Hivi Musukuma anajikuta kama nani kuwatisha wananchi kiasi hicho?

Hivi Musukuma anajikuta kama nani kuwatisha wananchi kiasi hicho?

Burkinabe

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2023
Posts
2,354
Reaction score
4,024
Asalaam Aleykum wana JF wenzangu.

Rejeeni mada tajwa hapo juu.

Mimi nikiwa kijana Mzalendo wa Kitanzania, huwa ninakerwa sana na baadhi ya wabunge akiwemo Joseph Kasheku aka Musukuma hasa kwa tabia zao za kuwaona wale wenye maoni ya tofauti na serikali (au maoni yao wenyewe) kama ni wajinga, waharifu n.k.

Hii imejidhihirisha pia juzi ambako baadhi ya video clips zinamwonesha akivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwashughulikia wale wanaopinga mpango wa serikali kuzimilikisha/kuzibinafsisha bandari zetu.
Hivi kweli hiyo ni akili kweli?!
Kwa hiyo kwa mtizamo wa Musukuma, anataka sisi wananchi wa kawaida tukae tu kimya hata pale tunaona mambo hayaendi sawa?
Je, huo ni uzalendo au ni ujinga?

Kwa ninavyojua, Mzalendo ni yule ambaye yuko tayari kufa akiitetea nchi yake kwa hali na mali.

Hivyo Musukuma badala ya kuwashambulia wale wenye maoni ya tofauti na yake kuhusiana na suala la Bandari, kwanza kabisa angewapongeza kwa uzalendo na mapenzi yao mema kwa kwa nchi yao, na pili angejielekeza zaidi kwenye kuwaelimisha zaidi wananchi (nikiwemo pia) juu ya umuhimu wa kumilikisha Bandari zetu kwa wageni, na faida za kiuchumi, ulinzi na usalama kwa nchi yetu zitakazopatikana..

Nahitimisha kwa kumtaka Musukuma pamoja na wabunge wenzake wenye tabia hiyo, watuache Watanzania wenzao pale tunapokuwa tunatoa maoni yetu juu ya nchi yetu. Tanzania ni yetu sote. Hivyo sote tunawajibika katika kuilinda na kuitetea nchi yetu.

Ahsanteni sana.
 
Msukuma anasema hajahongwa V8 kwakuwa ana hela na miradi mingi lakini akumbuke kila mmoja ana bei yake PRICE TAG kwahiyo yeye size yake ilikuwa ni hiyo usd 50,000 na hilo V8 nk

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndo maana wakasema wakati mwingine kunyamaza kimya nayo ni hekima. Sasa yeye, kadri anavyozidi kuongea ongea na kuwatisha wale ambao wako against na huo Mkataba, ndo anazidi kutuaminisha kwamba kuna kitu alipewa, siyo bure!
Maana hata kama ni wajinga kiasi gani, haiwezekani Watanzania mamia kwa maelfu wawe na wasiwasi na huo Mkataba, halafu yeye kazi kututisha-tisha Watanzania wenzake ili tuogope kutoa maoni yetu!

Namuhakikishia Musukuma kama kuna kitu kapokea, basi kitamtokea puani siku moja. Ni suala la muda tu. Time will tell.
 
Msukuma msimwonee yeye hana Akili na Elimu hana tuwalaumu wenye Elimu waliomtuma kuwakilisha nchi Dubai akaishia kukodolea mdada aliyekuwa anatimiza majukumu yake.
Tuna safari ndefu sana kama nchi!
Yaani hapa kwetu Tz ukiwa na umbuji wa kujieleza tu vzr na kujua kusoma na kuandika, basi umetoka!

Na ukishatoka, unaanza kuwadharau waliosota na kupigwa na umande!
 
Unaweza ukashangaa kodi anayolipa kwa mwaka ikawa inazidiwa na PAYE ya mwalimu Mkuu!
TRA watupe muhtasari wa kiasi cha kodi anazolipa kupitia bussiness zake. TUTAMALIZA UBISHI WOTE
 
Ana hela na wewe tafutq hela,kwa vitega uchumi vyake hskuna mbunge anaemzidi kwa hela,kwa nini asiongee anavyotaka,hatq akiwaambia vipi hawakoromi kwa kuwa hawana hela na pia ni mpambanaji
 
Msukuma msimwonee yeye hana Akili na Elimu hana tuwalaumu wenye Elimu waliomtuma kuwakilisha nchi Dubai akaishia kukodolea mdada aliyekuwa anatimiza majukumu yake.

Kuna watu wanatambia uganga na ulozi. Bahati mbaya sana, hata wasomi, badala ya kutumia maarifa, wengine wamekuwa wateja wa waganga hao, kwa kuamini nyota zao zitang'arishwa.
 
Asalaam Aleykum wana JF wenzangu.

Rejeeni mada tajwa hapo juu.

Mimi nikiwa kijana Mzalendo wa Kitanzania, huwa ninakerwa sana na baadhi ya wabunge akiwemo Joseph Kasheku aka Musukuma hasa kwa tabia zao za kuwaona wale wenye maoni ya tofauti na serikali (au maoni yao wenyewe) kama ni wajinga, waharifu n.k.

Hii imejidhihirisha pia juzi ambako baadhi ya video clips zinamwonesha akivitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuwashughulikia wale wanaopinga mpango wa serikali kuzimilikisha/kuzibinafsisha bandari zetu.
Hivi kweli hiyo ni akili kweli?!
Kwa hiyo kwa mtizamo wa Musukuma, anataka sisi wananchi wa kawaida tukae tu kimya hata pale tunaona mambo hayaendi sawa?
Je, huo ni uzalendo au ni ujinga?

Kwa ninavyojua, Mzalendo ni yule ambaye yuko tayari kufa akiitetea nchi yake kwa hali na mali.

Hivyo Musukuma badala ya kuwashambulia wale wenye maoni ya tofauti na yake kuhusiana na suala la Bandari, kwanza kabisa angewapongeza kwa uzalendo na mapenzi yao mema kwa kwa nchi yao, na pili angejielekeza zaidi kwenye kuwaelimisha zaidi wananchi (nikiwemo pia) juu ya umuhimu wa kumilikisha Bandari zetu kwa wageni, na faida za kiuchumi, ulinzi na usalama kwa nchi yetu zitakazopatikana..

Nahitimisha kwa kumtaka Musukuma pamoja na wabunge wenzake wenye tabia hiyo, watuache Watanzania wenzao pale tunapokuwa tunatoa maoni yetu juu ya nchi yetu. Tanzania ni yetu sote. Hivyo sote tunawajibika katika kuilinda na kuitetea nchi yetu.

Ahsanteni sana.
Anaringia uchawi tu hana lolote
 
Back
Top Bottom