joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,117
- 46,617
Ndugu zetu wakenya, ni wazi kwamba pamoja na shida nyingi za kiuchumi zinazoikumba serikali na wananchi wa Kenya, tatizo mama ni kukosekana kwa udhibiti wa uchumi wa Kenya, ambapo watu na makampuni machache yanamiliki sehemu kubwa ya uchumi wa Kenya.
Kitendo cha Kuwepo kwa watu wachache wenye nguvu za kiuchumi, kumewafanya wanasiasa wengi kuwa vibaraka wa matajiri na kuifanya serikali ya Kenya kuwa dhahifu sana mbele ya matajiri.
Magufuli amejaribu sana kupambana na hiyo hali kiasi cha kuweza kuongeza uwezo wa serikali ya Tanzania katika kumiliki uchumi wa nchi, hii ndio sababu kubwa ya Tanzania kuongoza Afrika ktk 1)Economic inclusiveness index, na 2) Kupunguza umasikini.
Kujifunza kwa jirani yako mambo mazuri ni ujasiri sio unyonge.