Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,843
- 31,057
Tunapoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020, tunasikia tambo tupu toka kwa viongozi wakuu wa CCM kuwa uchaguzi wa mwaka huu ndiyo "kiama" cha Upinzani na hatutausikia tena Upinzani ndani ya nchi hii baada ya uchaguzi huo utakaofanyika mwezi wa Oktoba mwaka huu!
Swali ninalojiuliza: Hivi ni kweli kuwa upinzani upo mahututi kiasi hicho na kwenye uchaguzi wa mwaka huu tutauzika rasmi?
Hata hivyo ninavyoamini Mimi ni kuwa upinzani ndani ya nchi hii upo imara kuliko kipindi chochote, tokea tuanze mfumo huu wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992, isipokuwa uwanja wa kufanyia siasa nchini ndiyo hauko sawa ndiyo sababu inayowafanya viongozi wakuu wa CCM wajiaminishe hivyo kwa kuwa wanajua kuwa vyombo vyote vya dola ambavyo vinatakiwa kwa mujibu wa sheria viwe "neutral" badala yake vipo upande wa chama tawala cha CCM kwa uwazi kabisa.
Hata hivyo mambo yanakuwa "vice versa" unapoingia kwenye mitandao ya kijamii, ikiwemo Jamii Forum, unaposoma maoni ya wananchi, unajionea wazi kuwa upinzani nchini upo imara zaidi ya tunavyoaminishwa na watawala wetu.
Sasa ni kitu gani kinachowapa kiburi kiasi hicho viongozi wakuu wa CCM hadi watambe kiasi hicho kuwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu watauzika rasmi upinzani wa nchi hii?
Jibu ninalopata hapa ni kuwa kiburi chote walichonacho viongozi wakuu wa CCM ni kutokana na Katiba ya nchi yetu namna ambavyo imempa madaraka makubwa mno Rais wa nchi, ambaye pia ndiyo Mwenyekiti wa CCM kitaifa na kumfanya mungu-mtu kwa kila alisemalo na kulifanya kuonekana kuwa kama ndiyo sheria na vyombo vyote vya dola kutekeleza kauli zake kwa vitendo bila kuangalia kuwa yupo sahihi au amepotoka.
Kwa mfano, Rais amepiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani, wakati huo huo akiruhusu mikutano ya chama chake cha CCM iweze kuendelea bila kubughuziwa na Jeshi la Polisi, na hilo linafanyika.
Tujiulize hivi: Rais anapata wapi madaraka ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani, ambavyo vipo kihalali kisheria?
Kama kweli CCM inajiamini kiasi hicho kuwa imewafanyia mambo mengi sana ya kimaendeleo wananchi na kuwa inakubalika sana na wananchi, basi ikubali kuundwa kwa Tume huru ya uchaguzi na hivi vyombo vya dola, kama Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa, vifanye majukumu yao kwa weledi na kwa mujibu wa katiba na visiegemee chama cha CCM na viwe "neutral" badala ya sasa hivi kuwa kama vitengo vya CCM.
Swali ninalojiuliza: Hivi ni kweli kuwa upinzani upo mahututi kiasi hicho na kwenye uchaguzi wa mwaka huu tutauzika rasmi?
Hata hivyo ninavyoamini Mimi ni kuwa upinzani ndani ya nchi hii upo imara kuliko kipindi chochote, tokea tuanze mfumo huu wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992, isipokuwa uwanja wa kufanyia siasa nchini ndiyo hauko sawa ndiyo sababu inayowafanya viongozi wakuu wa CCM wajiaminishe hivyo kwa kuwa wanajua kuwa vyombo vyote vya dola ambavyo vinatakiwa kwa mujibu wa sheria viwe "neutral" badala yake vipo upande wa chama tawala cha CCM kwa uwazi kabisa.
Hata hivyo mambo yanakuwa "vice versa" unapoingia kwenye mitandao ya kijamii, ikiwemo Jamii Forum, unaposoma maoni ya wananchi, unajionea wazi kuwa upinzani nchini upo imara zaidi ya tunavyoaminishwa na watawala wetu.
Sasa ni kitu gani kinachowapa kiburi kiasi hicho viongozi wakuu wa CCM hadi watambe kiasi hicho kuwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu watauzika rasmi upinzani wa nchi hii?
Jibu ninalopata hapa ni kuwa kiburi chote walichonacho viongozi wakuu wa CCM ni kutokana na Katiba ya nchi yetu namna ambavyo imempa madaraka makubwa mno Rais wa nchi, ambaye pia ndiyo Mwenyekiti wa CCM kitaifa na kumfanya mungu-mtu kwa kila alisemalo na kulifanya kuonekana kuwa kama ndiyo sheria na vyombo vyote vya dola kutekeleza kauli zake kwa vitendo bila kuangalia kuwa yupo sahihi au amepotoka.
Kwa mfano, Rais amepiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani, wakati huo huo akiruhusu mikutano ya chama chake cha CCM iweze kuendelea bila kubughuziwa na Jeshi la Polisi, na hilo linafanyika.
Tujiulize hivi: Rais anapata wapi madaraka ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa vya upinzani, ambavyo vipo kihalali kisheria?
Kama kweli CCM inajiamini kiasi hicho kuwa imewafanyia mambo mengi sana ya kimaendeleo wananchi na kuwa inakubalika sana na wananchi, basi ikubali kuundwa kwa Tume huru ya uchaguzi na hivi vyombo vya dola, kama Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa, vifanye majukumu yao kwa weledi na kwa mujibu wa katiba na visiegemee chama cha CCM na viwe "neutral" badala ya sasa hivi kuwa kama vitengo vya CCM.