Hivi mtu anaweza kuwa na UTI zaidi ya 500?

Zero Hours

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2011
Posts
12,942
Reaction score
18,669
Leo nimempeleka mke wangu maabara baada ya kusumbuliwa na tumbo muda mrefu.

Tulifanya vipimo mbali mbali ikiwemo cha UTI. Tukapewa majibu kuwa ana UTI nyingi sana yaani zaidi ya 500.

Na daktari akatuambia ya kawaida huwa ni chini ya 8. Akatushauri achome sindano ambazo ni 5000 kila moja kwa siku 5.

Binafsi sikuamini nikampeleka maabara nyingine tuhakikishe maana hawa madaktari wa mitaani huwa wapo kibiashara zaidi. Napo tulipopima tukaambiwa ni nyingi sana hadi haihesabiki.

Kusema ukweli leo ndiyo nimesikia UTI zaid ya 500 na mtu anatembea kawaida tu.

Je, kuna waliowahi pata UTI ya kiasi hicho na walitumia dawa gani kupona???
 
Hee ndyo nini tena iyo?
unachkua mkojo unaupanda ( culture sijui kiswahili kizuri ni kipi) kwenye maabara ili bacteria wakue technologist aweze kuwahesabu. anawez akakuta 500, 50, 1000 bacteria say kwenye mililitre of urine so calcured. Sasa sijui kama ulifanya hiyo test. najaribu kuwaza...
 
Sio oyo. Ni kuwa tulpeleka tu mkojo ndani ya dakika 10 tukpewa majibu
 

Dawa nzuri kwa UTI ni LEVOZ aisee lakini kuna jamaa yangu aliumwaga UTI,dawa za hospital hazikumsaidia akaenda hadi kwa masangoma wakampiga hela kwa madai ya kurogwa lakini mwishoni akaenda kwa mganga mmoja akamwambia hujapigwa juju wala nini akamuelekeza akatumie aloe vela
Hali ya mshkaji kwa sasa shwari kabisa
 
Kaka kuhusu u.t.i. naijua vizuri mimi nilifikisha 1000 daah yaani nilikua nashindwa ata kuzuia mkojo alafu pale mbele kuna toa kama usaha DR akanambia una hatari wewe
 
Hapati any kind of thrush kwenye maumbile yake?
 
Mkuu dawa ya UTI ni vidonge vya Antibiotics kama,Ciprofloxacin ,Ampiclox,Penicillin, (PPF)
Kwa UTI sugu,tumia Ciprofloxacin+Ampiclox+Penicillin pamoja.
Nione inbox
 

MKuu hiyo alo vera alitumia vipi tunaomba msaada
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…