAPOZEMBEA AU KUHARIBU HATA HAWATISHIKI. LABDA WASIKIE Mhe Rais ameulizia maendeleo ya ujenzi au wasikie Mhe waziri mkuu ameulizia ndipo wataanza kukimbizana na kuambiana jamani wakubwa wanafuatilia hili.

NADHANI NA UWAJIBIKATI KWA WATUMISHI WENGI NI YA HOVYOO SANA. PIA UBABAISHAJI NI WA KIWANGO CHA KUTISHA
 
Ile lami waliyoweka katikati ya vumbi na vumbi majuzi january walirudi wakisema wanaiendeleza uelekeo wa kwenda Msakuzi wamechonga barabara mpaka pale njia panda Makabe ila mkandarasi au sijui ndiyo tanroad ana ugomvi na dawasa na tanesco.

Kwamba mmoja ahamishe nguzo mwengine ahamishe bomba miezi inasogea tu na mvua hizi barabara kule walikovuruga kunazidi kuharibika,usikate tamaa japo tunacheleweshwa lakini labda ipo siku kutakaa sawa
Yule mkandarasi mhuni kweli kweli
Kawapigia lami kuanzia kati kamaliza 😄
Nchii f kweli kweli

Ova
 
Kuna mradi wq DMDP phase two watajenga barabara ya msumi kilometa 9.08 . Ujenzi unaanza mwezi wa saba. Kipindi wanatangaza zabuni ili mkandarasi apatikane. Tembelea page ya mkuu wa mkoa you tube autakuta kafafanua barabara ambazo zitapitiwa lami
Ktk makosa makubwa Watanzania tunafanya ni kuwaamini wanasiasa.

Mtu wa kupeleka barabara sehemu zote korofi kwa mkoa wa Dar alikuwa Dr Magufuli pekee(nazungumzia Dar sababu currently ndiko makazi yangu yalipo) the rest ni vichekesho vitupu,mimi naishi Makabe nyuma ya Msumi lakini huku ili mambo yaende tunatumia nguvu nyingi kweli kweli 2021 nilifunga maji ya dawasa ilini-cost karibia 800K na hiyo ni afadhali kuna ambao walitumia zaidi ya 1.5mill lakini form ya dawasa ada ya kufungiwa maji inasema gharama yake ni 255K.

Tatizo lililopo watu hawana mtu wa kuwasukuma,fedha zinatengwa but mpaka zije kufika kwenye mradi robo tatu yake wamegawana zinazobaki kidogo ndiyo zinaenda kwenye maendeleo kwa style hii hakuna siku tutafika.
 
Yule mkandarasi mhuni kweli kweli
Kawapigia lami kuanzia kati kamaliza 😄
Nchii f kweli kweli

Ova
Mjinga yule sehemu za kumwagwa zege vibarua wake walikuwa wanachanganya na chepe na kumwaga na vindoo kama vile wanajenga choo.

Ile ilikuwa kampuni uchwara kile kipande unachokiona pale kilijengwa zaidi ya miezi kumi.
 
Msumi ni Kilometer chache sana kutoka stendi ya mabasi ya Magufuli.

Sasa cha ajabu ni kwamba Msumi ipo kama vile hata wakuu wa Mikoa waliopita hapo Dar na wasasa si ajabu hawajui iko upande gani wa mji, achilia mbali DC.

Mbunge wa Ubungo (labda atapeleka pua) kwa ajili ya kampeni, Sina hakika na Mkurugenzi na blah blah wengine, kutoa umeme.
  • Msumi hakuna barabara.
  • Msumi hakuna zahanati zingatia ni eneo lenye kaya zaidi ya laki moja, Ref.Google Map.
  • Msumi hakuna kituo cha Polisi
  • Msumi hakuna maji ya bomba lakini kuna ofisi za CCM kila baada ya kilometer chache.
Kma si ushirikina wa Wamakonde ni nini?

Msumi hakuna madaraja baada ya kuzolewa na mvua, zingatia madaraja yote yalijengwa kwa nguvu za wananchi.

Tukisema Msumi hakuna Zimamoto tutakuwa tumeungana na washirikina manake mji mzima zimamoto ni moja tu pale faya kwa ajili ya Kariakoo na Muhimbili, hili hakuna kiongozi mwenye uwezo wa kulizungumzia manake akili zao ziko kunako matumbo yao.

Haya tuendelee Msumi Shule ya Msingi ni moja na haitoshi zingatia idadi ya kaya, nilisikitika mvua inanyesha wamesongana kibarazani kisa wanasomeaga chini ya mti.

Kuna majengo ya madarasa yapo upande wa kulia kama unaelekea msumi maeneo ya uwanjani sijui ni ya sekondari au ya msingi wenyeji mtatujuza.

Msumi hakuna kituo cha daladala ingawa daladala zipo kwa uchache zingatia hakuna barabara ndio kisa na wenye mabasi hawaitaki njia hiyo na abiria ni wengi sana sana kaya laki moja, mara waseme darajani mara waseme center lakini kote ni ushirikina tu.

Msumi hakuna miundo mbinu ya kukusanya taka.i.e Dampo kwa sasa hawataona athari.

Ngoja kidogo, kaya laki moja na kila siku watu wanazidi kuhamia, watu wa msumi hebu wekeni kero zenu hapa manake hampo jijini wala mamkoa.

Msumi Chui ametoroka msituni anaonekana mtaani, zingatia Msitu ameshapewa mwekezaji.
Heheee manake hapo kwanza acha nicheke
 
Mkuu samahani, nikitaka kufika huko napitia wapi ? Nipo serious nataka nikafanye ziara huko nipaone.
 
Niliwahi kupanga huko mwanzo mwa 2001 niliacha kodi sehemu ni ya ajabu sijapata kuona alaaniwe yule dadali mwongo🤨
Huwezi kuwa na akili timamu ukaishi Msumi binafsi nilikaa mwenzi mmoja wa mateso nikaikimbia kama jela😳
Kwa muktadha wa kupanga upo sahihi lakini kama una makazi yako kule na una familia kubwa kwa kipato hiki cha Mtanzania wa kawaida hauwezi mtu ukawa hauna akili.
 
Misumi ,msakuzi,mpiji na makabe kote huko hakuna maji,hospitali Kuna kizahanati tu na barabara ndiyo balaaa yaani makorongo Kwa kwenda mbele lakini yule mbuge wao Kila kuchangia anasifu rais kwa kazi nzuri kiasi kwamba akiwa karibu unaweza kuzaba Kofi.
Itoe Makabe bro,Makabe sisi kinatutesa barabara tu issue za maji tumeshavuka japo kwa maumivu makali labda sema hospital ndiyo hatuna tunategemea ya Mbezi au tuunge hadi Mpiji Magoe.
 
Itoe Makabe bro,Makabe sisi kinatutesa barabara tu issue za maji tumeshavuka japo kwa maumivu makali labda sema hospital ndiyo hatuna tunategemea ya Mbezi au tuunge hadi Mpiji Magoe.
Mbona hapo kwa lipelanya wanakaa watu wazito kiasi na wana magritte mazuri tu lakini njiaa ya huko hawaipigii makelele

Ova
 
Mbona hapo kwa lipelanya wanakaa watu wazito kiasi na wana magritte mazuri tu lakini njiaa ya huko hawaipigii makelele

Ova
Ni kweli hata huko Msumi kuna watu wenye uwezo wanaishi ila linapokuja suala la wananchi kupata shida sample huwa inachukuliwa kutokana na wale hohehahe wa maeneo husika.

Nilikuwa namjibu mdau hapo juu kuhusu mazingira ya Makabe.
 
Itoe Makabe bro,Makabe sisi kinatutesa barabara tu issue za maji tumeshavuka japo kwa maumivu makali labda sema hospital ndiyo hatuna tunategemea ya Mbezi au tuunge hadi Mpiji Magoe.
Mpiji magoe Hospital gan au ile ya wilaya kule mabwepande?
 
Y not,.ukinikuta na hii mvua inavyonyesha utanionea huruma.😜
Kuna siku nipo pale Mbezi nikamsikia jamaa wa Bajaj anaitia ”Msumi na Bajaj buku nne” nikamwangaliaaa nikamuona hivi huyu anadhani hela watu wanaenda kuokota?nikaishia kumtukana kimoyo moyo.

Sema mkuu Msumi hata kama mateso yakizidi wokovu unakaribia ila nyie mnapata shida aisee,mtu anasubiri Eicher au DCM kwa dakika 45 inakuja anapanda halafu inaenda kuzimikia pale Mazulu au au njia panda Goba na hapo limekata spring au limetumbuka clutch na ni wazi kuendelea na safari itakuwa kesho lakini mnaendelea kuvumilia.

Hatari sana.
 
Ni jimbo la Kibamba lote, mawasiliano ya barabara ni mtihani mkubwa sana, kipindi hiki watu wanaacha magari yao nyumbani, njia hazipitiki, wengine tupo 2.5km away from makao makuu ya wilaya ila network ya barabara utadhani tupo mashamba ya mpunga huko.

Futseke zao!
Hiyo ni kwembe,king'azi,malamba mawili,kibamba ni aibu maeneo hayo na serikali hauna hata habari,inafikiria kuongeza v8 za ma rc!!
 
Back
Top Bottom