Hivi ni kweli suala la Katiba Mpya ni suala la Rais kulikubali au kulikataa?

Hivi ni kweli suala la Katiba Mpya ni suala la Rais kulikubali au kulikataa?

Kwenye video hii, Tundu Lissu anazungumzia suala la katiba mpya na kudai kwamba Rais [kwa sasa ni Samia Suluhu Hassan] ndiye mwenye uwezo wa kuamua tupate katiba mpya au la!

Anzia dakika ya 6:00 - 6:16 hivi.



Hivi ni kweli kabisa Rais ndiye mwenye uwezo huo?

Tukiachana na mazoea ya kijinga, uoga, na upumbavu wetu kiujumla, uwezo huo Rais wetu anautoa wapi?

Rais wetu yupo juu ya kila kitu? Yupo juu ya katiba? Yupo juu ya wananchi?

Kwa nini yeye ndiye awe mwenye uwezo wa kuamua tupate katiba mpya au la and not we the people?

Hii nchi kila kitu mambo ni kinyumenyume tu!

Mkuu Nyani, hiyo ndiyo hali halisi ilivyo Tanzania whether ni katiba au mabavu.

Tumeona ni jinsi gani JPM alivyo ni jinsi gani alivyoitopisha katiba pale alipoingia madarakani na hakuna hata aliyetia neno. Maza kaingia kasema katiba baadaye ... kasema hivyo kwa sababu anayo hayo mamlaka ya kuaamua nini kifanyike na nini kisifanyike na kwa wakati gani.
 
Tangu lini changes zikaletwa na vyama vya siasa mkuu? Yaani mfano umwambie mtu kama Kibajaji katiba mpya inayotaka sifa ya mbunge iwe walau form six, muipitishe atakubali? Umwambie mbunge yeyote katiba mpya inayoweka ukomo wa kugombea ubunge au mbunge kufukuzwa na waliomchagua, waipitishe kweli?? Real changes lazima ziletwe na wananchi wenyewe mkuuu...
Mabadiliko, changes sijui sometimes Ni agenda za watu za kusukumia SIKU, ili madaraka na kulisha familia zao.

Hakuna siku yoyote itakuwa kutokea ukaambiwa haya mabadiliko yameshakushinda, Maisha Ni murua kama hao wanaodai mabadiliko hawajapata wanachokitaka.

Utaendelea kuishi kwa myth ya mabadiliko hivyo hivyo mpaka kiama.

Ona Wakenya ambao Wana Tume huru ya uchaguzi, mahakama huru mpaka inafuta uchaguzi na bunge huru.

Lakini masikini bado masikini tu.

Screenshot_2022-03-11-05-29-13-617_com.twitter.android.png
 
Ww Leo ukiitwa na rais hautokwenda?

Kwanza kabisa, hakuna popote nilipopinga mtu kukutana na rais. Tafadhali jifunze kusoma kwa ufahamu.

Pili, kuhusu swali lako.

Niliitwa kukutana na Kikwete nikakataa.

Nilikuwa na kazi zangu muhimu zaidi.
 
Hujasikia Mbowe amesema ni siri atakuwa anatoa kidogo kidogo, na amesema katiba mpya sio muhimu kwa sasa.

Nawaonea huruma wale vijana na tisheti zao #katibampya watavalia wapi tisheti zao.
Amesema wapi kwamba katiba mpya sio muhimu kwa sasa, acheni tabia ya kwamba lazima uvute kitu ndio uje kuandika humu.
 
Hujasikia Mbowe amesema ni siri atakuwa anatoa kidogo kidogo, na amesema katiba mpya sio muhimu kwa sasa.

Nawaonea huruma wale vijana na tisheti zao #katibampya watavalia wapi tisheti zao.

Mimi si CCM wala CHADEMA. In fact, kiushabiki, nipo zaidi kuwaunga mkono CHADEMA kudai katiba mpya.

Lakini, hiyo habari ya kusema siri Mbowe alichemka.

Kwanza kabisa, wananchi wana haki ya kikatiba ya kujua mambo muhimu yanayoendesha nchi yao. Hili jambo lipo katika katiba. Katiba ya sasa, si dai la katiba mpya.

Kwa hiyo, Mbowe anadai katiba mpya wakati hata ya sasa haitekelezi.

Kiongozi wa upinzani anatakiwa kusimamia uwazi, si usiri. Siri ipigwe vita, inatuletea rushwa na habari nyingi mbaya.

Lakini, hata kama kuna haja ya kuwa na usiri katika mazungumzo fulani, ukifanya mazungumzo ya siri hutangazi kwamba umefanya mazungumzo ya siri, kwa sababu kutangaza hivyo tu kutakuwa kushaanza kufunua ile siri, watu wataanza kuhoji siri hiyo siri gani, wengine wataweka assumptions zao mbaya kuliko ukweli.

Ndiyo maana watu wameanza minong'ono Mbowe kanunuliwa na CCM.

Utawalaumu vipi wakisema hivyo wakati Mbowe mwenyewe hataki uwazi juu ya mazungumzo yale?

That was a mistake on principle and tactically.

Tanzania hata viongozi wa upinzani wanaotakiwa waje na mawazo mbadala, bado wana mawazo ya kizamani ya kuthamini usiriusiri.

Sasa mtu kama Mbowe ambaye ana endekeza usiri anaweza kuongoza kampeni ya kuondoa usiri kwenye mikataba ya umma?

Hawezi. Akianza tu watu watamwambia mbona na wewe ulisema umefanya mkutano na rais mkaongea mambo ya siri?

Hana uwazi katika enzi inayohitaji uongozi wa uwazi.
 
Mimi si CCM wala CHADEMA. In fact, kiushabiki, nipo zaidi kuwaunga mkono CHADEMA kudai katiba mpya.

Lakini, hiyo habari ya kusema siri Mbowe alichemka.

Kwanza kabisa, wananchi wana haki ya kikatiba ya kujua mambo muhimu yanayoendesha nchi yao. Hili jambo lipo katika katiba. Katiba ya sasa, si dai la katiba mpya.

Kwa hiyo, Mbowe anadai katiba mpya wakati hata ya sasa haitekelezi.

Kiongozi wa upinzani anatakiwa kusimamia uwazi, si usiri. Siri ipigwe vita, inatuletea rushwa na habari nyingi mbaya.

Lakini, hata kama kuna haja ya kuwa na usiri katika mazungumzo fulani, ukifanya mazungumzo ya siri hutangazi kwamba umefanya mazungumzo ya siri, kwa sababu kutangaza hivyo tu kutakuwa kushaanza kufunua ile siri, watu wataanza kuhoji siri hiyo siri gani, wengine wataweka assumptions zao mbaya kuliko ukweli.

Ndiyo maana watu wameanza minong'ono Mbowe kanunuliwa na CCM.

Utawalaumu vipi wakisema hivyo wakati Mbowe mwenyewe hataki uwazi juu ya mazungumzo yale?

That was a mistake on principle and tactically.

Tanzania hata viongozi wa upinzani wanaotakiwa waje na mawazo mbadala, bado wana mawazo ya kizamani ya kuthamini usiriusiri.

Sasa mtu kama Mbowe ambaye ana endekeza usiri anaweza kuongoza kampeni ya kuondoa usiri kwenye mikataba ya umma?

Hawezi. Akianza tu watu watamwambia mbona na wewe ulisema umefanya mkutano na rais mkaongea mambo ya siri?

Hana uwazi katika enzi inayohitaji uongozi wa uwazi.

The truth of the matter is, politicians wote (wawe ndani ya CCM au ndani ya vyama vya upinzani) wanasukumwa na maslahi yao binafsi katika kuendesha harakati zao za kisiasa; hawasukumwi na maslahi ya mwananchi wa kawaida kama ambavyo wao huwa wanajaribu kutuaminisha. Ndiyo maana huwa hawachelewi kufika bei.

Kule Zanzibar, kwa mfano, mivutano kati ya CCM na CUF ilikuwa na kawaida ya kuwa mikubwa sana, lakini iliyeyuka kirahisi sana kila wakati Maalim Seif (RIP) alipopewa madaraka. Hakuna maslahi ya mwananchi wa kawaida yaliyokuwa yakizingatiwa ili kumaliza hiyo tension. Maslahi ya Maalim Seif na washirika wake fulani tu yalitosha kumaliza mvutano wa CCM na CUF.

Hata Mbowe na politicians wenzake, ambao leo wanaendesha harakati za kudai katiba mpya, wanafanya hivyo kwa matumaini kwamba mabadiliko hayo yanaweza kuwaweka mahali pazuri zaidi katika kupigania maslahi yao. Kama ikitokea kwamba Mbowe na wenzake somehow wamefanikiwa kukamata dola bila ya mabadiliko hayo ya katiba wanayodai, hakuna sababu yoyote ya kuamini kwamba Mbowe na washirika wake wataongoza mchakato wa mabadiliko ya katiba. Trust me, they won’t lead that effort! Hiyo itaachwa kuwa kazi ya wale walio nje ya utawala.

Politicians ni magwiji wa kutumia nguvu ya umma katika kufikia malengo yao binafsi ya kisiasa. That’s it!
 
The truth of the matter is, politicians wote (wawe ndani ya CCM au ndani ya vyama vya upinzani) wanasukumwa na maslahi yao binafsi katika kuendesha harakati zao za kisiasa; hawasukumwi na maslahi ya mwananchi wa kawaida kama ambavyo wao huwa wanajaribu kutuaminisha. Ndiyo maana huwa hawachelewi kufika bei.

Kule Zanzibar, kwa mfano, mivutano kati ya CCM na CUF ilikuwa na kawaida ya kuwa mikubwa sana, lakini iliyeyuka kirahisi sana kila wakati Maalim Seif (RIP) alipopewa madaraka. Hakuna maslahi ya mwananchi wa kawaida yaliyokuwa yakizingatiwa ili kumaliza hiyo tension. Maslahi ya Maalim Seif pekee yalitosha kumaliza mvutano wa CCM na CUF.

Hata Mbowe na politicians wenzake, ambao leo wanaendesha harakati za kudai katiba mpya, wanafanya hivyo kwa matumaini kwamba mabadiliko hayo yanaweza kuwaweka mahali pazuri zaidi katika kupigania maslahi yao. Kama ikitokea kwamba Mbowe na wenzake somehow wamefanikiwa kukamata dola bila ya mabadiliko hayo ya katiba wanayodai, hakuna sababu yoyote ya kuamini kwamba Mbowe na washirika wake wataongoza mchakato wa mabadiliko ya katiba. Trust me, they won’t lead that effort! Hiyo itaachwa kuwa kazi ya wale walio nje ya utawala.

Politicians ni magwiji wa kutumia nguvu ya umma katika kufikia malengo yao binafsi ya kisiasa. That’s it!
Ulichoandika kimenikumbusha jinsi Julius Nyerere alivyoendesha kampeni ya kudai uhuru kutoka kwa wakoloni, na kuzisema sheria zao dhalimu, mpaka kukawa na kesi kubwa sana Nyerere akashitakiwa na serikali ya ukoloni.

Baadaye, Nyerere akapewa nchi kuongoza.

Badala ya kuondoa sheria za kidhalimu za kikoloni kama za indefinite detention, Nyerere mwenyewe akawa anazitumia kudhoofisha wapinzani wake kina Chistopher Kassanga Tumbo na Joseph Kassela Bantu. Akapiga marufuku hata demokrasia ya vyama vingi.

Hizi sheria mpaka Justice Francis Nyalali aliziandika katika sheria 40 kandamizi, na zingine mpaka leo zipo.

Ndiyo hayo hayo uliyoyaandika hapo juu.
 
Acha kuniletea tafsiri ya kingereza kwenye kiswaili.Lakini pia wewe ni nani hadi utake kuambiwa kila kitu.Muhusika kasema mazingumzo mengine ni siri sasa wewe kinachokusumbua hapo ni nini?.
1.Kanuni za utawala bora zinaondoka kwenye usiri na kwenda kwenye uwazi.

2. Katiba ya Tanzania inasema Wananchi wana haki ya kujua taarifa za mambo muhimu yanayoendesha nchi yao.

3.Usiri ni chanzo cha mianya ya rushwa na hadaa.

4.Mbowe anadai katiba mpya wakati hata katiba ya sasa inayotaka uwazi hawezi kuitekeleza. Hapo anatupa maswali sana kama anataka katiba mpya kweli au ana ajenda zake kama alivyotuambia Pulchra Animo hapo juu?

5.Habari za usiri hazimsaidii hata Mbowe mwenyewe. Zinajenga sintofahamu miomgoni mwa jamii.

6. Katika "Information Theory", wasomi wa habari wanasema, usipoweka wazi habari zako, watu wengine watakuwekea habari zao wanazozisema kuwa ni zako. Maana yake, Mbowe akiendekeza usiri na kutoweka habari za mkutano wazi, akasema kuna maneno ya siri wameongea na rais, hapo ndipo watu wengine wanapoweza kupata nafasi ya kufanya the worst possible assumption na kusambaza.Hapo ndipo watu wataanza kusema Mbowe kapozwa, kanunuliwa etc. Hata kama hayo si kweli, ukweli kwamba Mbowe kuna kitu kaficha unawapa nguvu watu hawa kueneza maneno yao hata kama si kweli. Mbowe kufanya maneno kuwa siri, hajajitendea haki hata yeye mwenyewe, kajiweka kuwa suspect sana.

7. Mambo ya usiri ni mambo ya kizamani, sasa hivi wananchi tunataka uongozi trasparent, mikataba iwe wazi, chaguzi ziwe wazi etc. Sasa Mbowe anataka kuwa kiongozi mbadala anayetushawishi atakuwa tofauti na CCM kwa kufuata uongozi wa siri kama CCM? Hapo kuna tofauti gani sasa?

8. Siri ni dharau kwa Watanzania, kwamba wanaendeshwa kama watoto wadogo wanapimiwa cha kuambiwa vingine wanaambiwa vya wakubwa tu.

9.Mbowe anajiwekea precedent mbaya. CHADEMA hawajachukua urais washaanza kuendekeza usiri. Wakipata kuchukua nchi si watafungia magazeti kabisa kwa usiri?

10. Kama anaendekeza usiri basi anakosa moral authority ya kupinga mamuzi ya kisiasa yanayotolewa kwa usiri na minajili ya mambo kufanyika kwa "Usalama wa Taifa" bila maelezo ya kina. Hata yeye akubali kufungwa kwa "Usalama wa Taifa", bila maelezo zaidi.
 
Kwenye video hii, Tundu Lissu anazungumzia suala la katiba mpya na kudai kwamba Rais [kwa sasa ni Samia Suluhu Hassan] ndiye mwenye uwezo wa kuamua tupate katiba mpya au la!

Anzia dakika ya 6:00 - 6:16 hivi.



Hivi ni kweli kabisa Rais ndiye mwenye uwezo huo?

Tukiachana na mazoea ya kijinga, uoga, na upumbavu wetu kiujumla, uwezo huo Rais wetu anautoa wapi?

Rais wetu yupo juu ya kila kitu? Yupo juu ya katiba? Yupo juu ya wananchi?

Kwa nini yeye ndiye awe mwenye uwezo wa kuamua tupate katiba mpya au la and not we the people?

Hii nchi kila kitu mambo ni kinyumenyume tu!

1647435266280.png
 
Back
Top Bottom