Hivi ni kweli bara la Afrika lina rasilimali nyingi?

Hivi ni kweli bara la Afrika lina rasilimali nyingi?

ward41

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2022
Posts
749
Reaction score
2,533
images (92).jpeg

Nimesikia watu wakisema bara la Africa Lina utajiri mkubwa wa rasilimali. Cha kushangaza ktk somasoma yangu naona kama hatumo kivile.

Kwenye mafuta middle east, Canada, Russia, USA, Venezuela wanatamba. Kwenye gas ni haohao.

Madini ya chuma naona china, Iran, Chile, USA wanatamba. Kwenye rare earth naona china, north Korea.

DHAHABU naona china, Australia, Canada, Chile, Brazil wanatamba.

Kumbukeni wajomba hayo madini ndiyo yanayotamba Kwenye uchumi wa Sasa.

Kidogo naona DRC katutoa kimasomaso Kwenye cobalt na coltan.

Sasa hizo resources ziko wapi? Wese la Angola, Nigeria,Libya ni kidogo sana. They are not giants.

Je, ni Kweli tuna resources nyingi?
 
Tutathibitisha kwa mdomo? Ilihali hatuna vifaa vya kugundua izo rasilimali.

Tunategemea kutoka nje ya bara na sidhani kama wanatoa taarifa ya ukweli ukifikiria kwamba bado tuko chini ya influence yao.

Kwa fikra zangu tunaweza tukawa na rasilimali nyingi (Africa) zaidi ya mabara mengine ulimwenguni.

Tukiweza kuwa na full control kila kitu kutakua wazi juu ya rasilimali zetu.
 
Sijui source ya taarifa yako ni ipi ila definitely sio kweli.

katika mabara yenye utajiri mkubwa wa rasilimali ni Afrika, na asilimia 30% ya madini yote duniani yapo Afrika.
Lakini kutokana na Akili finyu na Ujinga wa Waafrika wengi Afrika ndio bara masikini zaidi duniani kwa kushindwa kuvuna na kutumia rasilimali zao wenyewe.
 
Nigeria ni ipo top five ya mataifa yanayozalisha mafuta. Ongezea Angola.

Congo inalisha aslimia 60 ya cobalt yote Dunia, bila kusahau kwa sehemu kubwa inachimbwa kienyeji.
Kuna rasilimali nyingi sana hazianza kuchimbwa na nyingine tafiti zinaendelea.
 
Sijui source ya taarifa yako ni ipi ila definitely sio kweli...
Madini Gani mkuu. Mimi nimekupa mfano wa hayo madini kama mafuta, gas, chuma, DHAHABU, rare earth, nk. Mbona liko wazi wenzetu wanayo mengi. Sisi Yako wapi
 
Nigeria ni ipo top five ya mataifa yanayozalisha mafuta. Ongezea Angola. Congo inalisha aslimia 60 ya cobalt yote Dunia, bila kusahau kwa sehemu kubwa inachimbwa kienyeji. Kuna rasilimali nyingi sana hazianza kuchimbwa na nyingine tafiti zinaendelea.
Hata top 10 Kwenye mafuta Nigeria hayupo. Ebu angalia vizuri
 
Asilimia 95 ya madini yaliyopo Africa yanapatikana kwenye mabara mengine duniani kwa wingi, pia madini machache kama Tanzanite yanayopatikana Tanzania peke yake hayana matumizi na umuhimu mkubwa kama "rare earths" ambazo hazipo Africa.
Madini Gani mkuu. Mimi nimekupa mfano wa hayo madini kama mafuta, gas, chuma, DHAHABU, rare earth, nk. Mbona liko wazi wenzetu wanayo mengi. Sisi Yako wapi
 
Back
Top Bottom