Hivi mtu akifa na hela zake ziko benki na Mpesa, tukiwa na cheti cha kifo tunaweza fuatilia?

Wajuzi naomba msaada.

Ndugu kafa. Ana akaunti benk ila password hazijulikani pia ana mpesa na pesa zipo ila no password. Mkewe ana death certificate. Atapataje pesa za mmewe? Pia ana cheti cha ndoa.

Msaada
Kama hivyo vipo atapewa ila kabla hajenda huko ajaribu kutafuta njia ya kujua kiasi gani maana kuna mikamouni mingine ikishajua hivyo inapunguza au kutaifisha mkienda mnaambiwa hamna salio
 
Aseee ha ha ha ha ha
 
Msimamizi wa mirathi akafungue kesi mahakamani kwanza, kisha mahakama ndio itatoa oda kama benki watoe hela za kwenye account zake na kumpa huyo mke wake.
Hapana chetu cha kifo hakitoshi ndugu. Inatakiwa kufungua kesi ye Mirathi na msimamizi anayeidhinishwa na Mahakama ndiye atakayefuatilia kwa kutumia nyaraka za Mahakama. Ukweli ni kuwa Kuna hela nyingi sana kwenye Mpesa au simu za marehemu ambazo zinaotea kwa kutokufuatiliwa.
 
Sheria ya mirathi kwa upande wa wajane kina mama inatakiwa kuangaliwa upya
Huwa najiuliza hivi inawezekanaje mkeo asiijue password ya kadi zenu za Bank?? Hapa huwa naona kama kuna shida kwa baadhi ya wanaume, aisee mimi card zetu tuna share password yake naijua na yangu anaijua hivyo yeyote anaweza kwenda kutoa pesa mda wowote zinapo hitajika.

Aisee hata nikifa ghafla mwenzangu anaweza kwenda chukua fedha zote
 
Hizo ni ndoa za machekibobu.
 
Ipo sawa maana sheria ya ndoa imewabeba sana
 
Kwa mujibu wa sheria,kama marehemu aliacha pesa hamuwezi kugewa moja kwa moja.ni lazima ufungue shauri la mirathi mahakama ya mwanzo.baada ya hapo atapewa barua msimamizi wa mirathi aipeleke benk au kampuni ya simu.Akishapeleka pesa zote zitapelekwa bank kuu.Kutoka kule ndio zitarudishwa mahakamani kama cheki na mahakama ndio itagawa cheki zile kwa warithi kama mlivyokubaliana katika kikao cha familia kumteua msimamizi wa mirathi.Ni process ndefu sana na inaweza kuchukua si chini ya mwaka mmoja toka marehemu afariki.kuwa na subira tu.Lakini kama angekua na password anatoa tu hela na habari inaishia pale
 
Mzee baba huko hazina ndipo kwenye shida.mara nyingi Bank hutoa check mapema na kuzipeleka hazina.Sasa kasheshe ni cheki kutoka hazina kurudi mahakamani.Haloo ni mwendo wa nenda rudi kesho.mara hazijasainiwa.mara hazionekani.zikionekana utaambiwa njoo wiki ijayo tena kwa maneno matamu wale watu hazina Mungu anawaona.kila siku ni story.mimi nilikua nikiambiwa njoo wiki ijayo narudi kesho asubuhi.nilifanya hivyo miezi sita chek zikatoka ila jasho la meno lilinitoka
 
Reactions: BAK
Hakuna kampuni inayolipa moja kwa moja kwa mtu.Ila nilipoenda NMB kutoa taarifa kwamba mteja wao amefariki nilipewa pole milion moja.Ndio yote tulitumia kujisogeza wakati Tunasubiri mirathi itoka nayo tulikamilisha kila kitu ila ikachukua mwaka mzima kutoka
 
Inategemea kama huyo mke ana akili timamu na uelewa wa kusimamia hilo. Wengine ni shida.... Akishika mzigo huo ni kutumbua tu....
 
[emoji23][emoji23]
 


Habari yako mkuu, naomba kuuliza swali. Kwa mfano marehemu kipindi cha uhai wake alimpa eneo ndugu yako wakiume kiwanja kama zawaidi. Japo haikuwa wazi , yaani marehemu Hakumtaarifu ndugu yeyote. Ikiwa na maana hata ndugu na familia ya marehemu inajua kuwa hiyo property ilikuwa ni ya marehemu. Japo mzawadiwa anaumiliki halali wa eneo kisheria yani alifuatikia hati ya kiwanja na kuipata.

Swali langu ni endapo property hiyo ikiorodheshwa na msimizi wa mirathi kama mali inayositahili kurithiwa, Je Mmiliki halali wa kisheria anawezaje kuichoma property hiyo kwenye orodha?
 
Hv ni kwann wanaume tu ndo tunandikaga wosia na utaribu wa mali tutapoanza kufa? Hv sisi wanaume ndo ishakua 22/7 kutangulia kufa? Au sisi tu ndo wenye mali?
 
Hongera sana mkuu
 
We nae umekalia kushobokea eti sheria mbovu. Ubovu wake huelezei, watu wanakuelewesha hapa bado umeshupalia (huku umebana pua) "sheria mbovu"
Umeamkaje na jazba lote hilo sasa Hahahaa.... ukiendelea hivyo utakujaga kufia usingizini haki🤣🤣🤣🤣 Wewe rudi uendelee kusoma Uzi utakutana na mijadala ya huo ubovu. Hata sijashupaa na kubana pua kama unavyodai, tuko kwenye mjadala kawaida tuu. Punguza chuki na jazba, Usikurupuke tena hivyo eeeh! Sawa!?

Sheria ya mirathi kwa upande wa wajane kina mama inatakiwa kuangaliwa upya
Upya kwa sababu gani? Ina mapungufu gani?
Huwa inakuwa kubwa Sana kama kuna watoto wa pande mbili tofauti na walikuwa hawapendani kingine kwamba na suala la elimu nalo tatizo kubwa Sana aisee ukikosa elimu sometimes huwa tatizo tena
Sasa inauzwaje kama mama ndo kabaki kichwa cha familia atakaeuza ni nani? mana tayari mama yupo muuze ili iweje tatizo ndo linakujaga hapo kukosa busara kwa baadhi ya Wana ndugu shida Sana
Busara v/s Sheria
Kumbuka pesa haina undugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…