Hivi mtu akifa na hela zake ziko benki na Mpesa, tukiwa na cheti cha kifo tunaweza fuatilia?

Mambo yote mahakamani.
Wala asiogope .atafute wakili wa kumuongoza atazipata bila wasiwasi.
"Haki ya mtu haipotei"
 
Hazina Tena kwa kujichotea.
Ndo maana huu UTAWALA hauna baraka.
Pesa za marehemu utazichukua vipi?
 
Wewe unavyodai eti mali ulitafuta na marehem mumeo zitauzwa na warithi kugawana.

Na sheria inasema warithi halali ni mke na watoto. Na wewe mke ndio msimamizi wa mirathi.

Sasa ulikua unatakaje? Kwamba ziuzwe zote upewe peke yako, watoto mliozaa (ambao ni watoto wako pia) wasipate, upate peke yako tu?

Una akili timamu?
 
Mfiwa pole sana, pata moyo mkuu.

Mwanasheria habari za wakati huu, pole na shughuli.

Kwa nini taratibu - kwa mujibu wa maelezo yako - zinawalazimu Wakristo kupitia kwa Hakimu Mkazi, na kwa mwanasheria, na kupeleka maombi maalum, hatua ambazo ni ndefu, ngumu na za gharama ilhali Muislamu "anajaza fomu tu" mahakama ya mwanzo ?
 

Achana na hizo ETI zako buana.

Huu ni mjadala uko jukwaani kujadiliwa, kila mmoja anajifunza na kutoa kile anachojua. Sasa shida yako hapo ni nini? Au shida ni comment ya mama D😎

Mimi akili timamu ninazo kabisa ndio maana napost ninachokijua na kusoma majibu kufahamu yale nisiyoyajua... ila naona kwa jazba hili kama zako haziko timamu halafu hata hujioni😂😂😂

Heri ya mwaka mpya 2021
 
Unajishebedua tu baada ya kugundua kuwa ulitia boko.
We kubali kuwa uliandika pumba. Uwe unauliza kwanza kama kitu hujui.
 
Swali zuri. Habari za wakati huu ni njema, na asante sana kwa kunipa pole ya majukumu, pole na kwako pia mkuu.

Kimsingi, huo ni utaratibu tu uliowekwa kisheria bila kujali misingi ya udini; kwamba kwasababu ni waislamu basi wawe na taratibu nyepesi, na wakristo wawe na mlolongo mrefu, ingeweza hata kuwa vice-versa. Hata hivyo, mawakili hawaruhusiwi kutoa uwakilishi katika Mahakama za Mwanzo, na ndiyo maana ukiwa na kesi Mahakama ya mwanzo ukataka kuweka wakili basi ni sharti uombe kuhamisha kesi hiyo iende Mahakama ya Wilaya/Mahakama ya hakimu mkazi.

Nilisahau kumalizia kwenye comment yangu ya msingi, kwamba akishapata ile hati ya usimamizi wa mirathi kutoka Mahakamani basi ataandika barua na kuipeleka kwenye mtandao husika wa simu huku akiiambatanisha hati yenyewe. Fedha zitatolewa na atapatiwa msimamizi wa mirathi kwa minajili ya kuzigawa kwa warithi wa marehemu. Asante.
 
Ngoja tupate ushauri wa wanasheria makanjanja!
 
Hivi wanakulipa fees hawa?

Mbona unajitutumua sana?
 
Hivi wanakulipa fees hawa?

Mbona unajitutumua sana?
Mkuu, Biblia Takatifu kwenye 1 Petro 4:8 na Warumi 12 inatufundisha kwamba "Kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, aitumie kwa kumuhudumia mwingine, kama wakili mwema wa neema mbalimbali za Mungu".

Naamini mimi kuwa Mwanasheria wala siyo kwa akili zangu mwenyewe bali ni kwa uweza wa Mungu, hivyo sinabudi kuwahudumia wengine.

Pesa zipo tu mkuu. Na Biblia hiyohiyo kwenye Kitabu cha Yoshua Bin Sirra inatufundisha kwamba, "yoyote autafutaye utajiri kwa nguvu hataupata".

Uwe na j2 njema mkuu.
 
Unajishebedua tu baada ya kugundua kuwa ulitia boko.
We kubali kuwa uliandika pumba. Uwe unauliza kwanza kama kitu hujui.
Watu huwa wanaulizie chumbani?
Nenda taratibu mwaka ndio kwanza umeanza huu
 
Hivi mfano nikifanya Huyo mchakato kumne MPesa ameacha 500 si hasara Hiyo!?

au inajulikana kwanza kiasi ndo hatua zinafuata?
 
Sheria umesema inaangalia dini yako kujua ufuate utaratibu gani. Halafu hapo hapo unasema utaratibu huu haujali misingi ya kidini. Huoni kwamba unaji contradict ?

Na unasema sheria imewekwa hivyo mlolongo wa Wakristo uwe mrefu...

Hukumuuliza professa wako chuoni KWA NINI MLOLONGO WA WAKRISTO UMEWEKWA UWE MREFU ???

Nimekuvumilia nimeshindwa ustaarabu. Umesoma wapi shule wewe schmucko ???
 

mkuu mimi baba yangu alikufa hivyo baba mkubwa ndie aliye kuwa msimamizi wa mirathi na mpaka sasa hakuna kina kinacho endelea licha ya mam kusem kuwa baba alituekea watoto wake fedha benk ambazo zingetusaidia pindi tutapo anza elimu ya juu ila mpaka sasa nipo mwaka wa mwisho chuo na sijajua ni jinsi gani ningeweza kufatilia hizo fedha benk licha ya kwamba ninacho cheti cha kifo cha baba
 
Hivi ni kwamba tunakosa watu sahihi wa kuoa/kuolewa nao mpaka tunashindwa kushare vitu muhimu kama hivyo vya kipesa?
 
Sio kwamba mmeshatapeliwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…