Piga vyungu kiongozi, sasa dawa ni ipi kukaa ndani? Ila hajakatazwa mtu kukaa ndani ni maamuzi tu.Kwa hiyo dawa ya hofu nayo ni kujifukiza?
Kwa hiyo tumsifu na kumpongeza Raisi Magufuli kwa juhudi zake za kuutokomeza ugonjwa wa hofu?Piga vyungu kiongozi, sasa dawa ni ipi kukaa ndani? Ila hajakatazwa mtu kukaa ndani ni maamuzi tu.
Hapo ni sawa kabisa na serikali kukabiliana na corona? Kwahiyo hapo wewe unajiskia huru kweli kweli 🤦🏾♂️. Kumbe ni uhuru wa either kutafuta kifo au kuugua na kusambaza virusi.
Uhuru wa kukosoa wenyewe hamna, lakini uhuru wa kupata corona mnao. Ama kweli kuishi kwingi ni kuona mengi!
Nguruvi3
Na wewe tumia akili ya kawaida tu, hapa kwetu shughuli zinaendea lakini ni kwa tahadhari.
Anga limefunguliwa lakini masharti ya afya yamepewa msisitizo.
Ni akili za kitumwa kujaribu kufanya kila kitu anachokifanya mzungu pasipo wewe mwenyewe kujiongeza.
Naona kumekuwepo na hali ya upotoshaji nchini kuwa hatua za lockdown hazina manufaa! Hili naona kama ni upotoshaji ambao unasababishwa na ukweli kwamba viongozi wengi wameingiza siasa kwenye vita dhidi ya corona na matokeo yake ndo haya ya upotoshaji pamoja na mambo mengine.
Mifano iko mingi, lakini kuna mfano nilioamuwa kuutumia kujenga hoja yangu. Mfano huu ni wa gavana wa Ohio kule marekani, anayeitwa Mike Dewine! Huyu alichukuwa hatua zote kabla ya Trump! Pamoja na kwamba Trump anaogopeka na viongozi wengi ndani ya chama chake cha republican, mfano maseneta na magavana, huwa wana wasiwasi wa kupingana naye kwasababu ya umaarufu alio nao ndani ya chama cha Tembo ama Republicans!
Sasa huyu alichukuwa hatua za lockdown toka mwanzo kabisa wakati Trump akiwa analeta utani na gonjwa hilo! Matokeo yake, jimbo lake linafanya vizuri sana na yeye amekuwa maarufu siyo tu kule Ohio, bali marekani nzima! Alikuwa na guts za kufanya maamuzi sahihi ya kulinda raia wake kuliko rais wa nchi! Na wananchi wanasema hatua hizo alitakiwa azichukuwe Trump mwenyewe, na pengine mikusanyiko iliyokuwa ikiendelea kwenye majimbo mengine mfano New York, New Orleans na kwingineko ambako michezo iliendelea kama kawaida na mikusanyiko mingine kama makanisani nk, ambapo matokeo yake ndo haya tunayoyaona wanakufa kwa kasi na maambukizi ambayo yalikuwa tayari yametapakaa.
Jimbo lake lina maambukizi machache na vifo vichache sana, na wameshaanza kufungua taratibu taratibu. Pia jimboni kwake alifanya mkakati siyo wa total lockdown, hiyo ni baadhi tu ya sehemu. Wale wanaojitetea kuwa lockdown ni mbaya, wanawaongopea wananchi kwa manufaa yao binafsi, most likely uchaguzi. Ni bora waseme lockdown siyo njia muafaka kwasababu ya mfumo wetu wa uchumi ulivyo na maisha ya wananchi wake, au pia kwamba wamechelewa kwasababu tuliendelea kupokea wageni wote hata kutoka China! Lakini haina maana kuwa partial lockdowns hazifai na wala hazikufaa! Na lockdowns kwenye maeneo korofi ni za muhimu!
Lakini pia tulipuuza tokea mwanzo na kuanza kusema wapinzani wanataka wananchi wafe na njaa! Hii ni propaganda ambayo matokeo yake si mazuri kwenye jamii inayokabiliana na janga hatari linalochukuwa maisha ya watu kila siku na pengine kila saa duniani.
Bila kupoteza muda, naweka hiki kipande hapo chini chenye kusapoti ninachokisema, pia link kama ukitaka kusoma habari yote na kujiridhisha wewe mwenyewe kuwa niyasemayo ni kweli.
Mike Dewine gavana wa Ohio, alipata umaarufu hata kumzidi Trump ambaye naye akaanzisha utaratibu wa kuongea na waandishi wa habari kila siku. Jambo ambalo Dewine alikuwa akilifanya jimboni kwake kila siku saa nane mchana, na wakati huo wana Ohio wanakuwa kwenye luninga zao wakimsikiliza. Ndiyo wakaanzisha usemi wa “it’s 2’oclock somewhere...wine with mr Dewine”, ambapo wakati wa lunch wanapata wine wakimsikiliza Dewine. Wala hawa kuwa na habari na Trump!
A Republican, he took early and bold actions to lock down his state, even as the head of his party, President Trump, dismissed the threat of the pandemic.
Ohio’s G.O.P. Governor Splits From Trump, and Rises in Popularity
Kwahiyo ndugu watanzania wenzangu, kabla ya kufanya upotoshaji, jiridhishe kwa kautafiti kadogo tu ili uweze kuwa huru kifikra! kama ikifikia mahali unamkabidhi mtu mwingine jukumu la kufikiria kwa niaba yako, ujuwe kuna shida kubwa sana kwa upande wako! Kusema lockdown haisaidii, ni sawa pia na kusema “to hell with social distancing”. Kwasababu huwezi kuwaambia watu wafuate masharti kwa ugonjwa ambao siyo hatari kabisa kwa jinsi unavyochukuliwa, kutokana na hatua za viongozi wetu, pamoja na matam
Siyo sahihi kusema lockdown haisaidii kwasababu zenu za kisiasa! Kwanza ingekuwa ni kwetu, huyo Dewine angekiona cha mtemakuni!
Lakini kwasababu ya kiasi cha demokrasia na mfumo wao wa uongozi, Dewine aliweza kuchukuwa maamuzi muhimu kwenye jimbo lake kinyume na rais wa nchi! Na ameonekana kwamba alikuwa sahihi na kiongozi shupavu!
Nyota yake inang’ara! Trump hawezi tena kusema kuwa lockdown haisaidii! Na kwetu Tanzania siyo sahihi kusema hivyo, semeni tu hamkuchagua lockdowns kwasababu mtakufa njaa, ama pia mlichelewa kuchukuwa hatua za kufunga mipaka!
Mag3 Nguruvi3 JokaKuu Kalamu1 imhotep Detective J
Samahani mkuu, kabla sijakujibu, naomba nikuulize kama umepitia michango ya nyuma tokea bandiko la kwanza.Umeandika saaana kuwakariri US ambako wana uchumi stable tofauti na afrika.
Jibu ni kwamba tumechukua right track kwa sababu madhara ya lockdown ni makubwa kuliko unavyowaza wewe na wenzio wenye kipato kizuri na mnachokiogopa ni kifo tu.
Lakini mnasahau nchi yetu wanaokimbiza kipati yaani hand to mouth ndio wengi kuliko wale mnaotembea na viyoyozi afrika.
Mind you hata huko US tayari hawataki lockdown.
Sent using Jamii Forums mobile app
Yeye wewe unajikinga na hii pandemic kwasababu mzungu amesema? Unajitibu kwasababu umeambiwa na mzungu?Ulaya na Marekani wamefungia mipaka na shughuli zingine, ni muda tu nyie na Kenya mtabadilisha gia angani sababu mizungu imesema.
Mbona Trump ni mweupe?Critics zitatoka nyingi lakini Kwa hili Raisi JPM ni mfano wa dunia, shida tu ni Raisi toka Africa tena Tanzania. Ingekua ni mweupe basi angekua kwenye headlines na promo kibao.
Karata alizo changa Raisi wetu kuchangua clinical approach badala ya epidemiological approach ndo tofauti kuu.
After all Raisi wetu ni mwanasayansi, jiulize ni Maraisi wangapi duniani ni wanasayansi na wanaelimu ya maabara.
JPM is the right president for our nation
especially at this era. Period. Kila Jambo na nyakati zake.
Usisahau kua ndo Raisi wa dunia Kwa sasa.Mbona Trump ni mweupe?
Sweden wasio na lockdown wana common sense nyingi kuliko mimi na wewe.Hata kama wanafungua huku kuna vifo vingi, haina maana kwamba kufunga hakujawasaidia kuokoa maisha ya wananchi.
Hao wa marekani wanaotaka kutoka nje ni wachache sana!group dogo sana la mashabiki wa Trump.
Wenzenu wakifungua hata kama vifo vingi, ni kwasababu ya kosa la kuchelewa kufunga, lakini siyo kwasababu ya kufunga. Common sense yenyewe ingetosha.
Rwanda ukubwa wake ni sawa na mkoa mmoja tu wa Tanzania Bara. Lockdown ni ngumu sana kuna matatizo mengine ya kiafya kama TB na HIV unapoweka lockdown unaongeza vifo vya hayo magonjwa.Fujo za watu wa Kenya kule East leagh? Wanakoishi wasomali?Uganda na Rwanda umezisahau. Kama Rwanda wamelisha nchi sisi tumeshindwa vipi kuilisha Dar? Tena siyo wote Dar ambao wangehitaji msaada.
Usijiweke group moja na mimi hapo unapojitolea mfano na wa Swedish. GTO with you little self esteem bra.Sweden wasio na lockdown wana common sense nyingi kuliko mimi na wewe.
Ni akili za vumbi kuwa na lockdown wakati familia moja ina watu nane wenye kuishi nyumba moja na kutumia mpaka sahani zile zile kila siku.
Wapi nimesema lockdown ya Tanzania nzima?Rwanda ukubwa wake ni sawa na mkoa mmoja tu wa Tanzania Bara. Lockdown ni ngumu sana kuna matatizo mengine ya kiafya kama TB na HIV unapoweka lockdown unaongeza vifo vya hayo magonjwa.
Sio kila lenye kuwezekana nch fulani basi na nyingine inaweza kulifanya.
Lockdown kwa bongo sahau mkuu.Usijiweke group moja na mimi hapo unapojitolea mfano na wa Swedish. GTO with you little self esteem bra.
Yeye wewe unajikinga na hii pandemic kwasababu mzungu amesema? Unajitibu kwasababu umeambiwa na mzungu?
Effect za lockdown Ohio zinaweza lingana na effect zake na inchi kama zetu za third world?,acha kupotosha watu,huko wanaweza kununua mahitaji yao ya mwezi mzima mtu anakaa ndani anajitafunia,ukimfungia wa buguruni utampesa tu,maana kula yake lazima atoke akapige kibarua na hela atayopata siku hiyo ni ya kumtosha siku mbili tu,unataka yatokee watu wajae barabarani kudai vyakula ili inchi iwe katika utulivu ziro ndio ufurahi?Naona kumekuwepo na hali ya upotoshaji nchini kuwa hatua za lockdown hazina manufaa! Hili naona kama ni upotoshaji ambao unasababishwa na ukweli kwamba viongozi wengi wameingiza siasa kwenye vita dhidi ya corona na matokeo yake ndo haya ya upotoshaji pamoja na mambo mengine.
Mifano iko mingi, lakini kuna mfano nilioamuwa kuutumia kujenga hoja yangu. Mfano huu ni wa gavana wa Ohio kule marekani, anayeitwa Mike Dewine! Huyu alichukuwa hatua zote kabla ya Trump! Pamoja na kwamba Trump anaogopeka na viongozi wengi ndani ya chama chake cha republican, mfano maseneta na magavana, huwa wana wasiwasi wa kupingana naye kwasababu ya umaarufu alio nao ndani ya chama cha Tembo ama Republicans!
Sasa huyu alichukuwa hatua za lockdown toka mwanzo kabisa wakati Trump akiwa analeta utani na gonjwa hilo! Matokeo yake, jimbo lake linafanya vizuri sana na yeye amekuwa maarufu siyo tu kule Ohio, bali marekani nzima! Alikuwa na guts za kufanya maamuzi sahihi ya kulinda raia wake kuliko rais wa nchi! Na wananchi wanasema hatua hizo alitakiwa azichukuwe Trump mwenyewe, na pengine mikusanyiko iliyokuwa ikiendelea kwenye majimbo mengine mfano New York, New Orleans na kwingineko ambako michezo iliendelea kama kawaida na mikusanyiko mingine kama makanisani nk, ambapo matokeo yake ndo haya tunayoyaona wanakufa kwa kasi na maambukizi ambayo yalikuwa tayari yametapakaa.
Jimbo lake lina maambukizi machache na vifo vichache sana, na wameshaanza kufungua taratibu taratibu. Pia jimboni kwake alifanya mkakati siyo wa total lockdown, hiyo ni baadhi tu ya sehemu. Wale wanaojitetea kuwa lockdown ni mbaya, wanawaongopea wananchi kwa manufaa yao binafsi, most likely uchaguzi. Ni bora waseme lockdown siyo njia muafaka kwasababu ya mfumo wetu wa uchumi ulivyo na maisha ya wananchi wake, au pia kwamba wamechelewa kwasababu tuliendelea kupokea wageni wote hata kutoka China! Lakini haina maana kuwa partial lockdowns hazifai na wala hazikufaa! Na lockdowns kwenye maeneo korofi ni za muhimu!
Lakini pia tulipuuza tokea mwanzo na kuanza kusema wapinzani wanataka wananchi wafe na njaa! Hii ni propaganda ambayo matokeo yake si mazuri kwenye jamii inayokabiliana na janga hatari linalochukuwa maisha ya watu kila siku na pengine kila saa duniani.
Bila kupoteza muda, naweka hiki kipande hapo chini chenye kusapoti ninachokisema, pia link kama ukitaka kusoma habari yote na kujiridhisha wewe mwenyewe kuwa niyasemayo ni kweli.
Mike Dewine gavana wa Ohio, alipata umaarufu hata kumzidi Trump ambaye naye akaanzisha utaratibu wa kuongea na waandishi wa habari kila siku. Jambo ambalo Dewine alikuwa akilifanya jimboni kwake kila siku saa nane mchana, na wakati huo wana Ohio wanakuwa kwenye luninga zao wakimsikiliza. Ndiyo wakaanzisha usemi wa “it’s 2’oclock somewhere...wine with mr Dewine”, ambapo wakati wa lunch wanapata wine wakimsikiliza Dewine. Wala hawa kuwa na habari na Trump!
A Republican, he took early and bold actions to lock down his state, even as the head of his party, President Trump, dismissed the threat of the pandemic.
Ohio’s G.O.P. Governor Splits From Trump, and Rises in Popularity
Kwahiyo ndugu watanzania wenzangu, kabla ya kufanya upotoshaji, jiridhishe kwa kautafiti kadogo tu ili uweze kuwa huru kifikra! kama ikifikia mahali unamkabidhi mtu mwingine jukumu la kufikiria kwa niaba yako, ujuwe kuna shida kubwa sana kwa upande wako! Kusema lockdown haisaidii, ni sawa pia na kusema “to hell with social distancing”. Kwasababu huwezi kuwaambia watu wafuate masharti kwa ugonjwa ambao siyo hatari kabisa kwa jinsi unavyochukuliwa, kutokana na hatua za viongozi wetu, pamoja na matam
Siyo sahihi kusema lockdown haisaidii kwasababu zenu za kisiasa! Kwanza ingekuwa ni kwetu, huyo Dewine angekiona cha mtemakuni!
Lakini kwasababu ya kiasi cha demokrasia na mfumo wao wa uongozi, Dewine aliweza kuchukuwa maamuzi muhimu kwenye jimbo lake kinyume na rais wa nchi! Na ameonekana kwamba alikuwa sahihi na kiongozi shupavu!
Nyota yake inang’ara! Trump hawezi tena kusema kuwa lockdown haisaidii! Na kwetu Tanzania siyo sahihi kusema hivyo, semeni tu hamkuchagua lockdowns kwasababu mtakufa njaa, ama pia mlichelewa kuchukuwa hatua za kufunga mipaka!
Mag3 Nguruvi3 JokaKuu Kalamu1 imhotep Detective J
Mkuu USA maana yake ni muunganiko wa nchi zaidi ya 40 yaani ni kama kuichukulia Afrika Mashariki, kati na Kusini.USA wanakufa kama Kuku usipotoshe