Hivi ndivyo tulivyotapeliwa na Ontario wa TMT kwenye Forex

Hivi ndivyo tulivyotapeliwa na Ontario wa TMT kwenye Forex

Cre forex alifundishwa na mkewe yule anayempost insta , yan yeye mentor wake ni mkewe[emoji23][emoji23][emoji23] [emoji23][emoji23][emoji23]


Cre hajafika kiwango cha kuwa mentor sema analazimisha tu mambo...kwa kifupi Cre anatakiwa bado awe chini ya mentor..
 
Cre forex alifundishwa na mkewe yule anayempost insta , yan yeye mentor wake ni mkewe[emoji23][emoji23][emoji23] [emoji23][emoji23][emoji23]
Afu mshkaji huwa hata haoni aibu anasema kabisa mke wake ndio aliomfundisha kudanlodi masese.

Nlishangaa sana yaani jamaa ana miaka miwili tangu aanze kutrade akiwa kafundishwa na mke wake then awe professional trader!? Wakati najua it takes year of intensive study and dedication ili MTU awe consistency profitable trader!?

Bora Dawa ni mkali kuliko Cre.
 
Mpaka sasa sijatapeliwa na wala sijamhusisha roboti kwenye kutrade,

Nilinunua signals mwanzoni nikaona sio issue nikatafuta mentor wangu,

Niliona toka mwanzo staili aliyokuw anatumia mwana kufundishia haikuwa poa hata kidogo

By the way dogo ashukuliwe kwa kufungua akili
Baniani mbaya kiatu chake dawa!
Mkuu tangu uanze umepata faida dollars ngapi kwa mtaji kiasi gani
 
Nilishtuka baada ya kufananisha analysis za astroforex kwenye web yao ambapo kipindi kile wale jamaa walisema buy EURUSD lazima ifike 1.2400 huku wakitoa sababu pamoja na chat ambapo cre anakwambia sell EURUSD and hold lose inafika $55 na mtaji wenyewe $100 unamuliza mentor should we cut lose yeye anakujibu hold tangu siku hiyo nikagundua huyu mentor uwezo mdogo na magumashi tu sikuwahi kufuata tena call zake na mwishowe nikajitoa magroup yao.
Niliamua kukomaa na video za youtube za muhindi wa urbanforex na baadhi ya vitabu mpaka sasa mambo yapo fresh.


Mkuu usinikumbushe hii kitu...siku hyo nilipoteza zaidi ya Dollari 1000...na nilimfuata Cre private nikamwambia EURUSD ni buy anakomaa kuwa ni selll... Nilikuwa na trades za buy EURUSD nikatoka nikaingia sell ndo nakaishia kupoteza hela. Baadae namuuliza anaanza story zake za market makers sijui. Cre bado ni mweupe sana kwenye chart analysis na kusoma candlesticks na reversal patterns maana kama unakumbuka kipindi hcho EURUSD ilikuwa imeprint double bottom kwenye H4 tf...na niliiona ndo nikaingia trades za buy baadae Cre anasema sell na mimi nikakubaliana naye na kuexit trades zangu za buy nikaingia sell ndo yakanikuta yakunikuta. Cre mweupe sana mkuu we acha tu..analazimisha tu mambo na kujisifusifu kifala ila ni mweupe sana sana sana.
 
Mkuu usinikumbushe hii kitu...siku hyo nilipoteza zaidi ya Dollari 1000...na nilimfuata Cre private nikamwambia EURUSD ni buy anakomaa kuwa ni selll... Nilikuwa na trades za buy EURUSD nikatoka nikaingia sell ndo nakaishia kupoteza hela. Baadae namuuliza anaanza story zake za market makers sijui. Cre bado ni mweupe sana kwenye chart analysis na kusoma candlesticks na reversal patterns maana kama unakumbuka kipindi hcho EURUSD ilikuwa imeprint double bottom kwenye H4 tf...na niliiona ndo nikaingia trades za buy baadae Cre anasema sell na mimi nikakubaliana naye na kuexit trades zangu za buy nikaingia sell ndo yakanikuta yakunikuta. Cre mweupe sana mkuu we acha tu..analazimisha tu mambo na kujisifusifu kifala ila ni mweupe sana sana sana.
Daah! Pole sana..yule bwege Mimi alishanitoka moyoni zamani sana na panki lake kama Shabaranks. Anafanya mizaha na hela za watu!? Yaani order yako ikienda hata pips mbili in profit unamsikia "GJ respect my name"...morfaka! Ikienda against anakwambia hold una dola 500 ikifika loss ya dola 450 anakwambia cut losses guys..! Later on unamsikia goodnight and Shalom! Ahahaha ndo kashawaachia manyoya hivyol.

The Cre world is cruel and criminally.
 
Daah! Pole sana..yule bwege Mimi alishanitoka moyoni zamani sana na panki lake kama Shabaranks. Anafanya mizaha na hela za watu!? Yaani order yako ikienda hata pips mbili in profit unamsikia "GJ respect my name"...morfaka! Ikienda against anakwambia hold una dola 500 ikifika loss ya dola 450 anakwambia cut losses guys..! Later on unamsikia goodnight and Shalom! Ahahaha ndo kashawaachia manyoya hivyol.

The Cre world is cruel and criminally.


Jamaa fala sana yaani...ubishi tu wa kijinga...ukimwambia kitu hataki kukubali mwishoni anaanza kuleta visingizio...yaani nimetoka kumchukia we acha tu.
 
Ila mliopitia TMT na nyinyi ni wajinga wa kiwango cha 5G! Wewe unatrade na JP Markets lakini ukitaka kudeposit au kuwithdraw unapitia TMT what the f**ck! Halafu tangia lini uchaguliwe brocker? Tangia lini uwe trained kwa siku tano then unaambiwa uweke 200$ na wewe unakubali?

Poleni sana
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119][emoji119]
 
Kwenye maisha kuna mambo yakishatokea unapaswa kuyapokea Kama sehemu ya funzo flani muhimu kwako kisha pale kwenye makosa parekebishwe then let it go!!!
 
Kuharibu company name kwa sababu ya cheating or failing to abide with the business ethics and responsibility ni hatari na it may destroy the company brand forever if not handled well.

Iliwahi kuwatokea Volkswagen walipocheat ile Diesel emission test walitetereka sana kama kampuni mauzo ya magari yakashuka drastically, it took them decades to rebuild people's trust.

Samsung wao walikuwa na cheating ya batteries zao..zilikuwa zina overheat na kulipuka while kwenye vipimo vya sample walidanganya. Hawa hadi Rais wa Korea wamemponza anafungwa miaka 24 na faini dola milini 17 juu kwa kudanganya na kupokea rushwa yao.

Uaminifu ni mtaji mkubwa. TMT hatuiombei ife ila wakiendelea na cheating and neglect business ethics they won't last na dogo atapanda karandinga.
 
Kuna watu kibao humu JF walituasa kwamba Forex ni utapeli hilo kwanza napingana nalo kwa nguvu zote sababu sio kweli kwamba forex ni utapeli kabla sijafunguka mengine niwathibitishie nimejiridhisha bila hata lepe la mashaka kwamba Forex is real and its my future lifestyle na binafsi sijioni nikikoma kufanya Forex licha ya haya magumu ninayopitia bali mawazo yao ninayachukuliaga kama catalyst ya kutaka kuzidi kuijua hii biashara kwa mapana zaidi kujua weakness na strength zake na kujua potential scammer, wezi na matapeli wakoje maana wametawala hii biashara kwa kiasi kikubwa kutokana na kuwa na money liquidity kubwa kuliko soko lolote duniani..more than 6 trillion USD is traded daily on the Global financial market..hiki ni kiasi kikubwa sana hivyo matapeli huwa wanazengea zengea kwenye magap Kama haya yenye mkwanja mrefu..my economic cake pie is in Forex that's why I wont quit it easily.

But changamoto kubwa ya Forex ni hawa brokers na trainers..ninaposema trainers nazungumzia mtu kama Ontario hawa waliochungulia fursa mapema na kuintroduce kwa watu nchini kwa kigezo cha kuitoa elimu kwa bei sawa na bure tusijue wana agenda yao ya siri na Wasauzi ya kutaka kuwaliza watanzania wenzao.

Ontario ni mtunzi mzuri wa story na ana kipawa cha kusimulia na kushawishi kwa ufasha na ni mtu mwenye uelewa mpana wa mambo but anakosa kitu muhimu sana katika maisha uwezo wa kusocialize na watu in harmony..he is not a leader he is a boss na ukiangalia there is a thin line between a leader and a Boss..Ontario ana dharau, kiburi, na kejeli mbaya sana bila kujalisha umri wa anaeongea nae. Hana attentive listening ukiongea nae anakuangalia kama Choo na hajali lolote najua wengi waliokutana nae watakiri huu ukweli mchungu kwake ukiona mtu ana urafiki na Ontario ujue huyo mtu analazimika kujishusha sana kwa huyu dogo ili waende along. Huwa nashangaa ni rafiki sana na Bold. Pole sana Bold..I know what you going through.

Wahenga humu walituhasa kwamba ukiitwa kwenye fursa tafakari mara mbili yaweza kuwa wewe ndio fursa.anyways tulipoitwa kwenye fursa mwanzoni mambo yalienda vizuri na humu tulikuwa tunavurumusha screenshot za profit tu kwa maelekezo ya Ontario ili tuwakoge haters hadi haters wakafyata but kadri siku zilivyoenda mambo yakawa kimya ikawa ni loss daily tu watu wamechukua viinua mgongo vyote vikafyekwa sokoni. Hakyamungu!

Saga lilianza around mwezi wa kumi baada ya Ontario kula njama ya siri na broker awe anampa pips 2 kwa kila kichwa na zikiwa zinatoka calls kibao kombo kwa siku na zote zilikuwa sio accurate hivyo na watu kutengenezewa mazingira ya kutrade more often inamaanisha wakitrade watu 1000 wakafungua position 7 kila mmoja na idadi ya spreads pips anazopewa kutoka kwa broker kwa mtu mmoja ni 2..kimahesabu anapata 1000×7×2= 14,000 pips hizi ni dola kibao kwa siku ..wandugu wanojua mahesabu zaidi wanajua ni madola kiasi gani jamaa kavuta, hili suala alituficha but aliwahi kusema "Bob Marley you can fool some people for sometime but you can't fool all the people all the time"... Tukashtuka..tukamuuliza..akakubali ila akakiri alituficha na hayo mamilion yanayopatikana ni kwa ajili ya kuendeshea ofisi ya TMT co Ltd iliyoko pale Jangid plaza.. Watoto wa maskini tukakubali tu kwa shingo upande ila tukawa tumeghafilishwa na kusikitishwa sana na hizi njama zao..hili likapita na tukajilazimisha kukimeza maana ukipenda boga upende na ua lake.

Tamaa ni mbaya sana..licha ya kuchukua mamilion kutokana na hizo pips hawakuridhika..bado tena walikuwa wanachukua pesa kibao kwa siri kwa ajili ya IB link kwa affiliate program waliotuunga nayo siku tunamaliza mafunzo kutoka kwa broker kwa sisi tukipata loss sokoni wao wanapata chochote maana broker wao ni market marker. Hakyamungu! People are heartless.

Kama ilivyo asili ya watu wenye tamaa mbaya wakivurugana basi wao hukimbilia kutafuta sympathy ya Wateja..juzi wakavurugana broker na TMT kama ilivyo tabia ya wezi na matapeli kugeukana.. Majuzi wenyewe wanakuja na habari kwamba yule Broker ni market Maker na mwizi..kweli? Wakati wewe mentor umeishi South afrika na umekuwa Trader kwa miaka kibao bado hujui status ya broker unae trade nae? Na inakuwaje mrecomend broker mwenye walakini na competency na efficiency yake? Broker nae anajitetea kwa kutuma texts kwa Wateja privately akimtuhumu huyo mentor kuwa ni batili na mbabaishaji na kuwasihi watu wamuignore!? Blalifuli!

Tangu mwanzo mchakato uligubikwa na walakini mkubwa uliokuwa unaendelea..kwanza kumlazimisha mtu afungue real account baada ya siku tano tu za kumaliza mafunzo na aweke laki tano kuanza kutrade ilikuwa ni ishara ya wizi wa wazi sema tulikuwa na trust na maneno sukari ya Ontario, thus we were blind and fear of missing out easy Money.. Hatukujua!

Kutoa calls zaidi ya 7 kwa siku ni ishara mbaya ya kuwafanya clients waovetrade then wao wapige hela. Wizi huu.

Kuwaambia watu waongeze position ilhali wako in deep red ilikuwa ishara ya wizi, kuwataka watu waburn account zao wao wanufaike.

Kudiscourage matumizi ya stop loss ilhali ndio silaha ya kukinga mtaji wako kwenye Forex ilikuwa ishara ya wizi.

Watu wapoteze zaidi ili mpate zaidi maana kila ijumaa ilikuwa tunapunwa hela yote ya wiki nzima.

Mungu sio Sholo Mwamba, Yule broker market maker aliekuwa anatupiga sisi kwa tamaa kapitiliza kawafanyia mtimanyongo hadi kampuni ya TMT kaipuna zaidi ya nusu billion mapema mwezi wa kwanza. Imagine kampuni hii Changa ya huyu dogo imewazaje kupata nusu billion kwa muda mfupi hivi? Ni mikwanja aliyotuibia sisi misukule wake. But in life! "easy come..easy go"..ukikipata kiwepesi..kitaondoka kiwepesi pia. Nusu billion gone in a single month. Kweli JP Market broker ni hayawani!

Nitoe Rai kwa Ontario...sio kwamba namchukia hapana Bali naamini biashara inayohusisha watu moja kwa moja haiwezi kutokana na tabia yake mbaya ya asili..biashara na dharau, kebehi, utapeli na matusi havichangamani milele. Ni vyema akaendela na kilimo apate mil 19 zake kwa siku. Ameharibu kitu muhimu sana katika maisha yake ya biashara "Brand" and trust ya watu wengi aliowavuta kwa maandishi matamu humu JF..Trust ya watu pekee ni mtaji mkubwa kuliko hata mtaji wa fedha.

Namshukuru kwa kutuletea fursa hii adhimu lakini isiwe sababu ya kutuibia, kututapeli na kutunyanyasa economically and emotionally.

Rai kwa traders waliopigwa za uso na ndugu yao.."if you want to be strong learn how to fight alone" kwa kuwekeza Kwenye skills and self learning tunaweza kuwa self consistency profitable traders..let's ignore TMT they are scammer and predators and I don't recommend anyone to trust them.

Don't hate the game, hate the player.

Oooooopsiiii! Finally misukule wa Ontario tuko huru but tuko nyang'anyang'a kiuchumi. But it feels good kuwa huru.

Forex sio utapeli, matapeli ni mawakala wake.

Ni bora walimkavu...kuliko walimwengu!

Freedom!.
Asante mkuu kwa upendo,,kuleta hii mada hapa jukwaani ili uwaokoe na wengine,,its pure love,,,wewe ni shujaa wa siku[emoji123],,haijalishi umeangukaje what matters ni unasimamaje baada ya kuanguka.poleni lkn ichukulie tu km moja ya changamoto za maisha
 
lakini Mbona Ontario alikuwa anahimiza watu wajiongeze kwa kutafuta skills kupitia vitabu vya mambo ya forex!? alikuwa anasisitiza sana. Tatizo kunauwezekano vitabu havikusomwa vya kutosha na ipasavyo. Hivyo watu wakatumbukiza miguu miwili kwenye bwawa la forex bila kupima kina chake.
 
Kifup yule mentor hana strategy, huwa anatumia support & resistance only kufanya maamuz,
Ulitaka awe anatumia nini mkuu??? Ninavyojua mimi true forex trader ni yule atumiae candlestick,resistance and support, kuchambua soko.....Yaani kuwa pure price action trader.


Nijibu kwanza nilichokuuliza kabla sijaongea ninachotaka kuongea
 
Daah! Pole sana..yule bwege Mimi alishanitoka moyoni zamani sana na panki lake kama Shabaranks. Anafanya mizaha na hela za watu!? Yaani order yako ikienda hata pips mbili in profit unamsikia "GJ respect my name"...morfaka! Ikienda against anakwambia hold una dola 500 ikifika loss ya dola 450 anakwambia cut losses guys..! Later on unamsikia goodnight and Shalom! Ahahaha ndo kashawaachia manyoya hivyol.

The Cre world is cruel and criminally.
Zile call alikuwa anafanya makusudi,BB broker hawezi fanya uhuni wake bila msaada wa mtu wake ataepotosha newbies. Mission accomplished
 
Back
Top Bottom