Hivi, nani anatakiwa kuchinja nyama?

Hivi, nani anatakiwa kuchinja nyama?

Ntarudi mwishoni wacha waje wachangie wengine kwanza!
Najua una kaudini kiasi ila umesahau kuuliza kwanini J,pili iwe siku ya mapumziko na isiwe Ijumaa na J,pili?

hivi uwarabuni huwa nisiku gani vile..na kuna skuku yoyote inapambwa kama x'mass..world wide?
 
Kwani hamna mashehe vijana?
Hebu tupe ushahidi wa mashehe wanaochinja huko machinjioni, mimi napita pita sana vingunguti kununuwa nyama, sijakutana na shehe anaechinja huko bali nimekuta vijana ndio wanachinja huko.

Au una maana ipi unaposema "mashehe"?
 
Hii ishu ina migogo baadhi ya maeneo na watu wanataka kuanza kugoma kununua nyama. Niliwahi kutana nayo na kwenye maoni ya katiba mpya. Kisheria na kijamii nani wanaruhusiwa kuchinja mifugo machinjioni? Tumezoea mashehe ndo wanachinja, je wachungaji/wainjilisti na mapadre/makatekista wanaruhusiwa kuchinja? Kama ndio kwa nini haikuwekwa zamu? Kama hapana kwa nini iwe hivyo? Kuna ndugu zangu wauza nyama na wengine ni walokole wamenifuata na kuniuliza kuhusu hilo, ukichukulia nina kaelimu ka kukariri wakajua najua kila kitu. Naomba wanasheria, wanajamii, mabwana mifugo na wengine wenye ujuzi wa hili jambo mnijuze ili nisitoe ufafanuzi wa kimgogoro.

Serikali imekuwa inawaendekeza Waislamu mpaka wameota Mapembe hadi leo. Suala la kuchinja Wanyama katika Bucha zinazo ongozwa na Serikali isiyokuwa na dini haliwezi kuendesha kwa mfumo wa dini .Yafaa wale wanaochinja wawe wataalamu kutoka wizara ya mifugo.

Hata hivyo Waislam haohao wanakula Nyama ya kuku katika hotel mbalimbali pia wanakula wanyama pori bila kujua ni nani amechinja. Pia wanakula Nguruwe!!!
Kuwaendekeza Waislamu ndiko kunakoleta hata kiburi wakati wa Kuwaapisha Maraisi utaona Wanataka waende kusoma dua!! Hapo unachanganya Maombi na uganga wa Kienyeji
 
Samahani kama nitawaudhi wengine.
Kwanza kabisa mimi siamini dini nyingine ila dini yangu.
Katika mafundisho nakumbuka wayahudi walipaswa kuchinja mzaliwa wa kwanza mwana kondoo na kupaka damu yake ktk door post ili usiku malaika akipita atambue hapa ni kwa myahudi asiwadhulu.
Katika hili hapakusemwa wapeleke mnyama wao wakachinjiwe! Bali wachinje wale na kwa maelekezo.
For the passover walikuwa wakichinja na wanakula kwa maelekezo!
Hata wale kware walipokuwa wanaokota kule jangwani mungu aliwaagiza wachinje wale wasibakize na maelekezo mengine hakuelekeza kwamba peleka kwa kasisi akuchinjiee hapana.
Siku za karibuni pamejitokeza watu wanaojiona wao ni bora kuliko wengine wakiingia kwetu kabla hajala anauliza nani kachinja!
Hii imefanya baadhi ya familia zetu kuwafikiria kuto wakwaza hivyo kuwaita wachinje.
Lakini hakuna lolote zaidi ya kushika kisu na kukata shingo! Kwanza mara nyingi issue za kuku mama anamaliza mwenyewe huko jikoni na mie nakutana na nyama mezani, kwenye mbuzi nashiriki maana anaweza kumshinda nguvu, na pia naelekeza vijana wafanye!
Hebu jiulize hao kuku wanaoliwa chips huko mitaani wanachinjwa vipi.
 
Ntarudi mwishoni wacha waje wachangie wengine kwanza!
Najua una kaudini kiasi ila umesahau kuuliza kwanini J,pili iwe siku ya mapumziko na isiwe Ijumaa na J,pili?

umekurupuka usingepost huu utumbo.. Soma post tena n comment accordingly
 
wakristu nahisi hawana kikwazo kinachowazuiya kula nyama kwa namna yeyote alivyochinjwa!
Kwahiyo ni bora tufuate utaratibu ambao hauna shida kwa jamii yote ili kuepusha usumbufu na pia ni {ajira kwa wengine!}
Mungu ibariki Tanzania.[/QUOTE]MKUU HAPO KWENYE AJIRA UMENENA!
 
Sijapitia comment zote ila title ya thread yako inazua mtafaruku wa kufikiri. Sidhan kama NYAMA INACHINJWA. Japokuwa kwenye maelezo yako umesomeka vizuri.
 
mkuu nimesema ni mambo yanayoongelewa mtaani na yaliongelewa kwenye utoaji wa maoni ya katiba. Unajua kuna mambo yalikuwepo inabidi tupate ufafanuzi, je na nchi zingine wanafanya hivyo?

Umeshajiuliza katika nchi ya Vatican huwa anaxhinja nani?.
 
Yeyote anaweza kuchinja hasa ikizingatiwa kuwa hizi dini nyemelezi zimemkuta mswahili akijua kuchinja kupika na kula. Nadhani anayeweza kuchinja ni suala la mwenye mnyama. By the way, nani anastahili kuchinja samaki, nyati, Swala, Nyumbu na wengine wengi? Sijui hawa walioweka masharti ya kuchinja mfano ng'ombe kama wanao kwao zaidi ya kuwafaidi toka kwetu.

Mkuu umenena ukweli mtupu!
 
Hii ishu ina migogo baadhi ya maeneo na watu wanataka kuanza kugoma kununua nyama. Niliwahi kutana nayo na kwenye maoni ya katiba mpya. Kisheria na kijamii nani wanaruhusiwa kuchinja mifugo machinjioni? Tumezoea mashehe ndo wanachinja, je wachungaji/wainjilisti na mapadre/makatekista wanaruhusiwa kuchinja? Kama ndio kwa nini haikuwekwa zamu? Kama hapana kwa nini iwe hivyo? Kuna ndugu zangu wauza nyama na wengine ni walokole wamenifuata na kuniuliza kuhusu hilo, ukichukulia nina kaelimu ka kukariri wakajua najua kila kitu. Naomba wanasheria, wanajamii, mabwana mifugo na wengine wenye ujuzi wa hili jambo mnijuze ili nisitoe ufafanuzi wa kimgogoro.

Kuruhusiwa na nani?

Hapo kwenye bold kidogo pananitia shaka uelewa wako wa ustaarbu wa watu wengine. Hivi ndugu yangu kweli unataraji umkute Padre machinjioni anachinja mbuzi!

Mimi sioni unachouliza kwa nia njema hapo, ila kwa kukukomoa nitakujibu kwa nia njema.

Waislam wana desturi ya uchinjaji kutokana na maagizo ya dini yao. Ili nyama iwe halali kwao kuna mambo kadhaa yanapaswa kuzingatiwa. Kwa hiyo kwa mazingira yao inalazimu muislamu kuchinja ndio wale (japo ukiweka ubwabwa na nyama mezani hamna atakayekumbuka hilo).

Kwa Wakristo, lipo sharti moja linalohusu machinjio ambalo ndugu zetu wachaga limewashinda. Maandika yanaharamisha unywaji wa damu ya mnyama uliyemchinja. Zaidi ya hapo hakuna mbwembwe wala kitu gani. Kwa wenzetu wenye machinjio ya kisasa, mnyama hupigwa shoti ya umeme kabla ya kuchinjwa ili asisikie maumivu jambo ambalo kwa Waislam ni batil, wao huamini mnyama anapaswa kujutia kuzaliwa.

Kwa hiyo kama una 'ngubi' wako unataka kumwangusha ni vyema ukamuita Muislam akuchinjie ili wenzetu wasishindwe kula.
 
Lakini hakuna lolote zaidi ya kushika kisu na kukata shingo! Kwanza mara nyingi issue za kuku mama anamaliza mwenyewe huko jikoni na mie nakutana na nyama mezani, kwenye mbuzi nashiriki maana anaweza kumshinda nguvu, na pia naelekeza vijana wafanye!
Hebu jiulize hao kuku wanaoliwa chips huko mitaani wanachinjwa vipi.

Kuku wa chips mangi anawachinjia kwenye gogo. Anashika mdomo shingo gogoni panga linapita, kwachu.

Hata samaki na kumbi kumbi hatuulizani
 
mambo mengine ni yakijamii zaidi,kwa upande huu,jamii imegawanyika katika pande mbili,kuna anayekula nyama iliyouwawa kwa namna yoyote,eidha kwa rungu,risasi,kisu,sumu,n.k pia tendo hilo laweza ambatana na tamko lolote likitegemeana na mtendaji au lisiambatane na tamko.Kundi la pili tendo la kuuwa linafanyika na mwislamu tu ambaye anatumia kisu tu,kwa maana hiyo tendo lake ni kuchinja na si vinginevyo,na kuchinja huko kunafanyika baada ya dua maalum aliyoambiwa na muumba wake atumie kabla ya kuchinja mnyama au ndege yeyote kwa ajiri ya kitoweo.

Ndio maana kiustaarabu kwa kuwa kundi la kwanza lenyewe halina shida basi jamii imeamua kuwaruhusu wale wa kundi la pili wafanye tendo hilo kwa kuwa katika familia zetu tuko mchanganyiko.

Pia ukisoma bibilia yote hutapata andiko linalofundisha namna ya kuchinja,lakini quran inaeleza ustaarabu wa kuchija kwa hiyo ndilo linalofanyika katika machinjio yetu.

Lakini kitoweo chako nyumbani kama wewe ni kundi la kwanza anaweza chinja yoyote hata kama si mwislam ila akija mgeni wako mwambie hii hajachija mwislamu kwa hiyo kwa ustaarabu na ukarimu wa mtu hutumia nyama iliyochinjwa kwa dua maalum ya mwislam ili kila mtu aweze kula.
 
Hii ishu ina migogo baadhi ya maeneo na watu wanataka kuanza kugoma kununua nyama. Niliwahi kutana nayo na kwenye maoni ya katiba mpya. Kisheria na kijamii nani wanaruhusiwa kuchinja mifugo machinjioni? Tumezoea mashehe ndo wanachinja, je wachungaji/wainjilisti na mapadre/makatekista wanaruhusiwa kuchinja? Kama ndio kwa nini haikuwekwa zamu? Kama hapana kwa nini iwe hivyo? Kuna ndugu zangu wauza nyama na wengine ni walokole wamenifuata na kuniuliza kuhusu hilo, ukichukulia nina kaelimu ka kukariri wakajua najua kila kitu. Naomba wanasheria, wanajamii, mabwana mifugo na wengine wenye ujuzi wa hili jambo mnijuze ili nisitoe ufafanuzi wa kimgogoro.

.
Sidhani kama kuna mwenye haki ya kuandaa chakula cha mwingine na kwa huyo anaeandaliwa akanyimwa haki hiyo. Ninasimama katika katiba ya nchi isiyo na dini na kwa maana hiyo inaziheshimu na kuzidhamini dini za watu wake kila mmoja kwa jinsi yake ikiwa tu havunji sheria ya nchi. Ndio basi tujiulize ni sheria ya nchi nyama yote inayouzwa kwa halaiki kuchinjwa kwa mungu wa kiisilamu? Sidhani kama ni hivyo na kama ikithibitika ni hivyo basi wakristo tuna haki ya kukataa sheria hii ya kushurutishwa. Katika imani uetu sisi tunaamini kuwa kama wanyama wetu hatutawachinja kwa uhuru wa sheria ya Mungu wetu, basi tutaruhusu adui namba moja wa Mungu wetu yaani majini(mapepo) kushiriki katika chakula chetu. Wakristo kwa asili hatuna adui katika uzao wa binadamu kwani tumeagizwa kupendana mmoja kwa mwingine na kama kuna kuhafilika basi turejeshane kwa upendo ila sii hata siku moja tumeagizwa kuwa na ushirika kwa namna yeyote ile na jini(pepo). Haya mapepo tunayo amri ya Bwana Yesu kuwakanyaga na nguvu zao zote waka hakuna kitakachotudhuru. Haya mapepo ndio shina haswa la mateso ya uzao wa Adamu. Sasa ikiwa ya kwamba tuna njia ya kukifanya chakula chetu wasishiriki ili wafe kabisa tutafanya hivyo. Na kwa kufanya hivyo yaani kuyaangamiza majini kabisa katika mazira yetu hakuna sheria ya jamhuru ya serikali ya muungano wa Tanzania tutakayovunja.
.
 
Hapa ruksa kuchinja kila mtu ...hizi taratibu za kuchinja haziko kisheria ni mapokeo tu watu wanaamua kuyaendekeza...Zamani ilikua hata kuku home ukitaka kuchinja basi unawatafuta wale jamaa wanaelekeza kitu kibra kinachinjwa siku hizi watu wanachinja wenyewe........
 
Hilo si suala la mashehe bali kila muislam anaejua taratibu za kuchinja anaweza kuchinja. Mnyama yoyote anataka kuchinjwa lazima jina la M/MUNGU (ALLAH) litamkwe na aelekezwe Makka (Kibla) pamoja na mambo mengine. Kama dini nyengine hazizingatii hayo isiwe tabu, tueleweshwe tu tunapofika kwenye butcher
 
Back
Top Bottom