Hivi ni lazima kila raia wa Tanzania awe na kovu la ile sindano ya ndui begani?

Hivi ni lazima kila raia wa Tanzania awe na kovu la ile sindano ya ndui begani?

Mnamo mwanzoni mwa miaka ya 1700, mji wa Boston, Massachusetts kama ilivyokuwa kwa dunia nzima kipindi hiko, ulikumbwa na ugonjwa mbaya wa Ndui uliosababisha vifo vya watu wengi. Inakadiliwa watu zaidi ya milioni 300 walifariki kwa ugonjwa wa Ndui duniani kote.

Ugonjwa wa Ndui kipindi hiko ulikuwa kama hukumu ya kifo kwa waliougua na hata wagonjwa wachache waliopona waliachwa na makovu na vilema kwenye miili yao.

Lakini mnamo mwaka 1716, mtumwa wa kiafrika aitwaye Onesimus alimwambia mmiliki wake, bwana Cotton Mather, kuwa anafahamu siri ya ugonjwa wa Ndui. Onesimus alieleza kuwa alipokuwa Afrika alifanyiwa upasuaji mdogo na kupewa sehemu ya ugonjwa kwenye mwili wake na hivyo kumsababishia kinga dhidi ya kuugua tena ugonjwa huo.

onesimus 1.jpg


Upasuaji huo mdogo ulijumisha kusuguliwa juu ya ngozi kwa maji maji kutoka kwenye vidonda vya mgonjwa wa Ndui na hivyo kumfanya kuwa na kinga ya ugonjwa huo.

Mather, alishangazwa na simulizi hiyo ambapo ilimbidi kufanya uchunguzi kwa watumwa wengine wa kiafrika ambao pia walimthibitishia juu ya ukweli wa tiba hiyo. Simulizi ya tiba hii kutoka kwa mtumwa wa kiafrika haikupata ushawishi mkubwa kwenye jamii ya watu weupe ila Mather aliendelea kuhubiri juu ya teknolojia hii.

Mnamo mwaka 1721, Mather pamoja na daktari mzungu Boylston Zabdiel walifanikiwa kujaribu teknolojia hiyo kwa mara ya kwanza ambapo walianza na mtoto wa Mather na baadhi ya wakazi wa Boston. Tiba hiyo ilionyesha mafanikio makubwa sana kwani kati ya watu 242 waliopata tiba hiyo ya chanjo ni watu 6 tu waliofariki kwa ugonjwa wa Ndui ikilinganisha na uwiano wa vifo 7 kwa kila wagonjwa 40 bila ya chanjo.

Mwaka 1796. Edward Jenner alifanikiwa kutengeneza chanjo ya kwanza rasmi kutokana na kirusi cha Ndui wa ng’ombe na hatimaye chanjo ya Ndui ikawa ni ya lazima kwa wakazi wote wa Boston, Massachussets.

Kutokana na mafanikio hayo na maboresho mbalimbali, mwaka 1980, shirika la afya duniani WHO walitangaza kuwa ugonjwa wa Ndui umetokomezwa rasmi katika uso wa Dunia.

Mwaka 2016, Onesimus alipewa heshima ya mtu bora wa wakati wote kwenye mji wa Boston. Mengi hayasemwi juu ya kifo cha Onesimus ila alifanikiwa kununua uhuru wake mwenyewe kwa kumlipa mmiliki wake kiasi sawa cha kuweza kununua mtumwa mwingine.

Leo hii, zaidi ya miaka 300 baadae, tiba na teknolojia ya chanjo imepiga hatua kubwa ambapo magonjwa kama Surua na Polio ni magonjwa yanayokaribia kutokomezwa kabisa katika uso wa dunia.

Chanjo ni dawa ya kibaologia ambapo kipande cha ugonjwa au ugonjwa uliofubazwa uingizwa kwenye mwili wa binadamu kama namna ya kujenga kumbukumbu kwenye kinga ya mwili dhidi ya ugonjwa fulani.
Asante sana kiongozi.
 
Shida yangu NI kwanini waliamua kuchanja wtz wote sehemu moja, mbona mataifa mengine hawana hii alama?

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
Nadhani Ni mpangilio tu wa kutambulisha watu wa nchi fulani kupitia alama chanjo.


Ukitaka kujua huyu Ni mtanzania utaangalia begani, Wakenya wao wanachanjwa katikati ya mkono wa kulia kinabaki kialama, Hawa wakitaka kuthibitisha umezaliwa Kenya kienyeji utaona wanakwambia nyoosha mkono.

Waethiopia wanachanjwa begani Kama sisi.
Kuna siku rafiki yangu muethiopia aliona alama yangu begani alikuwa surprised akasema nyie mnachanjwa begani Kama sisi.
 
Nadhani Ni mpangilio tu wa kutambulisha watu wa nchi fulani kupitia alama chanjo.


Ukitaka kujua huyu Ni mtanzania utaangalia begani, Wakenya wao wanachanjwa katikati ya mkono wa kulia kinabaki kialama, Hawa wakitaka kuthibitisha umezaliwa Kenya kienyeji utaona wanakwambia nyoosha mkono.

Waethiopia wanachanjwa begani Kama sisi.
Kuna siku rafiki yangu muethiopia aliona alama yangu begani alikuwa surprised akasema nyie mnachanjwa begani Kama sisi.
Kama ugonjwa ulitokomezwa kwanini mpaka sasa watu wanachanjwa?
 
Kwa maelezo ya wadau...hii alama si ya mtanzania pekee
Nchi zote barani Afrika, wanachanja chanjo ya ndui. Isipokuwa raia wao wanachanja mapajani au mkononi chini kidogo ya mabegani. Raia wa DRC wamechanjwa chini ya bega. Raia wa Burundi wamechanjwa mapajani. Ndui likuwa ugonjwa hatari sana, ambao kwasasa umeweza kuthibitiwa.
 
Kama ugonjwa ulitokomezwa kwanini mpaka sasa watu wanachanjwa?
Kwa uelewa wangu chanjo ndio inatokomeza ugonjwa. Mtu akichanjwa gonjwa likija halitamuathiri, usipochanja watu watakuwa hawana Kinga ya kupambana na ugonjwa so gonjwa likija litafagia tu. That's why chanjo zinakuwaga Ni za muendelezo, Mtoto akizaliwa lazima apewe ili imlinde.
 
Nadhani Ni mpangilio tu wa kutambulisha watu wa nchi fulani kupitia alama chanjo.


Ukitaka kujua huyu Ni mtanzania utaangalia begani, Wakenya wao wanachanjwa katikati ya mkono wa kulia kinabaki kialama, Hawa wakitaka kuthibitisha umezaliwa Kenya kienyeji utaona wanakwambia nyoosha mkono.

Waethiopia wanachanjwa begani Kama sisi.
Kuna siku rafiki yangu muethiopia aliona alama yangu begani alikuwa surprised akasema nyie mnachanjwa begani Kama sisi.
Mimi nimezaliwa Msoga Chalinze na wala sina hiyo alama yenu ya kitaifa.
 
Kwa uelewa wangu chanjo ndio inatokomeza ugonjwa. Mtu akichanjwa gonjwa likija halitamuathiri, usipochanja watu watakuwa hawana Kinga ya kupambana na ugonjwa so gonjwa likija litafagia tu. That's why chanjo zinakuwaga Ni za muendelezo, Mtoto akizaliwa lazima apewe ili imlinde.
Huko nchi za wenzetu watoto wanadungwa? Au ni ka program ka muda mrefu kakuhafifisha kizazi.. Cha jamii fulani.

Twende tu hapo kwa wadzabe wawe kama mfano wetu.
 
Ndui ni smallpox, chanjo yake huwa ukichomwa panavimba na kutengeneza lengelenge (blister) ambalo likikauka huacha kovu. Ndio hiyo alama ya ndui.

Yes ni lazima kuchoma, kuna magonjwa ambayo yalisumbua miaka ya nyuma na kuua watu wengi sana duniani lakini baada ya kupatiwa chanjo ni lazima kila kichanga achomwe. Mfano hiyo smallpox, chickenpox, polio n.k

Ukiona wamama wanapeleka vichanga vyao clinic moja ya sababu ni kuenda kuchomwa hizo chanjo.

Mzee umechemka sio smallpox bro ni BCG
 
Chanjo(vaccine) dhid ya ugonjwa wa kifua kikuu kawaida unaweza kuwekewa wadudu walio dhohofika ila wapo hai, live attusinate ama walio kufa, ama genes za wadudu sasa kwenye ndui unawekewa wadudu wa walio hai wa TB ila wamedhohofishwa ili kinga ya mwili iwatambue kwa ajili ya kutengeneza kinga dhidi yake
Sasa mara zote huchomwa chini ya ngozi epedermis na hutengeneza kovu kma ndui na tz walichagua bega la kushoto.
Pia katika madhara ya hii chanjo muda wowote immute yako ikishuka wale jamaa wanaamka na kukuletea tb inaweza ikwa ya mapafu(pulmonary tb) ama extrapulmonary tb kifupi ndo hivyo mkuu
 
Chanjo(vaccine) dhid ya ugonjwa wa kifua kikuu kawaida unaweza kuwekewa wadudu walio dhohofika ila wapo hai, live attusinate ama walio kufa, ama genes za wadudu sasa kwenye ndui unawekewa wadudu wa walio hai wa TB ila wamedhohofishwa ili kinga ya mwili iwatambue kwa ajili ya kutengeneza kinga dhidi yake
Sasa mara zote huchomwa chini ya ngozi epedermis na hutengeneza kovu kma ndui na tz walichagua bega la kushoto.
Pia katika madhara ya hii chanjo muda wowote immute yako ikishuka wale jamaa wanaamka na kukuletea tb inaweza ikwa ya mapafu(pulmonary tb) ama extrapulmonary tb kifupi ndo hivyo mkuu

Bacillus Calmette–Guérin inaitwa BCG Kwa kifupi na anachoma mtoto baada ya kuzaliwa on same day
 
Hii kitu Asilimia kubwa sana watanzania walichomwa, wengi hata bila kujijua tunaiona ukubwani.

Naomba kujua:

Je, inamaanisha au inakinga nini?
Je, bado ipo mpaka leo?
Je, ni kila nchi ipo au ni Tz pekee?
Je, ilikua ni lazima kuchoma?
Je, ni official kiafya?
Je, ambao hawakuchomwa inaweza waletea shida yeyote?

Kwa nini inakua na nadharia tofauti tofauti kwa jamii.
"Mkononi sina tattoo bali na alama ya ndui,mtanzania namba moja majungu hayasumbui" - Prof Jay.
 
Back
Top Bottom